Kila Juni 13, ni Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Uelewa kuhusu Ualbino.
Mwaka huu 2025 Kaulimbiu inaangazia umuhimu wa kuzuia Saratani ya Ngozi kwa Watu wenye Ulemavu wa Ngozi (Ualbino) kupitia uelimishaji, uchunguzi wa afya na upatikanaji wa Mafuta ya kuzuia Mionzi ya Jua (Sunscreen)
Ukosefu wa upatikanaji wa mafuta maalum ya ngozi, mavazi ya kujikinga na jua, pamoja na huduma za uchunguzi na matibabu ya Saratani ya Ngozi, unasababisha vifo vinavyoweza kuzuilika kabisa
Soma https://jamii.app/AlbinismAwareness
#JamiiForums #JamiiAfrica #AlbinismAwarenessDay
Mwaka huu 2025 Kaulimbiu inaangazia umuhimu wa kuzuia Saratani ya Ngozi kwa Watu wenye Ulemavu wa Ngozi (Ualbino) kupitia uelimishaji, uchunguzi wa afya na upatikanaji wa Mafuta ya kuzuia Mionzi ya Jua (Sunscreen)
Ukosefu wa upatikanaji wa mafuta maalum ya ngozi, mavazi ya kujikinga na jua, pamoja na huduma za uchunguzi na matibabu ya Saratani ya Ngozi, unasababisha vifo vinavyoweza kuzuilika kabisa
Soma https://jamii.app/AlbinismAwareness
#JamiiForums #JamiiAfrica #AlbinismAwarenessDay
❤1
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
DODOMA: Akisoma majibu ya barua yao ya Rufaa yaliyotumwa kwao Juni 6, 2025 kutoka Ofisi ya Wizara ya Mambo ya Ndani, Wakili Peter Kibatala ametoa maelezo akisema barua iliyotumika kulifungia Kanisa la Glory of Christ Tanzania Church maarufu kwa jina la Kanisa la Ufufuo na Uzima haitambuliki na Mamlaka iliyotajwa kulifungia
Ameyazungumza hayo leo Juni 13, 2025 baada ya kutoka katika Mahakama Kuu Kanda ya Dodoma kwenye kesi ya kupinga kufutwa kwa kanisa hilo, ambapo upande wa Kanisa ukiwakilishwa na Wakili Kibatala unaiomba Mahakama kutoa amri ya muda itakayoruhusu kuendelea kwa ibada na shughuli nyingine za kidini
Soma https://jamii.app/KanisaLaGwajima
#JamiiForums #JFMatukio
Ameyazungumza hayo leo Juni 13, 2025 baada ya kutoka katika Mahakama Kuu Kanda ya Dodoma kwenye kesi ya kupinga kufutwa kwa kanisa hilo, ambapo upande wa Kanisa ukiwakilishwa na Wakili Kibatala unaiomba Mahakama kutoa amri ya muda itakayoruhusu kuendelea kwa ibada na shughuli nyingine za kidini
Soma https://jamii.app/KanisaLaGwajima
#JamiiForums #JFMatukio
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
DODOMA: Naibu Katibu wa Kanisa la Glory of Christ Tanzania Church, Askofu Maximilian Machumu “Mwanamapinduzi” amesema taarifa kuwa Msajili wa Jumuiya za Kiraia, Emmanuel Kihampa amefungia Kanisa lao si za kweli bali lililofungiwa ni Kanisa la Glory of Christ Church ambalo halina uhusiano na Kanisa lao
Ikumbukwe, Juni 2, 2025 ilisambaa barua iliyoonesha imetoka kwa Kihampa akifungia Kanisa hilo linaloongozwa na Askofu Josephat Gwajima lakini Wanasheria wakiongozwa na Wakili Peter Kibatala wamesema majina ya Kanisa hayaendani na jina sahihi la Wateja wake (Kanisa la Glory of Christ Tanzania Church)
Soma https://jamii.app/AskofuMaximilianMachumu
#JFMatukio #JamiiForums
Ikumbukwe, Juni 2, 2025 ilisambaa barua iliyoonesha imetoka kwa Kihampa akifungia Kanisa hilo linaloongozwa na Askofu Josephat Gwajima lakini Wanasheria wakiongozwa na Wakili Peter Kibatala wamesema majina ya Kanisa hayaendani na jina sahihi la Wateja wake (Kanisa la Glory of Christ Tanzania Church)
Soma https://jamii.app/AskofuMaximilianMachumu
#JFMatukio #JamiiForums
BAADA YA SAMIA KUKUTANA NA VIPNGOZI WA YANGA, SIMBA; VIONGOZI TPLB WAJIUZULU
Baada ya mgogoro wa muda mrefu kuhusu Yanga na Simba kucheza mchezo wa Ligi Kuu, Mwenyekiti wa Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB), Steven Mnguto amewasilisha barua ya kujiuzulu huku Rais wa #TFF, Wallace Karia akimsimamisha Kazi Afisa Mtendaji Mkuu wa #TPLB, Almasi Kasongo
Haya yametokea ikiwa ni saa chache baada ya Rais Samia kufanya mazungumzo na Viongozi wa Klabu za #Simba na #Yanga na kisha taarifa kutoka kuwa mchezo huo uliokuwa uchezwe Juni 15, 2025 umeahirishwa hadi Juni 25, 2025
Soma https://jamii.app/TPLB_Wajiuzulu
#JamiiAfrica #JFSports
Baada ya mgogoro wa muda mrefu kuhusu Yanga na Simba kucheza mchezo wa Ligi Kuu, Mwenyekiti wa Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB), Steven Mnguto amewasilisha barua ya kujiuzulu huku Rais wa #TFF, Wallace Karia akimsimamisha Kazi Afisa Mtendaji Mkuu wa #TPLB, Almasi Kasongo
Haya yametokea ikiwa ni saa chache baada ya Rais Samia kufanya mazungumzo na Viongozi wa Klabu za #Simba na #Yanga na kisha taarifa kutoka kuwa mchezo huo uliokuwa uchezwe Juni 15, 2025 umeahirishwa hadi Juni 25, 2025
Soma https://jamii.app/TPLB_Wajiuzulu
#JamiiAfrica #JFSports
❤1
Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Askofu Wolfgang Pisa, akizungumza wakati wa Ibada, Juni 3, 2025 alisema “Tuwe Wazalendo wa kuishi kwa Amani, tulijenge Kanisa na Taifa letu kwani ni vitu viwili ambavyo haviwezi kutengana.”
Soma https://jamii.app/AskofuWolfgangPisa
#JamiiForums #JamiiAfrica #Quotes #JFNukuu
Soma https://jamii.app/AskofuWolfgangPisa
#JamiiForums #JamiiAfrica #Quotes #JFNukuu
❤4
Mdau wa JamiiForums.com anaeleza kuwa licha ya Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini (#RITA) kuweka tangazo Mtandaoni kuwa Kituo cha Miito (CALL CENTER) kipo wazi Saa 2 Asubuhi hadi Saa 10 Jioni lakini simu yao 0800 117 482 haipokelewi na kuna muda inakatwa
Anaeleza lengo la RITA kuwa na Huduma nyingi Mtandaoni ni kusogeza Huduma karibu na Wananchi, lakini ni kawaida kuona malalamiko ya maombi kufanyiwa kazi kwa muda mrefu, akitoa mfano Kusajili Cheti inaweza kuchukua hadi Miezi Miwili ‘Account Status’ haibadiliki
Soma https://jamii.app/HudumaRITA
#JamiiForums #HudumaZaKijamii #JamiiAfrica #Uwajibikaji #Accountability #JFMdau2025
Anaeleza lengo la RITA kuwa na Huduma nyingi Mtandaoni ni kusogeza Huduma karibu na Wananchi, lakini ni kawaida kuona malalamiko ya maombi kufanyiwa kazi kwa muda mrefu, akitoa mfano Kusajili Cheti inaweza kuchukua hadi Miezi Miwili ‘Account Status’ haibadiliki
Soma https://jamii.app/HudumaRITA
#JamiiForums #HudumaZaKijamii #JamiiAfrica #Uwajibikaji #Accountability #JFMdau2025
❤1
Ushiriki wako kama kijana katika mchakato wa maamuzi, kuanzia ngazi ya familia, jamii hadi taifa ni njia ya kuhakikisha kuwa maamuzi yanayoathiri maisha yako yanazingatia mahitaji na sauti yako
Shiriki kwenye midahalo, mikutano ya kijamii na michakato ya Kidemokrasia, uweze kuchangia mawazo, kuchochea mjadala na kushinikiza mabadiliko ya Sera kwa maslahi ya wengi
Zaidi soma https://jamii.app/VijanaUshiriki
#JamiiAfrica #JamiiForums #JFVijana #RestlessDevelopment #UshirikiWaVijana
Shiriki kwenye midahalo, mikutano ya kijamii na michakato ya Kidemokrasia, uweze kuchangia mawazo, kuchochea mjadala na kushinikiza mabadiliko ya Sera kwa maslahi ya wengi
Zaidi soma https://jamii.app/VijanaUshiriki
#JamiiAfrica #JamiiForums #JFVijana #RestlessDevelopment #UshirikiWaVijana
Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limesema “Ni kweli Kituo cha Kupoza Umeme cha llamilo (Simiyu) kimechelewa Utekelezaji wake kutokana na sababu za Kiutendaji na kwamba Mkandarasi wa Ujenzi ameshapatikana, na Utekelezaji utaendelea ili kuimarisha hali ya upatikanaji wa Umeme.”
Ufafanuzi huo umetolewa baada ya Mdau kueleza licha ya Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani, kuweka jiwe la msingi la Mradi Machi 2021 na kuahidi Unenzi kukamilika baada ya Mwaka mmoja lakini sasa inaelekea Miaka mitano hakuna kilichofanyika, changamoto ya kukatika umeme mara kwa mara ipo vilevile, akahoji, kama Wananchi walidanganywa?
Taarifa ya #TANESCO imeongeza kuwa “Serikali kupitia Wizara ya Nishati na TANESCO tutahakikisha tunakamilisha kwa awamu ujenzi wa Miradi yote ya Gridi Imara iliyopangwa kama ilivyokusudiwa katika maeneo yote nchini.”
Soma https://jamii.app/UmemeSimiyuMradi
#Governance #Accountability #Transparency #JamiiAfrica #Uwajibikaji #ServiceDelivery #JamiiForums #JFMdau2025
Ufafanuzi huo umetolewa baada ya Mdau kueleza licha ya Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani, kuweka jiwe la msingi la Mradi Machi 2021 na kuahidi Unenzi kukamilika baada ya Mwaka mmoja lakini sasa inaelekea Miaka mitano hakuna kilichofanyika, changamoto ya kukatika umeme mara kwa mara ipo vilevile, akahoji, kama Wananchi walidanganywa?
Taarifa ya #TANESCO imeongeza kuwa “Serikali kupitia Wizara ya Nishati na TANESCO tutahakikisha tunakamilisha kwa awamu ujenzi wa Miradi yote ya Gridi Imara iliyopangwa kama ilivyokusudiwa katika maeneo yote nchini.”
Soma https://jamii.app/UmemeSimiyuMradi
#Governance #Accountability #Transparency #JamiiAfrica #Uwajibikaji #ServiceDelivery #JamiiForums #JFMdau2025
❤2
DIGITALI: Wadukuaji wamekuja na mtindo mpya wa kusambaza Kiunganishi (Link) zitakazofanya udukuliwe taarifa zako utakapobofya link hiyo
Wadukuzi hao hujifanya wana picha zako hivyo hukuambia ubofye link ili kupata picha na ukibofya utatakiwa kuingiza taarifa zako kama Namba ya Simu
Ukipata ujumbe huo usifungue ili kuepusha kudukuliwa
Soma https://jamii.app/UsifungueUjumbeHuu
#JamiiForums #JamiiAfrica #JFDigitali #Accountability #Uwajibikaji
Wadukuzi hao hujifanya wana picha zako hivyo hukuambia ubofye link ili kupata picha na ukibofya utatakiwa kuingiza taarifa zako kama Namba ya Simu
Ukipata ujumbe huo usifungue ili kuepusha kudukuliwa
Soma https://jamii.app/UsifungueUjumbeHuu
#JamiiForums #JamiiAfrica #JFDigitali #Accountability #Uwajibikaji
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
PWANI: Siku moja baada ya Naibu Katibu Mkuu wa Kanisa la Glory of Christ Tanzania Church (Nyumba ya Ufufuo na Uzima), Askofu Maximilian Machumu (Mwanamapinduzi) kutangaza kuwa Kanisa lao halijafungwa na Serikali, Tawi la Kanisa hilo la Kibaha limefungwa na Watu wanaodhaniwa kuwa ni Askari Polisi kwa kuweka utepe na kuwataka Waumini waliokuwemo kuondoka
Kupitia ukurasa wake wa Mtandao wa X (Twitter), Mwanamapinduzi ameonesha Video na kuandika kuwa Jeshi la Polisi limefunga Kanisa hilo
Ikumbukwe, Juni 2, 2025 ilisambaa barua iliyoonesha Msajili wa Jumuiya ya Kiraia amelifungia Kanisa linaloongozwa na Askofu Josephat Gwajima lakini Wanasheria wakiongozwa na Wakili Peter Kibatala wamesema majina ya Kanisa hayaendani na jina sahihi la Mteja wake (Kanisa la Glory of Christ Tanzania Church)
Soma https://jamii.app/KanisaKibaha
#JamiiForums #JFMatukio #JamiiAfrica
Kupitia ukurasa wake wa Mtandao wa X (Twitter), Mwanamapinduzi ameonesha Video na kuandika kuwa Jeshi la Polisi limefunga Kanisa hilo
Ikumbukwe, Juni 2, 2025 ilisambaa barua iliyoonesha Msajili wa Jumuiya ya Kiraia amelifungia Kanisa linaloongozwa na Askofu Josephat Gwajima lakini Wanasheria wakiongozwa na Wakili Peter Kibatala wamesema majina ya Kanisa hayaendani na jina sahihi la Mteja wake (Kanisa la Glory of Christ Tanzania Church)
Soma https://jamii.app/KanisaKibaha
#JamiiForums #JFMatukio #JamiiAfrica
Mdau anaeleza hoja ya Watoto wa Shule kupumzika wakati wa likizo ilishatolewa maelekezo na Waziri wa Elimu kupitia kwa Kamishna wa Elimu kuwa mwongozo uliopo wakati wa likizo ni marufuku Watoto kwenda Shuleni kufundishwa
Anakumbushia tukio la hivi karibuni la Mwanafunzi kuchoma Moto majengo ya Shule ya Sekondari Jenista Mhagama (Songea), alipoulizwa alisema alitaka Shule ifungwe ili aende likizo, akisema ingawa njia hiyo si sahihi lakini ni ujumbe kuwa Wanafunzi wanatakiwa kupata Haki ya kupumzika
Mdau anadai alitegemea Waziri wa Elimu angetoa tamko haraka lakini anaona kimya, hivyo anahoji wanaosimamia Sekta ya Elimu ni wasomi, je, hawaoni umuhimu wa kupumzika? Hawajui kufanya hivyo ni mateso kwa Watoto? Hawajui Mtoto ana haki ya kupumzika, kujichanganya na Jamii na kucheza?
Soma https://jamii.app/LikizoKwaWanafunzi
#Elimu #Accountability #JamiiAfrica #Uwajibikaji #JamiiForums #Governance
Anakumbushia tukio la hivi karibuni la Mwanafunzi kuchoma Moto majengo ya Shule ya Sekondari Jenista Mhagama (Songea), alipoulizwa alisema alitaka Shule ifungwe ili aende likizo, akisema ingawa njia hiyo si sahihi lakini ni ujumbe kuwa Wanafunzi wanatakiwa kupata Haki ya kupumzika
Mdau anadai alitegemea Waziri wa Elimu angetoa tamko haraka lakini anaona kimya, hivyo anahoji wanaosimamia Sekta ya Elimu ni wasomi, je, hawaoni umuhimu wa kupumzika? Hawajui kufanya hivyo ni mateso kwa Watoto? Hawajui Mtoto ana haki ya kupumzika, kujichanganya na Jamii na kucheza?
Soma https://jamii.app/LikizoKwaWanafunzi
#Elimu #Accountability #JamiiAfrica #Uwajibikaji #JamiiForums #Governance
❤1👍1
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
RUVUMA: Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Stephen Wasira, amesema uwepo wa #Demokrasia na Uhuru wa kutoa maoni sio ruhusa ya kuvunja Sheria, kutukana Watu na anayefanya hivyo anastahili kuchukuliwa hatua
Wasira ameeleza hayo Juni 12, 2025 alipokuwa akizungumza na Viongozi wa CCM katika Jimbo la Peramiho, Wilayani Songea
Soma https://jamii.app/WasiraRuvuma
#JamiiForums #Democracy #Kuelekea2025 #Siasa #UchaguziMkuu2025
Wasira ameeleza hayo Juni 12, 2025 alipokuwa akizungumza na Viongozi wa CCM katika Jimbo la Peramiho, Wilayani Songea
Soma https://jamii.app/WasiraRuvuma
#JamiiForums #Democracy #Kuelekea2025 #Siasa #UchaguziMkuu2025
❤2
Kila mtu ana ndoto au mawazo ya mafanikio, lakini ni wachache sana wanaochukua hatua ya kweli kuyafanikisha
Tofauti kati ya waliofanikiwa na waliokwama ni hii: Wale wachache (1%) hawakai kungoja muda mzuri wanachukua hatua mara moja
Kuwa mmoja wa wanaochukua hatua
#JamiiAfrica #JamiiForums #Maisha #GoodMorning #AmkaNaJF
Tofauti kati ya waliofanikiwa na waliokwama ni hii: Wale wachache (1%) hawakai kungoja muda mzuri wanachukua hatua mara moja
Kuwa mmoja wa wanaochukua hatua
#JamiiAfrica #JamiiForums #Maisha #GoodMorning #AmkaNaJF
DAR: Kanisa la Glory of Christ Tanzania Church (Nyumba ya Ufufuo na Uzima) lililopo eneo la Ubungo limewekwa ulinzi mkali na Askari Polisi leo Juni 15, 2025 huku njia zote zinazowezesha Watu kufika kwenye kanisa hilo zikiwa zimezuiwa
Aidha, licha ya Askari hao kuwepo eneo hilo baadhi ya Waumini wamejitokeza maeneo ya karibu na kanisa hilo
Ikumbukwe Juni 13, 2025, Naibu Katibu wa Kanisa hilo, Askofu Maximilian Machumu (Mwanamapinduzi) alisema taarifa kuwa Msajili wa Jumuiya za Kiraia, Emmanuel Kihampa amefungia Kanisa lao, si za kweli bali lililofungiwa ni Kanisa la Glory of Christ Church ambalo halina uhusiano na Kanisa lao, hivyo Jumapili hii wanatarajia kurejea Kanisani kuendelea na Ibada
Soma https://jamii.app/KanisaUfufuoUlinziPolisi
#JamiiAfrica #JamiiForums #JFMatukio
Aidha, licha ya Askari hao kuwepo eneo hilo baadhi ya Waumini wamejitokeza maeneo ya karibu na kanisa hilo
Ikumbukwe Juni 13, 2025, Naibu Katibu wa Kanisa hilo, Askofu Maximilian Machumu (Mwanamapinduzi) alisema taarifa kuwa Msajili wa Jumuiya za Kiraia, Emmanuel Kihampa amefungia Kanisa lao, si za kweli bali lililofungiwa ni Kanisa la Glory of Christ Church ambalo halina uhusiano na Kanisa lao, hivyo Jumapili hii wanatarajia kurejea Kanisani kuendelea na Ibada
Soma https://jamii.app/KanisaUfufuoUlinziPolisi
#JamiiAfrica #JamiiForums #JFMatukio
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Baadhi ya Waumini wa Kanisa la Glory of Christ Tanzania (Kanisa la Ufufuo na Uzima) linaloongozwa na Askofu Josephat Gwajima ambalo Juni 2, 2025 lilifungiwa, wamejitokeza eneo la pembezoni mwa Kanisa hilo lililopo Ubungo wakipiga maombi huku Kanisa hilo likiwa limezungukwa na Askari Polisi
Juni 14, 2025, kupitia ukurasa wake wa Instagram, Askofu Gwajima alitangaza uwepo wa ibada leo Juni 15, 2025 eneo la Ubungo
Soma https://jamii.app/WauminiGwajimaWasaliNje
#JamiiAfrica #JamiiForums #JFMatukio
Juni 14, 2025, kupitia ukurasa wake wa Instagram, Askofu Gwajima alitangaza uwepo wa ibada leo Juni 15, 2025 eneo la Ubungo
Soma https://jamii.app/WauminiGwajimaWasaliNje
#JamiiAfrica #JamiiForums #JFMatukio
Ajira kwa Vijana ni nyenzo muhimu kwa maendeleo ya Mtu Binafsi, Jamii na Taifa kwa ujumla. Ajira humfanya mtu awe na ari ya kutosha, kuwajibika na kushiriki kikamilifu katika nyanja zote za Kijamii na Kiuchumi
Kwa mujibu wa Utafiti wa Nguvu Kazi (ILFS 2021), Tanzania, ilikuwa na nguvu kazi ya Watu wapatao 25,861,023 ambapo kati ya Nguvu kazi hiyo, Vijana ni 14,219,191 sawa na 55.6%.
Soma https://jamii.app/UwajibikajiWaVijana
#JamiiAfrica #JamiiForums #JFVijana #RestlessDevelopment #UshirikiWaVijana
Kwa mujibu wa Utafiti wa Nguvu Kazi (ILFS 2021), Tanzania, ilikuwa na nguvu kazi ya Watu wapatao 25,861,023 ambapo kati ya Nguvu kazi hiyo, Vijana ni 14,219,191 sawa na 55.6%.
Soma https://jamii.app/UwajibikajiWaVijana
#JamiiAfrica #JamiiForums #JFVijana #RestlessDevelopment #UshirikiWaVijana