JamiiForums
57.9K subscribers
31.4K photos
1.62K videos
29.1K links
Official JamiiForums Telegram Channel | Be Informed, Engaged & Entertained
Download Telegram
MAREKANI: Kampuni ya #META imeanza kutekeleza mpango wake kwa kuwapunguza kazi Wafanyakazi 4,000 katika sehemu mbalimbali Duniani wanaoshindwa kufanya vizuri na kujiandaa kwa ajili ya uwekezaji mkubwa kwenye matumizi ya Akili Mnemba (AI)

Januari 2025, Kampuni ya Meta ilitangaza mpango wa kupunguza takriban 5% ya Wafanyakazi kwa kuzingatia utendaji wao kazini

Aidha, kampuni hiyo imewapa Wafanyakazi walioathiriwa na punguzo hilo nchini Marekani malipo ya kuachishwa kazi ya mishahara ya Wiki 16 na nyongeza ya wiki mbili kwa kila Mwaka wa utumishi

Soma https://jamii.app/MetaJobLayoff

#JamiiForums #Governance #SocialJustice
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
#SIASA: Makamu wa Rais wa Tanzania, Dkt. Philip Mpango amesema ameamua kukaa kando kwa hiari na kuwaachia wengine nafasi ya kumsaidia Rais Samia Suluhu Hassan baada ya kutumika vya kutosha katika nafasi mbalimbali Serikalini

Ameyasema hayo leo, Februari 11, 2025 alipofungua Kikao Kazi cha Tano cha Mamlaka ya Serikali Mtandao Jijini Arusha

Kauli ya Dkt. Mpango inakuja baada ya yeye (Dkt. Mpango) kuomba kupumzika kutumikia kama Makama wa Rais na Chama cha Mapinduzi (#CCM) kumpitisha Dkt. Emmanuel Nchimbi kuwa Mgombea Mwenza katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba 2025

Soma https://jamii.app/MpangoKukaaKando

#JamiiForums #Governance #UchaguziMkuu25
Leo wanakupa pesa ili uwachague lakini kesho wakishapata madaraka wanakusahau na maisha yako hayawezi kubadilika kwa pesa ya siku moja

Usidanganyike na ahadi za muda mfupi, chagua kiongozi mwenye maono, uadilifu na anayejali maslahi ya Wananchi. Fanya maamuzi sahihi

#ChaguaKiongoziSioPesa #KemeaRushwa25 #Accountability #Demokrasia #ServiceDelivery #Uwajibikaji
DAR: Baada ya Mdau wa JamiiForums.com aliyejitambulisha kuwa Mhitimu wa Chuo cha IFM kudai yeye na wenzake waliohitimu ngazi ya Shahada hawajapewa Vyeti vilivyotakiwa kutoka Desemba 2024, Rais wa Wanafunzi wa IFM, Fabian Mkondo amesema malalamiko hayo yamefikishwa kwa Uongozi wa Chuo na yanafanyiwa kazi

Akizungumza na JamiiForums, Mkondo amesema “Chuo kipo kwenye kipindi cha Mitihani, ndio maana ‘focus’ ipo huko sana lakini naamini Chuo kitashughulikia na suala hilo litamalizika.”

Aidha, jitihada za JamiiForums kuupata Uongozi wa Chuo cha IFM bado zinaendelea.

Soma https://jamii.app/LateVyetiIFM

#JamiiForums #Uwajibikaji #Accountability #JFMdau2025
Usikose kuungana nasi Februari 13, 2025, kuanzia Saa 12:00 Jioni hadi Saa 2:00 Usiku, kwa mjadala wa kina kuhusu zawadi wanazotoa Wanasiasa wakati wa Uchaguzi. Je ni rushwa? Wananchi wanatofautishaje?

Katika Mjadala huu pia tutajadili namna vitendo vya rushwa vinavyoweza kuathiri maamuzi ya wapiga kura na mustakabali wa uongozi bora

Washiriki watapata fursa ya kushiriki kwa kutoa maoni, mapendekezo au kuuliza maswali

Kushiriki, bofya hapa: https://twitter.com/i/spaces/1ZkKzYMNvbDxv

#ChaguaKiongoziSioPesa #Accountability #Demokrasia #ServiceDelivery #Uwajibikaji
Haki za Mtuhumiwa wakati wa Kuhojiwa (Rights During Interrogation) zinamlinda Mshukiwa dhidi ya vitendo vya Udhalilishaji na Ukatili wakati wa uchunguzi. Haki hizi zinahakikisha Uchunguzi unafanyika kwa Haki na kwa kuheshimu Utu wa Mtuhumiwa

Haki Muhimu zinajumuisha Mtuhumiwa kutolazimishwa kujitoa hatiani au kutoa ushahidi unaoweza kumletea madhara. Pia, ana Haki ya kutotoa maelezo yoyote yanayoweza kutumiwa dhidi yake Mahakamani

Pia, ana Haki ya kuhakikisha Wakili wake anakuwepo wakati wa mahojiano ili kuepuka Unyanyasaji au matumizi mabaya ya Sheria na kuhakikisha ushahidi unapatikana kwa njia halali na ya Haki.

Soma zaidi https://jamii.app/RightToFairTrial

#JamiiForums #HakiZaKiraia #CivilRights #HumanRights #KesiYaHaki #HakiZaBinadamu #UtawalaWaSheria
Mwanachama wa JamiiForums.com amelalamikia changamoto ya Mtandao kwenye kutuma maombi ya nafasi za Ajira zilizotolewa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (#TRA) na kutoa wito kwa Mamlaka hiyo kutatua tatizo hilo ili waombaji wapate Huduma kwa urahisi

Soma https://jamii.app/AjiraMtandaoTRA

#JamiiForums #TEHAMA #ICT #SerikaliMtandao #DigitalSpace #DigitalRights #JFMdau2025
Hajat Fatma Mwassa ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Kagera aliyasema hayo Februari 11, 2025 wakati wa Kikao cha Wadau wa Elimu, Kata ya Bakoba ambapo amewasisitiza Vijana kutokuwa na tabia ya Uchawa kwa kuwa kufanya hivyo ni kuonesha Ufukara wa Akili

Soma https://jamii.app/MwassaNukuu

#JamiiForums #Governance #JFNukuu #JFQuotes
SINGIDA: Siku moja baada ya Mwanachama wa JamiiForums.com kueleza kukerwa na tabia ya kuchelewesha uzoaji taka Mitaani, taka zimeanza kuchukuliwa katika Makazi ya Watu leo, Februari 12, 2025

Mdau alidai Wananchi wanatoa taka nje Siku ya kubeba ila Wahusika hawaji kuchukua na kuwa hiyo ilikuwa ni Wiki ya tatu hawajafika huku taka zikizagaa kwenye Mitaa

Soma https://jamii.app/TakaZabebwaSingida

#JamiiForums #Accountability #Uwajibikaji #HudumaZaKijamii #JFMdau2025
Katika Mjadala huu, TAKUKURU itafafanua maana ya rushwa katika uchaguzi na vitendo vinavyoweza kuchukuliwa kama rushwa, huku Washiriki wakipata fursa ya kushiriki kwa kutoa maoni, mapendekezo au kuuliza maswali

Jiunge nasi Februari 13, 2025, kuanzia Saa 12:00 Jioni hadi Saa 2:00 usiku, kupitia #XSpaces ya JamiiForums

Kushiriki, bofya https://twitter.com/i/spaces/1ZkKzYMNvbDxv

#ChaguaKiongoziSioPesa #Accountability #Demokrasia #ServiceDelivery #Uwajibikaji
AFYA: Mkurugenzi wa Kinga wa Wizara ya Afya, Dkt. Ntuli Kapologwe ameshinda nafasi ya Mkurugenzi Mkuu wa Jumuiya ya Afya ya Nchi za Afrika Mashariki, Kati na Kusini (ECSA – HC) na kuwashinda Wagombea wengine sita waliokuwa wakiwania nafasi hiyo

Dkt Ntuli atachukua nafasi ya Prof. Yoswa Dambisya kutoka #Uganda aliyeshikilia nafasi hiyo kwa miaka 10

Hii ni mara ya pili kwa Tanzania kushika nafasi hiyo katika kipindi cha miaka 51 cha Jumuiya hiyo, kwa mara ya kwanza, Mtanzania Dkt. Winny Mpanju alihudumu kama Mkurugenzi Mkuu kati ya mwaka 1983 na 2000.

Soma https://jamii.app/DktNtuliECSAHC

#JamiiForums #Governance #Accountability
Mjadala unaoendelea Jukwaa la Siasa ndani ya JamiiForums.com, mwanachama anasema ahadi za kutatua changamoto ya Ajira kwa Vijana inatumika Kisiasa tu ila hakuna Mwanasiasa anayejua hasa nini atafanya ili kutatua hili

Unakubaliana naye?

Unaweza kushiriki Mjadala huu zaidi kwa kubofya https://jamii.app/TatizoAjiraVijana

#JamiiForums #EmploymentCrisis #Politics