JamiiForums
52.9K subscribers
34.3K photos
2.43K videos
31.3K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
MBARONI KWA KUJIANDIKISHA MARA 2 KWENYE DAFTARI LA WAPIGA KURA

- Ni Ngeze Mwagilo (29), Mkazi wa Kasanga Manispaa ya Morogoro

- Anadaiwa kujiandikisha katika Kituo cha Kasanga na kisha kwenda kujiandikisha katika Kituo cha Kiwanja cha Ndege

Zaidi, soma https://jamii.app/MbaroniUandikishaji2-Moro
MALAWI YAKANUSHA KUWA NA MGONJWA WA EBOLA

> Mamlaka ya Afya imekanusha ripoti ya kwamba mtu amegunduliwa kuwa na Ebola kwenye eneo la Karonga linalopakana na Tanzania

> Ofisa wa Afya amesema mtu huyo alikuwa na maambukizi ya Bakteria na si Ebola

Soma - https://jamii.app/MalawiDenouncesEbola
KAMPUNI ZA BOEING NA PORSCHE ZAUNGANA KUUNDA MAGARI YA KUSAFIRI ANGANI

> Boeing ya Marekani na Porsche ya Ujerumani zimetia saini makubaliano (MoU) kwa ajili ya uundwaji wa magari ya umeme yatakayokuwa na uwezo wa kupaa na kutua wima (Vertical Take-off and Landing (VTOL)) ili kuingia katika soko la 'Taxi'

Soma - https://jamii.app/PorscheBoeingFlyingCars
AZAKI ZATAKIWA KUENDESHA SHUGHULI ZAO KWA UWAZI ILI KUPATA UNAFUU WA KODI

> Waziri wa Fedha amezitaka Asasi za Kiraia kuendesha shughuli zao kwa Uwazi na Uwajibikaji kwa kufuata Sheria za Nchi, Matakwa na Vigezo ili kupata unafuu wa kodi

> Pia, amezitaka kuwasilisha mapendekezo juu ya Sheria za Kodi ili kilio chao cha msamaha wa kodi kifanyiwe kazi

Soma - https://jamii.app/AZAKIUwaziKodi
SHIRIKA LA NDEGE LA SWISS LASIMAMISHA SAFARI ZA AIRBUS A220

> Shirika la Ndege la SWISS International Airlines limesimamisha safari za ndege zake zote aina ya Airbus A220 kutokana na matatizo ya injini zake aina ya PW 1500G zinazotengenezwa na Kampuni ya Pratt & Whitney ya Canada

Soma - https://jamii.app/SwissGroundsA220
TMA YATOA ANGALIZO LA KUWEPO KWA MVUA KUBWA UKANDA WA PWANI KWA SIKU 2

> Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), imetoa angalizo la kuwepo kwa mvua kubwa ktk Mikoa ya Tanga, Dar, Pwani, Kaskazini mwa Morogoro na Visiwa vya Unguja na Pemba

> Mvua hizo zitaanza Oktoba 16 hadi Oktoba 17, 2019

Soma - https://jamii.app/TahadhariMvuaPwani
UFAHAMU NA ELIMU YA UGONJWA WA MAFINDOFINDO (TONSILS)

> Mafindofindo hujitokeza pale viungo viwili vidogo nyuma ya koo vinapozidiwa nguvu katika kupambana na wadudu wabaya ndani ya mwili

> Dalili zake ni Maumivu ya koo, maumivu wakati wa kufungua kinywa, ugumu katika kumeza mate/chakula, homa, kuvimba kwa Lymph Nodes kwenye shingo

> Tiba unayoweza kujipatia mwenyewe ni kunywa/kusukutua maji ya uvuguvugu kila mara (angalau mara 4 kwa siku) yenye chumvi, asali pamoja na ndimu/limao. Jambo hili huleta maumivu makali lakini utapona haraka

Soma - https://jamii.app/UgonjwaTonsils
#JFAfya
KENYA: BASI LA KANISA LAKAMATWA LIKISAFIRISHA MISOKOTO YA BANGI

> Polisi wamekamata basi la Kanisa la PEFA likiwa na Misokoto 230 ya bangi iliyokuwa imesundwa kama mizigo

> Bangi hiyo inakadiriwa kuwa na thamani ya zaidi ya Tsh. Milioni 1

Soma - https://jamii.app/KanisaKusafirishaBangi
SERIKALI YASHINDA RUFAA YA KUPINGA WAKURUGENZI KUSIMAMIA UCHAGUZI

> Mahakama ya rufaa imetoa uamuzi huo baada ya kujiridhisha na hoja za Serikali kuwa Wakurugenzi hao kabla ya kuwa wasimamizi wa uchaguzi hula viapo vya kukana uanachama wao

> Kesi hiyo ilifunguliwa na Bob Wangwe

Soma - https://jamii.app/WakurugenziUsimamiziUchaguzi
#JFLeo
KIWANGO CHA MAAMBUKIZI YA VIRUSI VYA UKIMWI KITAIFA CHASHUKA

> Kiwango kimeshuka kutoka 7% mwaka 2003/04 hadi kufikia 4.7% 2016/17 huku maambukizi kwa wanaume ikiwa ni 3.4% na wanawake ni 6.3%

> Hatua zilichochangia ni pamoja na huduma za ushauri nasaha na upimaji, tohara kwa wanaume, huduma za kondomu

Soma https://jamii.app/KushukaMaambukiziVVU
MGOGORO TANESCO NA IPTL: TANZANIA YAAMRIWA KULIPA DOLA MILIONI 185

> Mahakama ya Migogoro ya Kimataifa (ICSID), imeamuru Serikali ya Tanzania kulipa Dola 185.4 milioni (zaidi ya Tsh. Bilioni 426) kwa kukiuka mkataba

> TANESCO liliingia makubaliano ya kuzalisha umeme na IPTL 1995 lakini 2013 kukatokea kutoelewana

Soma - https://jamii.app/TzMalipoIPTL
WADAIWA SUGU WASABABISHIA UMOJA WA MATAIFA UKATA

- Inadaiwa Umoja huo unaweza kushindwa lipa Wafanyakazi na Watoa Huduma wake iwapo wadaiwa wasipolipa kufikia Oktoba 31

- Wadaiwa hao ni US, Argentina, Mexico, Israel, Iran, Venezuela na Brazil

Soma https://jamii.app/UkataUmojaWaMataifa
WAFANYABIASHARA WA VYUMA CHAKAVU WALIOKIUKA MAELEKEZO YA SERIKALI KUFUTIWA VIBALI

- Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, Mh. George Simbachawene ameagiza kufutwa kwa vibali vya wafanyabiashara wote wanaosafirisha vyuma chakavu ambao hawakufuata maelekezo ya Serikali

- Kampuni ambazo makontena yake yalikuwa yakifanyiwa uchunguzi ni J. M Kambi and General Services ( makontena 88), JBR Group of Companies ( makontena 35), Villa Plast Ltd ( makontena 3) , Three Star Metal Group ( makontena 12) na Steel Com Ltd ( makontena 2)

Soma - https://jamii.app/WafanyabiasharaVyumaChakavuWafutiwaVibali
Mfanyabiashara Mohamed Yusufali, aliyekuwa akikabiliwa na kesi mbili za Uhujumu Uchumi, arejea Uraiani

- Aliwahi kutajwa na Rais Magufuli kuwa alikuwa akiibia Serikali Tsh. milioni 7 kwa dakika kupitia Mashine za Kodi za Kielektroniki (EFD)

Soma > https://jamii.app/MohamedYusufaliIsFree
WATUMIAJI WA VIDEO ZA NGONO ZA KUDHALILISHA WATOTO MBARONI

- Watu 337 kutoka Nchi 38 wamekamatwa kufuatia kugundulika na kufungwa kwa moja ya mtandao mkubwa wa udhalilishaji Watoto Duniani unaotengeneza video za ngono za Watoto

Soma https://jamii.app/DarkWebChildAbuse-Arrest
WAFANYAKAZI WA TIGO WAHUKUMIWA KIFUNGO CHA NJE KWA KUWATAPELI WATEJA

> Mahakama ya Kisutu, Dar imewahukumu wafanyakazi 3 wa Kampuni ya Tigo na wafanyabiashara 2 kifungo cha nje cha miezi 6 kwa kutapeli wateja kwa ujumbe wa maandishi

> Pia imetaifisha simu 31 na laini zake pamoja na sare ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi la Tanzania (JWTZ)

Soma - https://jamii.app/WafanyakaziTigoJela
MUUGUZI ADAIWA KUMBAKA BINTI WA MIAKA 16 ALIYEKUWA AKIMUUGUZA MAMA YAKE

- Ni katika Hospitali ya Wilaya ya Igunga, Mkoani Tabora

- Mganga Mkuu wa Wilaya, Dr. Ruta Deus amethibitisha kutokea kwa tukio hilo lililotokea Oktoba 10, 2019

Soma https://jamii.app/MuuguziAbakaBintiMiaka16
WANAFUNZI 30,675 KUNUFAIKA NA MKOPO KWA AWAMU YA KWANZA 2019/20

- Mkopo wenye thamani ya Tsh. Bilioni 113.5 umetolewa kwa Wanafunzi wa mwaka wa kwanza

- Wanafunzi waliopata mkopo wanatakiwa kuingia katika akaunti zao walizoombea mkopo

Zaidi, soma https://jamii.app/MkopoAwamu1-2019-20