GEITA: Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita limesema linaendelea kuchunguza tukio la kutoweka kwa Elisha Juma, mkazi wa Mtaa wa Kadisi, Kata ya Katente, Wilaya ya Bukombe, ambaye pia ni mwimbaji wa nyimbo za injili.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Agosti 21, 2025, Polisi wameeleza walipokea malalamiko kwamba mnamo Agosti 19, 2025 saa 10:00 jioni, Elisha alichukuliwa na watu watatu wasiojulikana akiwa studio ya MAS J, Kilimahewa kata ya Bulangwa, waliokuwa na gari jeupe lisilojulikana usajili wake.
Aidha, Jeshi limetoa wito kwa yeyote mwenye taarifa ya kuweza kusaidia kupatikana kwa Elisha asisite kuziwasilisha ili zifanyiwe kazi.
Zaidi soma https://jamii.app/JumaElishaWasiojulikana
#JamiiAfrica #JamiiForums #Governance #Accountability #JFMatukio #UtawalaBora #HakiZaBinadamu
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Agosti 21, 2025, Polisi wameeleza walipokea malalamiko kwamba mnamo Agosti 19, 2025 saa 10:00 jioni, Elisha alichukuliwa na watu watatu wasiojulikana akiwa studio ya MAS J, Kilimahewa kata ya Bulangwa, waliokuwa na gari jeupe lisilojulikana usajili wake.
Aidha, Jeshi limetoa wito kwa yeyote mwenye taarifa ya kuweza kusaidia kupatikana kwa Elisha asisite kuziwasilisha ili zifanyiwe kazi.
Zaidi soma https://jamii.app/JumaElishaWasiojulikana
#JamiiAfrica #JamiiForums #Governance #Accountability #JFMatukio #UtawalaBora #HakiZaBinadamu
❤2
MOROGORO: Mdau wa JamiiForums.com kupitia Jukwaa la Habari na Hoja Mchanganyiko ametoa wito kwa Mamlaka za Serikali kuanzia ngazi za Vitongoji, Wenyeviti wa Vijiji, Madiwani, Askari, Wilaya, Mkoa na Mamlaka husika kufuatilia na kutatua mgogoro wa Wakulima na Wafugaji hasa maeneo ya Dumila na Kimamba.
Pia, Mdau amezitaka Mamlaka za juu kudhibiti vitendo vya #rushwa vinavyoendeleza kukandamiza suluhisho la Mgogoro huo akisema "Rushwa imetawala sana Kilosa, Viongozi Wanapokea kutoka kwa Wafugaji ili kuwakandamiza Wakulima, inauma sana na inatuumiza wengi wetu ambao hatuna kipato kikubwa."
Soma zaidi https://jamii.app/WafugajiWakulima
#JamiiAfrica #JamiiForums #JFMdau2025 #JFHuduma #Uwajibikaji
Pia, Mdau amezitaka Mamlaka za juu kudhibiti vitendo vya #rushwa vinavyoendeleza kukandamiza suluhisho la Mgogoro huo akisema "Rushwa imetawala sana Kilosa, Viongozi Wanapokea kutoka kwa Wafugaji ili kuwakandamiza Wakulima, inauma sana na inatuumiza wengi wetu ambao hatuna kipato kikubwa."
Soma zaidi https://jamii.app/WafugajiWakulima
#JamiiAfrica #JamiiForums #JFMdau2025 #JFHuduma #Uwajibikaji
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Akizungumza leo Agosti 21, 2025 katika Mkutano wa Wadau wa Sekta ya Habari Kanda ya Mashariki kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, Waziri wa Habari Prof. Palamagamba Kabudi amewataka Waandishi wa Habari kuacha rushwa na bahasha za kahawia, akisema Wananchi wanahitaji habari zenye uzito wa hoja, siyo uzito wa posho.
Ameongeza “Rushwa hupoteza uaminifu wa Vyombo vya Habari, kudhoofisha #demokrasia, inakuza ufisadi na kuhatarisha maisha ya waandishi waadilifu."
Zaidi soma https://jamii.app/KabudiRushwa
#JamiiAfrica #JamiiForums #UchaguziMkuu2025 #Governance
Ameongeza “Rushwa hupoteza uaminifu wa Vyombo vya Habari, kudhoofisha #demokrasia, inakuza ufisadi na kuhatarisha maisha ya waandishi waadilifu."
Zaidi soma https://jamii.app/KabudiRushwa
#JamiiAfrica #JamiiForums #UchaguziMkuu2025 #Governance
❤1
Afya ndiyo msingi wa Maisha. Bila Afya njema, utajiri na upendo hauwezi kuwa kamilifu.
Itunze na kuijenga Afya yako Mdau 🙂↕️
Tembelea JamiiForums.com kushiriki kwenye mijadala mbalimbali yenye tija.
#JamiiAfrica #JamiiForums #AmkaNaJamiiAfrica #GoodMorning #Maisha
Itunze na kuijenga Afya yako Mdau 🙂↕️
Tembelea JamiiForums.com kushiriki kwenye mijadala mbalimbali yenye tija.
#JamiiAfrica #JamiiForums #AmkaNaJamiiAfrica #GoodMorning #Maisha
❤1
NJOMBE: Mdau wa JamiiForums.com ambaye ni Mkazi wa Njombe Mjini ametoa wito kwa Halmashauri hiyo kuweka wazi ikiwa imetoa maelekezo kwa Shule za Msingi kutoza Wanafunzi hadi Tsh. 10,000 kwa ajili ya mitihani ya kila wiki, na kuongeza kuwa gharama hizo zimekuwa mzigo kwa Wazazi na Walezi.
Zaidi soma https://jamii.app/ShuleNjombeHalmashauri
#JamiiForums #JamiiAfrica #JFHuduma #Accountability #JFMdau2025 #JFUwajibikaji
Zaidi soma https://jamii.app/ShuleNjombeHalmashauri
#JamiiForums #JamiiAfrica #JFHuduma #Accountability #JFMdau2025 #JFUwajibikaji
❤1
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
KAGERA: Askofu Dkt. Benson Bagonza wa KKKT Dayosisi ya Karagwe akiongoza Ibada ya Jumapili katika Jimbo la Ihembe, Wilaya ya Karagwe, Agosti 11, 2025, amewaasa Watanzania kutumia busara katika kuchagua Viongozi kwenye Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29, 2025, ili kupata Viongozi wanaostahili.
Zaidi soma https://jamii.app/BagonzaUchaguziBusara
#JamiiForums #JamiiAfrica #Demokrasia #Siasa #UchaguziMkuu2025
Zaidi soma https://jamii.app/BagonzaUchaguziBusara
#JamiiForums #JamiiAfrica #Demokrasia #Siasa #UchaguziMkuu2025
❤1
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Makamu Mwenyekiti wa ACT Wazalendo - Bara, Isihaka Mchinjita, akihojiwa na kituo cha Redio cha #EastAfrica, Agosti 20, 2025 ameeleza kuwa Luhaga Mpina si mgeni ndani ya chama hicho kwani alijiunga nacho muda mrefu na tayari ni sehemu ya harakati zao.
Aliongeza kwa kusema kuwa mjadala mkubwa ulijikita kwenye namna bora ya kumtumia Mpina ili kuleta faida ya kisiasa kwa chama, ama kubaki kama Mbunge wa Kisesa au kuingia moja kwa moja kwenye siasa za kitaifa, na baada ya tathmini, chama kiliona atakuwa na mchango mkubwa zaidi kitaifa kuelekea uchaguzi mkuu.
Zaidi soma https://jamii.app/MpinaActUfafanuzi
#JamiiForums #JamiiAfrica #Demokrasia #Siasa #UchaguziMkuu2025
Aliongeza kwa kusema kuwa mjadala mkubwa ulijikita kwenye namna bora ya kumtumia Mpina ili kuleta faida ya kisiasa kwa chama, ama kubaki kama Mbunge wa Kisesa au kuingia moja kwa moja kwenye siasa za kitaifa, na baada ya tathmini, chama kiliona atakuwa na mchango mkubwa zaidi kitaifa kuelekea uchaguzi mkuu.
Zaidi soma https://jamii.app/MpinaActUfafanuzi
#JamiiForums #JamiiAfrica #Demokrasia #Siasa #UchaguziMkuu2025
👍1👎1
BURUDANI: Mdau, ni nukuu/mstari/kauli ipi (Punchline) kutoka kwenye filamu uliyoipenda zaidi? Ulisikia kwenye filamu gani na kwanini unaikubali?
Kushiriki mjadala soma https://jamii.app/NukuuMuvi
#JamiiAfrica #JamiiForums #JFBurudani #JFMoviesQuotes
Kushiriki mjadala soma https://jamii.app/NukuuMuvi
#JamiiAfrica #JamiiForums #JFBurudani #JFMoviesQuotes
❤1
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Akizungumza Agosti 21, 2025, Naibu Katibu Mkuu wa CHAUMMA, Benson Kigaila amesema Chama kimefanikiwa kuteua wagombea wa Udiwani 3,182 kati ya Kata 3,962 Tanzania Bara, na wagombea hao wanaruhusiwa kuchukua fomu katika Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (#INEC) huku akibainisha kuwa mchakato kwa Kata zilizobaki unaendelea.
Zaidi soma https://jamii.app/WagombeaChaummaUdiwani
#JamiiForums #JamiiAfrica #Siasa #UchaguziMkuu2025 #Governance #UtawalaBora
Zaidi soma https://jamii.app/WagombeaChaummaUdiwani
#JamiiForums #JamiiAfrica #Siasa #UchaguziMkuu2025 #Governance #UtawalaBora
👎1
SOMALIA: Marais watatu wastaafu Sharif Sheikh Ahmed, Abdiqasim Salad Hassan na Mohamed Abdullahi Farmaajo wameungana kutoa tamko dhidi ya Serikali ya Rais Hassan Sheikh Mohamud, wakiilaani kwa uporaji na uuzaji holela wa ardhi ya umma bila kuzingatia taratibu za Kisheria na usimamizi unaostahili.
Viongozi hao wamesema Serikali imekuwa ikihamisha umiliki wa ardhi bila kuhusisha Mamlaka ya Mikataba ya Taifa, na kutoingiza mapato kwenye Hazina ya Taifa. Hali inayosababisha Wananchi maskini wa Mogadishu kufukuzwa na kuondolewa katika makazi yao.
Wametaka Wananchi na Wafanyabiashara kuepuka kununua au kushiriki katika mali zilizopatikana kwa njia zisizo halali, wakisema ni mikataba hatarishi na isiyo na uhalali, hatua ambayo imepongezwa na makundi ya uharakati.
Soma zaidi https://jamii.app/Somalia
#JamiiAfrica #JamiiForums #Accountability #Governance
Viongozi hao wamesema Serikali imekuwa ikihamisha umiliki wa ardhi bila kuhusisha Mamlaka ya Mikataba ya Taifa, na kutoingiza mapato kwenye Hazina ya Taifa. Hali inayosababisha Wananchi maskini wa Mogadishu kufukuzwa na kuondolewa katika makazi yao.
Wametaka Wananchi na Wafanyabiashara kuepuka kununua au kushiriki katika mali zilizopatikana kwa njia zisizo halali, wakisema ni mikataba hatarishi na isiyo na uhalali, hatua ambayo imepongezwa na makundi ya uharakati.
Soma zaidi https://jamii.app/Somalia
#JamiiAfrica #JamiiForums #Accountability #Governance
❤1