JamiiForums
52.7K subscribers
34.4K photos
2.45K videos
31.3K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
MHASIBU WIZARA YA AFYA MATATANI KWA UBADHIRIFU WA FEDHA

> Taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa nchini (TAKUKURU), mkoani Kilimanjaro inamshikilia Yahya Athuman kwa tuhuma za kufanya ubadhirifu wa zaidi ya Tsh. milioni 34 katika fedha za chanjo ya Rubella baada ya kumdanganya mwajiri wake

Soma - https://jamii.app/MhasibuUbadhilifuFedha
SUDAN KUSINI: MCHUMI AFUNGWA JELA KWA KUFANYA MAHOJIANO NA WANAHABARI

> Msomi Peter Biar Ajak amehukumiwa miaka 2 jela kwa hatia ya kuvunja amani

> Ajak alifanya mahojiano na vyombo vya kimataifa alipokuwa akituhumiwa kwa uhaini

Zaidi, soma => https://jamii.app/AjakHukumu
WAZIRI LUKUVI: WADAIWA SUGU LIPENI MADENI YENU KUEPUKA FEDHEHA

> Amewataka wadaiwa sugu wa kodi ya pango la ardhi kulipa madeni yao kabla ya Juni 21, 2019

Amewataka wafanye hivyo ili waepuke aibu, fedheha pamoja na hatua za kisheria

Zaidi, soma => https://jamii.app/LukuvuKodiArdhi
KENYA: MWANAFUNZI ALIYEJARIBU KUINGIA IKULU APIGWA RISASI

> Aliyepigwa risasi ni Brian Bera ambaye ni Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Kilimo na Teknolojia cha Jomo Kenyatta (JKUAT)

> Alijaribu kuingia Ikulu Jijini Nairobi kinyume cha sheria

Soma > https://jamii.app/KijanaIkuluKE
ZITTO KABWE AKAMATWA NA KUSHIKILIWA NA UHAMIAJI ZANZIBAR

> Katibu wa Uenezi wa ACT Wazalendo, Ado Shaibu amesema Zitto anashikiliwa tangu saa 8 mchana wa leo

> Zitto amekamatwa kwa madai kuwa haruhusiwi kusafiri kwenda nje ya nchi

Soma => https://jamii.app/ZittoUhamiajiZNZ
UPDATE: ZITTO KABWE AACHIWA HURU: Taarifa zinaeleza kuwa Kiongozi huyo wa Chama cha ACT Wazalendo ameachiwa baada ya kushikiliwa na Jeshi la Polisi Zanzibar tangu saa 8 mchana wa leo

> Aidha, inaelezwa kuwa simu na 'Laptop’ yake vinaendelea kushikiliwa

#JFLeo
WAZALISHAJI WA BIDHAA ZA CHUPA ZA PLASTIKI WATAKIWA KUSHIRIKI KUZIKUSANYA BAADA YA MATUMIZI

> Kwa mujibu wa Kanuni za Sheria inayohusika na usimamizi wa Mazingira inaeleza kuwa wazalishaji/msambazaji wa bidhaa hizo atapaswa kushiriki mchakato wa kukusanya kwa ajili ya kuzilejeleza(Recycling)

> Waziri wa Wizara ya Mazingira, January Makamba amepanga kuonana na wazalishaji na wasambazaji wa bidhaa za chupa za plastiki ili kutoa maelezo ya zoezi hilo

Soma => https://jamii.app/ChupaPlastiki
KOMBE LA DUNIA LA WANAWAKE: MAREKANI YAINYUKA THAILAND 13-0

> Marekani imeibuka na ushindi huo usiku wa kuamkia leo na kushika usukani wa Kundi F katika michuano hiyo inayoendelea nchini Ufaransa

> Huu ni ushindi ulioweka rekodi ya kipekee katika historia ya michuano hiyo

#JFSports #FIFAWWC
SERIKALI: VIWANDA 3,000 VIMEJENGWA MAENEO MBALIMBALI NCHINI

> Taarifa hii ni kwa mujibu wa Naibu Waziri wa Wizara ya TAMISEMI, Mwita Waitara

> Viwanda hivyo inadaiwa ni matokeo ya agizo la Serikali juu ya ujenzi wa viwanda 100 katika kila Mkoa lililotolewa Desemba, 2017

Soma > https://jamii.app/GvtViwanda3000
MAANDAMANO HONG KONG: POLISI WATUMIA MAJI YA PILIPILI KUTAWANYA WATU

> Wanaandamana kupinga muswada utakao ruhusu watuhumiwa wa makosa mbalimbali kusafirishwa na kwenda kushtakiwa Beijing, China

> Hong Kong ni jimbo la China lenye mamlaka kamili

Soma > https://jamii.app/MaandamanoHongKong
KIINGEREZA KUENDELEA KUWA LUGHA YA KUFUNDISHIA ELIMU YA JUU

> Serikali imesema Kiingereza kitaendelea kuwa lugha ya kufundishia na kujifunzia katika ngazi ya elimu ya Sekondari, vyuo vya kati na vyuo vikuu kwasababu ya umuhimu wake kitaifa, kikanda na kimataifa kwa mawasiliano na biashara ili kuwajengea wanafunzi ufahamu na umahiri wa lugha hiyo

Soma - https://jamii.app/EnglishTeachingLang
APANDISHWA KIZIMBANI KWA KUMSHIKA MTOTO SEHEMU ZA SIRI

> Vicent Marseli (37) amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kinondoni akikabiliwa na shtaka la kumshika sehemu za siri mtoto wa miaka mitatu ili kujiridhisha kimapenzi

Soma - https://jamii.app/KizimbaniDhalilishamtoto
UTEUZI: RAIS MAGUFULI ATEUA WENYEVITI BODI ZA TTCL NA AIRTEL

> Mohammed Abdallah Mtonga ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya TTCL

> Mtonga anachukua nafasi ya Dkt. Omari Nundu aliyeteuliwa Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni ya Airtel Tanzania

Soma > https://jamii.app/UteuziTTCLAirtel
NAIROBI, KENYA: MAHAKAMA YAONGEZA MUDA WA ZUIO LA WABUNGE KUJIONGEZEA POSHO

> Wabunge walipitisha azimio la kulipana posho kwa ajili ya nyumba kiasi cha Tsh. Milioni 5.5 kila mwezi

> Tume ya Mishahara ilifungua kesi kupinga posho hiyo

Soma => https://jamii.app/WabungeKEPosho
BURUNDI YASHINDWA KUTIMIZA VIGEZO VYA KUJIUNGA SADC

> Burundi imekwama kujiunga na Jumuiya ya Maendeleo kwa Nchi za Kusini mwa Afrika baada ya kushindwa kutimiza vigezo vya kuwa mwanachama

> Hali ya uhusiano na nchi jirani ikiwemo Rwanda ni miongoni mwa dosari za kutokamilika kwa vigezo vya kujiunga SADC

Soma - https://jamii.app/SADCDeniesBurundi
OMBI LA RUFAA DHIDI YA KANUNI MAUDHUI ZA MTANDAONI LAKUBALIWA

> Mahakama Kuu Kanda ya Mtwara, imekubali kutoa kibali cha rufaa dhidi ya Kanuni za Maudhui Mtandaoni ya 2018

> Pingamizi litawasilishwa Mahakama ya Rufaa kwa ajili ya kuamuliwa

Soma https://jamii.app/RufaaMtwara
UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KUGHARIMU TSH. BILIONI 82.9

> Serikali imesema uchaguzi wa Serikali za mitaa utakaofanyika Oktoba, 2019 utagharimu Tsh bilioni 82.9 huku ikivitoa hofu vyama vya upinzani kuwa utakuwa huru na wa haki

> Imekamilisha maandalizi ya kanuni za uchaguzi, kuhakiki maeneo ya utawala na kufanya mafunzo na mikutano kwa wadau

Soma - https://jamii.app/Bil82UchaguziMitaa
MAREKANI: WANAOBAKA WATOTO KUONDOLEWA NGUVU ZA KIUME

> Jimbo la Alabama limepitisha muswada wa sheria inayowalazimu watu waliopatikana na hatia ya kuwabaka watoto wenye umri chini ya miaka 13, kuondolewa nguvu za kiume kupitia njia ya kemikali

> Hadi sasa kuna majimbo 7 yakiwemo Louisiana na Florida, yenye sheria kama hiyo

Soma - https://jamii.app/SheriaKubakaWatoto