JamiiForums
52.8K subscribers
34.4K photos
2.45K videos
31.3K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
CHINA: MAAMBUKIZI MAPYA 57 YA #COVID19 YARIPOTIWA

> Maambukizi haya ni makubwa kwa China tangu Aprili

> Idadi hiyo inafanya China kuwa na jumla ya maambukizi 83,123 huku watu 78,369 wakiripotiwa kupona

Soma https://jamii.app/57ChinaCOVID19
#JFCOVID19_Updates
ATLANTA: POLISI WAMUUA MTU MWEUSI MWINGINE KWA RISASI

> Rayshard Brooks (27), amepigwa risasi na Polisi Ijumaa usiku

> Afisa aliyehusika na tukio hilo, Garrett Rolfe ameshafukuzwa kazi, Devin Bronsan aliyeshiriki kwenye tukio amebadilishiwa kazi

Soma https://jamii.app/MweusiMwinginePolisi
#JFLeo
MANYARA: MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA BABATI AFARIKI DUNIA

- Mkurugenzi Mtendaji Hamis Malinga amefariki dunia kwenye hospitali ya rufaa ya mkoa huo

- Mbunge wa Babati Vijijini, Vrajlal Jituson amesema Hamis alikuwa amelazwa hospitalini hapo

Soma https://jamii.app/HamisMalingaAfariki
PETER MSIGWA ATANGAZA NIA YA KUGOMBEA URAIS KUPITIA CHADEMA

> Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa amesema anasubiri chama chake kiweze kumpa ridhaa ya kugombea

> Amesema anataka kufanya mageuzi makubwa ya Kiuchumi, Kielimu na Utawala Bora

Soma https://jamii.app/MsigwaUraisTz
#JFSiasa
KENYA: MBARONI HUKU MADUMU 1,265 YA MAFUTA YA KUPIKIA YALIOISHA MUDA YAKIKAMATWA

- Maafisa wa upelelezi huko Changamwe, Kaunti ya Mombasa leo wamemkamata Deborah Taabu (50) aliyekuwa akimiliki mafuta ya kupikia yaliyoisha muda wa matumizi aliyotaka kwenda kuyauza

Soma https://jamii.app/ExpiredCookingOil
TABORA: MBUNGE WA VITI MAALUM (CUF), REHEMA MIGILA AHAMIA CCM

- Mbunge wa Viti Maalum (CUF) mkoa wa Tabora, Rehema Juma Migila amejiunga na CCM akidai kuridhishwa na utekelezaji wa ilani za chama hicho chini ya uongozi wa Rais Magufuli

Soma https://jamii.app/RehemaMigilaCCM
#CORONAVIRUS: UFARANSA KULEGEZA MASHARTI ZAIDI KUANZIA LEO

- Safari za nchi nyingine za Ulaya zitaruhusiwa. Migahawa na hoteli nchi nzima kufunguliwa

- Hata hivyo, Rais Emmanuel Macron ameonya kuna uwezekano ugonjwa utarejea

Soma https://jamii.app/COVID19Updates
#JFCOVID19_Updates
#CORONAVIRUS GHANA: RAIS ASEMA NI LAZIMA KUVAA BARAKOA

- Agizo hilo limetolewa na Rais Nana Akufo-Addo kufuatia ongezeko la visa vya #COVID19

- Ghana imerekodi visa 11,964, vifo 54 na wagonjwa 4,258 wamepona

Soma - https://jamii.app/CoronaGhana
#JFCOVID19_Updates
BUNGE LAPITISHA BAJETI YA SERIKALI KWA 2020/2021

- Bunge la Tanzania limepitisha Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2020/21 ya Tsh. Trilioni 34.88 kwa kupigiwa kura 304 za Ndiyo

- Kura za Hapana ni 63 na Wabunge 13 hawakuwepo Bungeni

Soma - https://jamii.app/Bajeti2020
MWANAMUZIKI HARMONIZE KUGOMBEA UBUNGE JIMBO LA TANDAHIMBA

> Mwanamuziki Rajab Abdul maarufu Harmonize, amesema ana mpango wa kugombea Ubunge katika Jimbo la Tandahimba Mkoani Mtwara, miezi kadhaa baada ya Rais Magufuli kupendekeza afanye hivyo

Soma - https://jamii.app/HarmonizeUbunge
MBUNGE ‘BWEGE’ ATANGAZA KUHAMIA ACT-WAZALENDO

- Mbunge wa Jimbo la Kilwa Kusini, Selemani Bungara (Bwege) ametangaza kukihama Chama 'Civic United Front (CUF)' na kuhamia Chama cha ACT-Wazalendo mara baada ya Bunge kuvunjwa kesho

Soma - https://jamii.app/BwegeACT
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
SERIKALI: HOSPITALI ZOTE ZIACHE KUWADAI WAGONJWA DAMU KABLA YA HUDUMA

- Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu ameziagiza Hospitali zote nchini, Zahanati na Vituo vya Afya kuacha kuwadai damu wagonjwa kabla ya kuwapa huduma

- Amesema masuala ya wanandugu kuambiwa wapeleke watu wa kuchangia damu kabla ya huduma ni kinyume na taratibu na kanuni za utoaji wa huduma za afya

Soma - https://jamii.app/DamuSalamaTZ
UGANDA: MAAMBUKIZI YA #COVID19 YAFIKIA 705

- Visa vipya 9 vimethibitishwa baada ya kupima sampuli 2,677

- Pia, madereva wa malori 37 wamekutwa na #Corona na kurudishwa nchini kwao, 1 ni raia wa Tanzania

- Wagonjwa 299 wamepona

Soma https://jamii.app/Corona705-UG
#JFCOVID19_Updates
KUWANIA URAIS ZANZIBAR: ALI ABEID KARUME NA MBWANA BAKARI JUMA WACHUKUA FOMU KUPITIA CCM

- Zoezi la kuchukua fomu za kuwania Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ule wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kwa tiketi ya CCM limeanza leo na litakamilika Juni 30, 2020

Soma - https://jamii.app/UraisZanzibar
LINDI: ACHARAZWA VIBOKO 12 KWA KUMBAKA MWANAFUNZI

- Mahakama ya Mkoa imemhukumu Kassimu Bidhali Chilumba (18), kuchapwa viboko 12 kwa kumbaka mwanafunzi wa Shule ya Sekondari Nyengedi

- Mshtakiwa amejitetea kuwa ibirisi wa mapenzi ndiye aliyemshawishi kufanya hivyo

Soma https://jamii.app/Viboko12Ubakaji
WANAOVUTA SIGARA: JE, WAKO HATARINI ENDAPO WATAAMBUKIZWA #COVID19?

> Wanaovuta sigara wapunguze au kuacha ili kuepuka hatari iwapo watapata na #CoronaVirus

> Wavutaji wanaweza kupata maradhi ya mapafu(Pneumonia) kuliko wasiovuta

> #CoronaVirus hushambulia mapafu na Sigara hudhoofisha mapafu, ni hatari zaidi endapo mtumiaji wa sigara atapata #COVID19

> Aidha, wapo watumiaji wanaochangia Sigara hiyo ni hatari zaidi kwasababu wanarahisisha maambukizi ya #COVID19

Soma > https://jamii.app/COVID19VsSigara

#IshiNaCOVID19
UGANDA: VIONGOZI WA UPINZANI WAUNGANA DHIDI YA RAIS MUSEVENI

- Kizza Besigye na Robert Kyagulanyi (Bobi Wine) wameunda muungano unaoitwa 'United Forces of Change'

- Wanalenga kusimamisha mgombea mmoja dhidi ya Rais Museveni ktk Uchaguzi 2021

Soma https://jamii.app/MuunganoWapinzaniUG
KENYA: WATUMISHI WANNE WA IKULU WAKUTWA NA #CORONAVIRUS

- Watumishi wote wa Ikulu akiwemo Rais Kenyatta na familia yake walipimwa Juni 11, 2020

- Msemaji wa Ikulu amesema Rais Kenyatta pamoja na familia yake hawana #Corona

Soma https://jamii.app/Covid19IkuluKE
#JFCOVID19_Updates
#CORONAVIRUS KENYA: MAAMBUKIZI YAFIKIA 3,727 BAADA YA VISA 133 KUREKODIWA

- Wagonjwa 33 wamepona na idadi ya waliopona #COVID19 hadi sasa kuwa 1,286

- Aidha, vifo vimeongezeka hadi 104 baada ya mgonjwa mmoja kufariki dunia

Soma - https://jamii.app/Corona3727-KE
#JFCOVID19_Updates
WABUNGE WATATU WA VITI MAALUM CHADEMA WAJIUNGA CCM

- Wabunge Dkt. Immaculate Sware Semesi, Anna Gidarya na Latifa Chande wametangaza leo Bungeni kujiunga na CCM

- Chande na Semesi ni miongoni mwa Wabunge waliotakiwa kujieleza baada ya kukiuka agizo la kukaa Karantini

Soma https://jamii.app/Wabunge3CDM-CCM
#JFSiasa