JamiiForums
52.6K subscribers
34.4K photos
2.45K videos
31.4K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
LEO JULAI 11: MAADHIMISHO YA SIKU YA KUPINGA RUSHWA BARANI AFRIKA

> Umoja wa Afrika unaitumia siku hii kuzikumbusha nchi Wanachama, sekta binafsi na asasi za kiraia kutumia siku hii kutathmini juhudi za kupiga vita rushwa kwa ajili ya maendeleo endelevu

Soma > https://jamii.app/RushwaAfrika
ADDIS ABABA, ETHIOPIA: WAKOSOAJI WA SERIKALI WAKAMATWA KWA KUDAIWA KUHUSIKA NA MAUAJI

> Waziri Mkuu wa Ethiopia, Abiy Ahmed aliyesifiwa kwa kuwaachia huru wafungwa wa kisiasa, ahofiwa kuwa mbioni kuirudisha nchi hiyo katika utawala wa mabavu

Zaidi, soma => https://jamii.app/WapinzaniVsSerikali-Ethiopia
CCM YAPATA MGOMBEA WA KUWANIA UBUNGE JIMBO ALILOONDOLEWA LISSU

- DC wa Ikungi mkoani Singida, Miraji Mtaturu ataiwakilisha CCM katika kinyang’anyiro cha Ubunge Jimbo la Singida Mashariki

- Ameshinda kura za maoni 396 kati ya 634 sawa na 63%

Zaidi, soma https://jamii.app/MirajiMtaturuUbunge
MWAKYEMBE: KAMA TFF IMEMFUKUZA AMUNIKE KWA KUIGA MISRI, NAO WAJIUZULU

- Amesema hana tatizo na uamuzi wa TFF iwapo wataonesha mkakati wa kutupeleka mbele kisoka

- Amewataka TFF kama waliiga, waige kikamilifu kwani Viongozi wa soka Misri walijiuzulu

Zaidi, soma https://jamii.app/MwakyembeVsTFF
NECTA YATANGAZA MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2019. UFAULU WAONGEZEKA KWA 0.74%

- Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) limetangaza matokeo ya kidato cha sita ya mwaka 2019 ambapo ufaulu umeongezeka kutoka 97.58% mwaka 2018 hadi 98.32% kwa mwaka huu 2019

Zaidi, soma https://jamii.app/MatokeoKidato6-2019
MAXENCE MELO KUHOJIWA KWA DCI JUU YA MADAI YA MUSIBA KUTAKA KUULIWA

- Ni kuhusiana na tuhuma za kupanga njama za kumuua Cyprian Musiba zilizoandikwa na magazeti ya Tanzanite na Fahari Yetu

- Magazeti hayo yamedai amepanga njama hizo kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi, TCRA, Balozi Emmanuel Nchimbi na Benard Membe

Zaidi, soma https://jamii.app/MaxMeloDCIMusiba
NAHODHA WA ARSENAL AGOMA KUSAFIRI NA TIMU

- Laurent Koscielny amegoma kwenda Marekani na timu hiyo kwenye maandalizi ya msimu mpya wa Soka wa mwaka 2019/20

- Anadaiwa analazimisha kuondoka klabuni hapo na tayari ana ofa kubwa kutoka vilabu vya Bordeaux, Lyon na Rennes
WAZIRI KABUDI AKANUSHA KUTHIBITISHA KIFO CHA AZORY GWANDA

- Amesema amepokea kwa masikitiko taarifa potofu zinazochapishwa kimakosa kuwa amethibitisha kifo cha Azory

- Amesema "Mpaka sasa hakuna uthibitisho kuwa Azory yuko hai au amefariki.”

Zaidi, soma https://jamii.app/KabudiAkanaKuthibitishaKifoAzory
ALGERIA: MBUNGE WA UPINZANI ACHAGULIWA KUWA SPIKA

> Aliyechaguliwa kuwa Spika ni Slimane Chenine kiongozi wa muungano wa vyama vitatu vidogo vya Kiislamu katika Bunge

> Hii ni Mara ya kwanza katika siasa za Algeria

Zaidi, soma => https://jamii.app/ChenineSpikaAlgeria
MBUNGE FRANK MWAKAJOKA (CHADEMA) MBARONI

- Mbunge huyo wa Tunduma amekamatwa na Polisi leo ikielezwa atafikishwa Mahakamani kujibu tuhuma za kumpiga Mtu mwaka 2018

- Inadaiwa amekamatwa kwa madai ya kumpiga Afisa Mtendaji, Deus Mwampashe

Zaidi, soma https://jamii.app/MwakajokaMbaroniTuhuma2018
AFCON2019: Timu ya Taifa ya Ivory Coast imetoshana nguvu na timu ya Taifa ya Algeria katika dakika 90 za mchezo wa robo fainali kwa kufungana goli 1-1

- Timu hizo zinaenda katika dakika 30 za nyongeza na zikitoka suluhu mshindi atatafutwa kwa mikwaju ya penati
DAR: WATU 7 WATUHUMIWA WA UJAMBAZI WAKAMATWA

- Walivunja maduka matatu na kuiba bidhaa mbalimbali, fedha na bajaji mbili huko Ukonga

- Polisi imesema Watuhumiwa hao walikuwa wakitumia gari aina ya Toyota Harrier nyeusi yenye namba T 666 DJG

Zaidi, soma https://jamii.app/Majambazi7Mbaroni-DarJul2019
AFCON2019: Algeria imefuzu kucheza nusu fainali baada ya kuiondosha Ivory Coast kwa penati 4-3

- Mchezo huo umeamuliwa kwa penati baada ya timu hizo kutoka sare ya goli 1-1 ndani ya dakika 120

- Algeria itakutana na Nigeria Julai 14, 2019 katika nusu fainali
TFF IMEMCHAGUA KOCHA WA AZAM KUKAIMU UKOCHA WA TAIFA STARS

- Ndayiragije Etienne anakaimu ukocha na ataiongoza Stars kufuzu CHAN

- Kocha wa Coastal Union, Juma Mgunda na Kocha Msaidizi wa Polisi Tanzania, Suleiman Matola wapo benchi la ufundi

Zaidi, soma https://jamii.app/NdiyaragijeKaimuStars
AFCON2019: Timu ya Taifa ya Tunisia 🇹🇳 imefanikiwa kufuzu kucheza hatua ya nusu fainali ya michuano hiyo baada ya kuifunga timu ya Taifa ya Madagascar 🇲🇬 goli 3-0

- Tunisia itapambana na timu ya Taifa ya Senegal 🇸🇳 katika mchezo wa nusu fainali mnamo Julai 14, 2019
MAREKANI: R. KELLY AKAMATWA TENA KWA TUHUMA ZA UNYANYASAJI WA KINGONO

> Akamatwa na Idara ya Polisi ya New York kwa tuhuma za kuwasafirisha Wanawake kwa ajili ya kuwatumikisha kingono

> Ametiwa nguvuni wakati akiwa katika Jimbo la Chicago

Soma > https://jamii.app/RKellyArrested
KENYA: AUA WATOTO WAKE NA KUWATUPA CHOONI

- Polisi katika Kaunti ya Nandi inamtafuta Mwanamke, Floxy Cheptoo(32) anayedaiwa kumuua Mtoto wake wa Kike(7) na wa Kiume(11)

- Miili iligundulika baada ya Mwanakijiji kubaini alama za damu chooni

Zaidi, soma https://jamii.app/AuaWatotoChooni-KE
RAIS WA UGANDA KUFANYA ZIARA BINAFSI, NCHINI

- Rais Yoweri Museveni Kesho, Julai 13, 2019 atafanya ziara binafsi ya siku moja kwa kumtembelea Rais Magufuli

- Atamtembelea Rais Magufuli Kijijini kwake, Mlimani katika Wilaya ya Chato, Mkoani Geita

Zaidi, soma https://jamii.app/MuseveniZiaraBinafsi-TZ