JamiiForums
52.8K subscribers
34.4K photos
2.44K videos
31.3K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Mabasi ya Mwendokasi (UDART), Waziri Kindamba amekiri kuwa usafiri wa Mwendokasi umekuwa changamoto na kero kwa Watumiani wengi, ndio maana hatua zimechukuliwa ikiwemo kuongeza mabasi mapya ya Kisasa 99

Ameeleza wameelemewa na mabasi chakavu na machache hali iliyosababisha kuagiza Mabaso 100 kutoka China na tayari moja limewasili likitumia gesi asilia, linabeba abiria 155 na linatarajiwa kuanza safari Jumatatu Mei 12, 2025 njia ya Morocco -Kivukoni

Mara kadhaa Wadau wa JamiiForums.com wamekuwa wamelalamikia changamoto mbalimbali za huduma ya usafiri huo, baadhi walisema mradi unazidiwa na wingi wa Wateja kuliko uwezo wa mabasi

Soma https://jamii.app/KindambaMwendokasi

#JamiiForums #ServiceDelivery #JFAccountability
👍4
Kusoma kwa undani habari hizi na nyingine zilizojiri juma lililopita bofya https://jamii.app/YaliyojiriJumaLililopita

#JamiiForums #YaliyojiriJumaLililopita #JFToons
👍1
MWANZA: Mdau anasema Mwanzoni mwa Machi, 2025, kuna Mdau alihoji kuhusu Meli ya New MV Victoria kutofanya kazi na Mamlaka kutotoa muongozo wowote, baadaye Kampuni ya Meli Tanzania (TASHICO) ikaeleza kuwa Meli ipo katika ‘service’ ya kawaida na inatarajia kurejea kazini ndani ya wiki tatu hadi Siku 30

Mdau anadai kufikia Mei 11, 2025, miezi miwili imekatika meli haijarejea na hakuna tamko lingine kuhusu kinachoendelea

Anatoa wito kwa TASHICO kujitokeza na kueleza kinachoendelea kwa kuwa ukimya wao unawaumiza wengi

Soma https://jamii.app/MvVictoriaMay

#JamiiForums #ServiceDelivery #Accountability
1
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
KILIMANJARO: Mkuu wa Shule ya Polisi Tanzania – Moshi (TPS), SACP Ramadhani A. Mungi amesema “Kundi la Vijana ndilo la uzalishaji, maendeleo ya Taifa hili yanatokana na Vijana kwa kuwa wao ndio wachapakazi, wana nguvu kubwa za mwili na akili, shughuli zote Kiuchumi asilimia kubwa zinaendeshwa na Vijana.”

Amesema hayo alipokuwa TPS wakati wa Ufunguzi wa Mafunzo ya Medani za Kivita kwa Wanafunzi wa mafunzo ya Awali Kambi ya Kamba Pori, Mei 6, 2025.

Soma https://jamii.app/NukuuYaMungi

#JamiiForums #JFNukuu #JFQuote #Governance
👍4
UCHAMBUZI: Mei 10, 2025, Chama cha #ACTWazalendo kilichambua Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (#CAG) Mwaka 2023/24 na kutoa mapendekezo kadhaa na hatua za kuchukuliwa na Serikali

Sehemu ya mapendekezo hayo ni kuwa “Tunasisitiza kwamba Serikali ihakikishe kwamba mfumo wake wa kielektroniki unafanya kazi wakati wote na maeneo yote na kuweka utaratibu wa kutokuruhusu miamala kufanyika nje ya mifumo hiyo.”

Mengine ni “Tunasisitiza Viongozi, Wawakilishi, Vyama vya Siasa, Wadau wa Maendeleo na Wananchi kuhakikisha wanakata mirija ya ubadhirifu ili kuhakikisha kunakuwepo na ustawi wa kweli wa Watu.”

Soma https://jamii.app/CAGUchambuziACT

#JamiiForums #Governance #Accountability #Uwajibikaji #CAGReport2025 #RipotiCAG2025
👍1
Mdau, ni kitu gani kikiboreshwa katika mfumo wa Uchaguzi kitakufanya ujisikie huru na tayari kushiriki Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025

Kutoa maoni na mapendekezo yako, usikose kujiunga nasi katika Mjadala muhimu kuelekea Uchaguzi Mkuu kupitia #XSpace ya JamiiForums, Mei 12, 2025, Saa 12:00 jioni – 2:00 usiku

Bofya hapa kujiunga: https://jamii.app/ReformsSpace

Tafadhali 'share link' hii na yeyote ambaye hutamani apitwe na Mjadala huu

#ReformsSpace #Uchaguzi2025 #Demokrasia #Uwajibikaji #FreeAndFairElections #Kuelekea2025
1👍1
UCHAMBUZI: Chama cha #ACTWazalendo kikichambua Ripoti ya CAG Mwaka 2023/24, kimesema Deni la Taifa limepanda kufikia Tsh. Trilioni 97.35 kutoka Tsh. Trilioni 82.25 Mwaka uliopita, hilo ni ongezeko la zaidi ya Tsh. Trilioni 15, hali hiyo inaweka hatari mustakabali wa Taifa kwa kuwa baadhi ya viashiria kama “uwiano wa kulipa deni kwa mapato” vinakaribia ukomo wa hatari uliowekwa na taasisi za kimataifa

ACT imesema kuwa ripoti ya #CAG imeonesha uwiano wa kulipa deni kwa mapato ya ndani umefikia 14.5%, ukikaribia kikomo cha tahadhari cha 18%, pia uwiano wa kulipa deni kwa mauzo ya nje ni 11.7%, ukielekea ukomo wa hatari wa 15%

ACT imeongeza "Maana yake, sehemu kubwa ya mapato ya Serikali inaishia kulipa madeni badala ya kuendeleza huduma kwa Wananchi. Mapato ya Serikali kwa Januari 2025, kwa Mfano ilikusanya Tsh. Trilioni 2.63 katika makusanyo hayo Serikali ilitumia Tsh. Trilioni 1.2 kulipia huduma ya deni"

Soma https://jamii.app/CAGUchambuziACT

#JamiiForums #Accountability #Uwajibikaji #CAGReport2025
👍2
KENYA: Rais Ruto alipokea rasmi ripoti ya Mchakato wa Upatikanaji wa Viongozi wa Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) Mei 6, 2025, kutoka kwa Mwenyekiti wa Jopo la Uteuzi, Dkt. Nelson Makanda baada ya kukamilika kwa mchakato wa usaili na uhakiki wa Wagombea

Hata hivyo Waangalizi wa Uchaguzi (ELOG) wamesisitiza kuwa #Uwazi wa mchakato huu ni muhimu kwa kuimarisha imani ya Umma katika Taasisi ya Uchaguzi, hasa kuelekea chaguzi zijazo

Usaili wa nafasi ya Mwenyekiti wa IEBC ulikamilika Machi 26, ambapo Wagombea 11 walihojiwa. Mei 8, Rais Ruto alimteua Erastus Edung Ethekon kuwa Mwenyekiti mpya wa IEBC, uteuzi unaosubiri kuidhinishwa na Bunge

Ethekon, ambaye aliwahi kuwa Wakili wa Kaunti ya Turkana, anatarajiwa kuchukua nafasi ya aliyekuwa Mwenyekiti wa IEBC, Wafula Chebukati, aliyefariki Februari 2025

Zaidi https://jamii.app/RipotiKE

#JamiiAfrica #JamiiForums #Kuelekea2025 #FreeAndFairElections #Demokrasia #Governance #Transparency
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (#LATRA) imesema magari ya usafiri wa Umma yatakayokatisha au kubadili “ruti” kinyume na Leseni zao, yatachukuliwa hatua ikiwemo kufungwa kwa kifaa cha VTS kwa ajili ya kufuatilia Mwenendo wa vyombo hivyo

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Udhibiti Usafiri wa Barabara wa LATRA, DCP Johansen Kahatano ambaye ameongeza kuwa wanafanya hivyo ili kukabiliana na ukatishaji wa ruti ambao unafanywa hasa na Daladala

Mfumo wa VTS unawezesha kufuatilia mwenendo wa chombo ikiwemo suala la mwendokasi na kuonekana katika Mfumo wa LATRA

Soma https://jamii.app/KukatishaRuti

Video Credits: Torch Media

#JFHuduma #JamiiForums
👍1
DAR: Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) imeanzisha Majimbo mapya 8 (Nane) ya Uchaguzi huku Majimbo 12 yakibadilishwa jina, hayo yameelezwa na Mwenyekiti wa INEC, Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele, leo Mei 12, 2025

Hivyo, idadi ya Majimbo kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 yatakuwa 272 kutokana na ongezeko la majimbo hayo yaliyotangazwa, ambapo 222 yakiwa Tanzania Bara, 50 yakiwa Tanzania Zanzibar

Soma https://jamii.app/TumeTangazoMei12

#JamiiForums #Democracy #Kuelekea2025 #UchaguziMkuu2025
👍1