JamiiForums
52.8K subscribers
34.4K photos
2.44K videos
31.3K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
ASASI ZA KIRAIA ZAIKUMBUSHA SERIKALI KUHUSU UTEKELEZAJI WA KATIBA MPYA

> Asasi za Kiraia nchini, zimeikumbusha Serikali kutimiza ahadi yake ya upatikanaji wa Katiba Mpya ya Jamhuri ya Muungano, kabla ya mwaka 2021

> Tanzania ilikubali kufanyia kazi mapendekezo 133 ya haki za binadamu ikiwemo Katiba Mpya, mbele ya mkutano wa nchi mwanachama wa Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa (UN) mwaka 2016

Soma - https://jamii.app/AZAKIKatibaMpya
MKURUGENZI AJENGA UKUMBI WA SHEREHE SHULENI, APEWA SAA 4 KUSITISHA UJENZI

> Waziri Mkuu ametoa muda wa saa 4 kwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Iringa awe ameandika barua ya kusitisha ujenzi wa ukumbi wa mikutano na sherehe katika eneo la shule ya msingi Gangilonga

> Amesema maeneo yote ya taasisi za elimu nchini hayaruhusiwi kujengwa miradi ambayo haihusiani na masuala ya elimu

Soma - https://jamii.app/UkumbiShereheShuleni
SERIKALI YAKIPA KIWANDA CHA DANGOTE SIKU 7

- Kimepewa muda huo kuwasilisha taarifa ya utendaji wake katika Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC)

- Waziri wa Uwekezaji, Angellah Kairuki amesema taarifa hizo hazijawasilishwa kwa miaka mitatu

Zaidi, soma https://jamii.app/SerikaliDangoteSiku7
YANGA YATOLEWA KATIKA MICHUANO YA LIGI YA MABINGWA AFRIKA

- Yanga imekubali kipigo cha goli 2-1 kutoka kwa Zesco United ya Nchini Zambia ktk mchezo wa marudiano

- Imetolewa kwa jumla ya goli 3-2 na sasa inaangukia kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho hatua ya mtoano
AZAM YATOLEWA KWENYE MICHUANO YA SHIRIKISHO AFRIKA

- Azam FC imekubali kipigo cha bao 1-0 ikiwa ugenini kutoka kwa klabu ya Triangle United

- Azam imeondoshwa kwenye Michuano hiyo kwa jumla ya goli 2-0 kufuatia kupoteza 1-0 nyumbani
MLIMA KILIMANJARO: MTALII AFARIKI BAADA YA PARACHUTI KUGOMA KUFUNGUKA

- Raia wa Canada, Justin Kyllo (51), amefariki baada ya parachuti alilokuwa akitumia kuruka kutoka kilele cha Mlima Kilimanjaro Mkoani Kilimanjaro kugoma kufunguka

Zaidi, soma https://jamii.app/MtaliiAfarikiKLM
MAREKANI YAWATAHADHARISHA RAIA WAKE WANAOTAKA KUJA TANZANIA

- Yadai kuna ongezeko la Uhalifu, tishio la Ugaidi na sintofahamu ktk Masuala ya Afya

- Yadai unyanyasaji wa kijinsia & uporaji ni kawaida na Polisi wanaweza kukosa rasilimali za kupambana

Zaidi, soma https://jamii.app/USTravelAdvisory-TZ
BUTIKU: TANZANIA SIO YA VYAMA BALI YA WATANZANIA, TUFUATE MISINGI YA KATIBA
-
Joseph Butiku, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Mwl. Nyerere, amevitaka vyama vya siasa kufuata misingi ya Katiba ili kuirudisha nchi kwenye mstari ulionyooka

> Amesema Taifa limetetereka katika kutumia Katiba na Sheria na ndio maana tulipojitahidi kurekebishika ilikua ngumu

Soma - https://jamii.app/ButikuKatibaSheria
YEMEN: WAASI WA HOUTHI WADAI KUWAKAMATA WANAJESHI WA SAUDI ARABIA

- Wanadai wamekamata Wanajeshi hao baada ya shambulio kubwa karibu na mpaka kati ya mataifa hayo

- Wamesema wote waliokamatwa wataoneshwa hadharani leo katika chaneli yao

Zaidi, soma https://jamii.app/WahouthiWanajesgiSaudia
TABORA: ABIRIA WABAINI GARI KUWA NA KUNGUNI, WAGOMA KUSAFIRI

- Abiria waliokuwa wakisafiri na basi la Arizona kutoka Kigoma kwenda Dar, wamegoma kuendelea na safari baada ya kufika Tabora na kubaini uwepo wa Kunguni katika viti vya basi hilo

Zaidi, soma https://jamii.app/KunguniBasiArizona
ITALIA: MBARONI AKIDAIWA KUTUMIA BANGI KAMA KIUNGO CHA CHAKULA

- Mpishi wa hotelini, Carmelo Chiaramonte amekamatwa na Polisi baada ya kukutwa na bangi nyumbani kwake

- Amekutwa na mvinyo uliochanganywa na bangi, zaituni, kahawa, na samaki

Zaidi, soma https://jamii.app/MpishiMbaroniBangi
CHINA YAGUNDUA ENEO LENYE TANI BILIONI 1 ZA MAFUTA

> Shirika la Mafuta la China (CNPC) limefanya utafiti na kugundua hifadhi mpya ya gesi na mafuta yenye tani bilioni 1 za mafuta katika eneo la Kaskazini Magharibi mwa China

> Jumla ya tani 640,000 za mafuta zinatarajiwa kuzalishwa ktk eneo hilo kwa mwaka huu, na litafikia tani milioni 3 kwa mwaka siku zijazo

Soma - https://jamii.app/DiscoverOilDeposit
RAIS MAGUFULI KUPOKEA TAARIFA YA WAHUJUMU UCHUMI KUOMBA MSAMAHA

> Leo, Rais John Magufuli anatarajiwa kupokea taarifa ya utekelezaji wa ushauri alioutoa wa kuwasamehe watuhumiwa wa Uhujumu Uchumi walio tayari kutubu na kurejesha fedha na mali walizotafuna

> Mkurugenzi wa Mashitaka Nchini (DPP) ndiye atakayewasilisha taarifa hiyo

Soma - https://jamii.app/RipotiMsamahaWahujumu
UGANDA YAZINDUA KIPIMO CHA KUPIMA UKIMWI KWA MDOMO

> Kifaa hicho kimetengenezwa na ‘Orasure Technologies’ mahususi kwa vijana kuanzia miaka 18 hadi 24 na wafanyabiashara ya ngono

> Hakihusishi damu wakati wa upimaji bali kinahitaji mate ambayo kama mtu ameathirika na VVU yanakuwa na tishu ambazo kifaa cha kupimia kitazisoma

Soma - https://jamii.app/NewHIVTestKit
KENYA: TAKRIBANI WATU 3 WASADIKIWA KUFARIKI BAADA YA GARI KUZAMA BAHARINI

> Watu hao akiwemo mtoto mdogo wanasadikiwa kufariki baada ya gari walilokuwemo kuteleza kwa nyuma kutoka kwenye kivuko na kuzama majini Jumapili jioni katika eneo la Mombasa

> Shughuli za uokoaji zinaendelea

Soma - https://jamii.app/CarSlidoffFerry
MICHEZO: Bodi ya Wakurugenzi ya Klabu ya Simba imemteua Mtangazaji wa BBC, Salim Kikeke kuwa Balozi wa klabu hiyo mjini London, Uingereza

Amekabidhiwa jezi na Mwekezaji na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa timu hiyo, Mohammed Dewji
SAUDI ARABIA: KITUO CHA TRENI YA MWENDOKASI CHA AL-HARAMAIN CHAUNGUA MOTO

> Kituo hicho kinaunganisha Miji Mitakatifu ya Mecca na Medina pamoja na mji wa Jeddah kwenye Bahari ya Shamu

> Takriban watu 5 wamejeruhiwa ktk ajali hiyo na Serikali imesitisha safari za Treni mpaka taarifa zaidi zitakapotolewa

Soma - https://jamii.app/FireBreaksoutAl-Haramain
UPDATE: AJALI YA GARI KUZAMA BAHARINI KUTOKA KWENYE KIVUKO

- Mariam Kigenda(35) na mwanae(4) wamefariki baada ya gari lao kuteleza kutoka kwenye kivuko na kuzama baharini katika Feri ya Likoni

- Walikuwa ndani ya gari hilo wakati wakivuka bahari kwa kutumia kivuko cha MV Harambee

Zaidi, soma https://jamii.app/CarSlidoffFerry
IRINGA: VIONGOZI WA KAMATI YA MAJI KUWEKWA RUMANDE KWA UBADHIRIFU

> Waziri Mkuu ameagiza kukamatwa na kuwekwa ndani Viongozi wa Kamati ya Watumiaji Maji wa Mradi wa Matunguru Tungamalenga kwa tuhuma za ubadhirifu wa Tsh. milioni 7

> Ni baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa wananchi

Soma - https://jamii.app/KamatiMajiUbadhirifu
NAMNA YA KUPANGILIA MFUMO WA ULAJI BORA KWA AFYA THABITI

> Mlo kamili hutokana na kuchanganya angalau chakula kimoja kutoka katika kila kundi la vyakula na viliwe kwa kiasi cha kutosha

> Ulaji wa mbogamboga na matunda husaidia kuimarisha mfumo wa kinga mwilini na kujikinga na maradhi mbalimbali

> Epuka vyakula vyenye mafuta mengi kwani husababisha madhara kama vile unene kupita kiasi, magonjwa ya moyo, kisukari na shinikizo la damu

Zaidi, soma - https://jamii.app/AfyaUlajiBora
#JFAfya
CHINA: MOTO WALIPUKA KWENYE KIWANDA NA KUUA WATU 19 NA KUJERUHI WENGINE 9

> Moto ulilipuka kwenye kiwanda kimoja kilichopo Mashariki mwa nchi ya China katika Jimbo la Ninghai

> Majeruhi wamekimbizwa Hospitali kwa ajili ya matibabu na uangalizi

Soma > https://jamii.app/MotoKiwandaChina