HabariTech
201 subscribers
33 photos
4 videos
1 file
125 links
Bila shaka unataka kuwa na uhuru wa pesa (upate utajiri). Ni wazi kwamba unatamani kuifahamu tech vizuri kwa kuwa umeambiwa utajiri upo huku.

Ni kweli tech inapesa nyingi, ila kwanza ungana nasi ili usitumie pesa nyingi kujifunza na uweze kuokoa muda.
Download Telegram
Je, wanaongea au kila mmoja yuko busy na simu yake?

Tumekuwa watu ambao tunatafuta kukubalika mtandaoni kuliko na watu wanaotuzunguka. Hii ni kwa sababu simu zetu zimekuwa vizuri sana kufanya kazi ambazo watengenezaji wake wamelenga kuliko sisi kujua inatakiwa kufanya nini. Kwa sababu hiyo tukikaa pamoja tunaona ni bora kuangalia videos TikTok kuliko kuzungumza na wanaotuzunguka.
Hii ni kwa sababu hatuko tayari kupokea maoni ya wanaotuzunguka pale ambapo kuna jamii za mtandaoni ambazo zinatupa majibu tunayotaka kusikia.

Mimi kama naamini dunia ni tambarare nitajiunga na jamii zinazokubaliana nami na sio na rafiki zangu wanao amini kwamba dunia ni duara.

Echo Chambers

Niliposema mitandao na simu zetu zinafanya kazi ambazo zimeundwa kufanya namaanisha hiki kitu kinaitwa echo chambers. Echo ni Mwangwi, yaani sauti yako kurudi kwako ukiongea.

Echo chambers kazi yake ni kukuonyesha wewe maudhui ambazo zinaendana na wewe ili kuendelea kukuweka kwenye mtandao husika.

Sio uongo kuwa instagram wanataka uendelee KUPERUZI mtandao wao na Ali Express wanataka uendelee KUNUNUA kutoka kwao.

Wanafanyaje ili kuhakikisha hilo?

Leo hii ukiingia google kutafuta neno “Good gaming PC available 2022” unaweza pewa link za maduka yanayouza PC. Ukifungua tu link moja wapo, nakuhakikishia ukipita AliExpress au instagram utaanza kuona matangazo kuhusu Gaming PCs.

Hii ni kwa sababu algorithm yao imeamini kwamba kwa muda huo umevutiwa na mada zinazohusu gaming PC. Hii ndiyo tunaita echo chamber. Na kwa sababu hii utajikuta unaendelea kuperuzi huo mtandao kwa kuwa wanakuonyesha unachotaka kuona.

Kinachoendelea hapa ni mitandao kukuamlia ufikirie nini kwa muda mrefu. Ukiongelea Samsung utaanza kuona matangazo kuhusu Samsung. Mpaka tweets na posts za watu utakazoona ni zile zinaongelea Samsung tena kwa kuwasifu.

Ghafla utajikuta unaanza kuwa shabiki wa Samsung. Unaweza jikuta unaenda mbali zaidi na kuanza tumia bidhaa zao (Simu, TV, fridge, nk). Kinachoogopesha hapa ni kwamba akija mtu wa iPhone kukwambia tofauti hautataka kumuelewa kabisa. Na hii inaweza kukupelekea kurudi kwenye point yangu ya Negaitvity.

Ufuatiliaji
Tumefikia hatua ambayo teknolojia inaendelea kukua kwa kasi ya ajabu sana na hakuna mtu anataka iache kukua. Teknolojia bora maana yake ni kwamba maisha yetu yanakuwa bora zaidi na rahisi zaidi, hata silaha za kijeshi zinakuwa za kisasa kuzidi miaka ya nyuma.

Bahati mbaya wakati kila kitu kutuhusu kinakuwa cha kidijitali, kuanzia mahusiano mpaka uhalifu. Serikali na kampuni za mitandao na mawasiliano inabidi zitafute namna mpya ya kudhibiti haya yote ili kuwa na control juu ya watu wake.
Namna ya udhibiti ambayo itatumika hapa haitakuwa rafiki kwetu sisi wananchi.

Mfano mzuri ni sera mpya ya Apple kufatilia picha zote ndani ya simu yako, kuona kama kuna child abuse (Unyanyasaji wa watoto) unafanyika na kukuripoti kwa mamlaka husika.

Kwa sasa hili ni jambo zuri, ila itakuaje huko mbeleni kama serikali zitaanza kuweka sheria kwamba hizi kampuni za simu zifatilie kila kitu unachofanya na simu yako. Na hapa sina maana ya vitu vya kihalifu, naongelea vitu kama kwenda google na kutafuta “Bunduki inafanya vipi kazi?”. Kwamba ukitafuta kitu kama hicho wewe ni mhalifu unatakiwa kuwekwa mbaroni?

Unaweza dhani ni kitu haiwezekani ila China tayari wanafanya kitu kama hicho. Wananchi wa China wanakuwa rated kulingana na vitu wanavyofanya kwenye jamii. Vitu vinavyo zingatiwa hapa ni kama kuweka muziki kwa sauti kubwa eneo la watu wengi sio sahihi au kuvuka barabara sehemu isiyo na kivuko cha watembea kwa miguu.

Hivi ni vitu vidogo ambavyo vikiendelea sana vinaweza pelekea mwananchi wa China kuzuiliwa kusafiri kwa ndege kutoka nje ya nchi au hata kuondolewa haki ya baadhi ya vitu kama kwenda kumbi za starehe.

Mwisho

Binafsi napenda sana teknolojia na sitaki kusema kwamba tuachane nayo kwa kuwa inatupeleka pabaya. Ukweli ni kwamba mpaka sasa imetuletea maendeleo mazuri.
Kama umetumia dakika 40 instagram kuangalia instagram models usioweza kuwa nao sio kwamba umepoteza muda. Hapana, hiyo ni instagram inafanya kitu ilitakiwa kufanya. Kitu ambacho ni kukuonyesha wewe maudhui unayopenda ili usiache kutumia Instagram.

Ninachojaribu kusema ni kwamba sio mbaya kama mara moja moja tutaacha kutumia mitandao ili kuona tunaelekea wapi sisi kama jamii.
Point ni Zile zile

Huwa tunasema "Serikali haitoi sapoti ya kutosha kwa vijana wa Kitanzania."

Wengine wanasema "Sina mtaji wa kutosha kuanza sasa hivi."

Wakati tunatoa hizi excuses kuna vijana tayari wamefanya makubwa na kuleta solutions zinazosaidia Watanzania wengi.

Kujua ni kina nani na wamefanya nini, ni kupitia magazine ya 5 ya HabariTech.

Link https://habaritech.gumroad.com/l/habaritech5
AVAX Staker Review: Katika video hii nitakuonyesha project yenye high risk ambayo unaweza pata faida ya mpaka 20% ROI kwa siku kulingana na muda unawekeza katika project hii.

Avax Staker ni nini?

Huu ni muda mzuri wa kuweka AVAX zako katika yield returns na kupata ROI nzuri. Hii ni project inayoendeshwa na jamii. Jamii hii inashawishi wana jamii wake kuwekeza asilimia ndogo ya faida zao ili kuifanya project iishi kwa muda mrefu.

Unaweza kutumia Avax Staker reward calculator kuona utapata faida kiasi gani kabla hujaamua kuwekeza AVAX zako katika project hii. Pia ni vizuri ukatumia Avax Staker referral program kupata faida zaidi na AVAX ulizonazo.

Tazama Full video kupitia link hii ya YouTube https://youtu.be/-xx0gNggWm4
Iwapo mtu unaswali zaidi usisite kuuliza hapa hapa kwa ajili ya manufaa ya wengine pia.

Maswali yanayokuja inbox sitayajibu.
Kama kuna mwingine hizi terms zina mchanganya. Majibu ni hayo.
This is a test message
Kutofautisha Simu Feki na Original

Ukikaa muda mrefu sana mtandaoni kuna uhakika utakutana na watu ambao wako tayari kutumia mamilioni kununua simu feki na ni mara chache sana huwa wanajua kwamba walichonunua ni feki.

https://habaritechtz.com/kutofautisha-simu-feki-na-original/
Kutofautisha Simu Feki na Original

Ukikaa muda mrefu sana mtandaoni kuna uhakika utakutana na watu ambao wako tayari kutumia mamilioni kununua simu feki na ni mara chache sana huwa wanajua kwamba walichonunua ni feki.

https://habaritechtz.com/kutofautisha-simu-feki-na-original/
Kuboresha Windows 10 Yako

Windows 10 inasifika kwa ubora ukilinganisha na matoleo ya nyuma ya Windows, kama vile windows 8, 7 na XP. Ndani ya windows 10 Kuna settings huwa zinakuwa activated by default.

https://habaritechtz.com/kuboresha-windows-10-yako/
Serikali ya US ilikuwa ikifuatilia mawasiliano ya watu, taarifa za jeshi na vikao muhimu vya nchi nyingi duniani.

Tanzania ni miongoni mwa nchi zilizokuwa katika radar ya Marekani. Marekani walikuwa wakifuatilia mawasiliano ya watu mtandaoni pamoja ma serikali.

Marekani wameweza kufanya yote haya kupitia vyombo vyake vya usalama (FBI, CIA na NSA). Hii ni katika mpango wao wa kuwa taifa kubwa kuzidi yote duniani.

Soma makala nzima katika blog yetu, link ipo kwenye bio

https://habaritechtz.com/edward-snowden-wanaona-calls-sms-emails-na-browser-history-bila-wewe-kujua/
*Kwanini Graphics Designers Wanashindwa Kutengeneza Pesa?*

Mara kwa mara tumesikia graphics designers wengi wakilalamika juu ya _kushindwa kutengeneza pesa kwa kazi zao._

Wengi ukiwasikiliza sababu zao ni zile zile ambazo hata sisi wenye uzoefu tulikuwa tukikosea miaka ya nyuma.

Leo nazungumza na graphics designers ili wafahamu ni wali wanakosea mpaka wanashindwa kujipatia kipato.

Hii inamfaa designer anayeanza au anayetaka kuanza graphics designing.

*https://habaritechtz.com/kwanini-graphics-designer-wanashindwa-kutengeneza-pesa/*
Ukivaa saa kama hujazoea unaweza kuona mkono unakuwa mzito sana, lakini watu wengi, wewe ukiwa miongoni mwao unapenda/unatamani kuvaa smartwatch.

Bahati mbaya kila ukigeuka kuangalia unakutana na smartwatch za hovyo lakini bei zake ziko juu vibaya mno.

Unaona hii video hapa inahusu bei ya smartwatches hapa Tanzania kuanzia grade ya 3 mpaka ya 1 kutoka china.

Grade 1 ni ile inakaribiana na Apple Watch kwa asilimia 70%.

Leo nataka kukwambia unaweza kuipata hii kwa bei iliyo chini ya hiyo kwa zaidi ya 75%

Ila kwanza angalia hiyo video

https://vm.tiktok.com/ZM2xcajxc/
okay