JamiiForums
βœ”
52.8K subscribers
34.4K photos
2.44K videos
31.3K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
ZANZIBAR: Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja, ACP Abubakar Khamis Ally amesema wanawashikilia Watu 12 kwa tuhuma za kukutwa wakila na kunywa hadharani wakati wa Mchana kipindi cha Mwezi Mtukufu wa #Ramadhan

Amesema Watuhumiwa hao ni kati ya 65 ambao wamekamatwa katika Operesheni ya kupambana na matukio ambayo ni kero kwa Jamii na kuwa makosa mengine ni Wizi, Uporaji na Dawa za Kulevya

Ameeleza kuwa Jeshi la Polisi linaendelea na taratibu nyingine ili kuwafikisha Watuhumiwa Mahakamani

Soma https://jamii.app/MatukioZanzibar

#JFMatukio #JamiiForums
πŸ‘Ž6πŸ‘4
Unamshauri Mdau huyu afanye nini? Arudi Kijijini au akomae na Jiji mpaka kieleweke?

Mjadala zaidi https://jamii.app/NarudiKijijini

#JamiiForums #Maisha
πŸ‘2❀1
MANYARA: Mahakama ya Wilaya ya Mbulu imemhukumu Melkiadi Zakaria Tlehema, aliyekuwa Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Hayloto Kata ya Nambris, kwa makosa mawili ya Ubadhirifu na Matumizi Mabaya ya Madaraka

Melkiadi ameamriwa kulipa faini ya Tsh. 200,000 au kwenda jela Miezi Mitano. Pia, ametakiwa kurejesha Fedha alizofanyia #Ubadhirifu kiasi cha Tsh. 1,869,500 ambazo ni makusanyo ya Fedha za Wananchi kwa ajili ya Ujenzi wa Shule ya Msingi #Hayloto.

Mshtakiwa amelipa faini na kurejesha kiasi cha Fedha alichofanyia Ubadhirifu.

Soma https://jamii.app/HukumuMtendajiHayloto

#JamiiForums #KemeaRushwa #TokomezaRushwa #Accountability #Burudani #Uwajibikaji
πŸ‘2
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kimesema kinafuatilia Usalama wa Mfanyakazi wake, Wakili Joseph Moses Oleshangay ambaye inadaiwa anapewa vitisho na kufuatiliwa na Watu tofauti baadhi wakijitambulisha kuwa ni Askari wa Jeshi la Polisi

Mkurugenzi Mtendaji wa #LHRC, Dkt. Anna Henga amedai tangu Mwaka 2023 Joseph amekuwa anafuatiliwa na Watu ambao hawafahamu baadhi wakimpigia simu za vitisho huku akisema tayari wametoa taarifa kwa Polisi na Mamlaka nyingine zinazohusika

Amesema β€œMatukio hayo yanaminya uhuru wa Joseph kufanya kazi yake, tumeamua kusema wazi kwa jamii ili lolote litakalomtokea ijulikane tumeshasema.”

Soma https://jamii.app/Oleshangay

#CivilRights #HumanRights #JamiiForums #DigitalRights
πŸ‘2
JamiiForums inakutakia Mapumziko mema ya Mwisho wa Wiki na Ijumaa Kuu iliyo njema kwako na kwa uwapendao

#JamiiForums #GoodMorning #AmkaNaJF #JFQuotes #Democracy #GoodFriday
πŸ‘6
Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) limesitisha shughuli za Sanaa, Starehe na Burudani katika Kumbi 504 za Tanzania Bara kutokana na kutotimiza vigezo baada ya kuhuisha vibali kuanzia Machi 28, 2024 mpaka watakapolipia vibali kupitia Mfumo wa AMIS

#BASATA imesema imefikia hatua hiyo baada ya Wamiliki wa Kumbi 149 kutimiza maelekezo ya usajili kati ya 653 waliyopewa maelekezo ya kufanya hivyo awali mnamo Februari 19, 2024 ambapo walipewa Siku 14 wakamilisha mchakato huo

Baadhi ya Kumbi hizo ni #BilicanasClub (Arusha), #Fuego Lounge, Dar Live, Lango la Jiji, Dar West Inn na Lamada Hotel

Zaidi soma https://jamii.app/BASATAFungia

#JFEntertainment #Governance #JamiiForums
πŸ‘4❀1
Mtu mmoja amefariki Dunia na wengine Watatu kujeruhiwa baada ya gari aina ya Toyota Coaster iliyobeba mashabiki kadhaa wa Timu ya #Simba kutoka #Mbeya kupata ajali ya kugongana na Lori maeneo ya Vigwaza Mkoani #Pwani, Alfajiri ya leo Machi 29, 2024

Taarifa ya kifo imetolewa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Pius Lutumo ambaye amesema β€œNipo eneo la tukio tunaendelea kutoa magari. Chanzo cha ajali na taarifa nyingine zinaendelea kuchunguzwa na zitatolewa baadaye.”

Mashabiki hao walikuwa njiani kuelekea Dar es Salaam kwa ajili ya kushuhudia mchezo wa timu yao dhidi ya #AlAhly ya Misri kwenye Uwanja wa Mkapa ikiwa ni Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika unaotarajiwa kuchezwa usiku wa leo

Soma https://jamii.app/AjaliMashabiki

#JFMatukio #JamiiForums
πŸ‘3πŸ’”3πŸ•Š1
Unauzungumziaje ushauri huu wa Mdau kutoka JamiiForums.com kwenye Jukwaa la Michezo (Jamii Sports)? Kapiga kwenye mshono au oyaoya?

Kwa mjadala zaidi https://jamii.app/MechiYanga

#JamiiForums #JFSports #JFMichezo
πŸ‘3❀1
#MANYARA: Mahakama ya Wilaya Kiteto imemhukumu Mambe Mohamed Mambe, Mwenyekiti wa Kijiji cha Nasetan kwenda Jela Miaka Minne au kulipa faini ya Tsh. 1,000,000 kwa kuomba na kupokea hongo ya Tsh. 60,000

Mambe aliomba hongo hiyo ili asimchukulie hatua za Kisheria Mwananchi ambaye alifanya mkutano wa Wafugaji bila kibali cha Serikali ya Kijiji

Mshtakiwa ameshindwa kulipa faini na amepelekwa Gerezani kutumikia kifungo chake

Soma https://jamii.app/MkitiJelaKiteto

#JamiiForums #Accountability #Governance #KemeaRushwa
πŸ‘2❀1
Mdau anawapongeza wanaofanya Jogging sababu wanaweka Afya ya Mwili sawa lakini anasema kuna wakati wanapita katikati ya Barabara na kusababisha foleni ya Magari

Anasema jambo hili zuri hugeuka kuwa Kero kwa wengine hivyo anashauri Askari wa Usalama Barabarani waweke Utaratibu mzuri kwa ajili ya kila Mtumiaji wa Barabara

Soma https://jamii.app/BarabaraJogging

#JamiiForums #ServiceDelivery
πŸ‘4
Timu ya #Simba inacheza dhidi ya #AlAhly ya Misri katika Robo Fainali ya Kwanza ya Ligi ya Mabingwa Afrika kwenye Uwanja wa Mkapa, Dar es Salaam, leo Machi 29, 2024

Kila timu imeshinda mechi tatu, haya ni matokeo ya mechi zilizopita baina ya timu hizo:

24/10/2023 Al-Ahly 1-1 Simba
20/10/2023 Simba 2-2 Al-Ahly
09/04/2021 Al-Ahly 1-0 Simba
23/02/2021 Simba 1-0 Al-Ahly
12/02/2019 Simba 1-0 Al-Ahly
02/02/2019 Al-Ahly 5-0 Simba
29/08/1985 Al-Ahly 2-0 Simba
22/08/1985 Simba 2-1 Al-Ahly

Soma https://jamii.app/SimbaAlAhly

#JFSports #CAFCL #JamiiForums
πŸ‘5❀1
DAR: Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imewahukumu Wakazi 11 wa Ifakara Mkoani Morogoro kifungo cha Miaka Mitatu Jela au kulipa faini ya Tsh. Milioni 6 kila mmoja kwa kukutwa na hatia ya kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu na kutoa taarifa za uongo Mtandaoni

Waliohukumiwa ni Fredrick Kanepela, Julius Mwabula, Amiry Luwiso, Tareeq Sadrudin, Ashraf Awadhi, Frank Kifyoga, Samson Tandike, Michael Haule, Mussa Maganga, Helman Lwambano na Kelvin Mkapila ambao walikiri makosa yao kati ya Washtakiwa 23, ambapo wengine waliosalia mashauri yao yanaendelea

Watuhumiwa hao walikamatwa maeneo tofauti kwa makosa ya kutuma jumbe za kitapeli ikiwemo kutuma ujumbe wa β€œNitumie hiyo hela kwenye namba hii”, 5 kati ya waliohukumiwa wameridhia kulipa faini, wengine 6 wameendelea kutumikia kifungo baada ya kushindwa kulipa faini

Soma https://jamii.app/TumaNambaHii

#DigitalWorld #JFMatukio #JamiiForums
πŸ‘6❀2
Mambo si mazuri kwa Timu ya #Simba, baada ya kukubali kichapo cha goli 1-0 kutoka kwa #AlAhly ya Misri katika mchezo wa Kwanza wa Robo Fainali uliomalizika kwenye Uwanja wa Mkapa, Dar es Salaam

Hii inakuwa mara ya kwanza kwa Simba kupoteza mchezo dhidi ya Al Ahly kwenye Uwanja wa Nyumbani, ambapo katika mchezo huu goli pekee limewekwa wavuni na Ahmed Nabil Koka katika dakika ya 4

Timu hizo zitarudiana Aprili 5, 2024 kwenye Uwanja wa Cairo Nchini Misri. Katika rekodi za jumla Al Ahly inakuwa imeshinda mechi 4, Simba ikishinda mara 3

Soma https://jamii.app/SimbaAlAhly

#JFSports #CAFCL #JamiiForums
🀣6πŸ‘5❀4