JamiiForums
52.7K subscribers
34.4K photos
2.45K videos
31.3K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
UMUHIMU WA KUWASILIANA NA MWANAO

> Iwapo wazazi watadumisha mawasiliano ya karibu na watoto, hapatakuwa na haja ya kutumia nguvu nyingi kumjenga mtoto

> Tumia muda kuwasimulia watoto hadithi za chimbuko la familia yao. Hii itawapa nafasi ya kujivunia utu wao

> Jenga tabia ya kuandikiana jumbe za maneno kwenye karatasi. Hii inakupa fursa ya kujua kama anaweza kusoma na vilevile utapata kuuona mwandiko wake

> Kuwa na subira katika maongezi na mwanao. Mvumilie na jitahidi usiwe mwongeaji sana bali msikilizaji

Zaidi, soma - https://jamii.app/MbinuMawasilianoMtoto
#JFMalezi
MADHARA YA MVUA AFRIKA MASHARIKI: WATU 105 WAPOTEZA MAISHA

> Nchini Tanzania, takriban watu 16 wamefariki, Sudan Kusini, watu zaidi ya 200,000 wameathiriwa na Kenya, zaidi ya watu 1,000 wameyakimbia makazi yao

> Rwanda, watu 70 wamefariki na 177 kujeruhiwa. Nyumba 4,095 na hekta 6,708 zimeharibiwa huku wanyama 167 wakifa

Soma - https://jamii.app/MadharaMvuaEAC
CCM YAFUTA KURA ZA MAONI BAADHI YA SEHEMU, UCHAGUZI KURUDIWA

> Katibu Mkuu wa CCM, Dkt. Bashiru Ally amesema kumekuwa na madai ya rushwa, upendeleo na kanuni za kuchuja wagombea hazikuzingatiwa kwenye baadhi ya maeneo

> Pia, kulikuwa na rafu za kuchomoa majina kwenye masanduku ya kura na masanduku kubomolewa

Soma - https://jamii.app/MarudioKuraMaoniCCM
RUKWA: RC AAGIZA KUKAMATWA KWA WALIMU 2 WANAOTUHUMIWA KUBAKA NA KUWAPA MIMBA WANAFUNZI

> RC Joachim Wangabo ameagiza kukamatwa kwa Mkuu wa Shule ya Sekondari Mzindakaya, Dastan Mlelwa na Mwalimu mmoja wa Shule ya Sekondari Mpui

Zaidi, soma => https://jamii.app/RCRukwaVsWalimu
ZIMBABWE: TEMBO 55 WAPOTEZA MAISHA KUTOKANA NA UKAME

> Tembo 55 wamekufa njaa tangu Septemba 2019 katika Mbuga ya Taifa ya Hwange kutokana na ukame wa zaidi ya miezi 2

> Theluthi moja ya watu nchini humo wameripotiwa kukabiliwa na uhaba wa chakula

Soma - https://jamii.app/UkameVifoTembo
UGANDA: AFISA WA MAGEREZA (MWANAMKE) APORWA SILAHA, ALIKUWA AKIPIGA SOGA WHATSAPP

> Hadijah Katono ameporwa silaha na kijana aliyekuwa amejihami kwa Mkuki

> Kijana huyo alimpiga mara 2 kisha kuchukua bunduki hiyo aina ya AK-47 na kutokomea

Soma https://jamii.app/MpigiPrisonOfficer
TTCL YAKUBALI KUPELEKA HUDUMA YA INTANETI BURUNDI

> Shirika la TTCL limesaini mkataba huo na Kampuni ya Mawasiliano ya Mkongo wa Taifa ya Burundi (BBS) wenye thamani ya Tsh. bilioni 13.8

> Mkataba huo utatekelezwa nchini Burundi kwa miaka 10

Soma > https://jamii.app/TTCLVsBSS
VLADMIR PUTIN: TUNAWEZA KUISAIDIA AFRIKA BILA MASHARTI YA NCHI ZA MAGHABIRI

> Rais wa Urusi amesema nchi yake inaweza kuisaidia Afrika bila masharti ambayo huambatanishwa kwenye misaada ya Mataifa ya Magharibi

> Amesema, Mataifa ya Magharibi yanatoa mashinikizo na vitisho dhidi ya Serikali Huru za Kiafrika ili kurejesha utawala wa kikoloni na kulinyonya Bara la Afrika

Soma - https://jamii.app/PutinMisaadaAfrika
SAME: WANANCHI WALALAMIKA WAJAWAZITO KUTUMIA CHUMBA KIMOJA NA WANAOSAFISHWA VIDONDA

> Inadaiwa ukosefu wa Wodi ya Wajawazito katika Zahanati ya Lugulu iliyopo Wilaya ya Same, umesababisha wanaotaka kujifungua watumie chumba kimoja na wagonjwa wanaosafishwa vidonda

> Aidha, baada ya kujifungua wanawake walikuwa wakibebeshwa uchafu kutokana na kukosekana kwa shimo maalum la kutupia taka zitokanazo na Uzazi

Soma - https://jamii.app/UkosefuWodiWajawazito
KUSUASUA KWA UJENZI WA KIWANDA CHA TANGA FRESH: SERIKALI YAUNDA TUME YA UCHUNGUZI

> Serikali imebaini mtambo wa kusindika maziwa ya muda mrefu ulionunuliwa, ulikwishatumika na umenunuliwa kwa zaidi ya Shilingi Bilioni 6

Kwa habari zaidi, soma > https://jamii.app/UchunguziTangaFresh
MAREKANI: RAIS MSTAAFU JIMMY CARTER AANGUKA NA KUVUNJIKA NYONGA, AKIMBIZWA HOSPITALI

> Jimmy Carter(95) sasa amelazwa katika Kituo cha Afya cha Phoebe Sumter baada ya kuanguka na kuvunjika nyonga

> Aliiongoza Marekani mwaka 1977 hadi 1981

Soma > https://jamii.app/JimmyCarterPelvic
CAG PROFESA ASSAD ASEMA KAMATI ZA BUNGE ZAANZA KUFANYIA KAZI RIPOTI YA OFISI YAKE

> Profesa Assad pia, amezipongeza Halmashauri zilizofanya vizuri kwenye ukusanyaji wa mapato ya Serikali kama ilivyotangazwa na Waziri, Selemani Jaffo

Zaidi, soma > https://jamii.app/CAGPongezi
MAREKANI: MWIZI AVUNJA NYUMBA NA KUINGIA NDANI, KABLA YA KUIBA AMUOGESHA MTOTO

> Elizabeth Hixon(22) anashikiliwa na Polisi baada ya kuvamia nyumbani kwa Areica Hill

> Kabla ya kufanya wizi alinza kumuogesha Mtoto wa Kiume aliyemkuta amelala

Soma > https://jamii.app/HouseBurglary
MAHUSIANO: JE, KUNA ULAZIMA WA KUMHUDUMIA MCHUMBA WA KIKE?
-
Mdau wa JamiiForums anasema, kwa upande wake amejiwekea malengo ya kumhudumia mpenzi wake pindi atakapokuwa Mke wake halali

> Kama mwanamke anakaa kwao, basi wazazi wake ndio wana wajibu wa kutoa huduma

Soma > https://jamii.app/HudumaMpenzi
UDSM KUANZA KUTOA MITIHANI YA KIMATAIFA YA UJUZI WA KISWAHILI

> Chuo Kikuu cha Dar es salaam kinatarajia kuanza kutoa Mitihani hiyo mwaka 2020, kwa lengo la kuhakikisha lugha ya Kiswahili inakua zaidi

> Itakuwa ikifanyika mara sita kwa mwaka kwa njia za kielektroniki katika vyuo na vituo mbalimbali vya Kiswahili duniani

Soma - https://jamii.app/UDSMKukuzaKiswahili
WIZARA YAPIGA MARUFUKU WANANCHI KUUZA NYAMA PORI

> Wizara ya Maliasili na Utalii imesema ifikapo Desemba 2019, kanuni zitakuwa zimekamilika na watatangaza kwa umma maeneo yatakapokuwepo mabucha na Serikali itaendelea kudhibiti biashara hiyo ili mwananchi aweze kununua nyama hiyo kwa njia halali

Soma - https://jamii.app/ZuioKuuzaNyamapori
MARA: FISI WAVAMIA MSIBA NA KUJERUHI WATU WAWILI

> Watu 2 wameshambuliwa na Fisi wasiojulikana idadi yao baada ya kuvamia kwenye mji uliokuwa na msiba, Wilayani Bunda

> Majeruhi ni David Robert aliyejeruhiwa sehemu mbalimbali ikiwemo mikono yake na Elizabeth Mgeta (60) ambaye amejeruhiwa mkono mmoja

Soma - https://jamii.app/FisiUvamiziMsiba
KENYA: ASKARI POLISI ALIYEPINGA KUPELEKWA MAENEO YA KAZI AMBAYO HAWEZI KUJIPATIA FEDHA, APEWA LIKIZO YA LAZIMA

> Jane Asimizi, amepewa likizo hiyo ya lazima baada ya kuonekana kupitia video akilalamikia kupangwa maeneo yesiyo na ulaji

Soma > https://jamii.app/AsimiziLeave
HOJA: Wanafunzi wengi wanapohitimu masomo hutegemea na huamini kuwa vyeti vyao ndivyo vitakavyowakomboa lakini si kweli. Badala ya kukazana kutembea na vyeti, weka juhudi katika kutumia fursa zinazojitokeza mbele yako
-
Endapo mtu akikupa nafasi ya kufanya kitu na huna uhakika kama utaweza kukifanya, kubali kukifanya, kisha jifunze namna ya kukifanya. Wenye uwezo wa kukariri ndio wanaofanikiwa shuleni, lakini katika maisha wenye ubunifu na uwezo wa kutatua matatizo ndio wanaofanikiwa
-
Kuongoza darasani hakumaanishi utaweza kufanya vizuri kwenye maisha nje ya darasa. Duniani kuna watu wengi ambao hawakufanya vizuri darasani lakini ni matajiri kutokana na uwezo wao wa kuchangamkia fursa na kutatua matatizo
-
Tembelea > https://jamii.app/ElimuVsFursaMafanikio
MAHAKAMA YATAKA UTHIBITISHO WA MAENDELEO YA AFYA YA LISSU

> Mahakama ya Kisutu imewataka wadhamini wa Tundu Lissu kwenda na uthibitisho wa maendeleo ya afya yake kesi hiyo itakapotajwa tena baada ya kudai kuwa Lissu bado anaumwa

> Hakimu ameahirisha kesi hiyo hadi Novemba 21, 2019

Soma - https://jamii.app/VithibitishoAfyaLissu