JamiiForums
55.4K subscribers
33.4K photos
2.03K videos
30.4K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
Yanayojiri katika Mjadala wa 'Haki ya Faragha na Ulinzi wa Taarifa Binafsi' unaoendelea Clubhouse

Fuatilia - https://www.clubhouse.com/join/jamiiforums/2gXFqw3K/MzaY4W7B

#DataPrivacy
KENYA YAKABILIWA NA UHABA WA KONDOMU

Imeelezwa, Vituo vya Afya vya Umma, Hoteli na Migahawa vinakabiliwa na uhaba huo kutokana na mvutano wa ushuru kati ya Wafadhili na Serikali

Kenya husambaza bure takriban Mipira milioni 180 kila Mwaka

Soma - https://jamii.app/LackCondomKE
UJERUMANI: Bunge limeidhinisha Sheria mpya za kukabiliana na ongezeko la maambukizi ya Virusi vya Corona

Miongoni mwa yaliyopitishwa ni Mtu atalazimika kuonesha uthibitisho wa ikiwa amechanjwa, amewahi kuugua Corona na kupona au kupima anapokuwa maeneo ya kazi na ktk usafiri wa Umma

Soma - https://jamii.app/GermySheriaUviko
#UVIKO3
UGANDA: WATUHUMIWA 5 WA MILIPUKO JIJINI KAMPALA WAUAWA NA POLISI

Wengine 21 wakamatwa ikiwa ni sehemu ya Uchunguzi wa Milipuko ya kujitoa mhanga iliyotokea mapema wiki hii

#Uganda imeimarisha usalama na Rais Museveni ameapa kuwashinda magaidi

Soma - https://jamii.app/5ArrestedUG
Vipo visababishi vingi vya Magonjwa ya Afya ya Akili ikiwemo sababu za Kijamii na Kisaikolojia kama Umasikini, kutengwa na Jamii, Utegemezi, Upweke na Upotevu wa vitu (kufiwa na Mtu wa karibu, kupoteza Mali, Kazi au kupata Ulemavu)

Pia, Mafarakano na mipasuko katika Jamii/Familia pamoja na matatizo ya Mahusiano, kukosa huduma muhimu, Unyanyasaji wa Kijinsia na Ubaguzi wa aina mbalimbali

Soma zaidi - https://jamii.app/SignsMentalDisorder
#AfyaAkili
COVID-19 HAISAMBAZWI NA TEKNOLOJIA YA 5G

Shirika la Afya Duniani (WHO) limesema Virusi vya Corona haviwezi kusambaa kupitia mawimbi ya redio au simu

Tayari #CoronaVirus imeenea katika Nchi nyingi ambazo hazina mitandao ya simu ya 5G

Soma - https://jamii.app/Corona5G

#UVIKO3
SUDAN: Mamlaka zimerejesha Huduma ya Intaneti takriban Mwezi mmoja tangu isitishwe baada ya Jeshi kuondoa Madarakani Serikali ya Mpito

Mahakama iliamuru Kampuni za Mawasiliano kurejesha intaneti tangu Novemba 09, lakini tatizo liliendelea

Soma - https://jamii.app/InternetSudan
MDAU: MBINU ZA MALEZI YA MTOTO NI MUHIMU ZIENDANE NA HATUA ZA UKUAJI WAKE

Mbinu za Malezi zinazoleta matokeo mazuri kwa Mtoto wa miaka 7 zinaweza zisiwe na matokeo mazuri kwa Mtoto mwenye miaka 13

Kuna umri Mtoto akifikia huwa na kawaida ya kuuliza 'kwanini' kwa kila jambo unalomwambia. Hali hii ni ya kawaida lakini usipoelewa unaweza kuhisi Mtoto ameanza Dharau

Soma - https://jamii.app/MbinuMaleziUmri
#ParentingTips
Katika usimamizi wa mali za Mamlaka ya Serikali za Mitaa, Ripoti ya CAG 2019/20 imeeleza kuwa Mali za kudumu zenye thamani ya Tsh. Bilioni 1.92 zilizonunuliwa na Mamlaka ya Serikali za Mitaa 10 hazitumiki

Mapungufu haya yanaweza kupelekea upotevu wa mali za Halmashauri na kukosekana thamani ya Fedha

Soma - https://jamii.app/MapungufuMali

#JFUwajibikaji
Siku ya Kimataifa ya Wanaume huadhimishwa kila Novemba 19, ikiwa ni fursa ya kuwasherehekea Wanaume. Siku hii inalenga kuwathamini Wanaume wote pamoja na Mchango wao katika Familia na Jamii kwa ujumla

Mwaka huu, Kaulimbiu ya Siku ya Wanaume inasema "Uhusiano bora kati ya Wanawake na Wanaume kwa lengo la kuimarisha Usawa wa Kijinsia na kutengeneza Dunia iliyo salama"

#JamiiForums #InternationalMensDay #MensDay
Mwaka 2019/20, CAG alifanya Ukaguzi wa utekelezaji wa mapendekezo katika ripoti 5 zilizotolewa Aprili 2016. Ripoti zilikuwa na mapendekezo 63 kwa Taasisi 4 zinazosimamia utafutaji na uendelezaji wa Mafuta na Gesi Asilia

Kati ya mapendekezo 63, ni mapendekezo 9 (14%) ndiyo yaliyotekelezwa kikamilifu. Mapendekezo 38 (60%) yako kwenye hatua mbalimbali za utekelezaji, mapendekezo 13 (24%) hayajatekelezwa kabisa

Soma - https://jamii.app/MapendekezoCAG

#JFUwajibikaji
MDAU: KWA RASILIMALI ZILIZOPO TANZANIA, TUNASTAHILI MAENDELEO TULIYONAYO?

Anasema Maendeleo tuliyonayo tangu Uhuru hayaendani na Rasilimali zilizopo, vilevile hayaendani na kasi ya mabadiliko ya Sayansi na Teknolojia

Ametaja sababu mojawapo inayopelekea kusuasua kwa Maendeleo ni kukosa Mfumo madhubuti wa Uongozi, akisema Nchi ilitakiwa iwe na misimamo yake na matakwa ya Ilani za Vyama yawe kama Mapendekezo

Soma Makala yake - https://jamii.app/MaendeleoTZ

#StoriesOfChange
MAMILIONI WAKABILIWA NA UHABA WA CHAKULA NCHINI SOMALIA

Zaidi ya watu Milioni 2 wanakabiliwa na uhaba wa Chakula na Maji kutokana na hali mbaya ya ukame

Umoja wa Mataifa (UN) wasema takriban watu 100,000 wamekimbia makazi yao kutafuta Chakula

Soma - https://jamii.app/ChakulaMajiSomalia
MDAU: NI MUHIMU KUAJIRIWA/KUJITOLEA KABLA YA KUANZISHA BIASHARA YAKO

Dawa ya kuondokana na tatizo la Ajira ni kujiajiri wenyewe, lakini kabla ya kujiajiri jambo muhimu tunapaswa kulifahamu vizuri ni Sekta Binafsi ilivyo na Idara gani ungependa kujiajiri

Mshiriki wa 'Stories Of Change' anasema Kampuni nyingi binafsi zina programu maalumu za kujitolea. Hii itakusaidia kujifunza jinsi Taasisi zinavyoundwa, kuajiri Watu na kuwasimamia na kutengeneza mahusiano ya kudumu kati ya Mteja na #Biashara.

Soma - https://jamii.app/FaidaKujitolea
CHINA: Umoja wa Mataifa umetoa rai kwa China kumwachia huru Zhang Zhan ambaye alihukumiwa kifungo cha miaka 4 baada ya kuhoji namna Mamlaka zinavyoshughulikia #COVID19

Familia na Ripoti kadhaa zimedai anakaribia kifo kutokana na mgomo wa kula

Soma - https://jamii.app/UNZhangChina
#AUSTRIA: Kansela Alexander Schallenberg amesema hatua ya kufungwa kwa shughuli za Umma itaanza kutekelezwa Jumatatu ili kudhibiti Maambukizi

Ulazima wa kumtaka kila Mtu kupata Chanjo dhidi ya Virusi vya Corona utaanza Februari mosi

Soma - https://jamii.app/LockdownAustria
#UVIKO3