Deep Web:
60 subscribers
5.97K photos
5.6K videos
26 files
19.8K links
Jua Zaidi Ya Unacho Kijua
Download Telegram
Paul Bonaventure

Conclave yaingia hatua ya siri kuu Makardinali wamefungiwa ndani ya Sistine Chapel.

Hatimaye, milango ya Kanisa la Sistine imeshafungwa rasmi.

Makardinali 133 kutoka pembe zote za dunia sasa wamefungiwa ndani, wakiwa wameingia kwenye sehemu takatifu ya historia ambayo imekuwa kitovu cha maamuzi makubwa ya Kanisa Katoliki kwa karne nyingi.

Kuanzia sasa, dunia haitaweza tena kuwaona wala kusikia lolote kutoka kwao.

Simu zimekabidhiwa, mawasiliano ya nje yamekatwa kabisa, na vyombo vya habari vimewekwa mbali.

Ndani ya ukuta huo wa kihistoria, utulivu wa ajabu umetanda ni sauti ya roho mtakatifu inayosubiri kupenya mioyo ya watakatifu hawa wa Kanisa ili kumpata Papa mpya.

Ni ukimya unaobeba uzito wa maelfu ya sala, matumaini ya mamilioni ya waumini, na historia ya karne nzima.
Paul Bonaventure

Karibu kwenye darasa la Meditation ujifunze na kujua mambo mbalimbali kukuhusu.

Utajifunza namna Meditation inavyo badilisha maisha yako ndani ya muda mfupi na kuongeza uelewa wako wa ndani.

Njoo Inbox nikupe utaratibu wa kujiunga na darasa hili la kipekee.
.
.
Paul Bonaventure

Kinachoshuhudiwa sasa nje ni kitu kimoja tu, moshi.

Ndio lugha pekee itakayobeba ujumbe kutoka ndani, moshi mweusi kuashiria kura bado hazijafikia uamuzi, na moshi mweupe utakapopanda juu kuelekea anga la Roma.

Utakuwa ni tangazo la ushindi wa kiroho, kwamba Papa mpya amepatikana.

Macho yote ya waumini duniani yako juu ya bomba hilo dogo linalochomoza kwenye paa la Sistine Chapel.

Dakika, saa, hata siku zitapita, lakini hakuna atakayejua ni nani anayepewa kura nyingi zaidi, nani anayeonyesha dalili ya kuungwa mkono.

Hadi sauti ya kengele kuu ya Mtakatifu Petro itakapolia, na mwinjilisti wa kwanza kututangazia. Habemus Papam! "Tunaye Papa!".
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
Mfalme👑🇹🇿

Elimu na Taarifa juu ya vidonda vya tumbo kwa asilimia kubwa hazina ukweli na utaendelea kuteseka kama utaendelea kufuata wanachokisema.
Paul Bonaventure

Maliza na Mungu 🙏🏾
Paul Bonaventure

Anza na Mungu 🙏🏾
Paul Bonaventure

Karibu kwenye darasa la Meditation ujifunze na kujua mambo mbalimbali kukuhusu.

Utajifunza namna Meditation inavyo badilisha maisha yako ndani ya muda mfupi na kuongeza uelewa wako wa ndani.

Njoo Inbox nikupe utaratibu wa kujiunga na darasa hili la kipekee.
.
.
Paul Bonaventure

Mpangilio wa siku ya pili ya Conclave, Safari ya kura inaendelea.

Siku ya pili ya Conclave huanza mapema na inafuata ratiba iliyopangwa kwa nidhamu kali, ikiambatana na maombi, ukimya wa kiroho, na mchakato makini wa upigaji kura.

Hii hapa ni mfululizo wa kinachoendelea leo ndani ya Sistine Chapel, mahali ambapo historia ya Kanisa Katoliki huandikwa kwa siri kubwa.

Makardinali huanza siku kwa Misa Takatifu na sala za kuomba mwanga wa Roho Mtakatifu.

Huu ni wakati wa tafakari na kusikiliza dhamiri kabla ya kuketi tena kupiga kura.

Kila Kardinali hupewa karatasi ya kura iliyoandaliwa rasmi.

Kura huandikwa kwa mkono kwa umakini mkubwa. Jina moja tu, kwa mwandiko mzuri.

Makardinali mmoja mmoja huinuka na kwenda mbele ya madhabahu, akiweka kura yake kwenye kifuko maalum cha dhahabu huku akisema kiapo.

“Ninamchagua yule ambaye mbele ya Mungu naamini anastahili kuchaguliwa kuwa Papa.”
Paul Bonaventure

Baada ya kila mtu kupiga kura, kura huhesabiwa hadharani mbele ya wote, lakini kwa usiri wa nani alipigia nani.

Kura hizo huunganishwa, kuchambuliwa, na kama hakuna aliyefikia theluthi mbili (kura 89 kati ya 133), huchomwa kwa moto wa kemikali maalum kutoa moshi mweusi.

Ingawa hairuhusiwi kampeni, makardinali wanaweza kuzungumza kwa uchache wakati wa kula au kupumzika, wakitafakari majina yanayojitokeza mara kwa mara.

Kura nyingine mbili hufanyika jioni kwa utaratibu ule ule.

Ikiwa bado hakuna mshindi, moshi mweusi huonekana tena.

Ikiwa jina moja litafikia kura 89 au zaidi, mara moja moshi mweupe hupaa ishara ya ushindi.

Kardinali huyo huchaguliwa kuwa Papa mpya.

Huulizwa, “Je, unalikubali uchaguzi huu wa kuwa Papa?” na “Ni jina gani unalotaka kutumia?”

Baadaye, dunia husikia, Habemus Papam! (Tunaye Papa!)

Leo inaweza kuwa siku ya kihistoria.
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
Mfalme👑🇹🇿

Kina mama wenye mimba huingiwa na uoga kupitiliza juu ya afya zao na Mtoto wake wa tumboni kitu ambacho hupelekea kufanya chochote anachoshauriwa ili mradi afya yake na Mtoto wake ziwe salama na hicho ndio chanzo kinachofanya washawishike kirahisi hata kama wanadanganywa.
Paul Bonaventure

Pili, Madhabahu Takatifu, Kwenye madhabahu ndipo sanduku la kura huwekwa.

Kabla ya kupiga kura, kila Kardinali hufika mbele yake kwa utaratibu, akiweka kura yake huku akisema maneno ya kiapo kwa sauti ya chini.

Hii ni ishara ya kwamba kila kura ni tendo la ibada, si la siasa.

Tatu, Viti vya Makardinali, Sawasawa na usawa.

Viti vyao huwekwa kwa mpangilio wa mduara, bila mtu kuwa juu ya mwingine.

Huu ni ujumbe wa unyenyekevu, kwamba hata mwenye nafasi kubwa bado ni miongoni mwa watumishi sawa mbele ya Roho Mtakatifu.
Paul Bonaventure

Nne, Moto wa Kura, Moshi Mweusi na Mweupe

Kila kura ikishamalizwa, huunguzwa, Moto huo huambatana na hisia za matumaini au masikitiko.

Moshi mweusi ni ishara ya “subira”, huku mweupe ni ushindi wa sala na umoja wa Kanisa.

Tano, Kengele ya Mtakatifu Petro.

Inapopatikana Papa mpya, si moshi pekee huonekana, ila kengele kubwa ya Mtakatifu Petro hulia, ikitangaza kwa sauti, “Tazama, mlinzi mpya wa kondoo wa Bwana amepatikana.”

Conclave si mkutano wa kura tu. Ni liturujia ya kiroho. Ni ibada iliyojaa uzito wa historia na hofu ya Mungu. Ni tukio lisilokuwa na mfano ambapo ukuta wa sanaa unakuwa pia ukuta wa neema.
Paul Bonaventure

Ishara za kiroho na slama maalum ndani ya Sistine Chapel wakati wa Conclave.

Ndani ya kuta za Sistine Chapel, palipojaa kazi ya sanaa ya Michelangelo juu ya dari na ukuta wa mwisho.

Makardinali huketi si tu kama wanasiasa wa kiroho, bali kama waumini walioitwa kushiriki katika tukio takatifu linalogusa historia ya milele.

Ndani ya ukimya na uzuri huo wa kale, kuna ishara nyingi za kiroho na heshima kuu zinazoshuhudiwa wakati wa Conclave.

Kwanza, Dari ya Michelangelo, Uumbaji wa Mwanadamu na hukumu ya mwisho.

Makardinali wanaketi chini ya uchoraji mashuhuri wa Michelangelo unaoonyesha siku ya hukumu na muumbaji akimpa Adamu uhai.

Ni ukumbusho kuwa wana jukumu la kuchagua mtu atakayeongoza roho za mamilioni kwa unyenyekevu, si kwa mamlaka.

Hukumu ya Mwisho iliyo juu ya madhabahu huwafanya wajitafakari. Je, chaguo letu litastahili mbele za Mungu?
Paul Bonaventure

Karibu kwenye darasa la Meditation ujifunze na kujua mambo mbalimbali kukuhusu.

Utajifunza namna Meditation inavyo badilisha maisha yako ndani ya muda mfupi na kuongeza uelewa wako wa ndani.

Njoo Inbox nikupe utaratibu wa kujiunga na darasa hili la kipekee.
.
.
OBBY

Nzinga hakuishia kujiita mfalme pekee alianza kuishi kama mwanaume, akivaa kama mwanaume na alianza kua na mahawala wengi wakiume aliokua akiwavalisha nguo za kike na kutoa amri ya lazima kuitwa mfalme.

Alibadirisha walinzi wake (bodyguards) kua wakike. Waliokua wamepewa mafunzo makali ya vita na mapigano.

Akatengeneza sehemu za kulala pamoja ndani ya ikulu yake ambamo walinzi wake wa yeye mwenyewe walilala pamoja huku akitoa amri ya kuzuia walinzi wake na viongozi wake kuingia kwenye mahusiano
OBBY

Serikali ya Angola ilijenga sanamu kwaajili ya kumkumbuka Nzinga mwaka 2002 moja ya mtaa katika jiji la Luanda umepewa jina la Nzinga
Mwaka 2014 Bank kuu ya Angola ilotengeneza sarafu yenye thamani ya kwanza 20 (kwanza ni pesa ya Angola) yenye picha ya Nzinga.
OBBY

Aliekua mume wake, Kasanje aliungana na viongozi wengine na kumshambulia Nzinga lakini hawakufanikiwa. Nzinga aliunda ushirikiano na waholanzi na kuwasaidia kuuteka mji wa Luanda kutoka kwa wareno.

Mpaka kufika mwaka 1644 wareno walimuona Nzinga kua adui yao namba moja, alikua na jeshi lenye nguvu sana na tajiri kutokana na biashara ya watumwa aliyokua akifanya na waholanzi. Mwaka huo huo Nzinga aliingia vitani na Wareno na aliwashinda ingawaje miaka miwili baadae (1646)walifanikiwa kumshinda.
Wareno walirudi kwa nguvu kushambulia jiji la Luanda na waliishia kusaini mkataba wa amani na waholanzi walioamua kuondoka kabisa Angola na kurudi Ulaya hivyo kuendelea kutawala Angola. Nzinga na Wareno waliendelea kupigana vita kwa muda wa miaka 25. Vita ilichosha pande zote na kufika miaka ya 1650 walianza mazungumzo ya Amani na kufanikiwa mwishoni mwa mwaka 1656 wakiwekeana mipaka ya utawala wao na mashart mengine.