JamiiForums
55.4K subscribers
33.4K photos
2.03K videos
30.4K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
Yanayojiri katika Mjadala na ambao bado hawajapata Chanjo ya #COVID19 unaoendelea Clubhouse

#JamiiForums #UVIKO3 #CoronaVirus
MDAU: BODABODA ZITASABABISHA WATOTO WENGI KUWA NA MATATIZO YA KIFUA

Mshiriki wa #StoriesOfChange anasema baadhi ya Wazazi huruhusu Watoto kupelekwa Shule kwa pikipiki, na baadhi ya Madereva huwaweka watoto mbele

Anashauri kujali usalama wa Mtoto na si kuwahi Shule

Soma - https://jamii.app/BodabodaWatoto
#SUDAN: Jenerali aliyeongoza Mapinduzi ya Kijeshi hivi karibuni, Abdel Fattah al-Burhan amejiteua kuongoza Baraza Tawala la Mpito

Jenerali Mohammed Hamdan Dagalo ambaye ni Mshirika wake wa karibu ameteuliwa kuwa Makamu wa Rais

Soma - https://jamii.app/AjiteuaSudan

#Democracy #JFLeo
NI KWELI AJIRA INA UNAFUU NA UHAKIKA ZAIDI KULIKO KUJIAJIRI?

Mdau wa JamiiForums.com anasema Kuponda kuwa Ajira ni Utumwa ni sawa na "sizitaki mbichi hizi" kwasababu Ajira hazipo nyingi, na zikitangazwa hata waliojiajiri wanazishambulia pia

Anasema #Biashara ni nzuri ikiwa kuna Mfumo wa kupigana jeki na kubebana. Mfano Mzazi akifariki kuwe na Mtoto kaandaliwa kuendeleza

Una maoni gani kuhusu hoja hii?

Mjadala - https://jamii.app/UhakikaAjira
#JFLeo
MDAU: WAZAZI TOENI URITHI KWA WATOTO. ELIMU SIO URITHI

Mdau wa JamiiForums.com anasema Baba ana majukumu ya kuhakikisha ulinzi na usalama ndani ya Familia, kuihudumia Familia pamoja na kuzalisha Mali na kuandaa Urithi kwa kizazi chake

Anasema siku za hivi karibuni kumezuka tabia hasa Wababa kuleta visingizio kuhusiana na masuala ya kumuandaa Mtoto na Ulimwengu. Elimu sio Urithi bali ni Hitaji muhimu ambalo Mzazi lazima umpe Mwanao

Mjadala - https://jamii.app/ElimuSioUrithi
#Maisha #Familia
IKULU, DAR: Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan apokea kifimbo cha Malkia wa Uingereza kuashiria Uzinduzi wa Michezo ya Jumuiya ya Madola

> Kifimbo hicho kinaashiria kuanza kwa Michezo ya Jumuiya ya Madola mwaka 2022

Soma https://jamii.app/KifimboChaMalkia

#JFSports
ECUADOR: Wafungwa 68 wa gereza la Litoral Mjini Guayaquil wamefariki na wengine wengi kujeruhiwa katika mapigano ya magenge mawili hasimu

> Magereza yana wafungwa 55% zaidi ya uwezo. Wafungwa takriban 300 wamefariki kwa vurugu za mahasimu mwaka 2021

Soma https://jamii.app/EcuadorWafungwa
CHANJO HAZISABABISHI MIMBA KUHARIBIKA

Kituo cha Kudhibiti Magonjwa(CDC) kinahimiza Wajawazito, wanaotarajia kupata Ujauzito na wanaonyonyesha kupata chanjo kujikinga na #COVID19

Manufaa yake kwa Wajawazito hushinda hatari zinazoweza kutokea

Soma https://jamii.app/ChanjoMimba
#UVIKO3
SUDAN: Watu 5 wameuawa na wengine kujeruhiwa wakati wa Maandamano ya kudai Utawala wa Kidemokrasia Jumamosi

Inadaiwa Vikosi vya Baraza la Mapinduzi ya Kijeshi vilivamia Hospitali ya Al Arbaeen huko Obdurman na kushambulia Watu

Soma https://jamii.app/5DeadSudan

#HumanRightsViolation
IFAHAMU CHANJO AINA YA #ASTRAZENECA

Imethibitishwa na Shirika la Afya (WHO) kuwa salama kukinga #CoronaVirus kwa Watu wenye miaka 18 na zaidi

Inatolewa kwa Dozi mbili ambapo Dozi ya pili hutolewa wiki 8 mpaka 12 baada ya Dozi ya kwanza

Soma - https://jamii.app/FahamuChanjo

#UVIKO3