JamiiForums
56.4K subscribers
32.7K photos
1.81K videos
29.9K links
Official JamiiForums Telegram Channel | Be Informed, Engaged & Entertained
Download Telegram
Kitu gani Mpenzi/Mwenza wako amewahi kukufundisha?

Mjadala https://jamii.app/MafunzoMpenzi

#JamiiForums #Maisha #LifeLessons #JFChitChats #JFStories
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimeripoti kuwa Jeshi la Polisi limemkamata Makamu Mwenyekiti wa Chama hicho, John Heche, leo Aprili 22, 2025 eneo la Kariakoo na kwamba baada ya kumshikilia alipelekwa Kituo cha Polisi Msimbazi, kisha kumtoa kituoni hapo na kumpeleka kusikojulikana

Katibu Mkuu wa #CHADEMA, John Mnyika ameiambia JamiiForums kuwa ”Ni kweli Heche anashikiliwa na Polisi, tunaelekea Kituoni kujua kinachondelea, tutatoa taarifa zaidi baadaye.”

Soma https://jamii.app/HecheKukamatwa

#JamiiForums #Democracy #JFMatukio
Mdau wa JamiiForums.com anasema Iwe Mvua au Jua, Giza au Nuru ila anachokijua ipo Siku ataendesha Gari aina ya 'Hilux'

Na wewe una kitu gani ambacho unapambana lazima uje kukimiliki kwenye Maisha yako?

Shiriki mjadala huu zaidi https://jamii.app/NiniUtamiliki

#JamiiForums #Maisha #LifeLessons #JFChitChats #JFStories
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
DODOMA: Waziri wa OR-TAMISEMI, Mohamed Mchengerwa ameeleza tuhuma zilizotolewa na Mbunge wa Arusha Mjini, Mrisho Gambo, hazina ukweli wala uthibitisho na kwamba hakuna upotevu wa fedha katika ujenzi wa jengo la Utawala la Halmashauri ya Arusha Jiji

Mchengerwa amesema uchunguzi wa tuhuma hizo zilizotolewa na Gambo Bungeni umekamilika kama alivyoelekezwa kufanya na Spika Tulia Ackson, ambapo amedai kuna cheche za Siasa ambazo hazifai ndani ya taasisi zenye misingi ya Kisheria

Soma https://jamii.app/BungeniAprili22

#JamiiForums #Governance #Kulekea2025 #Siasa
KATAVI: Mdau wa JamiiForums.com anaeleza Daraja la Milala Shongo lililopo Kijiji cha Milala, Manispaa ya Mpanda limekuwa tatizo la muda mrefu kwa Wananchi wanaopita hapo, hivyo kuwa kikwazo cha mawasiliano na kusababisha shughuli za kiuchumi kusimama

Anaeleza asilimia kubwa wanaopata changamoto ni Wanawake na Watoto ambao wanashindwa kuvuka, hasa wakati wanapoenda katika matibabu kwa kuwa wakati wa mvua maji hujaa na kukata mawasiliano

Anadai siku za nyuma kulikuwa na mchakato wa kujenga Daraja hilo lakini ghafla mpango ukasimama na hawajui nini kilitokea, anatoa wito kwa mamlaka husika kujenga Daraja hilo kwa kuwa hali ni mbaya wakati huu wa mvua

Soma https://jamii.app/MilalaShongo

#JamiiForums #Accountability #ServiceDelivery
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Aprili 14, 2025 Mdau wa JamiiForums.com aliandika kuwa kuna changamoto ya chemba kutiririsha Majitaka katika Mitaa ya Nyamwezi na Mhonda, mlango wa kuingilia Soko Kuu (Shimoni) na kueleza kwamba, hali hiyo imekuwa hivyo tangu Machi 2025

Aprili 22, 2025, Mdau mwingine amepita katika eneo husika na kueleza kuwa Miundombinu imerekebishwa na majitaka hayatiririki Mitaani kama ilivyokuwa awali

Soma https://jamii.app/UsafiKariakoo

#Accountability #Uwajibikaji #PublicHealth #JamiiForums
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, amewaonya Watu ambao wameanza kuwasili kwaajili ya kuhudhuria kesi ya Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Tundu Lissu, Mahakamani Aprili 24, 2025, akisema moto wa kisheria utashuka kwa nguvu zote kwa watakaodhamiria kuharibu Amani iliyopo

Soma https://jamii.app/ChalamilaKesiLissu

#JamiiForums #Governance #UchaguziMkuu2025 #Kuelekea2025
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Mdau wa JamiiForums.com anasema Wananchi wanaoishi Mbagala - Sabasaba, wanapata changamoto ya Mazingira kuchafuliwa na kuwa hatari kwa #Afya kutokana na Machinjio ya Ng’ombe ambayo yapo kwenye Makazi ya Watu

Anaeleza Maji machafu ambayo yanatoka kwenye Machinjio hayo tanatiririka kwenye Makazi ya Watu na hakuna jitihada zinazofanywa na Mamlaka kudhibiti hali hii, akidai hali imekuwa mbaya zaidi msimu huu wa Mvua

Soma https://jamii.app/MajiMachinjioMBG

#JamiiForums #Accountability #Uwajibikaji #PublicHealth
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
DODOMA: Spika wa Bunge, Dkt. Tulia Ackson, ametangaza kuchukua uamuzi wa kuwapeleka Mbunge wa Arusha Mjini, Mrisho Gambo pamoja na Waziri wa OR-TAMISEMI, Mohamed Mchengerwa mbele ya Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge, baada ya mvutano wa tuhuma zilizotolewa na Gambo kuhusu matumizi mabaya ya fedha

Gambo alitoa madai hayo, Jumatano Aprili 16, 2025 alipochangia hotuba ya makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI 2025/26, ambapo jana Aprili 22, 2025, Mchengerwa alijibu kuwa tuhuma hizo hazina ukweli

Soma https://jamii.app/GamboNaSpika

#JamiiForums #Accountability #Siasa
MALEZI: Mdau wa JamiiForums.com anasema Wazazi/Walezi, daima wana jukumu kubwa sana la kusisitiza Maadili kwa Watoto wao katika kipindi cha Ukuaji na wanavyochunguza Jamii inayowazunguka

Anasisitiza, usifuate mkumbo wa kuwaiga baadhi ya rafiki zako au Wanafamilia namna wanavyolea Watoto wao, zingatia kile unachotaka kukiona kwenye Maisha ya Wanao

Soma zaidi https://jamii.app/NguvuMtotoBora

#JamiiForums #Accountability #Uwajibikaji #Maisha #Malezi #Parenting
Mdau wa JamiiForums.com anasema alimpa Simu Mtoto wake ili acheze 'Game' kisha akatoka nje kwa dakika chache na alivyorudi ndani alikuta Mtoto anaichovya Simu kwenye Beseni la Maji huku anaipaka sabuni

Nawe unakumbuka hasara gani uliyowahi kuipata kupitia Mwanao au Mfanyakazi wako?

Tembelea Mjadala huu zaidi https://jamii.app/HasaraNyumbani

#JamiiForums #Maisha #JFStories #JFChitChats
DAR: Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kupitia ukurasa wake wa Instagram kimeandika kuwa Msafara wa Makamu Mwenyekiti Bara, John Heche umezuiwa na Jeshi na Polisi asubuhi ya leo Aprili 24, 2025 maeneo ya Daraja la Selandar wakati akielekea Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu

Taarifa imeeleza Heche alikuwa njiani kuelekea kufuatilia kesi ya Uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu ambapo amepelekwa Kituo cha Polisi cha Oysterbay akiwa na Mwenyekiti wa chama hicho Mkoa wa Mara, Chacha Heche pamoja na Walinzi wawili

Pia, chama hicho kimeeleza kuwa Katibu Mkuu wa Chama, John Mnyika naye amekamatwa na Polisi maeneo ya Fire akielekea Mahakamani kufuatilia kesi hiyo

Soma https://jamii.app/Aprili24Updates

#JFMatukio #JamiiForums #Kuelekea2025 #Democracy
DAR: Shauri la jinai linalomhusu Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Tundu Lissu, katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu linadaiwa litafanyika kwa njia ya Mtandao leo Aprili 24, 2025

Hata hivyo taarifa zisizo rasmi zinadai Lissu amegoma kushiriki katika Kesi hiyo kwa njia ya Mtandao akitaka afikishwe Mahakamani. Juhudi za kupata taarifa rasmi za Mamlaka zinaendelea

Kwa mujibu wa Wakili ambaye ni sehemu ya jopo la Mawakili wanaomtetea Lissu, ameiambia JamiiForums kwamba tayari wameingia Mahakama (Virtual court) kwa ajili ya kuanza kusikiliza kesi zinazomkabili mteja wao.

Soma https://jamii.app/LissuKesi

#JamiiForums #Kuelekea2025 #UchaguziMkuu2025 #Demokrasia
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
#HAKIZABINADAMU: John Pambalu (Mkurugenzi wa Mafunzo CHADEMA), Twaha Mwaipaya, Lucas Ngoto (Mwenyekiti wa CHADEMA Kanda ya Serengeti) pamoja na baadhi ya Wanachama wengine wamedaiwa kupigwa na kuumizwa leo Aprili 24, 2025

Soma https://jamii.app/PambaluKupigwaPolisi

#JamiiForums #JamiiAfrica #Kuelekea2025 #UchaguziMkuu2025
Motisha huja na kuondoka, ni hisia ya muda. Nidhamu ni maamuzi ya kila Siku ya kufanya kile kilicho sahihi hata kama huna hamasa.

Mafanikio ya kweli yanategemea nidhamu, si motisha pekee.

Tunakutakiwa Wikiendi njema

#JamiiForums #Lifelessons #Maisha