JamiiForums
33.8K subscribers
37.4K photos
2.98K videos
32.9K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
Mdau ametoa wito kwa mamlaka husika kuondoa vifusi vilivyotelekezwa kwenye barabara ya Tegeta kwa Ndevu tangu Desemba 2025 na kuachwa hadi sasa kwani vimekuwa kero kwa watumiaji wa barabara hiyo.

Zaidi tembelea https://jamii.app/BarabaraTegeta

#JamiiForums #Uwajibikaji #JFMdau2026
DAR: Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP), Faustine Mafwele ni miongoni mwa Mashahidi 43 wanaotarajiwa kutoa ushahidi katika kesi ya askari wanaotuhumiwa kughushi vibali vya kumiliki silaha.

Kesi hiyo inawakabili Watu tisa, wakiwemo maofisa sita wa Jeshi la Polisi, inasikilizwa na Hakimu Mwandamizi, Geofrey Mhini, na inatarajia kuanza kusikilizwa Aprili 2026.

Bofya kusoma zaidi https://jamii.app/MafweleUshahidi

#JamiiForums #JFSheria
1
Mdau umewahi kukosa uhuru wa kununua bidhaa Duka la Dawa sababu ya kukuta Watu wanapiga soga na mhusika au wahusika? Tuambie ilikuaje...

Zaidi tembelea https://jamii.app/DukaDawaHuduma

#JamiiForums #JFMdau2026 #JFHuduma
👍1
Machi 18, 2026: Moja kati ya mijadala mingi inayoendelea ndani ya JamiiForums.com wakati huu📌📌

Kufuatilia zaidi tembelea https://jamii.app/SenegalNoUbingwa

#JamiiForums #JFSports
Mdau ni methali au msemo gani ungeutumia kufanya maamuzi?

Kwa mijadala mingi yenye tija tembelea JamiiForums.com

#JamiiForums #GoodMorningWithJF #MorningPost
Mdau wa JamiiForums.com ametoa wito kwa mamlaka kurekebisha na kuziba dimbwi kubwa la maji liliopo Mbande hadi Kisewe Stendi, eneo la Kituo cha Polisi kwani limekuwa likichangia kuharibu vyombo vya usafiri vinavyopita eneo hilo na kuwa kero kwa wananchi wanaotumia barabara hiyo.

Zaidi tembelea https://jamii.app/KeroMbande

#JamiiForums #JFMdau2026 #Uwajibikaji

Nawe pia unaweza kuwasilisha Kero yako kupitia FichuaUovu ndani ya JamiiForums.com📌📌
SENEGAL: Shirikisho la Soka la Senegal (#FSF) limethibitisha kupokea uamuzi uliotolewa na Kamati ya Rufaa ya Shirikisho la Soka Afrika (#CAF) kuhusu kupokwa ubingwa wa Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2025.

Bofya https://jamii.app/SenegalRufaa

#JamiiForums #JFSports #AFCON2025