This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DODOMA: Serikali imesema Huduma za Afya ya Akili zimeshajumuishwa kwenye vifurushi vya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), hivyo Wananchi wanaonufaika na bima wanaweza kupata matibabu hayo kwa mujibu wa mwongozo wa matibabu uliopo
Naibu Waziri wa Afya, Dkt. Godwin Mollel amesema ushauri nasaha pamoja na huduma za kibingwa kama vile utengamao, zote zimetajwa kama huduma muhimu kwenye Mwongozo wa Matibabu (Standard Treatment Guideline – STG) na zinagharamiwa na NHIF
Ikumbukwe Machi 12, 2025, Mdau wa JamiiForums.com aliandika “Huduma ya Saikolojia ipatikane kwenye Bima ya NHIF, kuna watu wengi wana changamoto ya Afya ya Akili”
Soma https://jamii.app/AfyaYaAkiliNHIF
#JamiiForums #Accountability #MentalHealthAwareness #AfyaAkili #JFAfyaAkili
Naibu Waziri wa Afya, Dkt. Godwin Mollel amesema ushauri nasaha pamoja na huduma za kibingwa kama vile utengamao, zote zimetajwa kama huduma muhimu kwenye Mwongozo wa Matibabu (Standard Treatment Guideline – STG) na zinagharamiwa na NHIF
Ikumbukwe Machi 12, 2025, Mdau wa JamiiForums.com aliandika “Huduma ya Saikolojia ipatikane kwenye Bima ya NHIF, kuna watu wengi wana changamoto ya Afya ya Akili”
Soma https://jamii.app/AfyaYaAkiliNHIF
#JamiiForums #Accountability #MentalHealthAwareness #AfyaAkili #JFAfyaAkili
Ukaguzi wa Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwenye Miradi ya Umeme Vijijini kwa Mwaka 2023/24, ulibaini REA ilishindwa kufanya utafiti wa mahitaji ya Umeme kama inavyotakiwa na badala yake ilitegemea takwimu zilizopitwa na wakati, hali iliyosababisha makadirio yasiyo sahihi ya mahitaji ya umeme.
Pia, kulikuwa na ongezeko la Tsh. Bilioni 15.34 kutokana na maandalizi hafifu ya mchanganuo wa bei za vipande vya 1 hadi 6
Vilevile, Transfoma zenye uwezo mdogo kuliko zilizoainishwa kwenye upembuzi yakinifu zilinunuliwa na kufungwa bila kufanya tathmini ya mahitaji ya Umeme, hali inayoweza kusababisha upungufu wa Miundombinu na matatizo ya kukatika kwa Umeme.
Soma zaidi https://jamii.app/CAGTransfomaREA
#JamiiForums #JamiiAfrica #Accountability #Uwajibikaji #CAGReport2025 #RipotiCAG2025 #ServiceDelivery #HudumaZaKijamii
Pia, kulikuwa na ongezeko la Tsh. Bilioni 15.34 kutokana na maandalizi hafifu ya mchanganuo wa bei za vipande vya 1 hadi 6
Vilevile, Transfoma zenye uwezo mdogo kuliko zilizoainishwa kwenye upembuzi yakinifu zilinunuliwa na kufungwa bila kufanya tathmini ya mahitaji ya Umeme, hali inayoweza kusababisha upungufu wa Miundombinu na matatizo ya kukatika kwa Umeme.
Soma zaidi https://jamii.app/CAGTransfomaREA
#JamiiForums #JamiiAfrica #Accountability #Uwajibikaji #CAGReport2025 #RipotiCAG2025 #ServiceDelivery #HudumaZaKijamii
Kama vile Michezo (Games) inavyokuwa na changamoto ambazo Wachezaji lazima wazishinde ili kuendelea, vivyo hivyo Maisha hutuletea Vizuizi, Matatizo na Shida ambazo tunahitaji kuzishinda
Uzoefu wa Maisha hutufundisha mambo muhimu, na kutusaidia kukua, kujiimarisha na kuendelea kupevuka.
#JamiiForums #JamiiAfrica
Uzoefu wa Maisha hutufundisha mambo muhimu, na kutusaidia kukua, kujiimarisha na kuendelea kupevuka.
#JamiiForums #JamiiAfrica
#UREMBO: Mdau wa JamiiForums.com anasema Mwanamke anapokuwa na Uraibu wa Urembo bandia kwake anaona ni dalili za changamoto ya Afya ya Akili kwasababu Mwanamke anapokuwa na Msongo wa Mawazo wa kutokubalika huanza kuuchukia mwonekano wake wa Asili
Unakubaliana na Mtazamo huu?
Mjadala zaidi https://jamii.app/UremboBandia
#JamiiForums #JamiiAfrica #Maisha #JFChitChats #JFStories
Unakubaliana na Mtazamo huu?
Mjadala zaidi https://jamii.app/UremboBandia
#JamiiForums #JamiiAfrica #Maisha #JFChitChats #JFStories
MWANZA: Mdau wa JamiiForums.com ambaye ni mkazi wa Ilemela anadai madhara ya Wachimbaji Moramu kuacha mashimo makubwa ni Watu au mifugo kudondokea kwenye makorongo, mashimo kujaa maji na kuwa chanzo cha mbu na madhara mengine mengi
Anatoa wito kwa Mamlaka zinazohusika kusimamia wanaochimba Moramu wawe na mikakati ya kupunguza madhara, anayemaliza kuchimba lazima afukie
Aidha, ameshauri Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Mwanza wafike katika eneo hilo wajionee hali ilivyo tete
Soma https://jamii.app/MoramuIlemela
#Uwajibikaji #Accountability #Governance #PublicHealth
Anatoa wito kwa Mamlaka zinazohusika kusimamia wanaochimba Moramu wawe na mikakati ya kupunguza madhara, anayemaliza kuchimba lazima afukie
Aidha, ameshauri Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Mwanza wafike katika eneo hilo wajionee hali ilivyo tete
Soma https://jamii.app/MoramuIlemela
#Uwajibikaji #Accountability #Governance #PublicHealth
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
DODOMA: Kasalali Mageni, Mbunge wa Sumve (CCM) amesema Jimbo lake lina Barabara hewa za lami, akidai ni kutokana na kusainiwa kwa mikataba ya ujenzi ambayo haina utekelezaji kwa miaka mingi na kuwa hali hiyo inasababisha wabaki wakipigwa vumbi na Viongozi wa Kitaifa kutofika kutokana na ubovu wa barabara zilizopo
Amesema hayo Mei 6, 2025, Bungeni wakati akichangia Bajeti ya Wizara ya Ujenzi iliyowasilishwa na Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega aliyeomba Bunge limpitishie Tsh. Trilioni 2.28 kwaajili ya miradi ya maendeleo na matumizi mengine
Baadaye Waziri Ulega alisema "Mtani wangu usiwe na wasiwasi, nimekusikia na jambo lipo katika vitabu. Nataka nikuhakikishe nina safari ya Mwanza, nitakwenda hadi Sumve na ninajua sasa hivi watani mnapenda sana maendeleo na mimi nataka usikasirike na hutaharibikiwa kwa sababu ya barabara."
Soma https://jamii.app/JimboLaSumve
#JamiiForums #Accountability
Amesema hayo Mei 6, 2025, Bungeni wakati akichangia Bajeti ya Wizara ya Ujenzi iliyowasilishwa na Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega aliyeomba Bunge limpitishie Tsh. Trilioni 2.28 kwaajili ya miradi ya maendeleo na matumizi mengine
Baadaye Waziri Ulega alisema "Mtani wangu usiwe na wasiwasi, nimekusikia na jambo lipo katika vitabu. Nataka nikuhakikishe nina safari ya Mwanza, nitakwenda hadi Sumve na ninajua sasa hivi watani mnapenda sana maendeleo na mimi nataka usikasirike na hutaharibikiwa kwa sababu ya barabara."
Soma https://jamii.app/JimboLaSumve
#JamiiForums #Accountability
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
Bunge la Ulaya (EU) limejadili kuhusu mashtaka yanayomkabili Mwenyekiti wa #CHADEMA, #TunduLissu na kutoa azimio kuwa aachiwe huru bila masharti
Wakichangia hoja hiyo, jana Mei 7, 2025, Wabunge mbalimbali wametoa wito wakieleza haki itendeke katika shauri hilo na kulinda uhuru wa Kisiasa, usalama wa Waandishi wa Habari, Watetezi wa Haki za Binadamu ili kuendeleza ushirikiano uliopo baina ya Bunge hilo na Tanzania
Pia, wamegusia kuruhusiwa kwa Vyama vya Upinzani kushiriki katika Uchaguzi Mkuu wa 2025 kwa Uhuru na Haki
Soma https://jamii.app/BungeUlayaLissu
#JamiiForums #Governance #Democracy
Wakichangia hoja hiyo, jana Mei 7, 2025, Wabunge mbalimbali wametoa wito wakieleza haki itendeke katika shauri hilo na kulinda uhuru wa Kisiasa, usalama wa Waandishi wa Habari, Watetezi wa Haki za Binadamu ili kuendeleza ushirikiano uliopo baina ya Bunge hilo na Tanzania
Pia, wamegusia kuruhusiwa kwa Vyama vya Upinzani kushiriki katika Uchaguzi Mkuu wa 2025 kwa Uhuru na Haki
Soma https://jamii.app/BungeUlayaLissu
#JamiiForums #Governance #Democracy
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
KIGOMA: Baada ya Mdau wa JamiiForums.com kueleza kuwa Aprili 29, 2025 kulitokea taharuki wakati Jeshi la Polisi lilipotumia mabomu ya machozi katika Kambi ya Wakimbizi ya Nyarugusu, ufafanuzi umetolewa wa kilichotokea
Awali, Mdau alidai baadhi ya Wakimbizi wamekuwa wakiuza pombe haramu na hata walipoonywa na Viongozi hawakujali na walishiriki kuanzisha vurugu Askari walipofika kukagua
Kamanda wa Polisi Mkoa, SACP Filemon Makungu amezungumza na JamiiForums na kusema wamewakamata na kuwafikisha Mahakamani Wakimbizi 25 kwa kufanya vurugu na kuzuia maafisa wa Idara ya Wakimbizi kukagua vijiwe vya kuuza bidhaa zilizopigwa marufuku kambini
Soma https://jamii.app/WakimbiziKigoma
#JamiiForums #Accountability
Awali, Mdau alidai baadhi ya Wakimbizi wamekuwa wakiuza pombe haramu na hata walipoonywa na Viongozi hawakujali na walishiriki kuanzisha vurugu Askari walipofika kukagua
Kamanda wa Polisi Mkoa, SACP Filemon Makungu amezungumza na JamiiForums na kusema wamewakamata na kuwafikisha Mahakamani Wakimbizi 25 kwa kufanya vurugu na kuzuia maafisa wa Idara ya Wakimbizi kukagua vijiwe vya kuuza bidhaa zilizopigwa marufuku kambini
Soma https://jamii.app/WakimbiziKigoma
#JamiiForums #Accountability
PWANI: Mdau wa JamiiForums.com anadai Wakazi wa Kitongoji cha Miale, Kata ya Mkuranga wakipata dharura gari ndogo au Bajaji haviwezi kupita katika barabara ya Mtaani hapo kutokana na ubovu
Anadai mara kadhaa wamewasilisha malalamiko yao na maombi yao ya kuboreshewa Barabara kwa TARURA, lakini wamekuwa hawapati mwitikio wa kuridhisha, hata wale wanaochota mchanga nao hawashughuliki na maboresho, badala yake wanazidi kuharibu
Anaeleza kuwa eneo hilo linahitaji kifusi cha mawe ili likae sawa, tofauti na hapo Wakazi wa huko watakosa sehemu ya kupita
Soma https://jamii.app/MialeMkuranga
#JamiiForums #Accountability #Governance #ServiceDelivery
Anadai mara kadhaa wamewasilisha malalamiko yao na maombi yao ya kuboreshewa Barabara kwa TARURA, lakini wamekuwa hawapati mwitikio wa kuridhisha, hata wale wanaochota mchanga nao hawashughuliki na maboresho, badala yake wanazidi kuharibu
Anaeleza kuwa eneo hilo linahitaji kifusi cha mawe ili likae sawa, tofauti na hapo Wakazi wa huko watakosa sehemu ya kupita
Soma https://jamii.app/MialeMkuranga
#JamiiForums #Accountability #Governance #ServiceDelivery
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DODOMA: Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha ya Wizara ya Maji kwa Mwaka 2025/2026, Waziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema Wizara hiyo imefikisha Huduma ya Maji Vijijini kwa zaidi ya Asilimia 83 ya malengo yake ya kufikisha Asilimia 85 kufikia Desemba 2025, amesema hayo Bungeni leo Mei 8, 2025
Soma https://jamii.app/AwesoMajiVijijini
#JamiiForums #ServiceDelivery #Accountability
Soma https://jamii.app/AwesoMajiVijijini
#JamiiForums #ServiceDelivery #Accountability
Mdau wa JamiiForums.com ameanzisha Mjadala kuhusu Matumizi ya Akili Mnemba (AI) kwa kuzingatia Maadili (Ethical use of AI) akilalamikia suala la baadhi ya Watu kuitumia AI kudhalilisha wengine, badala ya kujinufaisha kwa kuongeza Maarifa na kipato
Ametoa mfano wa kauli iliyotolewa na mmoja wa Watumiaji wa Mtandao wa X ya kukemea matumizi mabaya ya AI kufuatia matukio ya hivi karibuni
Wewe unaitumia #AI kufanyia nini?
Mjadala https://jamii.app/MatumiziAI
#JamiiForums #JamiiAfrica #AIBenefits #Technology #Cyberbullying
Ametoa mfano wa kauli iliyotolewa na mmoja wa Watumiaji wa Mtandao wa X ya kukemea matumizi mabaya ya AI kufuatia matukio ya hivi karibuni
Wewe unaitumia #AI kufanyia nini?
Mjadala https://jamii.app/MatumiziAI
#JamiiForums #JamiiAfrica #AIBenefits #Technology #Cyberbullying
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
DODOMA: Mbunge wa Biharamulo, Eng. Ezra Chiwelesa amepinga baadhi ya maazimio yaliyotolewa na Bunge la Ulaya, lililojadili kuhusu mashauri ya Mwenyekiti wa #CHADEMA, Tundu Lissu ambapo ametoa wito kwa Serikali kukataa maelekezo ya Bunge hilo
Soma https://jamii.app/ChiwelesaBungeni
#JamiiForums #Governance #Diplomacy
Soma https://jamii.app/ChiwelesaBungeni
#JamiiForums #Governance #Diplomacy
DAR: Timu ya #Simba imeendeleza mbio za Ubingwa wa Ligi Kuu Bara kwa kasi, hiyo ni baada ya kuichapa #PambaJiji Magoli 5-1 kwenye Uwanja wa KMC Complex
Kiungo mshambuliaji Jean Ahoua amefunga magoli matatu (hat trick dakika ya 15, 36 na 48) huku mawili yakifungwa na Leonel Ateba (80 na 84), goli la Pamba Jiji limewekwa wavuni na Mathew Tegisi dakika ya 85
Ushindi huo unaifanya Simba ifikishe alama 66 katika michezo 25 ikiwa nyuma ya #Yanga yenye pointi 70 katika michezo 26 wakati Pamba Jiji ipo nafasi ya 13 kwa kuwa na pointi 27 katika mechi 27
Soma https://jamii.app/SimbaPamba
#JamiiForums #JFLigiKuu25 #JFSports
Kiungo mshambuliaji Jean Ahoua amefunga magoli matatu (hat trick dakika ya 15, 36 na 48) huku mawili yakifungwa na Leonel Ateba (80 na 84), goli la Pamba Jiji limewekwa wavuni na Mathew Tegisi dakika ya 85
Ushindi huo unaifanya Simba ifikishe alama 66 katika michezo 25 ikiwa nyuma ya #Yanga yenye pointi 70 katika michezo 26 wakati Pamba Jiji ipo nafasi ya 13 kwa kuwa na pointi 27 katika mechi 27
Soma https://jamii.app/SimbaPamba
#JamiiForums #JFLigiKuu25 #JFSports
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
VATICAN: Robert Francis Prevost (69), raia wa Marekani ametangazwa kuwa Papa Mpya wa 267 wa Kanisa Katoliki, leo Mei 8, 2025 akichukua nafasi hiyo baada ya kifo cha Papa Francis (88) aliyefariki Aprili 21, 2025
Mara baada ya Papa kutambulishwa imeelezwa atakuwa anatambulika kwa jina la Pope Leo XIV
Idadi ya Wapigakura ilikuwa ni Makardinali 133 walio chini ya umri wa Miaka 80 na Mshindi alihitajika kupata angalau Kura 89, sawa na theluthi mbili ya kura zote
Soma https://jamii.app/PapaMpya
#JamiiForums
Mara baada ya Papa kutambulishwa imeelezwa atakuwa anatambulika kwa jina la Pope Leo XIV
Idadi ya Wapigakura ilikuwa ni Makardinali 133 walio chini ya umri wa Miaka 80 na Mshindi alihitajika kupata angalau Kura 89, sawa na theluthi mbili ya kura zote
Soma https://jamii.app/PapaMpya
#JamiiForums