JamiiForums
52.9K subscribers
34.3K photos
2.42K videos
31.3K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DEMOKRASIA: Mwananchi wa Mtaa wa Somelo, Kata ya Zingiziwa, Ilala amembana Diwani wake kwa maswali, akitaka kufahamu yapi ameyafanya Diwani huyo tangu alipoingia Madarakani, akidai toka wamchague hajawahi kufika hata kuwashukuru Wananchi wake kwa kumchagua

Zaidi https://jamii.app/DiwaniWaSomelo

#JamiiForums #JamiiAfrica #HudumaZaKijamii #ServiceDelivery #Accountability #Governance
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DODOMA: Akichangia makadirio ya mapato na matumizi ya Bajeti Wizara ya Uchukuzi 2025/2026, Mei 15, 2025, Mbunge Livingstone Lusinde amesema “Watu waheshimu miundombinu na utaratibu ili Taifa lisonge mbele lakini mambo madogo yasiwaumize kichwa mfano Mtu akisema No Reforms No Election, geuza kidogo na mwambie No Election No Reforms.”

Aidha, amesisitiza elimu itolewe kuhusu huduma ya usafiri wa Treni ya SGR na Treni ya Reli ya Kati kwa Wananchi ili watambue umuhimu wake na ili walinde miundombinu inayotumika

Soma https://jamii.app/LusindeMei15

#JamiiForums #Democracy #Kuelekea2025
MWANZA: Kampuni ya Meli Tanzania (#TASHICO) imesema inatarajia kutoa taarifa na tarehe rasmi ya kurejea kwa safari za kawaida kwa Meli ya New MV Victoria ambayo imekuwa katika matengenezo tangu Machi 4, 2025

Soma https://jamii.app/MvVictoriaMei15

#JamiiForums #ServiceDelivery #Accountability
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DODOMA: Akijibu hoja za Wabunge walioeleza kuwa kuna Wajawazito wengi na Watoto chini ya umri wa miaka mitano wamekuwa wakilipishwa fedha katika Hospitali za Serikali kinyume na maelekezo ya Serikali, Naibu Waziri wa Afya, Dkt. Godwin Mollel amesema kuna wakati busara inatumika licha ya uwepo wa Sheria na Kanuni

Soma https://jamii.app/MatibabuBure

#JamiiForums #PublicHealth #Accountability #JFHuduma
Mei 14, 2025, Kiongozi Mstaafu wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe kupitia Ukurasa wake rasmi katika Mtandao wa X alisema utani wa Kisiasa ni mzuri lakini ni muhimu sana kufanyika kwa namna ambayo unalinda Heshima na Utu wa Wanawake

Soma https://jamii.app/UtuWanawakeSiasa

#JamiiForums #JamiiAfrica #Kuelekea2025 #Demokrasia #JFWomen #WomenInPolitics
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DODOMA: Mbunge wa Bahi, Kenneth Ernest Nollo ameshauri Serikali kupunguza kodi ya kuingiza simu kutoka nje ya Tanzania ili kuwezesha Watanzania wengi kutumia Simu Janja kwa kuwa hali hiyo itasaidia ongezeko la Watumiaji wa Intaneti

Awali, Nollo alisema, takwimu za Mamlaka ya Mapato Tanzania (TCRA) za Machi 2025 zinaonesha kuna laini za simu Milioni 90, Watumiaji wa Intaneti ni Milioni 49, simu zinazomilikiwa zisizo simu janja ni milioni 56 wakati simu janja ni milioni 24, hali inayoonesha bado matumizi ya intaneti ipo chini

Soma https://jamii.app/KennethNollo

#JamiiForums #DigitalWorld #DigitalRights
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DODOMA: Mbunge wa Bahi, Kenneth Ernest Nollo amesema kuna mazingira kadhaa yanayosababisha Watu wengi kutotumia intaneti ikiwemo baadhi ya Mitandao ya Simu kuwa na huduma mbovu ya intaneti

Amesema hayo wakati anachangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari kwa Mwaka wa Fedha wa 2025/26, Mei 16, 2025

Soma https://jamii.app/NolloKuhusuIntaneti

#JamiiForums #DigitalWorld #DigitalRights
👍1
DAR: Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka (DART) ameeleza Matumizi ya Tiketi za Karatasi katika usafiri wa ‘Mabasi ya Mwendokasi’ yatafutwa rasmi ifikapo Juni 30, 2025 na baada ya hapo watakaotumia kadi ndio watakaoruhusiwa kusafiri kwa kutumia mabasi ya mfumo wa DART

Taarifa ya DART imeeleza kuwa utaratibu huo wa matumizi ya kadi hautahusisha Wanafunzi na katika kurahisisha zoezi hilo bei ya kadi moja itakuwa inauzwa kwa Tsh. 1,000 (ilikuwa inauzwa Tsh. 5000) kuanzia kesho Mei 17, 2025

Aidha, ikumbukwe Septemba 2024, Waziri wa TAMISEMI, Mohamed Mchengerwa alizindua matumizi ya Kadi hizo na kutoa maelekezo kuhakikisha zinatumika lakini kwa asilimia kubwa DART imeendelea kutumia Tiketi za Karatasi

Soma https://jamii.app/TiketiZaMwendokasi

#JFMatukio #ServiceDelivery #JamiiForums
1
Katika dunia yenye maneno mengi na vitendo vichache, uaminifu umekuwa rasilimali adimu. Si kila anayesema ukweli anaishi kwa ukweli na si kila anayeahidi ana nia ya kutimiza.

Uaminifu wa kweli huonekana pale mtu anapochagua kuwa mwaminifu hata kama hakuna anayemuangalia, anapotimiza wajibu wake bila kulazimishwa na anaposhikilia ahadi zake hata kama ni vigumu

Tunapokaribisha mapumziko ya Mwisho wa wiki tujiulize; Je, tunaishi yale tunayoyasema?

#JamiiAfrica #JamiiForums #AmkaNaJF #Maisha #LifeStyle #Lifelessons
👍1
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
Akihojiwa na Kituo cha #Clouds, Mbunge wa Jimbo la Morogoro Kusini Mashariki, Shabani Hamis Taletale (Babu Tale) amesema hana la kusema kuhusiana na Matukio ya Utekwaji wa Raia kwasababu hakuna mtu aliyetekwa jimboni kwake

Aidha, ameongeza kuwa hajawahi kushiriki kwenye mambo mengine sababu alipoingia #Bungeni 'focus' yake ilikuwa ni kwenye jambo moja tu (Jimbo lake) kuhakikisha wanapata Barabara na mwaka huu Rais ameridhia ombi lake hivyo amefanya kazi yake kikamilifu

Zaidi https://jamii.app/UtekajiMoro

#JamiiForums #JamiiAfrica #HumanRights #SocialJustice #Uwajibikaji #Accountability #Governance #Kuelekea2025
👎3👍2
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DODOMA: Mbunge wa Mbogwe, Nicodemus Maganga amewataka Wasimamizi wa Uchaguzi kutenda haki ili watoe matokeo sahihi na wasihusike katika kuongeza wala kupunguza idadi ya Kura Halali

Alitoa kauli hiyo, Aprili 15, 2025 wakati akichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Ofisi ya Waziri Mkuu kwa Mwaka wa Fedha 2025/26

Soma https://jamii.app/MagangaKuhusuHaki

#Governance #Accountability #JamiiForums #Democracy
👍31
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DODOMA: Mbunge wa Mbogwe, Nicodemus Maganga akichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Ofisi ya Waziri Mkuu kwa Mwaka wa Fedha 2025/26, Bungeni Aprili 15, 2025, alitoa wito kwa Wananchi kutowapigia kura Wagombea wanaotoa #Rushwa katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025

Zaidi https://jamii.app/MagangaKuhusuHaki

#Governance #Accountability #JamiiForums #Democracy #KemeaRushwa #Uwajibikaji
1
ARUSHA: Mchungaji wa Kanisa la Huduma ya Kristo lililopo Mtaa wa FFU, Kata ya Murieti, Steven Jacob (35) ambaye iliripotiwa ametekwa na ‘Watu Wasiojulikana’ Asubuhi ya Mei 16, 2025 amepatikana akiwa na majeraha kadhaa ya kupigwa

Awali, Kusaga TV ilinukuu familia ya Steven ikisema watekaji wakikuwa na gari aina ya Land Cruser nyeupe isiyokuwa na Namba za Usajili

Alipotafutwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, SACP Simon Maigwa amesema “Sina hiyo taarifa”. Jitihada za kumtafuta Kamanda wa Polisi Arusha, SACP Justine Masejo zinaendelea kutokana na simu yake kutopokelewa

Soma https://jamii.app/StevenJacobMchungaji

#JamiiForums #HumanRights #Accountability
👍2
MWANZA: Mdau wa JamiiForums.com anadai Barabara ya Musoma - Mwanza imekuwa ikitengenezwa mara kwa mara lakini hata miezi miwili haiishi inafumuka, ina matuta kuliko Barabara za Changarawe wakati ni barabara kubwa (cross country road)

Anadai kipande cha Nyanguge - Lugeye kilifumuka hata kabla ya mwezi mmoja kumalizika, kilichofuata wakaanza kuweka viraka

Anatoa wito Mamlaka husika kusimamia ubora kwa kuwa hali inavyoendelea wanaoumia ni wengi na madhara kwa Watu na Vyombo vya Usafiri yanaongezeka

Soma https://jamii.app/MusomaMwanza

#Accountability #JamiiForums
👍2
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
ARUSHA: Mchungaji wa Kanisa la Huduma ya Kristo lililopo Mtaa wa FFU, Kata ya Murieti, Steven Jacob Gumbo (35) ambaye iliripotiwa ametekwa na ‘Watu Wasiojulikana’ Mei 16, 2025 amezungumza na Wanahabri na kueleza kuwa Watu waliomchukua walijitambulisha kuwa ni Askari Polisi na wanamhitaji kwa ajili ya mahojiano

Amesema Watu hao walimchukua kwa nguvu huku wakimpiga, akapelekwa sehemu ambayo hakuifahamu na kuingizwa kwenye chumba kisha kuanza kumshambulia

Ameongeza “Naomba nisiongee mengi, sababu ya kutekwa ni ishu za Mtandao. Walichukua maelezo, wakanipeleka porini West Kilimanjaro, wakachukua simu yangu na kunitaka nifute video zangu zote, wakazungumza vitu ambavyo siwezi kuvisema kwa sasa kisha wakanitelekeza hapo.”

Soma https://jamii.app/MchungajiJacob

#JamiiForums #JFMatukio #HumanRights
Mtumiaji wa JamiiForums.com ame'share' picha zikionesha hali halisi ya Barabara ya Mbezi Makabe (Kwa Pesapesa) na changamoto ya usafiri wanayokutana nayo Watumiaji wa Barabara hiyo hasa msimu huu wa Mvua, akitoa wito kwa Mamlaka husika na Viongozi wa eneo hilo kushughulikia uboreshaji wa barabara hiyo

Zaidi https://jamii.app/MakabeKwaPesapesa

#JamiiForums #JamiiAfrica #Uwajibikaji #Accountability #ServiceDelivery #HudumaZaKijamii #Governance