GEITA: Jeshi la Polisi linawashikilia Askari wanne wa Jeshi la Uhifadhi (JESHI USU) kwa tuhuma za mauaji ya Eziboni Fikiri (20), Mkulima, Mkazi wa Kijiji cha Msonga, Wilaya ya Bukombe ambaye walimkuta akikata mti eneo la Pori la Hifadhi ya Kigosi, Wilaya ya Bukombe, Agosti 13, 2025.
Taarifa ya Polisi imesema Mwili umehifadhiwa Hospitali ya Wilaya kwa ajili ya uchunguzi huku Watuhumiwa wakihojiwa na kwamba uchunguzi utakapokamilika watafikishwa Mahakamani.
Ikumbukwe hatua hiyo imechukuliwa ikiwa ni saa chache tangu Mdau wa JamiiForums.com awasilishe andiko akitoa wito kwa Jeshi la Polisi na TFS kufuatilia tukio hilo akidai kuna ukimya na hatua hazijachukuliwa.
Soma https://jamii.app/Askari4MauajiGeita
#JamiiForums #JamiiAfrica #Accountability #Uwajibikaji
Taarifa ya Polisi imesema Mwili umehifadhiwa Hospitali ya Wilaya kwa ajili ya uchunguzi huku Watuhumiwa wakihojiwa na kwamba uchunguzi utakapokamilika watafikishwa Mahakamani.
Ikumbukwe hatua hiyo imechukuliwa ikiwa ni saa chache tangu Mdau wa JamiiForums.com awasilishe andiko akitoa wito kwa Jeshi la Polisi na TFS kufuatilia tukio hilo akidai kuna ukimya na hatua hazijachukuliwa.
Soma https://jamii.app/Askari4MauajiGeita
#JamiiForums #JamiiAfrica #Accountability #Uwajibikaji
🤬1
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
DODOMA: Baadhi ya Wanachama wa CCM Kata ya Bereko na Kisese Wilayani Kondoa wametaka mchakato wa kura za maoni za Udiwani na Ubunge wa Kondoa Vijijini urudiwe, wakisema mchakato huo uligubikwa na madai ya #Rushwa na kwamba Viongozi waliochaguliwa kwenye mchakato huo walipendelewa.
Akijibu tuhuma hizo Katibu wa CCM Wilaya ya Kondoa, Abdulrahim Dogo alipozungumza na ITV amesema “Kura za maoni haimaanishi aliyeongoza kwenye Kura za maoni ndio mshindi na ndio Kanuni yetu ya Uchaguzi, isipokuwa tu kura hizo zimepigwa kwa ajili ya kuvisaidia vikao vya juu vifanye uteuzi wa mwisho.”
Zaidi Soma https://jamii.app/KuraZaMaoniKondoa
#JamiiAfrica #JamiiForums #UchaguziMkuu2025 #Accountability #Democracy
Akijibu tuhuma hizo Katibu wa CCM Wilaya ya Kondoa, Abdulrahim Dogo alipozungumza na ITV amesema “Kura za maoni haimaanishi aliyeongoza kwenye Kura za maoni ndio mshindi na ndio Kanuni yetu ya Uchaguzi, isipokuwa tu kura hizo zimepigwa kwa ajili ya kuvisaidia vikao vya juu vifanye uteuzi wa mwisho.”
Zaidi Soma https://jamii.app/KuraZaMaoniKondoa
#JamiiAfrica #JamiiForums #UchaguziMkuu2025 #Accountability #Democracy
Mdau wa JamiiForums.com ametoa wito kwa mamlaka zinazohusika na Sekta ya Elimu kuheshimu uhuru wa Vyuo Vikuu katika kuandaa na kusimamia mitaala ili kuondoa mkanganyiko na mabadiliko yasiyo na tija kwenye mitaala hiyo na fani mbalimbali.
Amedai maelekezo yasiyo wazi kutoka mamlaka za udhibiti wa mitaala yamesababisha mkanganyiko na baadhi ya fani kufutwa, akitoa mfano wa Chuo cha #UDOM ambapo Programu ya Education with Psychology ilisitishwa bila ya alichokiita “mashauriano ya kutosha” kati ya chuo na mamlaka husika kufanyika.
Ameshauri mamlaka zishauriane na Vyuo Vikuu na kuhusisha wabobezi pamoja na Sekta Binafsi kabla ya kubadilisha au kusitisha mitaala ili kuhakikisha mitaala hiyo ina manufaa ya muda mrefu na ushindani wa Kimataifa.
Mjadala zaidi Soma https://jamii.app/FaniVyuoni
#JamiiForums #JFElimu #JFMdau2025 #Accountability
Amedai maelekezo yasiyo wazi kutoka mamlaka za udhibiti wa mitaala yamesababisha mkanganyiko na baadhi ya fani kufutwa, akitoa mfano wa Chuo cha #UDOM ambapo Programu ya Education with Psychology ilisitishwa bila ya alichokiita “mashauriano ya kutosha” kati ya chuo na mamlaka husika kufanyika.
Ameshauri mamlaka zishauriane na Vyuo Vikuu na kuhusisha wabobezi pamoja na Sekta Binafsi kabla ya kubadilisha au kusitisha mitaala ili kuhakikisha mitaala hiyo ina manufaa ya muda mrefu na ushindani wa Kimataifa.
Mjadala zaidi Soma https://jamii.app/FaniVyuoni
#JamiiForums #JFElimu #JFMdau2025 #Accountability
MWANZA: Mdau wa JamiiForums.com anatoa wito kwa Mamlaka kufuatilia tukio analodai linadalili za ‘kuminywa’ linalohusu Mtoto wa Kiume wa Miaka Minne Mkazi wa Nyakato kulawitiwa na jirani yake na kwamba suala hilo lilipofikishwa Kituo cha Polisi Kirumba kumekuwa na hali ya sintofahamu kuhusu kinachoendelea.
Mdau anadai Mtoto anaishi na bibi yake, alipofanyiwa ukatili huo mara mbili mtuhumiwa alimwambia asiseme kwa kuwa akisema bibi yake ‘atamchapa sana’. Bibi alipoona mjukuu anatembea kwa kuchechemea akamlazimisha kusema nini kimemsibu, ndipo Mtoto akaelezea na kumtaja jirani yao.
Mdau anaongeza kuwa Bibi na Mtoto walipoenda kuripoti Kituo cha Polisi Nyakato walimkuta Mtuhumiwa eneo hilo pia akipiga ‘stori’ na Askari, Mtoto akaonesha aliyemfanyia ukatili yupo eneo hilo, mtuhumiwa akakamatwa lakini baada ya kesi kuhamishiwa Kituo cha Polisi Kirumba ndipo kukatokea ‘sintofahamu’ na haijulikani nini kinachoendelea.
Soma zaidi https://jamii.app/UkatiliNyakato
#JamiiForums #JamiiAfrica #HumanRights #ChildRights #Accountability
Mdau anadai Mtoto anaishi na bibi yake, alipofanyiwa ukatili huo mara mbili mtuhumiwa alimwambia asiseme kwa kuwa akisema bibi yake ‘atamchapa sana’. Bibi alipoona mjukuu anatembea kwa kuchechemea akamlazimisha kusema nini kimemsibu, ndipo Mtoto akaelezea na kumtaja jirani yao.
Mdau anaongeza kuwa Bibi na Mtoto walipoenda kuripoti Kituo cha Polisi Nyakato walimkuta Mtuhumiwa eneo hilo pia akipiga ‘stori’ na Askari, Mtoto akaonesha aliyemfanyia ukatili yupo eneo hilo, mtuhumiwa akakamatwa lakini baada ya kesi kuhamishiwa Kituo cha Polisi Kirumba ndipo kukatokea ‘sintofahamu’ na haijulikani nini kinachoendelea.
Soma zaidi https://jamii.app/UkatiliNyakato
#JamiiForums #JamiiAfrica #HumanRights #ChildRights #Accountability
❤2
MWANZA: Baada ya Mdau wa JamiiForums.com kuhoji Kiongozi gani wa juu anayemlinda mtuhumiwa wa Ulawiti kwa Mtoto katika Kituo cha Polisi Kirumba, Mkuu wa Mkoa, Said Mtanda ametoa maelekezo kwa Mwananchi huyo kuhusu kipi anachotakiwa kukifanya.
RC Mtanda ameandika “Namshauri huyo aliyedhurumiwa haki yake kufika pia Ofisi ya Mkuu wa Wilaya au Mkoa, kwa Mwanza kila Jumanne tunakutana na Wananchi wenye changamoto za namna hizo, anaweza kuwa hajasikilizwa na taasisi moja lakini Kiongozi wa Serikali katika Wilaya ya Nyamagana ni Mkuu wa Wilaya amuone, yawezekana hajui. Kama hatasikilizwa aje Ofisi ya Mkuu wa Mkoa siku ya Jumanne.”
Ikumbukwe Mdau alisema Mtu huyo ambaye amemlawiti Mtoto wa Miaka minne eneo la Nyakato, alifikishwa Kituo cha Polisi akahojiwa, Mtoto akatoa maelezo, vipimo vya Hospitali ya Sekou Toure vikaonesha ameingiliwa lakini hakuna kinachoendelea, akidai kuna mazingira ya Mtuhumiwa kulindwa na Kiongozi wa ‘juu’.
Zaidi soma https://jamii.app/RCMtandaUfafanuzi
#JamiiForums #JamiiAfrica #HumanRights #ChildRights #Accountability
RC Mtanda ameandika “Namshauri huyo aliyedhurumiwa haki yake kufika pia Ofisi ya Mkuu wa Wilaya au Mkoa, kwa Mwanza kila Jumanne tunakutana na Wananchi wenye changamoto za namna hizo, anaweza kuwa hajasikilizwa na taasisi moja lakini Kiongozi wa Serikali katika Wilaya ya Nyamagana ni Mkuu wa Wilaya amuone, yawezekana hajui. Kama hatasikilizwa aje Ofisi ya Mkuu wa Mkoa siku ya Jumanne.”
Ikumbukwe Mdau alisema Mtu huyo ambaye amemlawiti Mtoto wa Miaka minne eneo la Nyakato, alifikishwa Kituo cha Polisi akahojiwa, Mtoto akatoa maelezo, vipimo vya Hospitali ya Sekou Toure vikaonesha ameingiliwa lakini hakuna kinachoendelea, akidai kuna mazingira ya Mtuhumiwa kulindwa na Kiongozi wa ‘juu’.
Zaidi soma https://jamii.app/RCMtandaUfafanuzi
#JamiiForums #JamiiAfrica #HumanRights #ChildRights #Accountability
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
KATAVI: Mwakilishi wa Wafanyabiashara Mjini Mpanda, Aman Mahella amehoji kwanini mikopo kwa Vijana na akinamama hutolewa karibu na Uchaguzi huku ikiambatana na ujumbe wa Kisiasa jambo linaloashiria rushwa?
Akizungumza katika mafunzo ya kupambana na #Rushwa kuelekea #UchaguziMkuu2025, yaliyotolewa na #TAKUKURU, Ijumaa Agosti 15, 2025, Mahella ametoa wito kwa Serikali kuimarisha mifumo ya kudhibiti rushwa ili kuondoa mianya hiyo wakati wa Uchaguzi.
Soma https://jamii.app/RushwaMikopoUchaguzi
#JamiiAfrica #JamiiForums #UtawalaBora #Uwajibikaji #Accountability #Governance
Akizungumza katika mafunzo ya kupambana na #Rushwa kuelekea #UchaguziMkuu2025, yaliyotolewa na #TAKUKURU, Ijumaa Agosti 15, 2025, Mahella ametoa wito kwa Serikali kuimarisha mifumo ya kudhibiti rushwa ili kuondoa mianya hiyo wakati wa Uchaguzi.
Soma https://jamii.app/RushwaMikopoUchaguzi
#JamiiAfrica #JamiiForums #UtawalaBora #Uwajibikaji #Accountability #Governance
DAR: Mdau wa JamiiForums.com amedai kuna changamoto ya upatikanaji wa kadi zinazotumika kununua tiketi katika usafiri wa Mabasi ya Mwendokasi na kutoa wito hatua zichukuliwe haraka kwa kuwa hali hiyo ni kero na inawakosesha baadhi ya Watu huduma.
Ikumbukwe Julai 26, 2025 Mdau mwingine alidai kuna kero kubwa ya kutopatikana kwa kadi hizo siku za wikiendi, Agosti 6, 2025, Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka (DART), Dkt. Athumani Kihamia alisema sio lengo lao kuuza kadi wakati wa Siku za Jumamosi na Jumapili, abiria anaweza kupata kadi kwa siku tano za wiki ambazo ni Jumatatu hadi Ijumaa.
Mjadala zaidi https://jamii.app/TiketiMwendokasi
#JamiiForums #JamiiAfrica #JFHuduma #Accountability #JFMdau2025 #JFUwajibikaji
Ikumbukwe Julai 26, 2025 Mdau mwingine alidai kuna kero kubwa ya kutopatikana kwa kadi hizo siku za wikiendi, Agosti 6, 2025, Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka (DART), Dkt. Athumani Kihamia alisema sio lengo lao kuuza kadi wakati wa Siku za Jumamosi na Jumapili, abiria anaweza kupata kadi kwa siku tano za wiki ambazo ni Jumatatu hadi Ijumaa.
Mjadala zaidi https://jamii.app/TiketiMwendokasi
#JamiiForums #JamiiAfrica #JFHuduma #Accountability #JFMdau2025 #JFUwajibikaji
❤1
Mdau wa JamiiForums.com kupitia jukwaa la Siasa ameibua hoja kuhusu magari yenye plate number za aina ya SSH 25-30 au SSH 2530, akisema kuna magari mengi yenye namba zinazofanana na wengi mtaani wanajiuliza iwapo wamiliki wake ni viongozi au la!
Amehoji iwapo tukio kama ajali au uhalifu likitokea litahusianishwa na gari lipi? Je, hii si aina ya kampeni ya mapema?
Kushiriki mjadala huu https://jamii.app/PlateNumberZaSamia
#JamiiForums #JamiiAfrica #Accountability #JFMdau2025 #JFUwajibikaji #Misinformation #Disinformation #MisDis2025 #TaarifaZaUchaguzi2025
Amehoji iwapo tukio kama ajali au uhalifu likitokea litahusianishwa na gari lipi? Je, hii si aina ya kampeni ya mapema?
Kushiriki mjadala huu https://jamii.app/PlateNumberZaSamia
#JamiiForums #JamiiAfrica #Accountability #JFMdau2025 #JFUwajibikaji #Misinformation #Disinformation #MisDis2025 #TaarifaZaUchaguzi2025
❤3
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
ARUSHA: Akizungumza na Waandishi wa Habari, Agosti 16, 2025, Katibu wa Itikadi, Siasa na Uenezi wa CCM, Saipulan Ramsey amesema “Chama Cha Mapinduzi hakijatoa kwa Mwanachama yeyote wala Mwananchi yeyote wala kutoa ruksa ya utengenezaji wa Namba za 'SSH 2530'. Ziko mamlaka husika zinazohusika na utoaji wa vibao vya namba za magari.”
Ameongeza “Chama hakina mamlaka ya kutengeneza vibao vya namba za magari, zipo mamlaka husika zinazoshughulika na jukumu hilo. Naomba mamlaka zinazohusika na utoaji wa namba za magari pamoja na usafirishaji zifuatilie yeyote aliyeweka namba hizo awaeleze amezipata wapi.”
Video Credit: Arusha Zone
Soma zaidi https://jamii.app/NambaZaSSH2530
#JamiiAfrica #JamiiForums #UtawalaBora #Uwajibikaji #Accountability #UchaguziMkuu2025
Ameongeza “Chama hakina mamlaka ya kutengeneza vibao vya namba za magari, zipo mamlaka husika zinazoshughulika na jukumu hilo. Naomba mamlaka zinazohusika na utoaji wa namba za magari pamoja na usafirishaji zifuatilie yeyote aliyeweka namba hizo awaeleze amezipata wapi.”
Video Credit: Arusha Zone
Soma zaidi https://jamii.app/NambaZaSSH2530
#JamiiAfrica #JamiiForums #UtawalaBora #Uwajibikaji #Accountability #UchaguziMkuu2025
❤1
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
MWANZA: Mkuu wa Mkoa, Said Mtanda, leo Jumatatu Agosti 18, 2025 amefafanua suala la Mtoto Mkazi wa Nyakato, Wilayani Ilemela aliyesemekana kulawitiwa na Steven Ibasa (Baba Claudia), kwa kueleza kuwa suala hilo limefikishwa Mahakamani na kwamba mtuhumiwa amekosa mtu wa kumdhamini, amepelekwa Gerezani Butimba.
Akiwa ofisini kwake, RC Mtanda amewataka Wananchi kuwa na imani na Muhimili wa Mahakama kwakuwa utatenda haki katika suala hilo.
Ikumbukwe, suala hilo liliibuliwa na Mdau wa JamiiForums.com akidai kuna mazingira ya kumlinda Mtuhumiwa huyo ambaye alishikiliwa katika Kituo cha Polisi Nyakato kisha Kituo cha Polisi Kirumba, hivyo akaomba Mamlaka za Juu kuingilia kati ili Haki ipatikane.
Soma zaidi https://jamii.app/SaidMtandaUpdates
#JamiiForums #JamiiAfrica #HumanRights #ChildRights #Accountability
Akiwa ofisini kwake, RC Mtanda amewataka Wananchi kuwa na imani na Muhimili wa Mahakama kwakuwa utatenda haki katika suala hilo.
Ikumbukwe, suala hilo liliibuliwa na Mdau wa JamiiForums.com akidai kuna mazingira ya kumlinda Mtuhumiwa huyo ambaye alishikiliwa katika Kituo cha Polisi Nyakato kisha Kituo cha Polisi Kirumba, hivyo akaomba Mamlaka za Juu kuingilia kati ili Haki ipatikane.
Soma zaidi https://jamii.app/SaidMtandaUpdates
#JamiiForums #JamiiAfrica #HumanRights #ChildRights #Accountability