JamiiForums
52.8K subscribers
34.4K photos
2.44K videos
31.3K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
DR-CONGO YAANZA KUTOA CHANJO YA CORONA

> Taifa hilo limepokea Dozi Milioni 1.7 za Chanjo ya #AstraZeneca na wameanza kutoa kwa hiari kwa raia

> Awali utoaji chanjo hiyo ulisitishwa baada ya mataifa mengine kushuku usalama na ufanisi wake

Soma https://jamii.app/ChanjoDRC
RC CHALAMILA: MNAOMUONGELEA VIBAYA MAGUFULI WAKATI HAYUPO, MNATUCHOSHA AKILI

- Asema kuna Watu wameacha kufanya kazi wanakaa ili kumjadili Hayati Dkt. John Magufuli

- Asema kama wanaongea yenye maana ilifaa wafikishe ujumbe wakati akiwa hai

Soma https://jamii.app/ChalamilaSemaMagu
TIGO NA ZANTEL ZAUZWA KWA KAMPUNI YA MADAGASCAR

> Millicom International inayomiliki Tigo na Zantel, imetia saini ya kuuza biashara zake kwa Kampuni ya Axian Group

> Wateja wamehakikishiwa hakutakuwa na mabadiliko katika utoaji huduma

Soma - https://jamii.app/MilicomYauzaKampuni
RAIS SAMIA ATEUA VIONGOZI DIT, NACTE, COSTECH, DMI, TLSB, TAEC, TAFORI NA BODI YA MAABARA

- Dkt. Richard Masika anakuwa M/kiti wa Baraza la Taasisi ya Teknolojia(DIT)

- Prof. Joseph Msambichaka ni M/kiti wa Bodi ya Tume ya Nguvu za Atomiki (TAEC)

Soma - https://jamii.app/UteuziDIT
KENYA: WATU MILIONI 1.4 WAKABILIWA NA NJAA

> Shirika la Msalaba Mwekundu limebainisha Watoto 400,000 wasio na lishe bora wanahitaji msaada wa dharura

> Hali ya njaa inaweza kusababisha mapigano kugombea rasilimali finyu zilizopo

Soma - https://jamii.app/NjaaaKenya
MDAU ASHAURI WANAUME KUTOKUWA NA BAADHI YA TABIA

> Mdau ameshauri Mwanaume kutotumia maneno kama ‘Xaxa’, 'Jomoni' au kutumia emoji za kuona aibu kwa Mwanaume mwenzako

> Je, ni vitu gani zaidi Mwanaume asifanye kwa Mwanaume mwenzake?

Soma https://jamii.app/TabiaZaKiume
BURUDANI: MUIGIZAJI GANI HUCHOKI KUANGALIA FILAMU ZAKE?

> Muigizaji nyota anaweza kutoa filamu mbovu na isiyofanya vizuri sokoni lakini bado watakuwepo watakaoifurahia

> Je unampenda muigizaji gani ambaye utaangalia filamu yake hata kama ni mbaya?

Soma https://jamii.app/FavoriteActors
URUSI YAMPELEKA ALEXEI HOSPITALI BAADA YA MASHINIKIZO

- Kiongozi Mkuu wa Upinzani Nchini Urusi, Alexei Navalny amepelekwa Hospitali ya Wafungwa siku ya 20 tangu alipogoma kula

- Wafuasi wake wamepanga maandamano siku ya kesho (Aprili 21)

Soma - https://jamii.app/AlexeiHospital
TANGA: WALIMU WANNE WANAISHI NYUMBA MOJA KUTOKANA NA NYUMBA KUEZULIWA NA UPEPO

> Shule ya Msingi Mandera iliyopo Mswaha, Wilayani Korogwe ina uchakavu mkubwa Vyumba vya Madarasa na Nyumba za Walimu hali inayowatia hofu walimu

Soma https://jamii.app/ChakavuMandera
WAFUGAJI WATAHADHARISHWA KUHUSU DAWA FEKI YA MIFUGO

> Ni Dawa ya Alben Blue 2.5% toleo Na. 019394 lililotengenezwa Novemba 2019 na mwisho wa matumizi Oktoba mwaka 2022

> TMDA imesema Dawa hiyo ya Mifugo imebainika haina viambata hai

Soma - https://jamii.app/MifugoDawa
#MAREKANI: ALIYEWAHI KUWA MAKAMU WA RAIS AFARIKI DUNIA

> Walter F. Mondale amefariki akiwa na miaka 93. Alikuwa Makamu wa Rais Jimmy Carter kuanzia 1977-1981

> Alishindwa kupata Urais 1984, lakini aliweka rekodi ya kuwa na Mgombea Mwenza Mwanamke

Soma - https://jamii.app/MakamuMarekani
UTAFITI-MAREKANI: MTU 1 KATI YA 4 ANAFIKIRIA KUACHA KAZI BAADA YA #COVID19

- 80% wataacha kazi kwa sababu wana wasiwasi juu ya maendeleo ya taaluma zao

- Wengine Corona imesababisha wajifunze ujuzi na ustadi mpya ili kupata kazi za aina nyingine

Soma - https://jamii.app/JobQuitCorona
WAZIRI UMMY AMSIMAMISHA KAZI MKURUGENZI WA SENGEREMA

- Waziri wa TAMISEMI amemsimamisha kazi Magesa Boniphace kuanzia leo baada ya kupokea malalamiko na tuhuma za Ubadhirifu wa fedha za Miradi ya Maendeleo kutoka kwa Wananchi na Mbunge wa Jimbo

Soma - https://jamii.app/DEDSengeremaOut
KENYA: WALIOMALIZA KIDATO CHA NNE WALALA NJE KUTOKANA NA ZUIO LA KUTEMBEA USIKU

> Wanafunzi waliotakiwa kurudi kwao wamelazimika kulala ktk Viwanja vya Uhuru vilivyopo Nairobi

> Muda wa kutotoka nje uliwakuta wakiwa hawajapata usafiri

Soma https://jamii.app/CurfewNairobi
KAJALA NA PAULA WAHOJIWA KUHUSU TUHUMA ZA KUSAMBAZA PICHA ZA UTUPU ZA HARMONIZE

> Kajala Masanja na mwanaye walikamatwa na Polisi Aprili 19 jioni walipowasili nchini wakitokea Dubai na walihojiwa kwa saa kadhaa. Wameachiwa kwa dhamana

Soma https://jamii.app/KajalaPaula
#JFBurudani
MHASIBU WA TPA KIGOMA AKAMATWA NA TAKUKURU KWA TUHUMA ZA UHUJUMU UCHUMI

> Madaraka Robert aliyekuwa anatafutwa na TAKUKURU tangu Agosti 2020 amekamatwa Nyasaka Mkoani Mwanza

> Anatuhumiwa kukwepa kodi zaidi ya Tsh. Milioni 153.5

Soma https://jamii.app/MhasibuTPAKigoma

#KemeaRushwa
RAIS WA CHAD AFARIKI BAADA YA KUTANGAZWA MSHINDI WA UCHAGUZI

- Jeshi Nchini #Chad limesema Rais Idriss Deby amefariki Dunia kutokana na majeraha aliyoyapata wakati akiwaongoza Wanajeshi wanaopambana na Waasi Kaskazini mwa Nchi hiyo

Soma - https://jamii.app/RIPIdrissDerby
WASHINGTON, USA: MAHAKAMA YAITUPILIA MBALI RUFAA YA FAMILIA YA VALAMBHIA DHIDI YA TANZANIA

> Familia ya Valambhia ilitaka kulipwa zaidi ya Tsh. bilioni 149 kwa madai ununuzi wa vifaa vya kijeshi kati ya Kampuni ya TEL na Tanzania miaka ya 1980

Soma https://jamii.app/WashngtonDC
KAPUFI: IDADI YA WATU SIO TATIZO BALI KUWA NA WATU WENGI AMBAO NI TEGEMEZI

- Mbunge wa Mpanda amesema "Idadi ya Wazalishaji ikiwa ndogo tutaishia kutamani kujenga Madarasa mengi, kuongeza madawati na kukimbizana kufanya mambo kwa zimamoto"

Tazama - https://youtu.be/fJ4JksrEedU
#JFLeo
UFUGAJI: SABABU ZA KUKU KUPUNGUZA UTAGAJI WA MAYAI (2)

- Upungufu wa virutubisho muhimu katika chakula cha Kuku wa Mayai husababisha kupungua kwa uzalishaji wa mayai

- Kupukutisha Manyoya: Katika kipindi hiki Kuku hupunguza au kusimamisha utagaji kwasababu hutumia Protini nyingi na nguvu kuotesha manyoya mapya

- Mtiririko wa utagaji wa Mayai kwa Kuku unaweza kuathiriwa na Joto katika mazingira. Kwa kawaida Kuku anahitaji Joto lisiwe chini ya 11°C lisiwe zaidi 28°C

Soma - https://jamii.app/MayaiKukuChini