JamiiForums
52.8K subscribers
34.4K photos
2.44K videos
31.3K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
TCU YAFUTA BAADHI YA VYUO NA KUZUIA UDAHILI

- Miongoni mwa vilivyofutwa ni Chuo Kikuu cha Teofile Kisanji-Dar na Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Tiba na Teknolojia (IMTU)

- Kilichozuiliwa kudahili ni Chuo Kikuu cha Kumbukumbu ya Sebastian Kolowa

Zaidi, soma https://jamii.app/TCUVyuoUdahili-2020
HISTORIA: MVUA YA MAWE KUBWA KUWAHI KUTOKEA DUNIANI

> Ilitokea Nchini India katika Jimbo la Uttar Pradesh mnamo Aprili 30, 1888 na kuua Watu 246

> Ilikuwa na vimbunga na radi zenye nguvu, mawe ya mvua hiyo yalikuwa na ukubwa wa Yai la Bata Mzinga au Mpira wa 'Cricket'

Zaidi, tembelea https://jamii.app/MvuaMawe
UTEUZI: Rais Magufuli ameteua Wenyeviti wanne wa Bodi mbalimbali akiwemo Dkt. Masatu Masinde Leonard Chiguna anayekuwa Mwenyekiti wa Bodi ya TAA

- Pia, amemteua Katibu Mtendaji wa Baraza la Biashara la Taifa (TNBC) na Mkuu wa Chuo cha Maji

Zaidi, soma https://jamii.app/UteuziWenyevitiJan2020
ULINZI WA KIDIGITALI: JIFUNZE BAADHI YA 'APPLICATION' KWA USALAMA WAKO

> Cerberus itasaidia simu yako ikiibwa, X-Privacy kuzuia taarifa kuvuja, Cryptonite kutengeneza 'File' lenye ulinzi ndani ya simu

Kwa elimu na application nyingi zaidi fungua > https://jamii.app/UsalamaSimu
RUKWA: MLINZI AMCHINJA BOSI WAKE BAADA YA KUSHINDWA KUMLIPA MSHAHARA

> Polisi inamshikilia Mlinzi huyo aliyekuwa akidai Tsh. 360,000

> Marehemu alikatwa na kitu chenye ncha kali. Shingo, miguu na kiwiliwili chake vilitenganishwa

Zaidi, soma - https://jamii.app/MauajiMshaharaRukwa
UINGEREZA: DAWA YA SARATANI YAGUNDULIWA

> Wanasayansi wa Chuo Kikuu cha Cardiff wamegundua namna ya kutibu Saratani za aina zote

> Matokeo hayajajaribiwa kwa Wagonjwa lakini Wanasayansi hao wanasema yana uwezekano mkubwa wa kufanikiwa

Zaidi, soma https://jamii.app/DawaSaratani
MBU NDIO KIUMBE TISHIO ZAIDI DUNIANI

> Inakadiriwa watu 725,000 hadi 1,000,000 hufa kila mwaka kutokana na magonjwa yanayosababishwa na mbu

> Mbu aina ya Anofelesi husababisha vifo zaidi kwa kusambaza 'Plasmodiam' ambao husababisha Malaria

Zaidi, soma https://jamii.app/TishioMbu
ULINZI WA KIDIGITALI: Umewahi kukutana na neno 'Encryption'? Je, wajua maana na kazi yake?

> Encryption ni mchakato wa kufunga ujumbe au taarifa ili zisiweze kuinguliwa na Mtu asiyeruhusiwa, asiyehusika au asiyetakiwa. Ni moja kati ya hatua muhimu katika UlinziWaKidigitali

> Katika mchakato huu, taarifa au ujumbe hubadilishwa mantiki na muonekano ili kuzuia asiyehusika kuweza kuupata na kuuelewa

> Mfano: Katika simu au kompyuta ambayo imewezeshwa kufanya 'Encryption' ukituma ujumbe ulioandika (Habari ya Asubuhi) basi wakati wa kusafirishwa kwenda kwa mlengwa/walengwa utafungwa na kuwa (mfano: ₩¥Gskgzk:,÷..._52828) lakini ukimfikia mlengwa utasomeka (Habari ya Asubuhi)

> Kuna baadhi ya Programu Tumishi (Application) hutaka wahusika kubadilishana funguo kwanza kabla ya kuanza kuwasiliana kwa jumbe na taarifa zenye 'Encryption'
KIGWANGALLA: WALISHINDWA KUNIUA WAKATI ULE. NAINGIA VITANI KWA SILAHA ZOTE

- Adai kuna Watu wanalipwa, wanaandika kwenye gazeti vitu vya kipuuzi ili kumchafua

- Asema, vita na ushindi ni asili yake bila kujali nani atadhurika kwenye vita hiyo

Zaidi, soma https://jamii.app/KigwangallaVitani
DAR: WANAFUNZI 19,000 WALIOJIUNGA KIDATO CHA KWANZA, WAKOSA MADARASA

> Kuna upungufu wa Madarasa 381, Wilaya ya Temeke pekee ikiwa na Upungufu wa Madarasa 120

> Wilaya ya Temeke ina wanafunzi 5970 waliokosa nafasi za Kidato cha Kwanza

Zaidi, soma https://jamii.app/DarMadarasa
WATU MILIONI 470 HAWANA KAZI NZURI ULIMWENGUNI

> Asilimia 60 ya Nguvu Kazi Ulimwenguni kote ni wale wanaofanya kazi zisizo rasmi, ambapo malipo ni kidogo na bila marupurupu

> Vijana milioni 267 hawako kwenye ajira, elimu au mafunzo ya kazi

Zaidi, soma https://jamii.app/KaziUlimwenguni
TANZANIA MIONGONI MWA NCHI 7 ZINAZOWEZA KUWEKEWA VIKWAZO NA MAREKANI

- Belarus, Eritrea, Kyrgyzstan, Myanmar, Nigeria, Sudan na Tanzania huenda zikaongezwa katika orodha ya nchi ambazo Raia wake wamewekewa vikwazo kuingia Marekani

Zaidi, soma https://jamii.app/Tanzania-USATravelBan
Rushwa ya aina yoyote ina athari nyingi zikiwemo Kuumiza Wananchi, Kudhoofisha uwezo wa Serikali wa kutoa Huduma za Msingi, Kukosekana kwa Usawa na Haki na Kukatisha Watu tamaa

- Kwa mujibu wa Kifungu cha 25 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Na. 11/ 2007, adhabu ya mtu atakayebainika kuomba Rushwa ya Ngono ni faini isiyozidi Tsh. Milioni 5 au kifungo kisichozidi miaka mitatu au vyote kwa pamoja

#KemeaRushwa
TMA YATOA TAHADHARI YA MVUA KUBWA KWA MIKOA MINNE

> Mikoa hiyo ni Lindi, Mtwara, Ruvuma na Morogoro

> TMA pia imetoa tahadhari ya upepo mkali na mawimbi katika mikoa ya Lindi, Mtwara, Pwani, Dar, Tanga, Unguja na Pemba

Zaidi, soma https://jamii.app/TMAMvuaTahadhari
MACAU: MJI UNAOONGOZA KWA KIPATO KINACHOTOKANA NA KAMARI DUNIANI

> Mwaka 2016, Mji huu ulikadiriwa kuwa na kipato kilichotokana na Kamari cha Dola Bilioni 27.8 (Sawa na Tsh. Trilioni 64.2)

> Macau iliyopo China imeingia katika Kitabu cha Rekodi za Dunia cha Guinness 2019 kutokana na mapato hayo

Zaidi, soma https://jamii.app/KamariDuniani
NIGERIA: MAGAIDI WAUANA WAO KWA WAO

> Boko Haram walivamia kambi ya Dola la Kiislamu la Afrika Magharibi (ISWAP)

> Mapigano kati ya makundi hayo mawili ya Kigaidi Kaskazini Mashariki mwa Nigeria yamesababisha vifo vya wapiganaji wengi

Zaidi, soma https://jamii.app/MagaidiNigeria
ALIYESHTAKIWA KWA UHUJUMU UCHUMI ATEULIWA UENYEKITI WA BODI VETA. MASHTAKA YAKE YALIFUTWA

> Ni Peter Maduki, ambaye alishtakiwa kwa makosa 280 likiwamo la Utakatishaji Fedha

> Kesi iliondolewa Mahakamani siku moja baada ya kufunguliwa

Zaidi, soma https://jamii.app/UhujumuUteuzi
MAAMUZI YA KAMATI YA USIMAMIZI WA LIGI KUU TANZANIA

- Kocha wa Yanga, Luc Eymael ameonywa kwa kutoa matamshi na kufanya vitendo visivyofaa

- Yanga imetozwa Tsh. 500,000 kwa Mashabiki wake kurusha chupa za maji uwanjani na kuwarushia Waamuzi

Zaidi, soma https://jamii.app/MaamuziKamatiLigi
TUNDU LISSU: WADHAMINI HAWAWEZI KUNIRUDISHA TANZANIA, NITARUDI NIKIHAKIKISHIWA USALAMA WANGU

> Lissu aomba Mahakama kuwatendea haki wadhamini wake, Robert Katula na Ibrahimu Ahmed

> Amesema, uhai ni mkubwa kuliko kesi

Zaidi, soma https://jamii.app/LissuMahakamaWadhamini
MTWARA: WAZAZI WALIOGOMA KUPELEKA WATOTO SHULE KUSAKWA

> Wanafunzi 20,400 walitakiwa kujiunga Kidato cha Kwanza lakini 75% hawajaripoti Shule

> Mkuu wa Mkoa amesema, Wazazi waliogoma kupeleka watoto shuleni watachukuliwa hatua za kisheria

Zaidi, soma - https://jamii.app/WazaziElimuMtwara