JamiiForums
55.4K subscribers
33.4K photos
2.04K videos
30.4K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
AIRBUS KUSITISHA UZALISHAJI WA NDEGE AINA YA A380

> Shirika la Airbus limetangaza kusitisha uzalishaji wa ndege zake aina ya A380 Superjumbo ifikapo 2021 kutokana na kukosekana kwa soko

> Mteja mkuu alikuwa ni Shirika la ndege la Emirates

Soma - https://jamii.app/AirbusSeizeA380
TRUMP KUSAINI MUSWADA WA KUGHARAMIA MATUMIZI YA SERIKALI

> Muswada huo utazuia kufungwa tena kwa Serikali Kuu na kuwapa ahueni wafanyakazi takribani 800,000 waliopata kadhia ya kutolipwa mishahara mwezi Desemba

> Aahidi kutangaza hali ya dharura ili kupata pesa za kujenga ukuta

Soma - https://jamii.app/USFundingBill
KENYA: AFISA WA POLISI AHUKUMIWA KIFO KWA KUMUUA MAHABUSU

> Mahakama Kuu imempa adhabu ya kifo Afisa Mwandamizi wa Jeshi la Polisi, Nahashon Mutua kwa kosa la kumuua Mahabusu

> Mutua alimpiga na nondo Martin Koome hadi kufa mwaka 2013

Soma - https://jamii.app/AfisaPolisiAhukumiwaKifoKE
RAIA 13 WA ETHIOPIA WAKAMATWA MWANZA

> Jeshi la Polisi mkoani Mwanza linawashikilia raia 13 wa Ethiopia baada ya kukutwa wakiwa wamejificha kwenye shamba la mkazi mmoja wa mtaa wa Nyaburogoya Kata ya Nyegezi

> Walikamatwa Februari 13

Soma - https://jamii.app/WahamiajiEthiopiaWakamatwa
KENYA: MAAFISA WATANO WA POLISI WAKUTWA NA HATIA YA KUMUUA MTOTO

> Maafisa 5 wa Jeshi la Polisi, wamekutwa na hatia ktk kesi ya kumpiga na kitu kizito kichwani mtoto mwenye umri wa miezi 6, Samantha Pendo mwaka 2017 na kumsababishia kifo

Soma - https://jamii.app/Maafisa5HatianiMauajiMtoto
KAMPALA, UGANDA: WANAWAKE WAWILI WAFANYAKAZI WA BENKI WABAKWA NA MAJAMBAZI

> Wanawake hao ni wafanyakazi wa Benki ya Development Finance Company of Uganda(DFCU). Wamebakwa na majambazi waliojaribu kupora fedha katika benki hiyo

Soma > https://jamii.app/KampalaBankRobbery
SHINYANGA: WATU 2 WAFARIKI DUNIA BAADA YA KUANGUKIA KWENYE SHIMO LA MACHIMBO YA KOKOTO

> Shimo hilo limejaa maji kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha kwenye kijiji cha Kadoto huko Mwalukwa

Zaidi, soma => https://jamii.app/WafarikiShimoKokoto
SLOVENIA: MBUNGE AJIUZULU BAADA YA KUIBA MKATE

> Mbunge Krajcic wa Slovenia amejiuzulu baada ya kuiba mkate maarufu ''sandwich'' katika duka moja kwa madai kuwa wahudumu wa sehemu hiyo walimpuuzia

> Ameomba msamaha na kujutia kufanya hivyo

Soma - https://jamii.app/PmResignsStealingSandwich
AFARIKI KWA KUCHOMWA KISU NA MKEWE

> Mkazi wa Kijiji cha Lugalawa, Wilaya ya Ludewa-Njombe, Osmund Joseph Mwinuka(37) amefariki baada ya kuchomwa Kisu tumboni na mke wake kwa wivu wa Mapenzi

> Kamanda wa Polisi amethibitisha taarifa hiyo

Soma - https://jamii.app/MkeAuaMumeLudewa
KONDOMU ZADAIWA KUADIMIKA WILAYANI MAFINGA

> Kondomu za kike na kiume zimeonekana kupungua mjini hapo huku zilizopo zikielezwa kupanda bei na kuuzwa ghali kuanzia shilingi 1,000 mpaka 3,000

Soma - https://jamii.app/UhabaKondomuMafinga
SERIKALI KURUDISHA KODI KWENYE TAULO ZA KIKE KAMA HAZITASHUKA BEI

> Hii ni kutokana na wauzaji na wasambazaji wa taulo hizo kushindwa kupunguza bei licha ya kodi kuondolewa

> Waziri wa Fedha na wa Viwanda watakiwa kuanza kusimamia

Soma > https://jamii.app/BeiTauloKike
KILIMANJARO: MADUKA ZAIDI YA 150 YAFUNGWA KUPINGA ONGEZEKO LA KODI

> Wafanyabiashara katika kituo kikuu cha mabasi wamefunga maduka yao wakipinga ongezeko la kodi

> Manispaa imewataka walipe kodi ya 400,000/- hadi 450,000/- kwa kila pango

Soma > https://jamii.app/MgomoMadukaMoshi
ARUMERU: SERIKALI ITAWACHUKULIA HATUA ASKARI WANAOSAFIRISHA DAWA ZA KULEVYA

> Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola asema watakaobainika kutumia magari ya Jeshi la Polisi kubeba/kusafirisha/kusindikiza #DawaZaKulevya watawajibishwa

Zaidi, soma => https://jamii.app/KangiArumeru
KAGERA: WALIOKUTWA NA HATIA YA KUCHOMA KANISA WAHUKUMIWA KIFUNGO CHA MAISHA

> Mahakama imetoa hukumu hiyo kwa Watu watatu iliyowakuta na hatia ya kuchoma moto Kanisa Katoliki Kigango cha Nyarwele, Parokia ya Kimiza

Zaidi, soma => https://jamii.app/KageraKifungoMaisha
MAREKANI: MKE AMUUA MUMEWE ILI AFUNGE NDOA NA MPENZI WAKE

> Mfanyakazi wa gereza, Amy Murray(40) anatuhumiwa kumuua mumewe, Joshua Murray(72) kwa kumtilia sumu kwenye chakula, ili apate nafasi ya kufunga ndoa na mpenzi wake ambaye ni mfungwa

Soma https://jamii.app/WifeKillsHusbandUS
SAA 5 KABLA YA UCHAGUZI NIGERIA: TUME YATANGAZA KUAHIRISHA KWA WIKI MOJA

> Uchaguzi wa Rais na Wabunge umesogezwa mbele hadi Jumamosi tarehe 23 mwezi huu

> Aidha, uchaguzi wa Magavana umepangwa kufanyika tarehe 9 ya mwezi Machi 2019

Soma => https://jamii.app/NigeriaElectionDelayed
WANAWAKE WENYE MIAKA 30+ HATARINI KUUGUA SARATANI

> Breast Cancer Now limefadhili utafiti uliobaini kwamba, Saratani hutambulika mapema kwa wanawake wenye umri kati ya miaka 35 hadi 39 wanapofanyiwa uchunguzi kila mwaka(mammograms)

Zaidi, soma - https://jamii.app/WomenVsBreastCancer
#JFAfya
MISRI: MCHAKATO WA RAIS ABDEL FATTAH KUKAA MADARAKANI HADI 2034 WAANZA

> Mchakato huo utamuwezesha rais Abdel Fattah al-Sisi kukaa madarakani hata baada ya muhula wake kuisha 2022

> Wabunge 485 kati ya 596 wameunga mkono mabadiliko hayo

Soma => https://jamii.app/MisriRais2034

#JFInternational
KAYA 2,086 ZAKUMBWA NA MAFURIKO MTWARA

> Wananchi wa vitongoji vya Migombani-Mbuyuni na Mchangani wamelazimika kuyahama makazi yao kufuatia kufurika kwa maji ktk Mto Ruvuma

> Kumetokea uharibifu wa zaidi ya Ekari 3,014 za Mpunga na Mahindi

Soma - https://jamii.app/Kaya2086MafurikoMTR
ARUSHA: MKURUGENZI WA KAMPUNI YA OBC AFIKISHWA MAHAKAMANI

> Siku 3 zilizopita Serikali iliagiza kukamatwa kwa ndugu, Isack Mollel(59) Mkurugenzi wa Ortello Business Cooperation, kwa tuhuma za kuajiri Wafanyakazi 10 wa kigeni bila vibali

Soma => https://jamii.app/MkurugenziOBCMahakamani