JamiiForums
52.4K subscribers
34.4K photos
2.47K videos
31.4K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
BAADHI YA MAMBO YA KUYAJUMUISHA KATIKA MALENGO YAKO YA KUMLEA MTOTO

> Tenga muda wa faragha na watoto wako. Iwapo unao watoto zaidi ya mmoja, fanya kila uwezalo kupata muda na kila mmoja ili akueleze mipango aliyonayo na wewe umshauri

> Azimia kutomlinganisha mtoto wako na watoto wa wengine. Watoto huzaliwa na vipaji na karama tofauti hivyo usishawishike kutaka mtoto wako afanane na wa majirani

> Mfundishe mwanao stadi moja mwaka huu. Zipo stadi kadhaa muhimu katika maisha ikiwamo kupika, kufua, kutunza bustani, usimamizi wa fedha na kadhalika

Tembelea - https://jamii.app/MalengoKuleaMtoto
DRC: 6000 WAFARIKI KWA UGONJWA WA SURUA

- Hali hiyo imefanya kuwa, kati ya majanga makubwa ya milipuko mabaya zaidi ya magonjwa yanayoambukiza kutokea Duniani

- Kwa Tanzania hali iko tofauti kwa kuwa watoto hupatiwa chanjo ya surua wakiwa na umri mdogo

Zaidi, soma https://jamii.app/PolioDeathRateDRC
USIANZISHE BIASHARA YA MTAJI MKUBWA KWASABABU TU UNA FEDHA NYINGI

> Mdau katika Jukwaa la Biashara ndani ya JamiiForums.com anasema, kuna Kanuni Tatu za Msingi ambazo anaziamini zinafaa katika uwekezaji

> Anashauri kuwekeza kiasi ambacho uko tayari kupoteza iwapo hasara itatokea, wekeza kwa watu na sio vitu na wekeza katika kile unachokipenda na kukiamini na sio vutio la faida kubwa

> Anasema, kanuni hizi ni muhimu sana kwani unapozifuata kuna uwezekano mkubwa sana wa kufanikiwa katika biashara

Tembelea - https://jamii.app/BiasharaKubwaVsMtajiMkubwa
MURANG'A, KENYA: AWAUA WANAYE BAADA YA KUGOMBANA NA MUMEWE

- Esther Wambui (25), amewaua Watoto wake wawili wa Kike hapo jana huko Kimwiriini katika Kijiji cha Gatanga

- Aliwanywesha sumu watoto hao kabla na yeye kujaribu kujiua kwa simu hiyo

Zaidi, soma https://jamii.app/WomanPoisonsDaughters
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Kumetokea vurugu katika Kikao cha Baraza la Madiwani wa Jiji hilo, kwenye kikao maalum cha kujadili na kuamua hatma ya Meya wa Jiji la Dar, Isaya Mwita

- Chanzo cha vurugu ni kusainiwa kwa mahudhurio na Mjumbe ambaye hayupo ndani ya ukumbi wa mkutano

Zaidi, soma https://jamii.app/VuruguBarazaMadiwaniDar
MAREKANI YAZUIA MALI ZA MAKAMU WA KWANZA WA RAIS WA SUDAN KUSINI

> Wizara ya Fedha imezuia mali za Taban Deng Gai (69) nchini Marekani na imepiga marufuku Raia wake kushirikiana na Taban

> Anatuhumiwa kwa ukiukaji wa Haki za Binadamu na kuhusika na kifo cha Wakili Samuel Dong Luak na Mpinzani Aggrey Idry

Zaidi, soma - https://jamii.app/USBlacklistsTabanDeng
MATOKEO YA KIDATO CHA NNE KWA MWAKA 2019 YATANGAZWA

- Katibu Mkuu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA), Dkt. Charles Msonde, ametangaza matokeo hayo leo

- Pia, matokeo ya Upimaji ya Kidato cha Pili na matokeo ya Maarifa (QT) yatangazwa

Zaidi, soma https://jamii.app/MatokeoKidato42019
MABASI YANAYOSAFIRISHA VIFURUSHI BILA LESENI YA TCRA YAPEWA ONYO

> Naibu Waziri Nditiye ataka mabasi kufuata taratibu zilizowekwa na Mamlaka

> Ametoa wito kwa Shirika la Posta kuboresha huduma zao ili mizigo isafirishwe na Shirika hilo

Zaidi, soma - https://jamii.app/UkaguziBasiVifurushi
MKAKATI WA TAIFA DHIDI YA RUSHWA NA MPANGO WA UTEKELEZAJI(2017-2022)

> Umelenga kuimarisha na kuwezesha umma kushiriki katika kudai Haki & Uwajibikaji wa Serikali

> Mazingira wezeshi yatawekwa kuhakikisha ushiriki kamilifu wa Wananchi ktk Mapambano dhidi ya Rushwa

#KemeaRushwa
POLISI: TANZANIA IPO SALAMA DHIDI YA VITENDO VYA UGAIDI

> Polisi imewataka Raia wa Kigeni na watalii kuendelea na shughuli zao kama kawaida

> Wamesema kuwa ulinzi unaendelea kuimarishwa nchini kote

Zaidi, soma https://jamii.app/PolisiUsalamaTZUgaidi
ALIYESAFIRI KWA NJIA HARAMU MWILI WAKE WAKUTWA KWENYE GURUDUMU LA NDEGE

> Mwili ulipatikana asubuhi ya Jumatano, Januari 8, karibu na Mji wa Paris, ikitokea Abidjan

> Wengi wanaamini kwamba kijana huyo alikufa kutokana na kukosa hewa au baridi

Zaidi, aoma https://jamii.app/MwiliTairiNdege-UFR
IRAN: NDEGE ILIYOUA WATU 176 ILIKUWA IKIUNGUA KABLA YA KUDONDOKA

- Wachunguzi wamedai wafanyakazi hawakufanya mawasiliano ya redio kuomba msaada

- Pia, sanduku zote mbili ambazo zina data na mawasiliano ya kutoka kwenye ndege zimepatikana

Zaidi, soma https://jamii.app/UchunguziNdegeUkraine-IRN
MHAMIAJI AJIKATA KOO BAADA YA KUKATALIWA KUINGIA MAREKANI

> Raia huyo kutoka Mexico amejiua mita kadhaa kutoka Daraja la Kimataifa la Pharr – Reynosa, Texas

> Maafisa wa eneo hilo wamesema, mtu huyo bado hajatambulika hadi sasa

Zaidi, soma https://jamii.app/MhamiajiAjikataKoo-MXC
MAREKANI YASEMA IKO TAYARI KUFANYA MAZUNGUMZO NA IRAN

> Iko tayari kujadiliana bila masharti baada ya uhasama uliozuka baina yao

> Katika barua yake kwa Umoja wa Mataifa ilijitetea kuwa, ilimuua Qasem Soleimani kama hatua ya kujilinda

Zaidi, soma https://jamii.app/MarekaniMazungumzoIran
NETFLIX KUIFUTA FILAMU INAYOONYESHA YESU KAMA SHOGA

- Uamuzi ulifikiwa ktk kujibu ombi la Shirika la Katoliki lililosema filamu hiyo imeumiza heshima yao

- Uamuzi huo wa Mahakama ni halali hadi Mahakama nyingine itoe amri nyingine tofauti na hiyo

Zaidi, soma https://jamii.app/NetflixFilamuYesu
TETESI: YOUNG AKATAA MKATABA. MAN UTD YAJIONDOA KUMUWANIA ERIKSEN

- Nahodha wa Manchester United, Ashley Young anadaiwa kukataa mkataba wa kuendelea kuitumikia timu hiyo huku akihusishwa kuhamia Inter Milan

- Pia, Man. Utd inadaiwa kufutilia mbali mpango wake wa kutaka kumsajili Kiungo wa Tottenham, Christian Eriksen huku mchezaji huyo naye akihusishwa na Inter Milan
ARUSHA: MWALIMU MBARONI KWA KUMUOMBA MWANAFUNZI RUSHWA YA NGONO

- Ni William Mollel anayefundisha Kidato cha 5 na 6 shule ya Sekondari Embarway

- Inadawia, alikuwa akimnyanyasa Mwanafunzi huyo na kumuambia ili awe na amani, washiriki ngono

Zaidi, soma https://jamii.app/MwalimuEmbarwayMbaroni
TANZIA: Mwandishi Nguli wa Kazi za Fasihi ya Kiswahili Prof. Euphrase Kezilahabi amefariki leo baada ya kuugua kwa muda mrefu

> Atakumbukwa kwa kazi zake kama Rosa Mistika, Uwanja wa Fujo, Kaptula la Marx, Nagona na Mzingile na jinsi alivyotetea Mashairi ya Kisasa

Soma - https://jamii.app/RIPProfKezilahabi
#JFLeo
MPYA: Waziri Mkuu wa Canada, Justin Trudeau amesema taarifa zao za kiintelijensia zinaonyesha kuwa Ndege iliyoanguka juzi nchini Iran na kuua watu 176 wakiwemo raia 63 wa Canada ilitunguliwa na Iran

> Rais Trump pia amedai ana wasiwasi na chanzo cha ajali hiyo
KENYA: WAZAZI WADAIWA KUMUUA MWALIMU KUTOKANA NA MATOKEO MABAYA YA SHULE

> Wambua Mwangangi na Chris Kyalo Muli wamekamatwa kwa tuhuma za kumshambulia kwa panga Daisy Mbathe, Mwalimu wa shule ya Msingi Ndooni baada ya shule yake kutoa matokeo mabaya katika Mtihani wa Kitaifa wa KCPE kwa mwaka 2019

Soma - https://jamii.app/KifoMwlMatokeoMabaya