JamiiForums
56.3K subscribers
32.8K photos
1.82K videos
29.9K links
Official JamiiForums Telegram Channel | Be Informed, Engaged & Entertained
Download Telegram
#CORONAVIRUS: BRAZIL IMERIPOTI VISA VIPYA 33,274 NDANI YA SAA 24

- Jumla ya visa imefikia 499,966 ikiwa ni nchi ya pili kwa visa vingi nyuma ya Marekani (2,036,110)

- Pia, imerekodi vifo vipya 956 na kuwa na jumla ya vifo 28,849

Soma https://jamii.app/COVID19Updates
#JFCOVID19_Updates
TCRA-CCC YAZITAKA KAMPUNI ZA SIMU KUSHUSHA BEI ZA INTANETI KIPINDI CHA #COVID19

> Imeziandikia barua kampuni za simu kuzitaka kupunguza gharama za intaneti

> Imesema matumizi ya intaneti yameongezeka kutokana na baadhi ya Waajiriwa kufanyia kazi nyumbani

Soma https://jamii.app/BeiHudumaInternet
WHO: ZAIDI YA WATU MILIONI 40 WENYE MIAKA 13–15 WAMEANZA KUTUMIA TUMBAKU

> Mei 31 kila mwaka ni siku ya Kuhimiza Kupinga Matumizi ya Tumbaku Duniani

> WHO imeshauri watu wenye ushawishi kukataa udhamini wa kampuni za tumbaku

Soma https://jamii.app/TobaccoDay
#JFLeo #TobaccoExposed
MASHABIKI WA SOKA WARUHUSIWA KUHUDHURIA VIWANJANI

- Serikali imesema mashabiki waruhusiwe kuingia viwanjani kuona mechi za Ligi. Mchezo utakaohisiwa kuwa na mashabiki wengi, waruhusiwe nusu ya uwezo wa uwanja

- Aidha, imeruhusu Ligi za soka kuendelea kuchezwa kwa mtindo wa nyumbani na ugenini badala ya kituo kimoja

Soma https://jamii.app/SokaKushangilia
#JFMichezo #Sports
KENYA: WAFUNGWA 31 WAKUTWA NA #COVID19 KATIKA GEREZA LA NAIROBI

- Wamebainika baada ya sampuli 59 kupimwa Alhamis, Mei 28 katika Gereza hilo

- Kenya sasa ina jumla ya visa vya #CoronaVirus 1,888 baada ya wagonjwa wapya 143 kutangazwa jana, Mei 30

Soma https://jamii.app/31WafungwaKenya
#JFCOVID19_Updates
#COVID19-KENYA: VISA VYAFIKIA 1,962. WALIOPONA WAFIKIA 478

- Wagonjwa 74 wameripotiwa baada ya sampuli 1,574 kupimwa ndani ya saa 24

- Vifo vimefikia 64 baada ya mtu mmoja kufariki. Waliopona wamefikia 478 baada ya watu 14 kupona

Soma https://jamii.app/COVID19KE-1962
#JFCOVID19_Updates
UGANDA: WATUMISHI WA AFYA 7 WAPATA #CORONAVIRUS

- Wizara ya Afya imesema wauguzi 3, madaktari 2, na wafanyakazi 2 wa ngazi ya juu wamepata maambukizi

- Nchi hiyo imerekodi visa 417 vya #COVID19 hadi sasa, na wagonjwa 72 wamepona

Soma https://jamii.app/Corona417-UG
#JFCOVID19_Updates
WASHINGTON DC, USA: MAANDAMANO YATINGA IKULU, RAIS TRUMP AJIFICHA. MABOMU YA MACHOZI YARUSHWA

- Waandamanaji zaidi ya 1,000 walikuwepo nje ya Ikulu ya Marekani. Vurugu zimepelekea Rais Trump kuwekwa kwenye chumba kilichopo chini cha ardhi

- Floyd alifariki dunia Jumatatu iliyopita huko Minneapolis baada ya Polisi mzungu, Derek Chauvin kumkandamiza shingoni kwa kutumia goti. Tayari Chauvin amefunguliwa mashtaka ya mauaji

Soma https://jamii.app/GeorgeFloydMarekani
#GeorgeFloyd #BlackLivesMatter
IGP SIRRO: HATUTAKI KUTUMIA MABOMU KWENYE UCHAGUZI MKUU

> Asema “Tunataka uchaguzi wa mwaka huu uwe wa haki kama Rais alivyosema"

> Pia, amewataka washtakiwa/wafungwa wanaopata msamaha wa Rais kutoka gerezani, kuacha kujiingiza ktk matukio ya uhalifu

Soma https://jamii.app/SirroUhalifuTZ
#CORONAVIRUS-BRAZIL: VISA ZAIDI YA 16,000 VYAREKODIWA NDANI YA SAA 24

- Brazil ina visa 514,992 vya #COVID19. Vifo 29,314 vimerekodiwa na waliopona ni 206,555

- Ni nchi ya 2 kuathirika zaidi baada ya Marekani yenye visa 2,183,493

Soma https://jamii.app/COVID19Updates
#JFCOVID19_Updates
UGANDA: WASANII MBOSSO NA DIAMOND WASHINDA TUZO ZA HIPIPO

- Diamond Platnumz amepata tuzo 2 za Wimbo bora wa Afrika Mashariki (The One) na Msanii Bora wa Tanzania huku Mbosso akijishinda tuzo ya Africa Fans Favorite Fresh Talent (Msanii mpya, Kipenzi cha Mashabiki Barani Afrika)

Soma - https://jamii.app/HiPipoAwards2020
#JFBurudani
JUNI 01: MAADHIMISHO YA SIKU YA MAZIWA DUNIANI

- Lengo la #WorldMilkDay ni kuelimisha jamii kuhusu maziwa na umuhimu wake kama chakula

- Kaulimbiu ya mwaka huu ni "Miaka 20 ya Siku ya Maziwa". Kutokana na #COVID19 hakuna hafla zilizoandaliwa

Soma https://jamii.app/WorldMilkDay
KENYA YASHEREHEKEA MIAKA 57 YA SIKUKUU YA MADARAKA

- Kutokana na #COVID19, wageni wachache wamealikwa kushiriki hafla inayofanyika Ikulu, wananchi watafuatilia mtandaoni

- #MadarakaDay ni kumbukumbu ya Kenya kupata uhuru wa kujitawala

Soma https://jamii.app/MadarakaDay-KE
WHO: UONGOZI IMARA UMECHANGIA AFRIKA KUTOKUWA NA MAAMBUKIZI MENGI YA #COVID19

> Afrika ina 1.5% ya maambukizi yote ya #Corona yaliyoripotiwa duniani na ina 0.1% ya vifo vya #Corona duniani

> Watu 146,794 wameripotiwa kupata #Corona barani Afrika, watu 61,773 kati yao wamepona na 4,223 wamefariki

Soma - https://jamii.app/CoronaLeardershipAfrica
#CORONAVIRUS INDIA: MJI WA NEW DELHI KUFUNGWA KWA WIKI MOJA

- Maduka na saluni zote zitaendelea kutoa huduma, lakini Mamlaka zimeweka agizo la muda wa kutotoka ndani

- Watumishi wa Serikali wenye utambulisho wataruhusiwa kusafiri

Soma https://jamii.app/COVID19Updates
#JFCOVID19_Updates
RATIBA YA LIGI KUU BARA YATANGAZWA

> Juni 13, 2020 kutakuwa na mchezo kati ya Mwadui FC na Yanga SC katika Uwanja wa Kambarage, Shinyanga na Coastal Union vs Namungo katika Uwanja wa Mkwakwani, Tanga

> Juni 14, 2020 itakuwa Simba SC vs Ruvu Shooting katika Uwanja wa Taifa, Dar na Azam FC vs Mbao FC Uwanja wa Azam Complex, Dar saa 1 usiku

Soma - https://jamii.app/RatibaLigiBara
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
IGP SIRRO: POLISI MSIWE KERO KWA WANANCHI WANAOTII SHERIA

- Amewataka Polisi kutokuwa kero kwa wananchi wanaotii Sheria, na kuwa mwiba kwa wale wanaozivunja

- Ametoa wito kwa Polisi kuhakikisha watu wanaishi kwa amani na utulivu

Soma - https://jamii.app/PolisiKeroWananchi
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
AFRIKA KUSINI: WANANCHI WARUHUSIWA KUNUNUA VILEVI BAADA YA ZUIO LA MIEZI MIWILI

- Maduka yanafunguliwa saa tatu asubuhi na kufungwa saa 11 jioni huku misururu mirefu ya Wateja ikishuhidiwa

- Zuio hilo liliwekwa ili kuruhusu Polisi na Hospitali kuelekeza nguvu zao kwenye #COVID19, kwakuwa vurugu zinazosababishwa na ulevi ni tatizo kubwa nchini humo

Soma - https://jamii.app/UuzwajiVilevi-SA
JESHI LA POLISI LAKAMATA WATU 87 KWA TUHUMA ZA MAUAJI KATIKA MIKOA 4

> Polisi Mkoani Mbeya wakishirikiana na Polisi Mkoa wa Songwe, Rukwa na Katavi wamewakamata watu 87 kwa tuhuma za mauaji wakiwemo waganga wa kienyeji wanaopiga ramli chonganishi katika ukanda huo

Soma - https://jamii.app/87MbaroniMauaji
#CORONAVIRUS: ZINGATIA HAYA ILI KUWALINDA WANAFUNZI WAWAPO SHULENI

> Kuwajenga Kisaikolojia, Uwepo wa Wahudumu wa Afya, Vituo vya kunawa mikono, kubadili mpangilio wa kukaa darasani na bwenini na kusitisha mikusanyiko ya asubuhi

> Kukabiliana na dharura za kiafya, udhibiti wa wageni na kuwa na jumbe za tahadhari

> Elimu ya Afya kwa Walimu, kupima wanafunzi, lishe na michezo

Soma > https://jamii.app/Covid19Muongozo

#COVID19