Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kimesema kimepokea taarifa kutoka kwa Wananchi wa Wilaya ya Mkuranga - Pwani kuhusu kushikiliwa kwa Vijana wanne kwa zaidi ya siku 26 bila kufikishwa Mahakamani au kupewa haki yao ya dhamana kwa makosa ambayo yana dhamana Kisheria.
Taarifa ya LHRC iliyotolewa leo Agosti 15, 2025 imesema inatoa wito kwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani na Mkuu wa Polisi Wilaya ya Mkuranga kuhakikisha vijana wote wanaoshikiliwa wanaachiliwa bila masharti yoyote na kama kuna tuhuma za kijinai dhidi yao wafikishwe Mahakamani kwa mujibu wa Sheria.
Pia, LHRC imeeleza “Ibara ya 13(6) (b) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano inasema ni marufuku kwa Mtu aliyeshtakiwa kwa kosa la jinai kutendewa kama Mtu mwenye kosa hilo mpaka itakapothibitika kuwa anayo hatia ya kutenda kosa hilo.
Soma zaidi https://jamii.app/LHRCAgosti15
#JamiiForums #JamiiAfrica #HumanRights #Governance
Taarifa ya LHRC iliyotolewa leo Agosti 15, 2025 imesema inatoa wito kwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani na Mkuu wa Polisi Wilaya ya Mkuranga kuhakikisha vijana wote wanaoshikiliwa wanaachiliwa bila masharti yoyote na kama kuna tuhuma za kijinai dhidi yao wafikishwe Mahakamani kwa mujibu wa Sheria.
Pia, LHRC imeeleza “Ibara ya 13(6) (b) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano inasema ni marufuku kwa Mtu aliyeshtakiwa kwa kosa la jinai kutendewa kama Mtu mwenye kosa hilo mpaka itakapothibitika kuwa anayo hatia ya kutenda kosa hilo.
Soma zaidi https://jamii.app/LHRCAgosti15
#JamiiForums #JamiiAfrica #HumanRights #Governance
❤1
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
Akizungumza leo Agosti 15, 2025 Askofu Gwajima amesema kuwa Mwenyekiti wa #CHADEMA Tundu Lissu kuendelea kukaa Magereza sio picha nzuri.
Zaidi https://jamii.app/LissuMagerezaPichaMbaya
#JamiiForums #JamiiAfrica #HumanRights #Governance #KuelekeaUchaguzi2025
Zaidi https://jamii.app/LissuMagerezaPichaMbaya
#JamiiForums #JamiiAfrica #HumanRights #Governance #KuelekeaUchaguzi2025
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
Aliyekuwa Mbunge wa Kawe, Askofu Josephat Gwajima akizungumza kwa njia ya Mtandao, leo Agosti 15, 2025 ameomba mamlaka zifungulie Makanisa ya Ufufuo na Uzima nchini kote na kutoa tahadhari kwamba yasipofunguliwa ndani ya siku 10 atarudi tena na kutoa neno ambalo Watu watastaajabu.
Soma Zaidi https://jamii.app/GwajimaKujipendekeza
#JamiiAfrica #JamiiForums #HumanRights #HakiZaBinadamu
Soma Zaidi https://jamii.app/GwajimaKujipendekeza
#JamiiAfrica #JamiiForums #HumanRights #HakiZaBinadamu
❤1
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
Aliyekuwa Mbunge wa Kawe, Askofu Josephat Gwajima akizungumza kwa njia ya Mtandao, leo Agosti 15, 2025 amehoji kuhusu jaribio la kumuua Padre Fr. Kitima, akidai mpaka sasa hakuna aliyefikishwa Mahakamani.
Soma zaidi https://jamii.app/JaribioKitimaGwajima
#JamiiAfrica #JamiiForums #HumanRights #HakiZaBinadamu
Soma zaidi https://jamii.app/JaribioKitimaGwajima
#JamiiAfrica #JamiiForums #HumanRights #HakiZaBinadamu
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
Aliyekuwa Mbunge wa Kawe, Askofu Josephat Gwajima amesema Kiwango cha kupendwa kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kiko chini kuliko wakati wowote katika Historia ya siasa za Tanzania huku akitolea mifano kuwa kuna Viongozi wanaofunga “comments” katika mitandao yao ya Kijamii kuhofia maoni ya Wananchi.
Ameyasema hayo leo Agosti 15, 2025 wakati anazungumza kwa njia ya Mtandao
Zaidi https://jamii.app/CCMKuchukiwaHistoria
#JamiiAfrica #JamiiForums #HumanRights #FreedomOfExpression
Ameyasema hayo leo Agosti 15, 2025 wakati anazungumza kwa njia ya Mtandao
Zaidi https://jamii.app/CCMKuchukiwaHistoria
#JamiiAfrica #JamiiForums #HumanRights #FreedomOfExpression
❤1
MWANZA: Mdau wa JamiiForums.com anatoa wito kwa Mamlaka kufuatilia tukio analodai linadalili za ‘kuminywa’ linalohusu Mtoto wa Kiume wa Miaka Minne Mkazi wa Nyakato kulawitiwa na jirani yake na kwamba suala hilo lilipofikishwa Kituo cha Polisi Kirumba kumekuwa na hali ya sintofahamu kuhusu kinachoendelea.
Mdau anadai Mtoto anaishi na bibi yake, alipofanyiwa ukatili huo mara mbili mtuhumiwa alimwambia asiseme kwa kuwa akisema bibi yake ‘atamchapa sana’. Bibi alipoona mjukuu anatembea kwa kuchechemea akamlazimisha kusema nini kimemsibu, ndipo Mtoto akaelezea na kumtaja jirani yao.
Mdau anaongeza kuwa Bibi na Mtoto walipoenda kuripoti Kituo cha Polisi Nyakato walimkuta Mtuhumiwa eneo hilo pia akipiga ‘stori’ na Askari, Mtoto akaonesha aliyemfanyia ukatili yupo eneo hilo, mtuhumiwa akakamatwa lakini baada ya kesi kuhamishiwa Kituo cha Polisi Kirumba ndipo kukatokea ‘sintofahamu’ na haijulikani nini kinachoendelea.
Soma zaidi https://jamii.app/UkatiliNyakato
#JamiiForums #JamiiAfrica #HumanRights #ChildRights #Accountability
Mdau anadai Mtoto anaishi na bibi yake, alipofanyiwa ukatili huo mara mbili mtuhumiwa alimwambia asiseme kwa kuwa akisema bibi yake ‘atamchapa sana’. Bibi alipoona mjukuu anatembea kwa kuchechemea akamlazimisha kusema nini kimemsibu, ndipo Mtoto akaelezea na kumtaja jirani yao.
Mdau anaongeza kuwa Bibi na Mtoto walipoenda kuripoti Kituo cha Polisi Nyakato walimkuta Mtuhumiwa eneo hilo pia akipiga ‘stori’ na Askari, Mtoto akaonesha aliyemfanyia ukatili yupo eneo hilo, mtuhumiwa akakamatwa lakini baada ya kesi kuhamishiwa Kituo cha Polisi Kirumba ndipo kukatokea ‘sintofahamu’ na haijulikani nini kinachoendelea.
Soma zaidi https://jamii.app/UkatiliNyakato
#JamiiForums #JamiiAfrica #HumanRights #ChildRights #Accountability
❤2
MWANZA: Baada ya Mdau wa JamiiForums.com kuhoji Kiongozi gani wa juu anayemlinda mtuhumiwa wa Ulawiti kwa Mtoto katika Kituo cha Polisi Kirumba, Mkuu wa Mkoa, Said Mtanda ametoa maelekezo kwa Mwananchi huyo kuhusu kipi anachotakiwa kukifanya.
RC Mtanda ameandika “Namshauri huyo aliyedhurumiwa haki yake kufika pia Ofisi ya Mkuu wa Wilaya au Mkoa, kwa Mwanza kila Jumanne tunakutana na Wananchi wenye changamoto za namna hizo, anaweza kuwa hajasikilizwa na taasisi moja lakini Kiongozi wa Serikali katika Wilaya ya Nyamagana ni Mkuu wa Wilaya amuone, yawezekana hajui. Kama hatasikilizwa aje Ofisi ya Mkuu wa Mkoa siku ya Jumanne.”
Ikumbukwe Mdau alisema Mtu huyo ambaye amemlawiti Mtoto wa Miaka minne eneo la Nyakato, alifikishwa Kituo cha Polisi akahojiwa, Mtoto akatoa maelezo, vipimo vya Hospitali ya Sekou Toure vikaonesha ameingiliwa lakini hakuna kinachoendelea, akidai kuna mazingira ya Mtuhumiwa kulindwa na Kiongozi wa ‘juu’.
Zaidi soma https://jamii.app/RCMtandaUfafanuzi
#JamiiForums #JamiiAfrica #HumanRights #ChildRights #Accountability
RC Mtanda ameandika “Namshauri huyo aliyedhurumiwa haki yake kufika pia Ofisi ya Mkuu wa Wilaya au Mkoa, kwa Mwanza kila Jumanne tunakutana na Wananchi wenye changamoto za namna hizo, anaweza kuwa hajasikilizwa na taasisi moja lakini Kiongozi wa Serikali katika Wilaya ya Nyamagana ni Mkuu wa Wilaya amuone, yawezekana hajui. Kama hatasikilizwa aje Ofisi ya Mkuu wa Mkoa siku ya Jumanne.”
Ikumbukwe Mdau alisema Mtu huyo ambaye amemlawiti Mtoto wa Miaka minne eneo la Nyakato, alifikishwa Kituo cha Polisi akahojiwa, Mtoto akatoa maelezo, vipimo vya Hospitali ya Sekou Toure vikaonesha ameingiliwa lakini hakuna kinachoendelea, akidai kuna mazingira ya Mtuhumiwa kulindwa na Kiongozi wa ‘juu’.
Zaidi soma https://jamii.app/RCMtandaUfafanuzi
#JamiiForums #JamiiAfrica #HumanRights #ChildRights #Accountability
Umewahi kufanya hivyo Mdau? Ulichukua hatua gani baada ya kugundua hilo?
Tembelea JamiiForums.com kushiriki katika mijadala mbalimbali yenye tija.
#JamiiForums #JamiiAfrica #HumanRights #KauliZaChuki #StopHateSpeech #DigitalPeace #NoToHateSpeech #ResponsiblePosting #JamiiYenyeUelewa
Tembelea JamiiForums.com kushiriki katika mijadala mbalimbali yenye tija.
#JamiiForums #JamiiAfrica #HumanRights #KauliZaChuki #StopHateSpeech #DigitalPeace #NoToHateSpeech #ResponsiblePosting #JamiiYenyeUelewa
❤1
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
MWANZA: Mkuu wa Mkoa, Said Mtanda, leo Jumatatu Agosti 18, 2025 amefafanua suala la Mtoto Mkazi wa Nyakato, Wilayani Ilemela aliyesemekana kulawitiwa na Steven Ibasa (Baba Claudia), kwa kueleza kuwa suala hilo limefikishwa Mahakamani na kwamba mtuhumiwa amekosa mtu wa kumdhamini, amepelekwa Gerezani Butimba.
Akiwa ofisini kwake, RC Mtanda amewataka Wananchi kuwa na imani na Muhimili wa Mahakama kwakuwa utatenda haki katika suala hilo.
Ikumbukwe, suala hilo liliibuliwa na Mdau wa JamiiForums.com akidai kuna mazingira ya kumlinda Mtuhumiwa huyo ambaye alishikiliwa katika Kituo cha Polisi Nyakato kisha Kituo cha Polisi Kirumba, hivyo akaomba Mamlaka za Juu kuingilia kati ili Haki ipatikane.
Soma zaidi https://jamii.app/SaidMtandaUpdates
#JamiiForums #JamiiAfrica #HumanRights #ChildRights #Accountability
Akiwa ofisini kwake, RC Mtanda amewataka Wananchi kuwa na imani na Muhimili wa Mahakama kwakuwa utatenda haki katika suala hilo.
Ikumbukwe, suala hilo liliibuliwa na Mdau wa JamiiForums.com akidai kuna mazingira ya kumlinda Mtuhumiwa huyo ambaye alishikiliwa katika Kituo cha Polisi Nyakato kisha Kituo cha Polisi Kirumba, hivyo akaomba Mamlaka za Juu kuingilia kati ili Haki ipatikane.
Soma zaidi https://jamii.app/SaidMtandaUpdates
#JamiiForums #JamiiAfrica #HumanRights #ChildRights #Accountability