JamiiForums
57.3K subscribers
32.1K photos
1.7K videos
29.5K links
Official JamiiForums Telegram Channel | Be Informed, Engaged & Entertained
Download Telegram
TABORA: Mdau wa JamiiForums.com anaiomba Serikali kuingilia kati suala la baadhi ya Wananchi wa Mtaa wa Masimba, kutaka kuondolewa katika maeneo yao kinyume cha utaratibu, akidai anahisi baadhi ya Maafisa wa Ardhi wana maslahi binafsi

Mkuu wa Wilaya ya Tabora Mjini, Mhandisi Deusdedit Katwale amezungumza na JamiiForums na kusema “Nimeshaunda Kamati Maalum inafuatilia suala hilo itanipa ripoti ndani ya Wiki mbili, inawezekana anayelalamika hivyo ni Dalali kwa kuwa nilifika eneo la tukio na kutoa maelekezo.”

Soma https://jamii.app/MtaaWaMasimba

#JamiiForums #Accountability #CivilRights #Governance
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
IRINGA: Dkt. Godfrey Mtunzi kutoka Ofisi ya Mganga Mkuu wa Mkoa, amethibitisha uwepo wa Watu Wawili wenye dalili za kuwa na Ugonjwa wa Mpox katika Kata ya Kiesa na Kitanzini na kwamba wamefanyiwa vipimo ambavyo vimepelekwa Maabara Kuu kufanyiwa uchunguzi zaidi

Soma https://jamii.app/MpoxIringa

#JamiiForums #PublicHealth #Afya
MARA: Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Rorya, Abdul Mtaka, ameagiza taasisi za Mikopo zinazoshikilia kadi za benki za Watumishi wa Umma kama dhamana wanapokopa kuacha mara moja vitendo hivyo, kwa kuwa ni kinyume cha Sheria

Amesema “Wapo Watumishi wanaokopa katika Sekta rasmi zikiwemo Benki kwa kuzingatia utaratibu wa kiasi kinachotakiwa kusalia katika mishahara yao, baada ya hapo wanakwenda kukopa kwenye taasisi zisizo rasmi ambazo huchukua Kadi zao za Benki na namba za Siri na kuchukua fedha zinazoingia ili kurejesha mkopo.”

Ameongeza kuwa, vitendo hivyo vinawafanya Watumishi kutofanya kazi kwa ufanisi kwa kuwa wanajikuta hawana fedha za kukidhi mahitaji yao ya muhimu

Soma https://jamii.app/KaziZaBenki

#DataPrivacy #JamiiForums #Governance #DigitalSecurity #DataProtection
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Mratibu Kitaifa wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), Wakili Onesmo Olengurumwa, amesema mchakato wa ugawaji Majimbo una tatizo kutokana na vigezo vinavyotumuka, hivyo ameiomba Time Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) kufanya mjadala wa Kitaifa na Wadau wa Demokrasia kulijadili suala hilo

Amesema inatakiwa kufanyika tathmini kubwa ya Ugawaji wa majimbo, kwani vitu vya msingi vikizingatiwa kwenye mchakato inaweza kupunguza idadi ya majimbo hayo badala ya kuongeza, jambo linaloweza kupunguza gharama za uendeshaji

Amesema, mchakato huo upo Kikatiba lakini utaratibu wa sasa wa ugawaji majimbo haoni kama una uwiano sawa, kwani kuna maeneo ambayo ni makubwa kijiografia lakini kuna majimbo machache na mengine ni madogo lakini yana majimbo mengi

Soma https://jamii.app/MajimboUchaguzi

#Kuelekea2025 #UchaguziMkuu2025 #Democracy #Transparency #JamiiForums
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
Dar: Mwenyekiti wa ACT Wazalendo Taifa na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Othman Masoud Othman, amesema "Tuliamini kwenye siasa za maridhiano, tuliamini kwenye siasa za kistaarabu. Na tumeyafanya haya Tanzania Bara na Zanzibar kwa kuingia kwenye maridhiano. Malipo yetu yalikuwa ni nini? Malipo yetu ilikuwa viongozi wetu ikiwemo Mwenyekiti wetu wa Ngome ya Vijana kukamatwa, kutekwa na kuteswa"

Ameongeza kwa kusema kuwa Chama hicho kitashirikiana na Vyama vyote makini ambavyo viko tayari kupigania Demokrasia Nchini Tanzania.

Ameyasema hayo Machi 12, 2025 wakati akizungumza katika kongamano la viongozi wa ACT Wazalendo katika Makao Makuu ya Chama hicho Magomeni, Dar

Soma https://jamii.app/SiasaZaMapambano

#JamiiForums #Governance #UchaguziMkuu2025
Mwanachama wa Jukwaa la Habari na Hoja Mchanganyiko ndani ya JamiiForums.com, ameelezea kisa chake cha kutakiwa alipie gharama ya usafiri ili kupokea zawadi aliyotumiwa kutoka nje ya nchi na mtu ambae hawajawahi kuonana

Mdau, ushawahi kukutana na kisa kama hiki na ilikuwaje?

Mjadala zaidi https://jamii.app/KamaVileNtapeliwa

#JamiiForums #UtapeliMtandaoni #BewareOfScams #CyberSecurity #DigitalSafety #KataaUtapeliMtandaoni #KuwaMachoNaUtapeli
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
KENYA: Rais #WilliamRuto akizungumza na Wananchi wa Kibera, leo Machi 13, 2025 baada ya kusikia wakimuita jina lingine la utani la 'El Chapo', amesema “Mtaniua na majina. Mlianza na Justler, mkaenda Zakayo halafu Kasongo.”

Soma https://jamii.app/RutoNames

#KenyanPolitics #JamiiForums
Mwanachama ndani ya Jukwaa la Mahusiano, Mapenzi na Urafiki ndani ya JamiiForums.com ameomba ushauri wa nini cha kufanya kwani ana tatizo la kumchukia Mtu anayefanana na adui yake kwa sura

Unamshauri nini Mdau?

Mjadala zaidi https://jamii.app/AkifananaNaAduiYangu

#JamiiForums #LifeStyle #LifeTips
Ripoti ya Freedom House na Article 19 imeonesha wasiwasi miongoni mwa Wananchi wa Thailand juu ya juhudi za Serikali kudhibiti Vyombo vya Habari na kuzuia mtandao kupitia Sera ya "Single Gateway"

Sera hii ilipingwa vikali na Asasi za Kiraia na Wadau wa Teknolojia, kutokana na kutoa ruhusa ya kukandamiza Uhuru wa Kujielezea, matumizi ya mtandao n.k, ambapo jitihada zao zilizaa matunda kwa kufanikiwa kuzuia Sera hiyo kupitishwa

Soma https://jamii.app/DigitalThreatsIndoPacific

#DigitalThreats #DigitalSecurity #DataPrivacy #DataProtection #IndoPacificRegion #DigitalThreats
Ingawa AI inaweza kuharakisha usambazaji wa taarifa na mawazo, jambo linalochochea kwa kiasi kikubwa Uhuru wa Kujieleza - pia inaleta hatari mpya ikiwemo Ukatili wa Kijinsia, Hotuba za Chuki, Upotoshaji wa taarifa, Unyanyasaji Mtandaoni (#Cyberbullying)

Global Digital Compact, ambayo ni nyaraka shirikishi ya Nchi Wanachama wa Umoja wa Mataifa ya Septemba 2024, inasisitiza kukuza Uadilifu, Uvumilivu na Heshima katika anga za Kidijitali.

#WorldPressFreedomDay #WPFD2025 #PressFreedom #MediaAndAI #AIForMedia
ANGOLA: Msafara wa Viongozi wa #ACTWazalendo ukiongozwa na Kiongozi wa Chama, Dorothy Semu na Mwenyekiti, Othman Masoud Othman (Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar) umezuiwa kuingia nchini Angola na mamlaka za Serikali ya Angola na Hati zao za Kusafiria kushikiliwa

Pia, Mwenyekiti wa #CHADEMA, #TunduLissu amekiri kuwa naye ni mmoja kati ya Wanasiasa waliozuiliwa kuingia Angola pamoja na baadhi ya Wadau wengine kutoka Kenya, Sudan, Afrika Kusini, Namibia, Eswatini, Lesotho, Ujerumani, Marekani, Uganda, DRC na Msumbiji

ACT imesema Viongozi hao waliowasili kushiriki mazungumzo ya Jukwaa la Demokrasia Afrika [The Platform for African Democrats (PAD)] la Machi 13-16, 2025, yaliyoandaliwa na Taasisi ya The Brenthurst Foundation, wanashikiliwa katika Uwanja wa Ndege wa Luanda, huku Serikali ya Angola ikiwa haijaeleza sababu na kutoa amri warejeshwe Tanzania

Soma https://jamii.app/LissuACTAngola

#JamiiForums #Diplomacy #JFMatukio #AfricanPolitics
JamiiCheck.com ni Jukwaa maalum linalokuwezesha wewe Mwananchi kushiriki Mchakato wa kuthibitisha Uhalisia wa Taarifa zinazopatikana ndani na nje ya Mtandao. Kupitia Jukwaa hili, Utaweza kuwasilisha Taarifa unayohitaji ithibitishwe pamoja na kupata ripoti rasmi za Taarifa zilizothibitishwa

Pia, Jukwaa hili hutoa Maarifa na Nyenzo sahihi za Kutambua, Kuchambua na Kuthibitisha Uhalisia wa Taarifa mbalimbali unazokutana nazo kila siku.

Tembelea sasa Jukwaa hili uwe sehemu ya Watu wanaochukua hatua kuhakikisha Taarifa zinazopatikana Mtandaoni zinakuwa Sahihi wakati wote

#JamiiCheck #Misinformation #Misinformation #FactsMatter #MisDis05