JamiiForums
52.4K subscribers
34.4K photos
2.47K videos
31.4K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
#BURKINAFASO: JESHI LATEUA WAZIRI MKUU WA MPITO

Albert Ouedraogo ambaye ni Raia wa kawaida anatarajiwa kuunda Serikali Mpya ambayo jukumu lake kubwa litakuwa kudhibiti ghasia ambazo zimegharimu maisha ya maelfu, huku Mamilioni wakikimbia makazi

Soma - https://jamii.app/BurkinaPM
BURKINA FASO: SHAMBULIZI LAUA WANAJESHI 11

Mbali na vifo, Wanajeshi wengine kadhaa wamejeruhiwa. Waasi 15 wameuawa wakati wakitoroka baada ya kufanya shambulizi

#BurkinaFaso imekuwa ikisumbuliwa na mapigano yaliyopelekea maelfu ya Watu kuuawa

Soma - https://jamii.app/BurkinaFasoMachafuko
#BURKINAFASO: Jeshi limewataka raia kuondoka katika maeneo yanayotajwa kuwa na maslahi ya kijeshi kabla ya oparesheni zinazolenga kudhibiti ghasia kuanza

Mashambulizi yameendelea licha ya ahadi ya kuimarisha Usalama baada ya Mapinduzi ya Kijeshi

Soma - https://jamii.app/JeshiRaisBF
👍13🔥1
#BURKINAFASO: Mashirika ya kutetea #HakiZaBinadamu Nchini humo yamelishutumu Jeshi kwa kuwaua zaidi ya Watu 40 Kaskazini mwa Nchi hiyo

Jeshi la Burkina Faso limekanusha madai ya mara kwa mara ya ukiukaji wa Haki za Binadamu

Soma - https://jamii.app/JeshiKuuaRaia

#HumanRightsViolations
👏1🤔1
BURKINA FASO: ZAIDI YA WANAWAKE 50 WATEKWA

Matukio yametokea Kaskazini mwa #BurkinaFaso, ambapo Wanawake hao wametekwa katika makundi mawili kwa muda tofauti

Wanawake wengi wamekuwa wakitembea kimakundi kuingia Porini kutafuta Matunda na Chakula

Soma https://jamii.app/BurkinaFasoUtekaji

#HumanRights
👍1
UFARANSA YAMUITA NYUMBANI BALOZI WAKE WA BURKINA FASO

Hiyo inatokana na Uhusiano mbaya wa Kidiplomasia baina ya Mataifa hayo hivi karibuni

#BurkinaFaso inaamini #France haijawa na nguvu ya kutosha kukabili uasi unaoendelea Nchini humo

Soma https://jamii.app/FranceBurkinaFaso

#Diplomacy
👍7
BURKINA FASO YAWAFUKUZA WAANDISHI WA HABARI WA UFARANSA

Kitendo cha Wanahabari Sophie Douce na Agnes Faivre wanaoripoti katika magazeti ya Ufaransa kufukuzwa ni mwendelezo wa uhusiano mbovu baina ya Serikali za Mataifa hayo

Wamefukuzwa baada ya kuchapisha Taarifa ya Uchunguzi iliyoonesha Watoto wakifanyiwa ukatili katika Kambi za Kijeshi Nchini #BurkinaFaso

Soma https://jamii.app/BurkinaFasoFrance

#PressFreedom #ChildRights #Diplomacy
6👍3
RIPOTI: ENEO LA SAHEL NI HATARI ZAIDI KWA WAANDISHI WA HABARI

Reporters Without Borders imebaini vitisho, hatari ya utekaji nyara, hata mauaji, vimekuwa sehemu ya Maisha ya kila Siku ya Waandishi wa Habari katika eneo la #Sahel

Kuzorota kwa Vyombo vya Habari Nchini #Chad, #BurkinaFaso na #Mali kumechochewa na Mapinduzi ya Kijeshi ambayo yamesababisha Mazingira ya uhasama kwa Waandishi wa habari kutokana na #Sheria zinazolenga kubana Uhuru wa Vyombo vya Habari

Soma https://jamii.app/RipotiSahel

#PressFreedom
1👍1
#MICHEZO: Klabu ya #YangaFC imemtangaza Miguel Angel Gamondi (59) Raia wa Argentina kuwa Kocha Mkuu. Amewahi kufundisha timu za #WydadCasablanca ya Morocco, #MamelodSundowns ya Afrika Kusini na #CRBelouzdad ya Algeria

#MiguelAngel hadi anatangazwa Kama Kocha Mkuu wa #Yanga alikuwa amefundisha jumla ya vilabu 13 katika Maisha yake ya Soka na Timu ya Taifa ya #Burkinafaso

Soma https://jamii.app/YangaKochaMpya

#JFSports
👍12
Ufaransa imesitisha Misaada yote ya Kimaendeleo Nchini #BurkinaFaso baada Serikali ya Kijeshi kusema itapigana na yeyote atakayejaribu kuwavamia Kijeshi viongozi waliofanya Mapinduzi nchini Niger

Hatua hii inakuja baada ya muda uliotolewa na Jumuiya ya Afrika Magharibi #ECOWAS kwa Viongozi wa Mapinduzi ya Kijeshi nchini #Niger kurejesha Utawala wa Kiraia na Rais Mohamed Bazoum, kumalizika Agosti 6, 2023

Soma https://jamii.app/NigerCoup

#JamiiForums #NigerCoup #Democracy #Diplomacy #Diplomasia
👍2
Mtanzania ambaye ni Frateri wa Shirika la Wamisionari wa Afrika (White Fathers) Mzaliwa wa Parokia ya #Kabanga, Jimbo la #Kigoma, Melkiori Mahinini (27) ametekwa nyara na Watu wenye Silaha akiwa Parokia ya Mtakatifu Luka Gyedna, Jimbo la Minna Nchini Nigeria.

Taarifa iliyotolewa na Askofu wa Jimbo Katoliki la #Kigoma, Joseph Mlola, imesema Melkiori aliyekuwa kwenye Mwaka wake wa Uchungaji kabla ya Kuanza Masomo ya #Theolojia alitekwa Agosti 4, 2023 akiwa na Mwenzake, Padri Paul Sanogo, raia wa #BurkinaFaso

Aidha, Balozi wa Tanzania Nchini Nigeria, Dkt. Benson Bana, amesema taarifa alizozipata ni kwamba Watekaji wanataka Naira Milioni 100 (sawa na takriban Tsh. Milioni 325.1) ili kuwaachia huru wote wawili.

Soma https://jamii.app/MtanzaniaAtekwa

#JamiiForums #Kidnapping #SocialJustice
👍6