JamiiForums
52.8K subscribers
34.4K photos
2.44K videos
31.3K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
UGANDA: WATU 36 WAFARIKI KUTOKANA NA MAFURIKO

- Watu wengi bado hawajulikani walipo kutokana na mafuriko ya mvua zinazonyesha Mashariki mwa Uganda

- Aidha, maporomoko ya udongo yamewaacha maelfu ya watu bila makazi

Zaidi, soma https://jamii.app/UgandaFloods-Death36
MPYA: Milio ya risasi imerindima kati ya Al-Shabaab na Walinzi wa Hoteli ya Kifahari ya SYL katika Mji Mkuu wa Somalia, Mogadishu

- Al Shabaab wamevamia hotel hiyo karibu na Makazi ya Rais inayotumiwa zaidi na viongozi wengi wa Kisiasa

- Idadi ya Vifo bado haijajulikana

Zaidi, soma https://jamii.app/AlShabaabSYLHotel-Somalia
KENYA: MBARONI KWA KUSIMAMISHA MSAFARA WA RAIS NA KUOMBA KAZI

- Mwanaume mmoja, Uvinalies Nyabuto amekamatwa kwa kuusimamisha msafara wa magari wa Rais Uhuru Kenyatta

- Alishika bango la kumuomba Rais Kenyatta kazi kwenye Majeshi ya Ulinzi

Zaidi, soma https://jamii.app/MbaroniKumsimamishaRais-KE
SOMALIA: AL SHABAAB WALIOTEKA HOTELI KWA SAA 7 WAUAWA

- Majeshi ya Ulinzi yamefanikiwa kuwaua Wanamgambo wote watano walioteka hoteli ya Kifahari ya SYL huko Mogadishu

- Aidha, watu wengine watano wakiwemo raia wawili wameuawa katika tukio hilo

Zaidi, soma https://jamii.app/AlShabaabSYLHotel-Somalia
MICHEZO: KLABU YA NAPOLI YAMTIMUA KOCHA CARLO ANCELOTTI

- Timu ya Napoli ya Italia imemfukuza kazi kocha wao Carlo Ancelotti ikiwa ni chini ya masaa matatu baada ya kuiongoza timu hiyo kuingia hatua ya mtoano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya

Soma > https://jamii.app/AncelottiVsNapoli
#JFSports
RIPOTI: TATHMINI YA KIWANGO CHA KUJIFUNZA TANZANIA

- Taasisi za Twaweza na Uwezo Tanzania zinazindua ripoti hiyo ya mwaka 2019 leo jijini Dar

- Tangu mwaka 2011 ripoti hizo zimetoa mchango madhubuti katika kuongeza uelewa wa hali ya kisomo nchini

Fuatilia https://jamii.app/RipotiKiwangoKujifunza2019
MAREKANI YAWAWEKEA VIKWAZO VIONGOZI WA JESHI LA MYANMAR

- Marekani imefanya hivyo dhidi ya Viongozi wanne wa Kijeshi wa Myanmar akiwemo Mkuu wa Jeshi

- Marekani inalituhumu Jeshi la Myanmar kwa kukiuka haki za binadamu dhidi ya Warohingya

Zaidi, soma https://jamii.app/MarekaniVikwazoMyanmar
BALOZI WA SAUDI ARABIA NCHINI UTURUKI AZUIWA KUINGIA MAREKANI

- Marekani imemzuia Mohammed al-Otaibi, aliyekuwa Balozi wakati Mwanahabari Jamal Khashoggi alipouawa

- Khashoggi aliuawa ndani ya Ubalozi wa Saudi Arabia nchini Uturuki mwaka jana

Zaidi, soma https://jamii.app/BaloziSaudiMarufukuUSA
RIPOTI: KIINGEREZA BADO TATIZO KWA WANAFUNZI SHULE ZA MSINGI

- Katika Tathmini ya #Uwezo ya mwaka 2017, takribani 85% ya wanafunzi wa darasa la 3 walishindwa kusoma insha fupi ya Kiingereza ya darasa la 2

- Kwa upande wa wanafunzi wa darasa la 7, takribani nusu (53%) walishindwa kusoma insha hiyo hiyo ya darasa la 2

Je, kuna umuhimu wa Serikali kuangalia upya lugha ya ufundishaji katika shule za Sekondari iwapo Kiingereza ni tatizo kwa wanafunzi wa shule za Msingi?

Jadili na Fuatilia https://jamii.app/RipotiKiwangoKujifunza2019
KENYA: GAVANA MIKE SONKO AACHIWA KWA DHAMANA

- Gavana huyo wa Nairobi ameachiwa kwa dhamana ya pesa taslimu Ksh. Milioni 15 au bondi ya Ksh. Milioni 30

- Pia, anatakiwa kutokwenda ofisini na akitaka vitu vyake atasindikizwa na Wapelelezi

Zaidi, soma https://jamii.app/SonkoAachiwaDhamana
SHINYANGA: MABINTI WAOGESHWA DAWA KUVUTIA WANAUME. SERIKALI YAOMBWA KUZUIA

- Wasichana wa miaka kati ya 10 na 15 hupelekwa kuogeshwa dawa hiyo maarufu kama ‘Samba’

- Wadau wadai vitendo hivyo vinachochea Mimba za Utotoni na maambukizi ya UKIMWI

Zaidi, soma https://jamii.app/DawaKuvutiaWanaume
CPJ: KWA MWAKA 2019 HADI KUFIKIA DESEMBA 01, TAKRIBAN WANAHABARI 250 WAMEFUNGWA

- Ni kupitia ripoti yake ya mwaka 2019

- Ripoti inaonyesha China imefunga Wanahabari 48, Uturuki 47, Saudi Arabia 26, Misri 26, Eritrea 16, Vietnam 12 na Iran 11

- Erick Kabendera wa Tanzania aingia katika orodha

Soma > https://jamii.app/Wanahabari250Wafungwa2019
YANGA YAVUNJA MKATABA NA JUMA BALINYA

- Klabu ya Yanga imevunia mkataba na Mshambuliaji wake Raia wa Uganda, Juma Balinya kuanzia leo

- Hata hivyo, haijasema sababu za uamuzi huo dhidi ya Mchezaji huyo aliyekuwa Mfungaji Bora katika Ligi ya Uganda kabla ya kujiunga nao
MICHEZO: Klabu ya Napoli imemtangaza aliyekuwa Kocha wa AC Milan, Gennaro Gattuso kuwa Kocha wa timu hiyo akichukua nafasi ya Carlo Ancelotti

- Gattuso alijiuzulu kuifundisha AC Milan baada ya timu hiyo kushindwa kufuzu kushiriki Michuano ya Klabu Bigwa Ulaya msimu huu
SIMBA SC YAMTANGAZA KOCHA WAKE MPYA

- Imemtambulisha Raia wa Ubelgiji, Sven Vandenbroeck kuchukua nafasi ya Patrick Aussems aliyefukuzwa

- Vandenbroeck amewahi kuifundisha Timu ya Taifa ya Zambia na kushinda Ubingwa wa AFCON akiwa Kocha Msaidizi wa Cameroon mwaka 2017
NJOMBE: SIKU MOJA BAADA YA KUPEWA MSAMAHA WA RAIS AKAMATWA KWA WIZI

- Mussa Msola maarufu Hitler aliyekuwa miongoni mwa Wafungwa 5,533 waliopewa Msamaha wa Rais, Siku ya Uhuru, ametiwa mbaroni kwa tuhuma za kuvunja Nyumba ya Kulala Wageni

Zaidi, soma https://jamii.app/MfungwaMsamahaRaisMbaroni
TUMIA MITANDAO YA KIJAMII KUJINUFAISHA

> Mitandao ya Kijamii kama Facebook na Instagram, ukiitumia kwa mlengo chanya inaweza kukutajirisha kwasababu inatumiwa na watu wengi sana na imegeuza Dunia kuwa Kijiji kimoja kwani hukukutanisha na watu kiurahisi

> Inakuza watu kiakili kwani kuna kurasa nyingi nzuri zenye mafundisho tofauti ikiwemo ndoa, uchumi, biashara, mahusiano, na familia na inaweza kukusaidia kutatua changamoto mbalimbali katika maisha

Zaidi, tembelea - https://jamii.app/SocialMediaUse
NDEGE YA JESHI ILIYOPOTEA CHILE: MABAKI YAKE YAPATIKANA

- Mabaki yanayoaminika ni ya ndege ya Kijeshi iliyotoweka Jumatatu yamepatikana katika Mkondo Bahari wa Drake ikiwa ni takriban Kilometa 30 kutoka eneo ndege hiyo ilipopoteza mawasiliano

Zaidi, soma https://jamii.app/MabakiNdegeChile
KENYA: MABASI YA MODERN COAST YAGONGANA. WATU 7 WAFARIKI, 60 WAJERUHIWA

- Yamegongana usiku wa kuamkia leo katika eneo la Salama kwenye Barabara Kuu ya Mombasa-Nairobi

- Siku moja kabla basi jingine la Modern Coast liligongana na basi la Tahmeed

Zaidi, soma https://jamii.app/Ajali-7Wafariki62Wajeruhiwa
RAIS MAGUFULI: NDEGE YA TANZANIA ILIYOKUWA IKISHIKILIWA NCHINI CANADA IMEACHIWA

- Ndege ya Tanzania aina ya Bombardier Q400 iliyokuwa imeshikiliwa nchini Canada imeachiliwa

- Rais Magufuli amesema siku ya kuwasili nchini itatangazwa

Soma > https://jamii.app/NdegeCanadaHuru