JamiiForums
52.5K subscribers
34.4K photos
2.47K videos
31.4K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
KENYA: MBUNGE JAGUAR AKAMATWA NA POLISI

- Mbunge wa Jimbo la Starehe, Charles Njagua maarufu 'Jaguar' amekamatwa baada ya kuwataka Wafanyabiashara wa kigeni Jimboni kwake kufunga biashara zao na kuondoka la sivyo wataondolewa kwa nguvu

Zaidi, soma https://jamii.app/JaguarMbaroniKenya
MFANYABIASHARA KUTOKA KENYA ADAIWA KUTEKWA, JIJINI DAR

- Raphael O. Ongangi anadaiwa kutekwa Juni 24, 2019 na watu wenye silaha akielekea nyumbani kwake maeneo ya Masaki

- Alikuwa mshauri wa karibu wa Zitto Kabwe kabla ya Uchaguzi Mkuu 2015

Zaidi, soma https://jamii.app/MfanyabiasharaOngangiAtekwa-Dar
IDADI YA WARAIBU WA DAWA ZA KULEVYA YAPUNGUA

> Tanzania leo Juni 26, imeungana na mataifa mengine duniani kuadhimisha siku ya Kimataifa ya kupambana na matumizi na biashara ya dawa za kulevya

> Idadi ya waathirika katika vituo vya tiba imeongezeka kutoka wagonjwa 2,400 mwaka 2015 hadi wagonjwa 7000 mwaka 2018 na kufanya waraibu wa dawa za kulevya wanaojidunga kupungua kutoka 35% mwaka 2015 hadi 18.5% mwaka 2018

Soma - https://jamii.app/SikuDawaKulevya
#JFLeo
SERIKALI YATOA MAPENDEKEZO YA KUBADILI SHERIA KATI YA TBS NA TFDA

> Imependekeza marekebisho ya sheria ya viwango ili kuhamisha usimamizi wa masuala ya chakula na vipodozi kwa Shirika la Viwango Tanzania kutoka Mamlaka ya Chakula na Dawa

Soma - https://jamii.app/SheriaTBSnTFDA
#JFLeo
MBEYA: DAKTARI FEKI ANASWA. AKUTWA NA WAGONJWA ZAIDI YA 100

- Ni Abdallah Bushiri(42) aliyejifanya daktari wa binadamu na kufanyia watu upasuaji wakati hana taaluma hiyo

- Wagonjwa zaidi ya 100 wamekutwa nyumbani kwake wakisubiri matibabu

Zaidi, soma https://jamii.app/DaktariFekiMbeya-Juni2019
AFCON2019: Nigeria imefanikiwa kuibuka na ushindi wa goli 1-0 dhidi ya Guinea katika mchezo wa Kundi B na kuongoza kundi hilo ikiwa na alama 6

- Timu nyingine katika kundi hilo za Burundi na Madagascar zitakutana kesho saa kumi na moja na nusu jioni
MADEREVA BAJAJI WAGOMA KUNUNUA VITAMBULISHO VYA WAJASIRIAMALI

> Polisi Mkoani Rukwa wamefyatua mabomu ya machozi hewani ili kuwatawanya baadhi ya madereva wa bajaji wanaoendelea na mgomo wa kutoa huduma ya usafiri wakipinga kuuziwa vitambulisho vya ujasiriamali

> Wamesema wao vitambulisho haviwahusu kwani ni madereva kama walivyo madereva wengine na vyombo vyao vimesajiliwa

Soma - https://jamii.app/MgomoBajajiVitambulisho
#JFLeo
AFCON2019: Timu ya Taifa ya Uganda imetoka sare ya goli 1-1 na timu ya Taifa ya Zimbabwe katika mchezo wa kundi A

- Uganda imefikisha alama 4 ikiwa inaongoza kundi hilo huku Misri ikiwa nafasi ya pili ikiwa na alama 3 na michezo mmoja pungufu
MTUMISHI WA HIFADHI MATATANI BAADA YA KUKUTWA NA NYAMA YA NYUMBU

> Thomas Mugabo (56) amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mfawidhi Wilaya ya Serengeti kwa kosa la kukutwa na nyama ya nyumbu vipande 231 sawa na nyumbu mzima mwenye thamani ya Tsh. 1,430,000

Soma - https://jamii.app/HujumaNyamaNyumbu
CHELSEA YAKUBALIANA NA REAL MADRID KUMNUNUA KOVACIC

- Chelsea imefikia makubaliano na Real Madrid kumsajili moja kwa moja Mchezaji wake, Mateo Kovacic

- Chelsea inatumikia kifungo cha kutosajili kwa madirisha ya usajili katika misimu miwili, ila inaweza kusajili Wachezaji walio kwa mkopo Klabuni hapo
HAI: DIWANI ADAIWA KUBAKA NA KUMPA MIMBA MWANAFUNZI

> Diwani wa Kata ya Masama Mashariki Mkoani Kilimanjaro, John Munisi(38), amefikishwa Mahakamani akidaiwa kumbaka na kumpa mimba mwanafunzi(17) kidato cha nne wa Shule ya Sekondari Marire

> Alikana mashtaka na yupo nje kwa dhamana baada ya kukidhi masharti

Soma - https://jamii.app/DiwaniUbakajiMimba
JAGUAR AFIKISHWA MAHAKAMANI, ANYIMWA DHAMANA

- Mbunge wa Starehe, Charles Njagua maarufu Jaguar amekosa dhamana huku Hakimu akisema atatoa hukumu Ijumaa

- Aidha, simu yake ya mkononi inashikiliwa na Wapelelezi ila bado haijafanyiwa uchunguzi

Zaidi, soma https://jamii.app/JaguarMahakamaniUchochezi
NGARA: WANAFAMILIA WAFARIKI BAADA YA NYUMBA KUTEKETEA KWA MOTO

> Ajali hiyo ilitokea jana na waliofariki ni Abubakary Ramadhan Sudi(41) ambaye ni Baba, Zamrat Abubakary(4), Maryam Abubakari(7) na Suzy Abubakari
(36) ambaye ni mama na alifariki akiwa anapewa matibabu hospitalini

Soma - https://jamii.app/FamiliaKifoMoto
#JFLeo
TATIZO JINGINE LAGUNDULIKA KATIKA NDEGE ZA BOEING 737 MAX

- Wakaguzi wa Marekani wamegundua tatizo linaloweza kuchelewesha ndege hiyo kurudi kutoa huduma

- Bila kutaja tatizo wamesema wakati wa majaribio wamegundua "inayowezekana kuwa hatari"

Zaidi, soma https://jamii.app/TatizoJipyaBoeingMax
NGARA, KAGERA: WALIOKUWA WAKISAFIRISHA MITIHANI WAFARIKI AJALINI

- Ni Watu 2 akiwemo Askari wa JWTZ waliokuwa wakisafirisha mitihani ya majaribio ya kidato cha 4

- Gari walimokuwemo lilipinduka katika mteremko mkali ulioko barabara ya Kumnazi

Zaidi, soma https://jamii.app/AjaliWawiliWafariki-KumnaziKGR
MAUAJI AFISA WA JESHI ETHIOPIA: WATU 39 MBARONI WAKIHUSISHWA

> Polisi nchini Ethiopia wamewakamata watu 39 kutoka chama cha Impala kwa tuhuma za kuhusika na mauaji ya maafisa watano wa Jeshi katika jaribio la kuipindua Serikali katika jimbo la Amhara

> Kati ya waliofariki yupo Mkuu wa majeshi na aliyekuwa Gavana wa jimbo la Amhara

Soma - https://jamii.app/Revolution39Arrested
AFCON2019: Madagascar imeibuka na ushindi wa goli 1-0 dhidi Burundi katika mchezo wa Kundi B

- Madagascar inafikisha alama 4 huku Kundi hilo likiongozwa na Nigeria yenye alama 6, Guinea ina alama 1 na Burundi ina alama 0 ambapo timu zote zimecheza michezo miwili
AFCON2019: Michezo inayofuata ni ya Kundi C ambapo Senegal inakutana na Algeria majira ya saa mbili kamili usiku huu

- Katika Kundi hilo hilo Kenya ‘HarambeeStars’ inakutana na Tanzania ‘TaifaStars’ majira ya saa tano kamili usiku
NIGERIA: FEDHA ZILIZOKUWA ZIMEFICHWA NA RAIS MSTAAFU ZATAIFISHWA

> Fedha hizo ni zaidi ya Dola milioni 267 (zaidi ya Tsh bilioni 600) ambazo zilifichwa na Rais San Abacha katika benki iliyopo kisiwa cha Jersey

> Zilipatikana kwa njia za rushwa wakati wa utawala wake kati ya mwaka 1993 hadi kifo chake mwaka 1998

Soma - https://jamii.app/TaifishoFedhaRais
URUSI: WAWILI WAFARIKI, SABA WAJERUHIWA KATIKA AJALI YA NDEGE

- Ni baada ya ndege kutua kwa dharura katika uwanja wa ndege katika eneo la Buryatia huko Siberia na kuwaka moto

- Waliofariki katika ndege hiyo iliyokuwa imebeba watu 48 ni rubani na fundi

Zaidi, soma https://jamii.app/TwoKilledPlaneAcc-Urusi