CRYPTO CURRENCY
156 subscribers
907 photos
21 videos
3.12K files
637 links
Download Telegram
Forwarded from Daudi
Habari Wanandugu.

Ni jumamosi ya kwanza leo ya somo letu la laptop repair, na katika part 2 hii tutaangalia SOFTWARE Issues Tu.
Tujue Kidogo Nini Maana Ya Software Kwenye Laptop Au Computer Yoyote

Software Kwa Lugha Rahisi Ni Part Ya Computer Ambayo Huwezi Kuishika Na Mkono, Virtual Unakiona Lakini Huwezi Kukishika, Kama Vile Application, Themes, Cursor Etc
Software Ndio Inakupa Wewe Hali ya kuzungumza na computer, Kwa lugha nyingine ni USER INTERFACE.
Kwenye laptop repair practically, Software Inajumlisha, ALL Computer Apps, Operating System, BIOS, Etc.

Kwa Leo Tuangalie BIOS MENU Ambao Ni Msingi Mkubwa Wa Software Repair Na Kwa IT Professional Yoyote Hapa ndipo pa kuanzia kwenye software repair.

BIOS ni nini?
BIOS ni program iliyo na mahusiano mojamoja na laptop au computer yoyote kwa sababu ina chip iliyopo ndani ya motherboard, chip hiyo ndiyo inafanya kazi ya kuunganisha vifaa vyote vilivyopo ndani ya computer kufanya kazi kwa usahihi, kwa lugha sahihi huu ndiyo moyo wa software kwenye computer, hii ndio mwalimu mkuu wa software zote ikiwemo Operating System, Ukibonyeza Button ya kuwasha laptop anayeguswa na kutoa ruhusa ni bios na yeye ndio anaielekeza computer, Utachukua Software Wapi Either Kwenye HDD, USB Drive Au CD ROM,Etc.

BIOS Menu Ni Nini?
Ni Mpangilio Wa BIOS Katika Laptop Unaompa Ruhusa Mtumiaji Kufanya Chaguzi Mbali Mbali Kabla Ya Kufikia Katika Operating System.

Kipi Naweza Kukifanya Kwenye BIOS Menu?

* Unaweza Kuiwekea Password Laptop Yako (Hii ni safe Zaidi kuliko ya windows)
* Unaweza Kuangalia Taarifa Za Laptop Yako (System Info)
* Unaweza kuiamrisha laptop yako ifuate windows kutoka kwenye Nini Mfano: HDD, USB Drive Au CD ROM
* Unaweza Kufunga Matumizi ya Kifaa Kimoja Au Vingi Kwenye Laptop Yako, mfano: Port za USB, Speaker, Touchpad, WLAN Etc
* Unaweza Kupunguza Nguvu za matumizi ya Laptop yako kwa kutumia menu ya Multiprocessing na Virtual Technology
* Unaweza Kuangalia Life time na Status ya battery lako
* Kubadili saa na kujua OS Ya Kwanza Kuwekwa Kwenye Laptop Yako.
* Etc

NITAIPATAJE BIOS MENU?
Laptop zote zina bios menu tofauti, zinafanana baadhi kwa brand name mfano: DELL Nyingi Bios Ni F2 Na HP nyingi Bios Ni F9.
List Ya Bios Ipo Hapa Chini:
Forwarded from Daudi
Forwarded from Daudi
* Zima laptop yako
* Bonyeza Key Kama Zinavyoonekana Hapo Juu (Hutegemea na BRAND YAKO)
* Bonyeza kwa kuachia achia kama unaipiga ipiga mara nyingi maana mara nyingin hapa tunaotea
* Unabonyeza pale laptop inapowaka na kuonyesha brand name (kuwa makini sio zote zinaonyesha brand name nyingine zinakuwa kwenye FAST BOOT)
* Kama itagoma jaribu kwa kubonyeza huku ukiwa umeishikilia Function Key (Fn).

VILIVYOPO KWENYE BIOS MENU NA MATUMIZI YAKE

Hapa hutegemea na Bios Yenyewe Hapo Chini Nimetumia mfano wa Phoenix But Inaweza kuwa WARD Etc So Usikariri ila vingi vinafanana.

Tutumie mfano hapo chini.
Forwarded from Daudi
Forwarded from Daudi
MAIN = Hapo utaakuta sifa za laptop yako au STEM INFORMATION
Utajua Size ya RAM, HDD, Processor Na Serial Number Ya Laptop
Sio muhimu sana kwa repair technician

ADVANCED = Hapa ni muhimu kwa technician kwa maana hapa utapata Option ya Kuzima Ports, Au WLAN au Fn Key Au Speaker, Na Touchpad Hapa Utapata Menu ya Kupunguza Nguvu Ya Pc Na Processor, Na Kwa Gamers Amba Ndio Kuna Virtual Technology, Pia Hpa ndio kuna SATA MODE Ya HDD Ukibadili Hii Windows Hauwez Run Kwa Mode Tofauti na uliyoweka wakat unafanya installation.

SECURITY = Hapa utapata menu ya kufunga Password Za Laptop Yako (BIOS PASSWORD, HDD PASSWORD, ADMIN PASSWORD).

BOOT: Hapa utapata menu ya kuiamrisha laptop wapi ikachukue windows wakat inawaka, hapa ni muhimu sana wakati unataka kufanya installation ya windows kwa kutumia external device kama USB FLASH, UEFI MODE NA LEGACY MODE Zinapatikana hapa.

MATATIZO YA BIOS NA UTATUZI WAKE



Kuna matatizo mengi ya laptop lakini yafuatayo ni common na nimekumbana nayo sana.

1. BIOS PASSWORD
Hili ni tatizo sana na huwa nacharge pesa nzuri kulitatua, hii ni ile password tuliyoiona pale juu ambayo inatokea kabla booting haijafanyika.
Ukiwasha PC Utaona Hivi
Forwarded from Daudi
Forwarded from Daudi
JINSI YA KUTATUA TATIZO HILI
Kuna njia nyingi za kutatua BIOS Hutegemea Brand na Model Ya Laptop na Skills Alizo nazo Technician

* Kutumia Backdoor Password: hii ni common password ambazo zipo tayari kwenye bios kutoka kwa manufacture lengo la hizi ni kutumika wakat wa Emergency Ku Reset, Ili Kupata Hizi Password, Washa PC Nenda Kwenye BIOS Password Ingiza Randomly Psssword Zozote Mara 3, Then laptop itakuandikia SYSTEM DISABLE, Na itakupa namba Tano Copy Hizo Namba,Then Tafuta laptop nyingine nzima Nenda Kwenye Hii Site BIOS Master Password Generator for Laptops. Andika Disable code zako then Utapewa List ya Password Za Kujaribu Kufanya Reset.

* Toa CMOS Battery.
* Kama unaweza kufungua na kutoa CMOS Battery basi unaweza kufanya hivyo, Then ukawasha pc Unaweza Ukaitoa.
Forwarded from Daudi
1
Forwarded from Daudi
* CMOS Discharge.
* Hii ni advanced kwa tech yoyote anatakiwa kuifanya lakini ni lazima kuwa makini kwa maana ukishindwa kujua PIN Out za CMOS unaweza kuiharibu motherboard, Hii Inafanywa kwa kutoa CMOS Battery na kutafuta CMOS Pin Out Kweny Board na kupigisha Short. Means Unawasha laptop then unagusanisha hizo pin kwa kutumia Tweezer, The PC Itajizima, Ukiwasha Itakuwa haina Tena Password, Mchezo Huu Tunaufanya Sana Kwa Toshiba Na ACER, Kumbuka Kila motherboard ina PIN OUT Zake, So Kuangalia Schematica Au Ku Google Hakuepukiki.
* Mfano wa PIN OUT Huo hapo Chini:
Forwarded from Daudi
Forwarded from Daudi
c) Kufanya Short Kwenye SCL na SDA Chip.

SCL na SDA chip inabid uzifanyie location kwa kutumia Schematic, Pia Utafanya Kama kwenye CMOS Discharge Hapa Utaangalia PIN out,

Mfano Hapo Chini.
Forwarded from Daudi
Forwarded from Daudi
2. TOUCHPAD HAIFANYI KAZI, USB PORT HAZISOMI AU WLAN HAIFANYI KAZI.

Hili na nalo ni tatizo haswaa kwa laptop za TOSHIBA, Ukifanya Kutoa Tu CMOS Batterry Automatic CMOS Inafanya Reset, Mwisho wa siku inazima ToucHpad kwenye BIOS Menu.
USB Mode Pia Huwa Unazimwa 3.0, Mwisho wa siku Port Inakuwaga Umeme (5V) Lakini USB Device Haisomi Kabisa, Au WLAN.

SULUHISHO
Nenda Kwa BIOS Menu Upande Wa Advanced Then Angalia Kama Imezimwa Washa Na Epuka Kuchomoa CMOS Battery Mara Kwa Mara.

3. USB DEVICE HAIONEKANI WAKATI WA KUINSTALL WINDOWS KWA USB

Hii pia hutokea sana, haswaa kwa hizi laptop mpya, haijawahi kufanyiwa installation ya windows .

SULUHISHO
Nenda kwa Boot Menu Angalia Kama USB Boot Device Ipo Selected Au La, Then Iweke Iwe Your First Priority, Ukiwa unayafanya haya USB Flash Drive Yenye Windows Lazima Iwepo.

NB: Notice Za Session Hii nitazirusha Kwa mfumo wa PDF.

MATATIZO YAPO MENGI, KAMA KUNA YOYOTE MWENYE NAYO AFANYE NYONGEZA HAPO NA KARIBUNI KWA DISCUSSION.

KUMBUKA KILA WAKATI, UKIWA UNAJIFUNZA LAPTOP REPAIR MWALIMU WAKO MKUU NI INTERNET

Tukutane Next Week Kwa Part 2 E02 Kama Mungu Akipenda.
TUKUTANE JUMANNE KWA PART TWO TENA
BAADAYE TUTAENDELEA SEHEMU YA PILI

NITAIMALIZIA JIONI NIKIFIKA HOME ILI USIKI NIITUME
PART 2 EP01
Tuijue Laptop Na Tuifungue Kisha Tuifunge.
Habari za mda huu

Tumekutana Tena Katika Darasa Letu Huru La Laptop Repair, Na Part 2 Hii Tutakuwa Tunaangalia Matatizo Ya Hardware Tu.

Tuanze Kwanza Na Utangulizi Wa Laptop Kwa Siku Ya Leo, Tujifunze Kuhusu Basic Concept Ya Laptop Hardware, Tujifunze Kufunga Na Kuifungua Laptop Yenyewe Na Elimu Kidogo Ya Laptop Charger.

Laptop ni aina ya Computer ambayo ni portable ina maana mtu anaweza kuibeba na kuhama nayo kutokuwa nzito sana na rahisi kubeba.

Laptop kiutaalamu ina part 2, hardware na software, hardware part tunayoangalia hapa ni Kitu Chochote Unachoweza Kukishika Katika Laptop Kwa Lugha Rahisi.

Laptop inapewa nguvu ya umeme kutoka kwenye charger na battery lake kama charger haitakuwepo.

Charger Nyingi Za laptop zina range Voltage Kuanzia 18V, 19.5V Mpaka 20V DC.

Swali: Nitajuaje Kiasi Cha Umeme Kinachotoka Kwenye Charger?
Je Laptop Yangu Inatakiwa Kupokea Umeme Kiasi Gani?

Jibu: Nyuma Ya Charger Zote Za Laptop Kuna Indications Ya Umeme Unaotakiwa Kuingia Na Kutoka, OUTPUT na INPUT, Na Pia Nyuma ya Laptop Zote Kuna Indication Ya Moto Sahihi Unaotakiwa Kuingia Kwenye Laptop Yako. ANGALIA PICHA CHINI

Altenative: Unaweza Kuangalia Voltage Range Google Kwa Kutumia System Model Na Brand Name Hii Utaiona Nyuma Ya Case Y a Laptop Yako Na Pia Imeandikwa Kwenye Motherboard.

Mfano: TOSHIBA C850-PSCBWE-OHFOONEN ( Unapofanya Kutafuta Details Au Kitu Cha Laptop Mtandaoni Hakikisha, Unamalizia Hizo Model Item Numbers, Watu Wengi Huwa Wanafanya Search Kwa Kuandika Tu Herufi Za Mwanzo Mfano TOSHIBA C850 Basi, Ukifanya Hivi Kuna Posibility Kubwa Ya Wewe Kupata Details Zisizo Sahihi)

Kipi Cha Kuangalia Kwenye Charger Ya Laptop Kama Fundi Au Wakati Unanunua Charger?

1. Voltage SAHIHI
2. Watts (What Ndogo Hazitachaji Laptop Yako Au Zitaifanya Iwe Slowly Mfano: Kuna Watu Wakichomeka Charger Laptop Zao Touchpad Inakuwa Nzito)
3. Power Series (Laptop Nyingi Zina Power Series Moja, Means Kwenye Cord (Kile Kichuma Cha Charger Kinashabihiana Utoaji Wa Umeme Mfano: Pini Ya Kati Ni Ve+ Na Mzunguko Wa Duara Pembeni Ni Ve-, Lakini Laptop Nyingine Ni Tofauti)
4. Amps: (Kama utatumia charger yenye amps ndogo kuliko zinazotakiwa kwenye laptop, sio vizuri maana unaweza ukawa unachaji laptop kwa muda mrefu, au charger ikawa ina overheat sana au isicharge kabisa laptop yako.)
5. Case: (Kama Kuna Leakage Yoyote Kwenye Case Ya Charger Basi Achana Nayo, Kwa Maana Inaweza Kusababisha Jeraha La Short Kwa Mtumiaji)
6. Brand: Kama Wewe Ni Mtumiaji Wa HP Basi Tafuta charger ya Hp Maana Kuna Watu wengi huwa wanafoji charger za Dell Kwenye HP ambapo sio sahihi kwa maana charger nying za dell ni Njia 3 na HP ni Mbili Viceversa)

MATATIZO YA CHARGER

Kwa Fundi Wowote Wa Laptop Kituo cha kwanza cha kukimbilia ni charger ya laptop kwa upande wa hardware mfano: Laptop Haiwaki, Laptop Ina Blink, Laptop Haicharge, Laptop Inawaka Then Inazima Kabla Ya Booting.

Bahati mbaya sana laptop charger nyingi zimetengenezwa kiroho mbaya, huwezi kuifungua kwa screwdriver kwa maaana haina Screws, So Hawataki Uifungue Na Kuifanyia Repair Nadhani Sababu Ya Hatari Ya Short Ya Umeme. So Kuifungua Mara Zote Ni Kwa Kuivunja Mimi Huwa Natumia Hummering Method, Nagonga Nyundo Kwa Kutumia Screw Drive.

TATIZO LA 1
Power Cable (Flower), Imekufa Au Inamiss Njia Moja Hili Ni Tatizo Kubwa Kwa Maana Mara Nyingi Adapter Hawezi Kufa Kwa Sababu Ina Switching Power Supply Yenye Short Protection, ikitokea Fault Basi Inakata Moto Na Kuizima Kabisa (Utaona Adapter LED inazima Kama Vile Haina Moto)

UTAJUAJE
Kama Huna Multmeter Basi Tafuta Flower Cable Nyingine, Au Kwa Multmeter Tumia Diode Mode Ambapo utaangalia Continuity Ya Nyaya Zote Ambapo Kama Kuna Connection Basi Utasikia Beep Sound.

UTATUZI
Hizi Cable Ni Cheap Sana Kariakoo Huwa Wanauza 2500 Hadi 10000, So nashauri nunua tu nyingine, usiiunge, maana umeme unaopita hapa unaweza kusababisha majeraha kwako.

TATIZO LA 2
Charger Cord Imeharibika: (Inagusa Njia Nyingine Au Chuma Kimekatika Au Chuma Kimekosa Umeme Baada Ya Wire Kuachia, Hii Ni Common Sana kwa charger za DELL Especially za njia tatu, ambapo utaona charger inawasha laptop
lakin haichaji, pin ya kati ambayo ni ya signal inakuwaga na 4V ndiyo inakuwaga imemis hivyo ukifanya Test kwa Multimeter utaona una Njia Mbili Zenye 19V Lakin Charger Haichaji.

UTAJUAJE
Pima kwa kutumia Multimeter All Three Pins Kwenye Chager Cord lazima Ziwe Na Umeme, Au Ukichomeka Charger Halafu Ile LED Kweny Adapter Ikizima, au Ukiona Cheche Kwenye Charging Port Wakati Ukichomeka Charger.

SULUHISHO
Kama Kuna Uwezekano Wa Kuzi Arrange Tena Hizo Charger Basi Fanya Hizo Then Rudishia Na Hot Glue, Ikishindikana Basi Badili Adapter Nzima.

TATIZO LA 3
Adapter Kuungua: Hii sasa ni tatizo kubwa ila sio sana kwa maana ni mara chache sana kutokea kama charger adapter imeungua, suluhisho ya hili ni kufanya manunuzi ya adapter mpya kama huna skills advanced za electonics kwa maana utakuwa una deal na live AC Current, hivyo upo katika hali kubwa ya kupata madhara yatokanayo na umeme.
Kwa advanced learner unaweza kuipasua na kuangalia shida na mara nyingi inakuwaga ni Shorted Cap.

TUTAIANDALIA SESSION YAKE ADVANCED LAPTOP CHARGER REPAIR KWA SASA TUISHIE HAPA

TUIFUNGUE LAPTOP

Moja kati ya vitu muhimu na vya kuvifahamu sana na ni mtihani wa kwanza kwa mafundi wengi ni kujua kufungua laptop (DISASSEMBLE) Pamoja na kuirudishia, Hapa ndipo unapomaliza kuifunga laptop yote na kukuta Screw Zinabaki Hazijafungwa na hujui za wapi.
Kabla Hujafungua Laptop Hakikisha Una Vitu vifuatavyo:

1. Screwdrives (Kariakoo Set Elu 5-10)
2. Pry Tools (Hii kwa ajili ya kutolea lock za case ya laptop naa simu)
3. Tweezers (Kazi nyingi lakin hapa kubwa ni kutolea Ribbon cable)
4. Screw Container and Organizers (Hii ni simu haswaa kwa wale wanaobaki na screw baada ya kufungua)
5. Meza Safi Ya Kufanyia Kazi ( Hakikisha mahali unapofanya kazi ni safi na salama, hakuna vimiminika, hakuna uchafu uchafu, pako na mpangilio mzuri, hii itakurahisishia kutopoteza muda na vifaa)

HATUA ZA KUFUNGUA LAPTOP

1. Hakikisha laptop haina chanzo chochote cha umeme, Toa battery na hakikisha umeichomoa kwenye charger. (Hii inasaidia kuepuka short wakati wa kutoa cable cable slot zake, na pia kuepuka madhara ya umeme kwako pia inagawaje umeme unaokuja kwenye motherboard sio mwingi)
2. Anza Kufungua Screws Zinazohusika Na Vitu Muhimu Nyuma Ya Laptop, Kuna Screw Za KEYBOARD, CD DRIVE na Za Hard Drive Kwenye Bahadhi ya laptop za zamani haswaa dell mfano: 620, So anza kufungua kwanza hizi kama zipo.
3. Fungua Screw zote za nyuma ambazo zipo katikati au zimeshikilia part ya nyuma inayoweza kutoka kirahisi mfano: Cover la nyuma lenye Hard drive, RAM na Network card.
4. Jaribu Kutoa Hilo cover la nyuma, kama lipo na kama ukifanikiwa basi fungua nut nyingine zote unazoziona nyuma ya laptop yako.
5. Jaribu kuitoa keyboard na kama utafanikiwa basi fungua pia screw zilizopo chini ya keyboard ambazo huwa zinashikiria motherboard moja kwa moja. HAPA KUWA MAKINI NA CONNECTOR YA KEYBOARD NI RAHISI KUKATIKA
6. Hakikisha screw zote zimeisha, Then Anza Kujaribu Kutoa Cover Lolote Laptop Kwa Kutumia Pry Tools Fanya Taratibu Kubandua Ili Usije Vunja Lock Za Case, kwa laptop nying cover la juu ndio linatoka then la chini ndio linashikilia keyboard ila usikariri, laptop mpya kama Lenovo Case ya chini huwa inatoka kwanza, HAPA KUWA MAKINI SANA NA CONNECTOR ZA TOUCHPAD, SPEAKER, POWER BUTTON, Hakikisha zote umezichomoa.

7. Ukifanikiwa Vyote Hivyo Basi Utakutana Kitu Kama Hiki Hapa Chini, Wewe ni Shujaa Kwa Part Hii

Sio vitu vigumu ukijifunza unaweza.