JamiiForums
52.6K subscribers
34.4K photos
2.45K videos
31.4K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
Serikali imesema Tsh. Trilioni 1.58 zilitolewa katika ujenzi wa Barabara, Madaraja na Viwanja vya Ndege; Ujenzi na Ukarabati wa Miundombinu ya Reli ikiwemo Mradi wa ujenzi wa Reli ya Kiwango cha Kimataifa (SGR) Tsh. Trilioni 1.68

Aidha, Mradi wa Kufua Umeme katika Bwawa la Julius Nyerere (JNHPP) MW 2,115 na Mradi wa kusambaza Umeme Vijijini kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) zilitolewa Tsh. Bilioni 574.8; na Ujenzi na Ukarabati wa Viwanja vya Mpira kwa ajili ya Maandalizi ya AFCON 2027 Tsh. Bilioni 179.8

Soma https://jamii.app/BajetuKuu2025

#JamiiForums #JamiiAfrica #Accountability #BajetiKuu2025 #Governance #Uwajibikaji #Transparency
Serikali imesema Tsh. Bilioni 636.0 zimetolewa katika Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu na Vyuo vya Kati; Programu ya Elimu ya Msingi na Sekondari bila Ada Tsh. Bilioni 444.7

Waziri Mwigulu Nchemba amefafanua kuwa Miradi ya Maji Mijini na Vijijini Tsh. Bilioni 378.7; Ununuzi wa Dawa, Vifaa, Vifaa tiba na Vitendanishi kwa ajili ya Hospitali za Mikoa, Kanda na Rufaa Tsh. Bilioni 414.7; Ujenzi na Ukarabati wa Hospitali za Wilaya, Mikoa, Kanda na Rufaa Tsh. Bilioni 47.2; na Ujenzi wa Vituo vya Afya na Zahanati Tsh. Bilioni 7.3.

Soma https://jamii.app/BajetuKuu2025

#JamiiForums #JamiiAfrica #Accountability #BajetiKuu2025 #Governance #Uwajibikaji
1
Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba akisoma Bajeti Kuu Bungeni, amesema Hadi Aprili 2025, Deni la Serikali lilikuwa Tsh. Trilioni 107.70, ambapo kati ya kiasi hicho, Deni la nje ni Tsh. Trilioni 72.94 na Deni la ndani ni Tsh. Trilioni 34.76

Amesema, tathmini ya Uhimilivu wa Deni iliyofanyika Oktoba 2024 imeonesha kuwa deni ni Himilivu katika kipindi cha muda mfupi, wa kati na mrefu

Soma https://jamii.app/BajetuKuu2025

#JamiiForums #JamiiAfrica #Accountability #BajetiKuu2025 #Governance #Uwajibikaji
1
Serikali imesema Mwaka 1961 tulikuwa na Shule za Msingi 3,270, Walimu 9,885 na Wanafunzi 486,470. Shule za Sekondari 41, Walimu 764 na Wanafunzi 11,832. Vyuo vya Ualimu 8, Walimu 164, na Wanafunzi 1,723, Chuo kikuu kimoja, Wahadhiri 6 na Wanafunzi 14.

Hadi kufikia Mwaka 2024, Tanzania ilifikisha Shule za Msingi 20,533, Walimu 229,840 na Wanafunzi 11,391,185. Shule za Sekondari 6,269, Walimu 128,686 na Wanafunzi 3,314,198. Vyuo vya Ualimu 65, Walimu 1,633 na Wanafunzi 16,002, Vyuo Vikuu 79, Wahadhiri 8,625 na Wanafunzi 334,854

Serikali pia imeendelea kuongeza Vyumba vya Madarasa ya Elimu ya Msingi kutoka 128,425 Mwaka 2020 hadi Madarasa 155,330 Mwaka 2024 na Vyumba vya Madarasa ya Elimu ya Sekondari kutoka 46,928 Mwaka 2020 hadi 81,052 Mwaka 2024.

Soma https://jamii.app/BajetuKuu2025

#JamiiForums #JamiiAfrica #Accountability #BajetiKuu2025 #Governance #Uwajibikaji #Transparency
1👍1
Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba amesema "Kipindi cha Serikali ya Awamu ya 4 ulitokea uhalifu wenye sura ya Ugaidi uliohusisha urushwaji wa Mabomu kwenye Nyumba za Ibada, Mikusanyiko ya Watu na Mashambulizi ya Mtu mmoja mmoja wakiwemo Watu wenye Ulemavu wa Ngozi. Tumesahau hili? Vyombo vyetu vya Ulinzi na Usalama vilisimama imara na kukomesha Uhalifu huo”

Ameongeza "Kipindi cha Serikali ya Awamu ya 5, ulitokea uhalifu wa Watoto kutekwa na kuuwawa, Mtu mmoja mmoja kupigwa risasi kwenye makazi yake au katika Utekelezaji wa majukumu yake. Waliuawa Wenyeviti wa Vijiji, Vitongoji na Mitaa wanaotokana na CCM na tulishuhudia pia miili iliyokuwa kwenye Magunia na Mifuko ikiwa imetupwa Baharini. Na haya tumesahau? Vyombo vyetu vya Ulinzi na Usalama vilisimama imara na kukomesha Uhalifu huo.”

Soma https://jamii.app/BajetuKuu2025

#JamiiForums #JamiiAfrica #Accountability #BajetiKuu2025 #Governance #Uwajibikaji #Transparency
1
Serikali imesema Mafanikio makubwa yamepatikana ikiwemo kupandisha Vyeo Watumishi wa Umma 476,470 ambapo Jumla ya Tsh. Bilioni 689.9 zimetumika

Pia, kipindi cha kuanzia Mwaka 2021/22 hadi Mei 2025, Serikali imelipa madai ya malimbikizo ya Mishahara jumla ya Tsh. Bilioni 318.37 kwa Watumishi na Wastaafu 187,152.

Soma https://jamii.app/BajetuKuu2025

#JamiiForums #JamiiAfrica #Accountability #BajetiKuu2025 #Governance #Uwajibikaji #Transparency
Serikali imependekeza kutoza Ushuru wa bidhaa kwa kiwango cha Tsh. 50 kwa kilo ya 'crisps' zinazozalishwa Nchini, na Tsh. 100 kwa kilo ya 'crisps' zinazoingizwa kutoka nje ya Nchi

Akisoma Bajeti Kuu, Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba, amesema Lengo la hatua hii ni kupunguza athari za Kiafya ikiwemo ongezeko la uzito (Obesity) zinazotokana na matumizi ya bidhaa hizo na kuongeza Mapato ya Serikali. Hatua hii inatarajia kuongeza mapato ya Serikali kwa kiasi cha Tsh. Milioni 6,475;

Soma https://jamii.app/BajetuKuu2025

#JamiiForums #JamiiAfrica #Accountability #BajetiKuu2025 #Governance #Uwajibikaji #Transparency
Serikali imependekeza kupunguza kiwango cha Ushuru wa Bidhaa kwenye Vinywaji vya kuongeza nguvu (Energy drinks) vinavyozalishwa ndani ya Nchi kutoka Tsh. 561 kwa kila Lita hadi Tsh. 134.2 kwa kila lita

Waziri wa fedha, Mwigulu Nchemba amesema Lengo la hatua hii ni kuweka unafuu kwa Wazalishaji wa ndani, kuongeza Ushindani na kuchochea Uwekezaji Nchini. Hatua hii inatarajia kupunguza mapato ya Serikali kwa kiasi cha Tsh. Milioni 170.2

Soma https://jamii.app/BajetuKuu2025

#JamiiForums #JamiiAfrica #Accountability #BajetiKuu2025 #Governance #Uwajibikaji #Transparency
1
Serikali imependekeza kutoza ushuru wa bidhaa kwa kiwango 5% kwa Soseji na bidhaa zingine zinazofanana na hizo zinazozalishwa Nchini, na 10% kwa zile zinazoingizwa kutoka nje ya Nchi

Waziri Mwigulu Nchemba, amesema lengo ni kuongeza mapato ya Serikali, kuvutia Uwekezaji Nchini na kulinda Wazalishaji wa ndani. Hatua hii inatarajia kuongeza mapato ya Serikali kwa kiasi cha Tsh. Milioni 2,413.9

Pia imependekeza kutoza ushuru wa bidhaa kwa kiwango cha 10% kwenye sabuni zinazoingizwa kutoka nje ya Nchi, Lengo likiwa kulinda Wazalishaji wa ndani na kuongeza Ajira, hatua hii inatarajia kuongeza mapato ya Serikali kwa Tsh. Milioni 143,395.8

Soma https://jamii.app/BajetuKuu2025

#JamiiForums #JamiiAfrica #Accountability #BajetiKuu2025 #Governance #Uwajibikaji #Transparency
Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba amependekeza kufanya marekebisho kwenye Sheria ya Kodi ya Mapato, Kutoza kodi ya zuio kwa kiwango cha 10% kwenye malipo ya Kamisheni inayotokana na matangazo ya Michezo ya kubahatisha

Amesema Kodi hii itakuwa ni kodi ya mwisho (final), lengo la hatua hii ni kuendana na Kanuni za usawa za utozaji kodi na kupanua wigo wa kodi, na hatua hii inatarajia kuongeza mapato ya Serikali kwa kiasi cha Tsh. Milioni 6,787.2

Soma https://jamii.app/BajetuKuu2025

#JamiiForums #JamiiAfrica #Accountability #BajetiKuu2025 #Governance #Uwajibikaji #Transparency
1
Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba amependekeza kutoza ushuru wa bidhaa kwa kiwango cha 30% kwenye vifaa vya Sigara za Kielektroniki na vimiminika vya Sigara za Kielektroniki, ili kupunguza athari zinazotokana na matumizi ya bidhaa hizo na kuongeza wigo wa Kodi

Amesema hatua hiyo inatarajia kuongeza Mapato ya Serikali kwa kiasi cha Tsh. Milioni 3,322.2

Soma https://jamii.app/BajetuKuu2025

#JamiiForums #JamiiAfrica #Accountability #BajetiKuu2025 #Governance #Uwajibikaji #Transparency
1
Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba amependekeza kupunguza ada ya usajili wa pikipiki za biashara kutoka Tsh. 340,000 hadi Tsh. 170,000 kwa miaka mitatu, huku akisema ada hiyo husika italipwa wakati wa usajili wa awali pekee

Vile vile amependekeza kupunguza ada ya leseni ya uendeshaji wa pikipiki, bajaji na guta kutoka Tsh. 70,000 hadi Tsh. 30,000

Soma https://jamii.app/BajetuKuu2025

#JamiiForums #JamiiAfrica #Accountability #BajetiKuu2025 #Governance #Uwajibikaji #Transparency
3
Kukosea siyo tu jambo la kawaida, bali pia ni muhimu sana kwa ukuaji na kujifunza.

Tunajifunza kutokana na makosa yetu, tunaboresha ujuzi wetu na tunakuwa watu wenye Hekima zaidi.

Makosa yanatuonesha pale tulipofanya vibaya na kutupa fursa ya kurekebisha na kusonga mbele.

#JamiiAfrica #JamiiForums #Maisha #GoodMorning #AmkaNaJF
2
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
#DIPLOMASIA: #Israel imefanya mashambulizi Nchini #Iran katika Mji wa #Tehran ikiwa ni sehemu ya Oparesheni kwa kile ambacho Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu amesema walilenga kudhoofisha Miundombinu ya Nyuklia ya Iran na Viwanda vya Makombora ya masafa marefu

Pamoja na hivyo, Israel imetangaza hali ya hatari, ikisema inatarajia mashambulizi ya kulipiza kisasi kutoka kwa Iran, wakati ambapo Iran imesema mashambulizi hayo yameathiri Makazi ya raia na kuua Watu kadhaa wakiwemo Watoto

Wakati huohuo, Rais wa Marekani, #DonaldTrump amekiambia Kituo cha #FoxNews kuwa alikuwa na taarifa kuhusu mashambulizi hayo kabla lakini Nchi yake haikuhusika kwa namna yoyote

Soma https://jamii.app/IsraelAgainstIran

#Diplomacy #Governance #HumanRights #JamiiForums #JamiiAfrica
1
UTEUZI: Rais Samia amemteua Jaji wa Mahakama ya Rufani, George Mcheche Masaju kuwa Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, akichukua nafasi ya Prof. Ibrahim Hamis Juma ambaye amestaafu

Taarifa ya Katibu Mkuu Kiongozi, Dkt. Moses Kusiluka, imeeleza uapisho wa Jaji Mkuu utafanyika Juni 15, 2025 Ikulu, Chamwino - Dodoma, Saa 4.00 Asubuhi

Soma https://jamii.app/UteuziGeorgeMcheche

#Uteuzi #JamiiForums #Governance
1
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imesema mifumo ya Hali ya Hewa haioneshi uwepo wa mvua hivi karibuni hapa nchini badala yake kutakuwa na ukavu na ubaridi ambapo Wananchi wametakiwa kuchukua tahadhari za kujilinda na baridi

Meneja wa Utabiri wa TMA, Dkt. Mafuru Kantamla amesema mvua zilizonyesha hivi karibuni Ukanda wa Pwani zimetokana na ongezeko la Joto katika Bahari ya Hindi hususan katika Mwambao wa Pwani lakini hazitakuwa na mwendelezo kwa kuwa joto la Bahari limeanza kupungua kwa kasi

Soma https://jamii.app/HaliYaHewaJuni

Video Credits: Torch Media

#ClimateChange #JamiiForums #JamiiAfrica
1👍1
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DODOMA: Mdau wa JamiiForums.com anaeleza kuwa Daraja lililopo Kata ya Mkonze, Mtaa wa Muungano linalounganisha Mtaa wa Muungano na Goba limeharibika na halijafanyiwa maboresho kwa muda mrefu

Anadai vyombo vyote vya usafiri na wanaotembea kwa miguu wanalazimika kupita pembeni kwa kuwa eneo la katikati halipitiki

Anaongeza kuwa ikinyesha mvua ukiwa upande mmoja kati ya maeneo hayo lazima usubiri mpaka maji yapungue ndio uvuke, anatoa wito kuwa Daraja liboreshwe kwa kuwa hali ilivyo ni mateso kwa wapitaji wa hapo

Soma https://jamii.app/DarajaLaMuunganoGoba

#JamiiForums #Accountability #Miundombinu
2
KENYA: Maafisa Polisi wamemkamata Askari anayefahamika James Mukhwana kwa kuhusika na mauaji ya cha mwalimu na mwanablogu, Albert Omondi Ojwang' aliyefariki akiwa kizuizini baada ya kushikiliwa kwa kuchapisha taarifa za uongo

Kwa mujibu wa ripoti ya Polisi imesema kuwa Askari James wa Kituo cha Polisi cha Kati Nairobi alikamatwa Juni 12, 2025 na kuwekwa rumande katika Kituo cha Polisi cha Capitol Hill na anatarajiwa kushtakiwa kwa kosa la mauaji ya Ojwang'

Ikumbukwe Albert Ojwang' (Mwanaharakati na Mwanamtandao) alifariki Dunia Juni 8, 2025, Siku moja baada ya kukamatwa Nyumbani kwake Kakot, Homa Bay, akiwa chini ya uchunguzi kuhusu chapisho alilodaiwa kumdhalilisha Naibu Mkuu wa Polisi kwenye Mtandao wa Kijamii wa X

Soma https://jamii.app/AskariJamesKifoOjwang

#JamiiForums #JamiiAfrica #Uwajibikaji #Accountability
DAR: Klabu ya #Simba imesema Serikali imeruhusu watumie Uwanja wa Mkapa kufanya mazoezi Juni 14, 2025 ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya mchezo wao wa Ligi Kuu Bara dhidi ya #Yanga unaoratajiwa kuchezwa Juni 15, 2025

Barua hiyo imeeleza kuwa uwanja upo tayari kwa mchezo na wameruhusiwa kwa mujibu wa Kanuni kwa kuwa Simba itakuwa ugenini katika mchezo huo ambao Yanga imekuwa ikisisitiza haitaingiza timu uwanjani

Barua imeandikwa na Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Boniface Tamba kwenda kwa Simba na nakala kwa Afisa Mtendaji wa Bodi ya Ligi Kuu

Soma https://jamii.app/SimbaMazoezi

#JFSports #JamiiForums
2
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
SONGWE: Mdau anadai changamoto ya foleni ya magari ya mizigo mpaka wa Tanzania na Zambia upande wa Tunduma ni kero kubwa, inakwamisha Uchumi wa Watu wengi na kuwafaidisha wachache

Anadai kuna Kiongozi wa Usalama hapo anamiliki eneo la kuegesha (parking) anatoza Sh 10,000 kwa siku badala ya Tsh. 5,000 inayotozwa kwingine na kwamba Mwanausalama huyo anatoa kipaumbele kwa Wateja wake kuvusha magari huku wengine wakibaki kucheleweshewa mchakato

Pia, Mdau anadai hali ya Watumishi kukosa uadilifu inachangia foleni kwa kuwa michakato inafanyika kwa kasi ndogo kwa baadhi ya Maafisa kujali maslahi binafsi

Ikumbukwe, Aprili 2025, Mkuu wa Mkoa, Daniel Chongolo aliunda Kamati Maalumu kuchunguza msongamano huo ambapo baadhi ya Wadau walimwambia inatengenezwa na Watu wachache kwa sababu wanazozijua wao

Soma https://jamii.app/TundumaFoleniJuni

Video Credits: CHAWAMATA TV

#JamiiForums #ServiceDelivery #Accountability
SIMIYU: Mdau anakumbushia kuwa Machi 2021, Waziri wa Nishati (wakati huo), Dkt. Medard Kalemani alishiriki kuweka jiwe la msingi la Ujenzi wa Kituo cha Kupoza Umeme cha Imalilo, ambapo shamrashamra zilikuwa kubwa na kuwapa matumaini makubwa Wananchi

Mdau anasema Kalemani alieleza Kituo kitajengwa ndani ya Mwaka mmoja kwa gharama ya Tsh. Bilioni 75, anamnukuu "Umeme utakaozalishwa hapa ni mkubwa utauwezesha mkoa huu na mikoa jirani kuendesha shughuli za viwanda na uwekezaji unaohitaji umeme mwingi."

Hivyo, Mdau anadai kilichotokea mradi haujakamilika na hakuna majibu ya kueleweka kutoka kwa Mamlaka na kwamba changamoto ya kukatika kwa umeme mara kwa mara bado ipo kwa kuwa kituo hicho kilitegemewa kutatua changamoto hiyo

Soma https://jamii.app/UmemeSimiyu

#JamiiForums #Accountability #Governance
1