Utashi wa Mungu na Upendo wa Mungu - Luisa Piccarreta
42 subscribers
289 photos
54 files
586 links
Fahamu kuhusu kutimia kwa Sala ya Baba Yetu kupitia Maandishi ya Mtumishi wa Mungu Luisa Piccarreta, Binti Mdogo wa Utashi wa Mungu - Kuishi Utashi wa Mungu
Download Telegram
SAA YA SABA

Sasa tunajitumbukiza katika mabahari ya mwanga na ya utakatifu ya Mama wa Mbinguni. Pamoja naye tuwe tunaomba Ufalme wa Utashi wa Mungu ufike duniani.

Ewe Pendo Langu, ninaonja kuwa Pendo Lako limejaa mno na linafurikia ndani yangu. Ninakuona ukivua joho lako la Haki, na Ninyi Nafsi zote Tatu za Mungu mnajipanga na kujiweka tayari kwa ajili ya sherehe mpya; na inaelekea sherehe hii ni kubwa zaidi ya ile iliyokuwa imefanyika katika tendo lile la kumwumba binadamu. Ninyi Wenyewe, mnatoa nje yenu wenyewe, mabahari ya Maweza, ya Hekima, ya Pendo, na ya Uzuri upendezao usioelezeka. Halafu mnayakusanya mabahari hayo mahali pamoja. Kishapo, kutoka kwenye kina cha mabahari hayo, kwa nguvu na uwezo wa neno Lenu la uumbaji, mnamwita Malkia Mdogo ambaye mnamtia na uhai. Mnamtengeza awe safi kabisa, bila doa lolote, na mnamfanya awe amejaliwa na neema za uzuri upendezao. Ni mzuri hivi hata anamteka Yule Mwenyewe aliyemuumba.

Kipindi hicho cha kuibeba mimba ya huyu Malkia Immakulata, panazinduliwa sherehe nyingi baina ya Mbingu na ya dunia. Uumbwa wote unashangilia na unapiga magoti yao. Wote wanampongeza na wanamshangilia kama Malkia wao. Hata mimi ninapiga magoti yangu mbele yake huyu ambaye Mungu Baba, Mwana na Roho Mtakatifu wanamgombania, ili mmoja wao au mwingine anayemtaka ajiburudishe naye zaidi, na kama anamtaka, aweze kumfaidi kwa vikubwa zaidi. Katika hatua hiyo, ninyi Wote, Nafsi Tatu za Mungu, hamtendi kitu chochote tena, isipokuwa kujaa na kufurika Pendo ambalo mnaendelea kummwagia daima huyo Malkia Mzaliwa mpya. Na wala hamuachi kamwe kumwaga viwango vingine zaidi vya neema juu yake ili kukuza mabahari yake yawe makubwa zaidi na mapana bila ukomo wowote. Ndani ya binadamu huyu wa Mbinguni, mnamgundua Yule Mwanamke, ambaye ndiye atapasika kuwapatieni Ninyi kila kitu, atakayepasika kulipa fidia ya mambo yote, na atakayepasika kuwarejeshea ule utukufu wote wa Uumbwa. Kwa minajili hiyo basi, huku mkiendelea kumshikilia, mkimbana penye magoti Yenu ya Kibaba, mnamfunulia kumwonyesha na kumweleza juu ya kisa cha binadamu aliyekuwa ameanguka katika dhambi, mnamweleza juu ya uchungu wenu, na mnamweleza juu ya Utashi Wenu Mwabudiwa, ambao ulikuwa umegomewa na kusukumizwa mbali na binadamu. Mwishowe Ninyi mnayakabidhi mambo yote kwake huyo Malkia.

Katika hatua hii, Ewe Yesu Wangu, mimi ninatehemu, ninaonja uchungu sana sana kushuhudia jinsi Utashi Wako pendevu ukigomewa na kusukumizwa mbali. Papo hapo ninastaajabu ushujaa wa huyu Malkia Mdogo Mzaliwa mpya, ambaye anautoa uhai wake kama zawadi. Anaapa kuwa hapendi kusikia wala kuujua tena, na ndipo anautumbukiza ndani ya FIAT Yako, ambayo sasa ndiyo anayoitwaa iwe ni uhai wake. Anatoa mamlaka kwa FIAT hiyo, na ndani yake anaunda Ufalme wa kwanza wa Utashi Wako ndani ya roho yake. Na kutoka pale ndani ya roho yake ninasikia kiitikio chake hiki endelevu: “Ufike Ufalme wa Ukombozi, afike Neno hapa duniani, ifike na amani kati ya Muumba na mwanadamu! Mimi sitateremka toka hapa penye magoti yenu ya Kibaba, endapo Ninyi hamtanijalia hicho ninachowaombeni”. Na angalia sasa, Malkia Mdogo analia machozi, hata anailowesha mikono Yenu ya Kibaba kwa machozi yake. Mara nyingine anawatazama na kutabasamu na halafu anawaombeni. Kisha, anapojitumbukiza katika yale mabahari mliyompatia, anawaleteeni furaha mbalimbali na raha ya Utashi Wenu, hata anaweza kuwashindeni na kuwalegezeni, ili tu aje ampate Mkombozi ajaye. Oh, ni mbinu ngapi na ujanja gani wa pendo, alizotumia Mama yangu wa Mbinguni juu yenu! Ni jinsi gani alivyokuwa akiwateka kwa mitindo yake ya kupendeza ajabu, kiasi kwamba Wewe, Pendo Langu, mwishowe ukashindwa na kukubalia maombi yake na kilio chake kisichokoma.


Baba yetu...,
Salamu Maria...,
Atukuzwe Baba...
SAA YA NANE

Pamoja na Mama wa Mbinguni tunaendelea kumsihi Mungu Baba wa Mbinguni, ajalie kwamba Utashi wa Mungu ujulikane kwa watu wote na pia kwamba Ufalme Wake ufike.

Ewe Yesu, Uhai Wangu mtamu mno, ebu uchukue na uipeleke roho yangu hii ndogo pale juu ya magoti ya kibaba ya Mungu Baba yetu wa Mbinguni, ikawe pale pamoja na Mama yangu Malkia. Roho yangu iwe pale kusudi iwe inasali, inalilia na kutamani kwamba Ufalme wa FIAT Yako ya Kimungu ufike. Na kwa tabasamu zangu za pendo, kwa mabusu yangu ya upenzi, na kwa mabembelezo yangu kwenu Nyote Nafsi Tatu za Mungu, niweze kuziteka kwa nguvu ile ile ya utekaji iliyomo katika Utashi Wako. Niuteke Utatu Mtakatifu hadi ukubalie ombi langu la kuleta Ufalme Wako hapa duniani. Na kwa kweli, ninapojitumbukiza ndani ya mabahari ya Mama yangu, huyu binti mdogo wa Utashi Wako wa Kimungu, anapenda kutengeneza mabahari yake madogo madogo ndani ya mabahari ya Mama yake. Yeye Mama atatoa nafasi kwa binti kuweza kuingia ndani ya mabahari yake ili aweze kutengeneza mabahari yangu ndani ya mabahari yale yale yake Mama, ili niweze kuendelea kusihi Ufalme wa Ukombozi kama yeye alivyokuwa amesihi.

Basi sasa, ewe Mama Mtakatifu, toa mkono wako kwa Binti yako Mdogo, na wewe mwenyewe unisaidie niweze kuogelea katika bahari ya pendo lako, ili pale nikaweze kugonga muhuri wa ‘Ninakupenda’ yangu isiyokoma katika bahari yako ya pendo na pale niweze kutengeneza bahari yangu ndogo. Ndipo, kwa bahari ya pendo la Mama, pamoja na bahari ya pendo la Binti tunakusihi utupatie Ufalme wa FIAT Yako. Kishapo ninaendelea na kuingia katika bahari ya uabudu ya Mama yangu, ili pale ndani nikatengeneze bahari yangu ndogo ya uabudu kwa Muumba Wangu na nikaendelee kuomba Ufalme Wake. Naendelea kuruka juu ya mabahari ya sala zake, ya maombi yake, na matamanio yake, ili nitengeneze mabahari yangu ya sala, ya maombi na ya matamanio kwa ajili ya kuweza kusihi Ufalme wa FIAT kwa njia ya sala zile zile za Mama wa Mbinguni. Ewe Mama yangu Malkia, mabahari yako hayana ukomo. Kwa sababu hiyo, ipo daima nafasi kwa ajili ya kuweza kuingiza vitendo vidogo vidogo vya Binti yako Mdogo. Basi, unisaidie Wewe mwenyewe kuingiza haya mambo yangu yafuatayo, ndani ya bahari ya maumivu yako na ndani ya bahari ya uchungu wako mkali: ingiza maumivu yangu madogo madogo, ingiza miaka yangu mingi na migumu ya kitandani, maumivu ya kuachika na sadaka mbalimbali, na lile teso lililoniumiza zaidi kupita yote, la kuachika mara kwa mara na Yesu, teso linalonigharimu maumivu ya mauti endelevu.

Ewe Mama yangu, unganisha maumivu yangu hayo yote kwa pamoja, ukayaingize katikati ya bahari ya mateso yako mengi na makubwa. Ndipo na mimi niweze kutengeneza bahari yangu ndogo ya teso. Kwa bahari yako ya teso, pamoja na bahari ya kwangu, niweze kuomba bila kukatisha, kwamba Ufalme wa Utashi wa Mungu ufike haraka, kwamba uteremke na kuja kati ya wanadamu, na kwa sherehe ya ushindi, Utashi huo utawale na ushike himaya yake kati yao.

Ewe Mama yangu, je wewe hupendi kumfurahisha Binti yako Mdogo, kwa kuweza kusema pamoja nami, kuweza kubeba pendo moja tu, kuwa na Utashi mmoja tu, kuwa na tendo moja tu na kuwa na sauti moja tu isemayo: ‘MAPENZI YAKO YATIMIE’ hapa duniani kama kule Mbinguni’*** ?

Na kama vile wewe, kwa njia ya mabahari hayo, wewe, kwa kutolea tumbo lako pawe mahali pa kumpokelea, uliweza kumfanya Neno atoke Mbinguni na ukamfanya ateremke kuja hapa duniani, ndivyo na sasa, kwa njia ya mabahari haya, ufanye FIAT ya Juu itoke kwenye kiti chake cha Mbinguni na ifike hapa duniani. Mimi najitolea mwenyewe kuipokea, kusudi iingie na kubaki imebebwa mithili ya mimba ndani ya roho yangu, na pale itengeneze Ufalme wake ndani yangu mimi, na kutoka kwangu iweze kwenda kutawala katika wanadamu wote.

***Katika Kilatini: FIAT VOLUNTAS TUA, SICUT IN COELO ET IN TERRA!

Baba yetu...,
Salamu Maria...,
Atukuzwe Baba...
SAA YA TISA

Tunaendelea kufuatilia Utashi wa Mungu katika tendo la kutungwa mimba ya Neno na katika tendo la kuambatana na Yesu, Mfungwa Mdogo, katika tumbo la Mama Yake.

Ewe, Mama yangu Mkuu mwenye mamlaka, mimi ni mdogodogo mno. Sipendelei kubaki peke yangu bila wewe, kusudi katika matendo yako yote, uweze kuunganisha na matendo ya kwangu ili kufanya liwe tendo moja tu litakalotuwezesha wewe na mimi, kwa pamoja, kuomba Ufalme wa Utashi wa Mungu. Kwa minajili hiyo, katika FIAT ya Kimungu hiyo hiyo, mimi ninafuatilia sasa lile tukio la kutungwa mimba kwa Neno ndani ya tumbo lako la kimama. Ninalifuatilia kusudi, pale ndani ya tumbo lako, nikaingize na kuyapanga matendo yangu yote niliyokwisha kuyafanya ndani ya FIAT, halafu nikaweke juu yao mhuri wa ‘Ninakupenda’ yangu endelevu, ili yawe kama kikosi cha kukesha pamoja na Neno. Nitaweka hapo pia maumivu yangu madogomadogo ili wakati unapomtunga mimba ndani yako, mimi niwe ninamwingizia matendo ya kwangu pamoja na yale ya kwako, ili kwa pamoja yawe yanamfanya atungike mimba. Ndipo hapo mimi ninamwomba Ufalme wa Utashi wa Mungu, kwa nguvu ya lile pendo kuu aliloonyesha pale alipoteremka kutoka Mbinguni, na kuja kujifungilia ndani ya mahabusu haya membamba ya tumbo lako,

Oh, wewe kama Mama yangu, mimi ninapenda nijifungilie ndani ya tumbo lako nikiwa pamoja na Yesu Wangu mdogo, ili niwe ninakesha pamoja naye, katika upweke anaouonja ukimtesa. Hapo nitakuwa nikishuhudia kwa macho yangu maumivu yake yote, ili niweze kuyafuatilia kwa mhuri wa kauli yangu ya ‘NINAKUPENDA, NINAKUHESHIMU, NINAKUSHUKURU’. Hapo ninaona kwamba, maadam Mtoto Wangu Yesu anaanza kupata yale maumivu makali sana, na vifo endelevu, kutokana na zile mara zote ambapo wanadamu walikuwa wameusukumia mbali na kuugomea Utashi wa Mungu, na wala hawakuruhusu uanze kuendesha uhai wake katika roho zao. Kwa hivyo, Utashi ulikuwa unaonja kifo, na Wewe, ee Yesu, pale pale umekuwa ukipenda kubeba vifo vyote hivyo juu ya mabega yako. Umefanya hivyo kwa ajili ya kulipa malipizi kwa Utashi Mkuu wa Mungu. Kwa hiyo ninakuona, ingawa kama u kadogo bado, lakini unateseka na maumivu makali kabisa. Ninaonja moyo wangu ukipasuka ninapokuona unaingia katika hatua ya kufa. Kwa upande wangu, Ewe Mtoto wangu Mchanga na laini, ninapenda, hapa ndani ya roho yangu, niwe ninatoa uhai kwa FIAT ya Kimungu katika mara zile zote ambapo wanadamu wamekuwa wanaigomea na kuisukumizia mbali. Mara nyingi nimekuwa nikitaka kuulia mbali utashi wangu, kwa mara zile zote ambapo wanadamu wamekuwa wakiupatia fursa ya uhai. Badala yake, ndani ya Ubinadamu Wako mdogo, ninataka nitiririshe uhai wa Utashi Wako wa Kimungu ambao ninaubeba hapa ndani yangu. Ninafanya hivyo ili kusudi, hayo maumivu makali mno unayoyapata pamoja na maumivu ya kifo unayoyakabili, yaweze kupunguza makali yake.
Ewe Mpenzi sana Mtoto Mchanga, ni maumivu mangapi unayoyapata hapo ndani ya tumbo la Mama yetu Malkia! Ninakuona ukikosa umudu wowote, unashindwa hata kutikisa kidole chochote kile wala kamguu kako. Huna hata kanafasi kwa ajili ya kuweza kufungua hayo macho yako mazuri, hamna hata kamwanya kadogo kanakoweza kukupitishia walau mwonzi moja wa mwanga. Hapa, katika mahabusu haya membamba ya tumbo la kimama kila kitu ni kiza totoro. Hali hiyo yote inanieleza maumivu ambayo Wewe unayoyapata. Inanieleza jinsi wanadamu walivyosababisha Utashi Wako Mwabudiwa kukosa kabisa ujimudu wa aina yoyote. Inanieleza pia ni jinsi gani wanadamu wote wanavyokuwa ni vipofu hata kushindwa kuuangalia na kuujua Utashi wa Mungu. Na inanieleza kwamba, bila Utashi wa Mungu, roho zao wanadamu hubaki katika usiku wa kiza totoro. Na mimi, Ewe mpenzi wangu Yesu Mdogodogo, ninapenda nipeleke uhai wa Utashi Wako pale ndani ya yale mahabusu finyu, yaliyokuwa ndiyo makao yako ya kwanza hapa duniani. Kwa tendo hilo ninataka nitengeneze pambazuko katika lile giza totoro inayokuzunguka. Nataka nibandike hapo busu langu, nataka nibandike na mhuri wa ‘Ninakupenda’ yangu juu ya kila kiungo cha mwili wako ambacho kinakosa ujimudu wowote. Ndipo nitakuwa nikikuomba kwamba, kwa maumivu hayo unayopata, Utashi Wako wa Kimungu uanze kutekeleza ujimudu wake ndani ya wanadamu. Nitaomba kwamba kwa nguvu ya mwanga wake, ufukuzie mbali ule usiku wa giza la utashi wa kibinadamu, na badala yake, hapo ndani yao wanadamu, Utashi Wako utengeneze pambazuko endelevu lisilokoma la FIAT Yako.

Ewe Mtoto Wangu Mpendevu, kama mimi, katika ombi langu hili, sitaweza kukushinda Wewe sasa hivi wakati u bado kadogodogo, hata uweze kunijalia Ufalme wa Utashi Wako wa Kimungu, ebu basi unieleze, ni lini nitakuja kukushinda? Je, unajua lakini, Ewe Mtoto mpenzi, kwamba huyu msichana mdogo wa roho yangu, kwa maweza na nguvu ya FIAT Yako, anapenda akushinde Wewe kwa pendo. Kwa sababu hiyo basi, mimi, katika hiyo FIAT, ili kuja kunisaidia, ninaita matendo yote ya Utashi Wako wa Kimungu, yaje sasa na yasimame na yajipange kukuzunguka Wewe, kama kikosi cha jeshi lenye nguvu kabisa. Ninaita pia anga lote pamoja na jeshi lake lote la nyota, lifike kukuzunguka. Ninaliita na Jua pamoja na nguvu ya mwanga wake, na nguvu ya joto lake, ninaita na upepo pamoja na mvumo wake mkali wa himaya yake, ninaiita na bahari, pamoja na mawimbi ya dhoruba kali, na ninaita pia na Uumbwa wote. Mwishowe nitahamasisha na kunogesha mambo yote, nikiimbilia kwa sauti yangu, huku nikizunguka kufuatilia na kubandika juu ya matendo Yako yote, ule mhuri wa kauli yangu ya ‘Ninakupenda’ pamoja na ile kauli ya wanadamu wote. Hiyo ni kwa ajili ya kukuomba Ufalme wa FIAT Yako ya Kimungu.
Ewe Mtoto Wangu Mchanga na Laini, je unakiona, hicho kikosi cha kukupokea na kukusindikiza, nilichopenda kukuandalia, ili upate kukikuta wakati unapotoka tumboni mwa Mama? Kazi Zako zote zikiwa zimejipanga kama kikosi cha jeshi kinachokuzunguka Wewe, huyu msichana mdogo anapenda kukuambia Wewe na wanadamu wote: “Ninakupenda, Ninakupenda, Ninakupenda! Ninakuheshimu, Ninakushukuru, Ninakuabudu!” Na pamoja na watu wote ninapenda nibandike mhuri wa kauli yangu ya ‘Ninakupenda’ na nibandike pia busu langu la kwanza juu ya hiyo midomo yako inayotetemeka, wakati ukitoka tumboni mwa Mama na ukiwa unakimbilia kwenda kukumbatiwa na mikono ya Mama wa Mbinguni. Na yeye alikukumbatia sana na kukubana kifuani pake, alikubusu, na alipokupa maziwa yake unyonye alikupasha joto na kukutuliza usilie. Kwa jinsi nilivyo bado ni msichana mdogo mno, hata mimi napenda nikaingie pale katika mikono ya Mama nikumbatiwe, na juu ya busu lile lile analokupa, nami ninabandika busu la kwangu. Katika maziwa yake Mama, ninapenda kutiririsha ‘Ninakupenda’ yangu, kusudi, kama Mama anakulisha kwa maziwa yake, mimi nitakulisha kwa pendo langu. Kila kitendo anachokufanyia yeye Mama, nami napenda kukutendea hicho hicho. Ebu angalia, Ewe Mtoto Wangu Mpendwa, mimi hapa sipo peke yangu, nina kila kitu hapa: Lipo jua kwa ajili ya kukupasha joto, zipo hapa Kazi Zako zote kwa ajili ya kukutuliza usilie. Kwa minajili hiyo nipo nikifuatilia vilio vyako, malalamiko yako laini, na kwa vile unajiona hupendwi na wanadamu, mimi napenda niwe kama yaya Wako ili niwe ninakubembeleza kwa kukuimbilia: ‘Ninakupenda, Ninakupenda’ hata uweze kupata usingizi. Yote hayo ni kwa lengo kwamba mara nitakapokuona unashituka toka usingizini, mimi niwe ninakuomba Ufalme wa FIAT Yako.

Ewe Mama yangu, tafadhali unisaidie. Wewe, ukiwa pamoja na mimi, umwambie Mtoto huyu wa Kimungu: “Tafadhali umfurahishe huyu Binti yetu Mdogo ambaye hana kingine anachotaka na anachotamani na kulilia isipokuwa anaomba Utashi Wako ujulikane na utawale hapa duniani”.

Baba yetu...,
Salamu Maria...,
Atukuzwe Baba..
SAA YA KUMI

Tumfuate Mtoto Mchanga Yesu akiwa mikononi mwa Mama Yake wa Mbinguni, akiwa katika maumivu ya Kutahiriwa, na tufungilie tashi zote za kibinadamu ndani ya jeraha lake lenye maumivu
.
(Katika makala ya mkono hapa hufuata kile kilichoandikwa katika Juzuu Na. 17 - Hiki kinachofuata hapa chini ni kile ambacho kiliachwa kuandikwa katika Juzuu ile)

Ewe Mtoto Wangu Laini, kauli yangu ya ‘Ninakupenda’, ‘Ninakuheshimu’, na Ninakushukuru’ itakuwa inakufuata popote kwa ajili ya kukuomba FIAT Yako. Katika kila pigo la Moyo wako na katika kila pumzi yako, katika ulimi wako, katika mboni ya macho yako, kama vile matone ya damu yako yanavyojiongeza ndani ya Ubinadamu Wako mdogo, ndivyo na mimi nanuia kubandika mhuri wa ‘Ninakupenda’ yangu na busu langu juu ya kila moja ya mawazo yako matakatifu, juu ya mikono na juu ya viganja vya Mama wa Mbinguni na vya Mtakatifu Yosefu. Naweka huo muhuri kusudi hao wanapokubana kifuani pao, Wewe uwe unaionja ‘Ninakupenda’ yangu. Ninabandika muhuri hata katika pumzi za hao wanyama waliolala kimya hapo miguuni pako wakikupasha joto na kukuabudu kwa tendo lao la kufungua midomo yao na kucheua. Katika pumzi yao hiyo mimi napenda Wewe uwe unasikia ‘Ninakupenda’ yangu ambayo inakuomba FIAT Yako ya Kimungu.

Ewe Mtoto Wangu upendezaye na kuvutia sana, hiyo kauli yangu ya ‘Ninakupenda’ itakufuata hadi kule kwenye tendo la kukatwa kikatili wakati wa kutahiriwa. Katika ile Damu yako ya kwanza uliyomwaga, mimi nataka, kwa ‘Ninakupenda’ yangu, nipozeshe maumivu makali uliyopata. Juu ya kila tone la Damu hiyo, napenda kutia mhuri wa ‘Ninakupenda’ yangu, juu ya machozi yale uliyomwaga Wewe kutokana na maumivu, aliyomwaga Malkia Mwenye mamlaka kuu, na aliyomwaga Mtakatifu Yosefu walipokuwa wanakuona unavyoteseka. Damu ile, teso lile, na machozi yale, vyote vinaomba ushindi mkuu wa Ufalme Wako. Ewe Mpenzi Wangu Yesu Mdogodogo, napenda nikukumbatie kifuani penye moyo wangu ili nipozeshe maumivu na uchungu unaopata. Ndani ya hilo jeraha la kutahiriwa napenda kufungilia tashi zote za kibinadamu za wanadamu kusudi zisiwe na uhai wala ujimudu tena. Na kutoka katika jeraha hilo utokee sasa Utashi Wako wa Kimungu kuja kutawala kati yao wanadamu.

Baba yetu...,
Salamu Maria...,
Atukuzwe Baba..
SAA YA KUMI NA MOJA

Tunamfuata Mtoto Yesu anayekimbilia Misri. Tunaualika Uumbwa wote kuja kumbembeleza. Na pamoja nao wote tunaomba tuupate Ufalme wa Utashi wa Mungu.

Ewe Mtoto Wangu Mpendevu, pindi lile jeraha la kutahiriwa likiwa bado linatoa Damu, teso lingine zaidi laongezeka kukukabili Wewe: Ni mwuaji mkatili mmoja anayekutafuta ili kukuua. Wewe unapasika kwa lazima kutorokea Misri kwa ajili ya usalama wako. Hiyo ni tena ishara nyingine ya njama za utashi wa kibinadamu ambao unataka kuudhulumu Utashi Wako wa Kimungu ili kuuzuia usitawale.

Mtoto Wangu Maridadi, katika teso hili, ninapenda nitiririshe ‘Ninakupenda’ yangu, mabusu yangu ya upenzi, na pia utashi wangu ili usiwe na uhai tena, kwa ajili ya kuleta upatanisho na kujenga undugu baina ya utashi wa kibinadamu na Utashi wa Mungu na hatimaye kutengeneza Utashi moja tu. Na kwa nguvu ya hilo teso lako kali ninapenda nikuombe FIAT Yako. Basi kwa hiyo, pindi Mama anapokuwa amekubeba mikononi mwake, mimi ninafuata hatua za huyo Mama yangu. Na anapotembea, toka chini ya nyayo zake, ninapenda Wewe uwe unasikia ile kauli yangu ya ‘Ninakupenda’. Kwa sababu hiyo, hatua kwa hatua, juu ya kila atomu ya ardhi, juu ya kila unyasi au jani analokanyaga, mimi ninabandika hiyo kauli, na huku nikihamasisha mimi mwenyewe kwa sauti yangu, ninapenda Wewe uwe unasikia, toka pale kwenye nyayo za Mama yangu, kile kiitikio kinachosema: ‘Ninakupenda, Ninakuabudu, Ninakuheshimu, Ninakushukuru’. Na kama vile wewe unavyokimbia kwa lengo la kuniletea mimi uhai, mimi napenda nitoe uhai wangu uwe kwa ajili ya kutetea Uhai Wako, na napenda nikuombe sherehe ya ushindi wa Utashi Wako. Wakati huu unapokimbia, Ewe Pendo Langu, naonja moyo wangu ukipasuka, ninapokuona ukilia kwa uchungu, ukihema na ukitehemu. Moyo wangu unapasuka ninapoona jinsi unavyotafutwa, siyo kwa lengo la kukupatia mahali pa kulala, bali kwa lengo la kukuua. Mimi napenda nitulize machozi yako kwa pendo langu. Napenda pia kutwaa uwezo wa kuwa mahali mbalimbali katika Uumbwa kwa wakati ule ule. Kwa mfano, ili kukufurahisha, ninapenda usikie ‘Nakupenda’ yangu ikitokea toka kule ndani ya bahari. Mimi mwenyewe nikiwa ninahamasisha, kwa sauti yangu, matone yote ya maji, michezo yote ya samaki, napenda uwe unasikia ‘Ninakupenda’ ya viumbe vyote visivyo na sauti vinavyoishi pale baharini, na napenda usikie pia ule musiki wangu mzuri wa pendo, unaopita misiki yote, musiki wenye kile kiitikio changu: Ninataka FIAT Yako. Kwa wakati moja na uleule nataka niwe ndani ya Utashi Wako, juu ya ile milima mirefu kabisa, na katika mabonde yale ya kina kirefu. Nataka nikahamasishe mimea, maua, miti na mengine yote. Hao wote nataka wasikike wakisema: ‘Ninakupenda, Ninakupenda’. Juu ya mabawa ya Upepo ninapenda nikatengeneze sauti kali kupita zote ili Wewe uwe unasikia kauli ya ‘Ninakupenda’. Na katika mawimbi ya upepo nataka nipakie mabusu yangu motomoto na mapapaso yangu ya upenzi kwa ajili yako.
Ewe Mpenzi Wangu Mdogodogo, wakati wote unapotoroka, iwe usiku, iwe mchana, Wewe upo hadharani na unaonekana daima. Kwa hiyo ni vema tu kama mimi nipange kuviita vitu vyote vilivyoumbwa ili waje kumfurahisha Muumba wao. Basi ninaita sasa mwanga wote wa Jua. Unapoangazisha Uso Wako mzuri unatoa kauli kusema: ‘Ninakupenda’. Ninawaita na ndege wote waliopo angani, ili kwa nyimbo zao na sauti zao za kutetemesha, waweze kukutungia bembezi za pendo. Yaani tuseme, ninapenda nikupeleke hadi Misri ukiwa unasindikizwa na shangwe la ushindi la pendo langu, na kama kiitikio chake, ninakuomba Ufalme wa Utashi Wako. Sipo peke yangu, Ee Yesu, bali nipo pamoja na kazi zako zote. Je hivi husikii jinsi ilivyo nzuri na inavyopendeza: bahari, upepo, jua, nyota zinazometameta, vyote vikisema ‘Ninakupenda’? Anga, milima, mimea, vyote kwa pamoja na baina yao hupiga kelele kwa kadiri vinavyoweza vinasema: “Ninakupenda, Ninakupenda, tunautaka Utashi Wako unaotawala na unaoamrisha!”. Na mwangwi huo unasikika ukirudiwa katika kifua cha Mama Malkia na hata yeye anakuambia hivi: “Mwanangu, pendo langu hupatanisha na kuoanisha kila kitu, huunganisha tena vitu vyote, hushinda yote, na mwangwi huo unapopenya hadi ndani ya Moyo Wako, nao unakuomba FIAT Yako.

Baba yetu...,
Salamu Maria...,
Atukuzwe Baba...
SAA YA KUMI NA MBILI

Tupo na Yesu pale Misri; tunamtolea moyo wetu uwe makao yake, na pamoja na Malkia wa Mbingu, tunaomba Ufalme wa Utashi wa Mungu.

Mpenzi Wangu Mtoto Yesu, wakati mimi bado ninakufuata nakuta umekwisha kuwasili tayari pale Misri. Natambua kuwa popote unakoelekea unafuatwa na mateso, na machozi, na kusahaulika, kuachika na watu wote, kiasi kwamba unapasika kuingia kujihifadhi katika kibanda kidogo na duni sana; hakijawahi kukarabatiwa wala kusafishwa, hakina madirisha. Kinapigwa na pepo na huwa kinavuja maji wakati mvua zinaponyesha. Hakuna hata mtu mmoja duniani hapa anayekupa malazi. Oh, ni jinsi gani unavyolalamika, Ewe Mtoto Wangu Mchanga kabisa, unapoona kuwa Ubinadamu Wako mdogo unakabili mkasa ule ule wa Utashi Wako Mwabudiwa, yaani, kwamba hakuna mtu ambaye, kwa ukarimu na uhuru wake, anatoa nyumba ya roho yake ili kuukaribisha Utashi wa Mungu na kuuruhusu utawale pale na kuamrisha. Ingawa kama umekwisha kufika kati yao, hata hivyo, unaonekana kuwa kama mtangatangaji tu. Kwa miaka zaidi ya elfu sita, amekuwa akiomba nyumba bila kufanikiwa kupata. Na Wewe, Pendo Langu, unalia kwa ajili ya mateso ya FIAT Yako ya Kimungu.

Ewe Mdogodogo Wangu wa Mbinguni, unaona kuwa Mama yetu, wakati anapolia pamoja Nawe, yeye anaficha machozi yake ili kunyamazisha kilio chako. Anatolea roho yake safi kabisa kabisa iwe ndiyo makao ya kudumu ya Utashi Wako wa Kimungu. Hata mimi ninafuatilia kilio chako. Ninapenda nipanguse na kukausha huo Uso Wako Mtukufu wa kupendeza. Nataka nibandike mhuri wa ‘Ninakupenda’ yangu juu ya kila chozi, juu ya midomo ile inayotetemeka na inayolalamika. Kadhalika napenda kubandika na busu langu la upenzi. Nataka kukuomba FIAT Yako na ninakutolea moyo wangu uwe kama makao ya kudumu daima ya FIAT Yako ya milele.

Mtoto Wangu Mpendwa, uliye makao makuu ya uhai wangu, wakati wote unapoishi katika kibanda hicho duni, ninapenda kufuatilia matendo Yako yote, nafuatilia pia matendo ya yule Malkia Mtawala Mkuu wa Mbinguni. Wakati yeye anakubembeleza kwa kukutikisatikisa, na mimi nitapenda kukubembeleza kwa kukutikisatikisa na kukuimbia ili upate usingizi. Wimbo wangu ni huu: ‘Ninakupenda, Ninakupenda’. Wakati anapokuandalia kashati kakukuvalisha, mimi, katika ule uzi anaopitisha katika vidole vyake vya kimama, wakati wa kushona, nataka nitiririshe humo ile kauli yangu ya ‘Ninakupenda, Ninakuheshimu, Ninakushukuru, na Ninakuabudu’ kusudi wakati Mama yetu wa Kimungu atakapokuwa anakuvalisha, Wewe uwe unaonja kuwa vazi lako limeshonwa pamoja na ‘Ninakupenda’ yangu ambayo inakuomba FIAT Yako.
Ewe Moyo wa moyo wangu mdogo, wakati utakapoanza kujimudu na zile hatua za kwanza za kuyumbayumba, mimi napenda nitilie mhuri wa ‘Ninakupenda’ yangu, juu ya ile ardhi utakayokuwa unaikanyaga, ili kusudi uwe unasimama juu ya miguu yako mwenyewe. Na kwa mikono yangu, nitatengeneza uzio ili kukulinda na kukutegemeza usije ukayumbayumba na kuanguka. Ikitokea unayumba, mimi nitaweza kukukumbatia na kukubania kwenye moyo wangu. Ninagundua, Ewe Mtoto Wangu wa Mbinguni, kwamba mara baada ya kuacha kunyonya, na wakati huo ukiwa na uwezo wa kutembea mwenyewe, hata kama ungali bado ni kadogodogo, wewe unatoka na kujitenga na Mama kidogo, unapiga magoti yako madogo juu ya ardhi tupu, na huku ukipanua vimikono vyako vidogo, unasali, na unalia kwa ajili ya wokovu wa watu wote, na kwa kusihi sana na kuomboleza, unaomba Ufalme wa Utashi Wako wa Kimungu. Na kamoyo kako kadogo, kanapiga kwa nguvu kweli, kana kwamba kanataka kupasuka kwa sababu ya pendo na maumivu makali. Ewe Yesu Wangu Mdogo, ebu uniache tu mimi niweke kauli yangu ya ‘Ninakupenda’ hapo chini ya magoti yako madogo, kusudi hiyo ‘Ninakupenda’ yangu ilainishe na kulowesha kidogo hiyo ardhi isiwe kavu na ngumu mno kwa ajili ya viungo laini vya mwili wako. Tafadhali uniruhusu nitie mhuri wa ‘Ninakupenda’ yangu katikati ya mikono yako iliyopanuliwa na uniruhusu niishikilie hiyo mikono yako midogo miwili kwa mikono yangu ili usiteseke mno. Na wakati huo ninaposhikilia mikono yako, Wewe, Ee Mpenzi Wangu, unitwae mie kwa mikono yako hiyo midogo na unitolee kwa Baba wa Mbinguni, unitolee mimi Binti Mdogo wa Utashi Wako, huku ukinijalia nipate neema hii kwamba Utashi wa Mungu utawale ndani yangu mimi na ndani ya wanadamu wote.

Baba yetu...,
Salamu Maria...,
Atukuzwe Baba...
SAA YA KUMI NA TATU

Tunashuhudia siku ile Mtoto Yesu Mpenzi, kwa mara yake ya kwanza, alipojitokeza nje kwa watoto wa Misri. Tunamshuhudia akiwabariki, na sisi tunamwomba Yeye, kwa njia ya Baraka Yake, atie mhuri juu ya tashi za kibinadamu.

Ewe Mtoto Wangu wa Mbinguni, Pendo Lako linakusukuma utoke nje ya kile kibanda kidogo na uende nje. Na watoto wa Misri, wakivutwa na uzuri wako unaopendeza, wanakusanyika kwa wingi kukuzunguka, na Wewe, kwa upendo mkubwa unazungumza nao. Wakiwa wametekwa Nawe, wao wanakusikiliza. Baada ya kuwafundisha unahitimisha kwa kuwabariki na halafu unatoka ukikimbia kwenda kwa Mama Yako kwani pendo lake linaleta mwangwi ndani ya moyo Wako.

Wakati naye Mama anapokuita Wewe unakimbilia mara mikononi mwake. Ewe Pendo Langu, mimi ninapenda kukufuata katika kila kitu kwani napenda iwe inasikika tena ile kauli yangu ya ‘Ninakupenda, Ninakuabudu, Ninakuheshimu, Ninakushukuru’. Kauli hiyo iwe inasikika chini ya hizo hatua zako nyepesi, isikike unapotembeza hiyo mikono yako midogo, isikike katika maneno yako matamu, pendevu, yenye nguvu ya kuteka akili, na yaliyojaa uhai.

Napenda isikike hata katika mtazamo wa macho yako yanayovuta na kupendeza. Na katika hayo yote ninakuomba Ufalme wa FIAT Yako. Wakati huo unapowabariki watoto, ubariki hata mimi Binti Mdogo wa Utashi Wako na kwa Baraka Yako, ugonge mhuri wa uhai wa Utashi Wako ndani ya hii roho yangu ndogo. Ninaendelea kukufuata, Ewe Mtoto wa Kimungu, wakati unapokwenda kufanya matembezi katika mashamba na pale unapofurahia kupita kuchuma maua. Unaponyosha mkono wako ili kuchuma maua, mimi ninakupenda Wewe na juu ya kila ua unalochuma, mimi napenda kurudia kile kiitikio changu cha ‘Ninakupenda, Ninakupenda’.
Hata hapo ninakuomba upeleke kwa Baba Yako wa Mbinguni hili ua dogo la huyu Binti Mdogo wa Utashi Wako, ili kusudi asiweze tena kujua, wala asiweze kupenda na wala kutaka kitu kingine chochote isipokuwa FIAT Yako ya milele.

Baba yetu...,
Salamu Maria...,
Atukuzwe Baba...
SAA YA KUMI NA NNE

Tunamfuata Yesu ambaye, baada ya kukaa kama mkimbizi, sasa anarejea kwake Nazareti. Kwa kumnyeshea mvua ya kauli yetu ya ‘Ninakupenda’, tunamwomba, kwa sauti elfu na elfu, Ujio wa Ufalme Wake wa Kimungu.

Ewe Mtoto Yesu, Uhai Wangu, natambua kuwa kipindi chako cha kuwa mkimbizi kimemalizika na sasa unarejea Nazareti; na mimi nataka nikufuate hatua kwa hatua, yaani, napenda kuambatana nawe nikikusindikiza katika mvua inayokunyeshea kauli za ‘Ninakupenda, Ninakuabudu, na Ninakuheshimu’. Kwa hiyo, ili niweze kusaidiwa, ninaita msaada wa mwanga wa Jua unyeshe ‘Ninakupenda’ kama mwanga. Ninaita na mmetuo wa nyota zote nao uinyeshe ‘Ninakupenda’. Na ule mvumo wa upepo, iwe ule wa sauti ya kulia, au upepo ule unaopiga kelele kali, au ule unaopiga kama miluzi, nao ninauita uinyeshe ‘Ninakupenda, Ninakupenda’. Ninawaita na ndege wote wanaoruka hewani, ili nao wakusindikize kwa musiki wao, kwa nyimbo zao, na kwa sauti zao za kutetemeshwa, zote zikisema: ‘Ninakupenda, Ninakupenda’. Ninawaita na hao kondoo wadogo, nao walie na kuita wakisema ‘Ninakupenda’. Naiita na bahari, nayo itoke na kuvuka toka kule kwenye ufukwe wake, ili ikusindikize kwa mawimbi yake ya ‘Ninakupenda’. Lakini, je wafahamu ni nini hasa, anachotaka huyu Binti Yako Mdogo anapokunyeshea mvua hii ya ‘Ninakupenda’? Nataka kitu kimoja tu: Ukubali kunipatia Ufalme wa Utashi Wako. Na wakati unapojifungilia pale kijijini Nazareti, mimi ninajifungilia pamoja Nawe, ili niwe ninaendeleza hii mvua ya ‘Ninakupenda’ yangu, ili kusudi nikushinde Wewe kwa njia ya pendo hata uweze kunipatia mimi kile ambacho Wewe Mwenyewe unataka, ambacho na Mama Malkia anataka na ambacho na mimi pia ninataka: Yaani, kwamba Utashi Wako upate kujulikana na upate kutawala kati ya wanadamu.

Ewe Yesu, Uhai Wangu, mimi sasa nipo tayari na Wewe, hapa katika nyumba hii ya Nazareti. Hatua kwa hatua napenda kukufuata ili niendelee kugonga mhuri wa ‘Ninakupenda, Ninakuabudu, Ninakuheshimu, Ninakushukuru’ juu ya kila kitu unachofanya Wewe, na ili kusudi nikuombe Wewe Ufalme wa Utashi Wako. Iwapo mikondo ya pendo inatiririka kati ya Wewe na Mama Yako, ndivyo pamoja nayo inatiririka ‘Ninakupenda’ yangu. Hiyo yote ni kwa kusudi la kuwaombeni Wewe na Mama wa Mbinguni kuwa Utashi Wako ujulikane. Kama Wewe unakula chakula, hapo na mimi nagonga ‘Ninakupenda’ yangu, ili kwa kauli hiyo nikuombe lishe ya Utashi Wako kwa ajili ya wanadamu wote. Unapokunywa maji, mimi natiririsha ‘Ninakupenda’ yangu ndani yake, ili kukuomba kwamba maji safi ya Utashi Wako, yatiririkie katika matumbo yetu, kwamba, ndani ya watu wote yakatengeneze mzunguko wa damu, ambayo, katika viungo vyote vya mwili wetu, itakuwa ikituwezesha kuonja uhai wa Utashi Wako wa Kimungu. Unapogonga mti au ubao wowote kwa mikono yako hiyo ya uumbaji, hapo unakuwa ukigonga ubao wa utashi wangu wa kibinadamu ili kusudi upate kuongokea katika mwanga wa Utashi wa Mungu.
Hiyo ‘Ninakupenda’ yangu inaendelea kukufuata Wewe. Wakati wa shughuli zako za ufundi seremala, unapotwaa misumari na nyundo katika mikono yako, ninakufuata, ili kwa njia ya ‘Ninakupenda’ yangu, niweze kukuambia hivi: Pigilia kwa misumari tashi zote za kibinadamu ili ziruhusu Utashi Wako uweze kuishi kwa uhuru. Wakati ule unaporudi na kuingia peke yako chumbani mwako kwa ajili ya kusali au kwa ajili ya kulala, mimi huwa sikubali kukuacha peke yako. Mimi huwa ninapenda kuwa pale kando yako, na endapo sipati kitu cha kukuambia, basi nitakuwa nikipwepa hapo sikioni pako nikisema: “Ninakupenda, Ninakupenda, Ninakupenda, Ninakuabudu”. Na kwa sala zako Wewe Mwenyewe, nitakuomba Ufalme wa FIAT Yako, na nitakuomba pia, kwa nguvu ya usingizi wako, uutie usingizini utashi wa kibinadamu, ili kusudi usiwe tena na uhai wowote, na badala yake, niwe ninaupata daima uhai wa Utashi Wako wa Kimungu peke yake. Ewe Yesu Wangu Mtukufu, mimi ningejionja uchungu sana iwapo kama nisingeweza kukufuata katika mambo yote, na kama nisingekuwa naendelea kukushughulisha na usindikizi wangu na kama nisingekufanya uwe unasikia daima kiitikio cha kauli yangu ya ‘Ninakupenda, Ninakuabudu, Ninakuheshimu, Ninakushukuru’, kwa ajili ya kukuomba Wewe, nikiwa pamoja na matendo Yako, Ufalme wa Utashi Wako. Ni kwa vile, ninapokuwa kando yako, mimi huwa ninaonja mapigo yale yale ya Moyo Wako, yaani ya kuwa nao huo Moyo Wako unataka kitu hicho hicho, na hata wenyewe Utashi Wako wa Kimungu, nao unataka ujulikane kwa watu, na unataka utawale na kuamrisha kati ya wanadamu.

Kwa sababu hiyo, ninakufuata hata unapokwenda Hekaluni. Wewe lakini, kwa tendo lako la kumwepa Mama Yako, ulikuwa umeleta maumivu makali na ya uchungu aliyoyakabili katika muda wa siku tatu za kupotea kwako. Mimi ninatiririsha ‘Ninakupenda’ yangu ndani ya lile teso la Mama yako na katika tendo la kupotea kwako, ili kusudi niombe kwamba utashi wa kibinadamu upotelee mbali. Kwa jinsi hiyo sisi, tunapokosa kuuona, tuwe tunaamua kuishi kwa Utashi wa Mungu na tuishi katika ile furaha ambayo ninyi, Mama na Mtoto, baada ya kupoteana, mliweza kuionja kwa karibu zaidi, pale mlipokutana tena. ‘Ninakupenda’ yangu inakuomba kwamba wanadamu wasikuletee tena uchungu na maumivu yale ambayo utashi wa kibinadamu huwa unakuletea mara kwa mara, lakini badala yake wawe wanakupatia furaha zilizo safi na raha mbalimbali zilizo nzuri kabisa za FIAT Yako ya Kimungu inayotawala ndani yao.

Baba yetu...,
Salamu Maria...,
Atukuzwe Baba...
SAA YA KUMI NA TANO

Tumfuate Yesu kule jangwani. Tunapofika na kusimama pale kwenye mto Yordani, tumwombe atupatie Ubatizo wa wokovu wa Utashi wa Mungu ili kusudi watu wote waupate Uhai Wake.

Ewe Chema Changu Kikuu cha Mbinguni, mimi naharakisha kukufuata kwani vinginevyo muda hautanitosha kuweza kukufuatilia katika yote. Ninakuona tayari umejiandaa kutoka kwenda jangwani. Unamkumbatia Mama yako ukimbana kwenye Moyo wako unaoumia na kulia kwa pendo, na unamwambia: “Kwaheri, ubaki hapa, Ee Mama. Ninakuachia FIAT Yangu ya Kimungu, iwe hapa kama msaada kwako badala yangu, iwe kama uhai wako na kama mjumbe wa mawasiliano kati ya Mimi na Wewe’ . Utashi Wangu utakuwa unakuambia kila kitu atakachokuwa anatenda Mwanao, na wewe utakuwa ukinifuata katika kila kitu, kiasi kwamba, hata kama utakuwa mbali, FIAT itakuwa inakuleta karibu kabisa nami, hata tutajiona kuwa ni kitu kimoja tu”.

Ewe Yesu, nipe mkono wako na unichukue nije Nawe, ili chochote utakachokuwa unatenda kisiweze kunitoroka akilini mpaka niweze kufungilia ndani yake ile ‘Ninakupenda’ yangu, kwa ajili Yako, kusudi nikuombe Ufalme wa Utashi Wako wa Kimungu juu ya dunia. Kwa hiyo, wakati Wewe unaendelea kutembea peke yako, mimi ninakufuata hatua kwa hatua nikiwa nimebeba kauli yangu ya ‘Ninakupenda, Ninakuabudu, Ninakuheshimu, Ninakushukuru’. Katika kila pumzi yako nataka nikufanye uwe ukipumua ‘Ninakupenda’ yangu. Kila moja la neno lako nalifungilia ndani ya ‘Ninakupenda’ yangu. Katika kila mtazamo wa jicho lako nataka uwe unakutana na ‘Ninakupenda’ yangu. Na wakati unapowasili pale Yordani mimi napenda nitiririshe ‘Ninakupenda’ yangu ndani ya maji yale. Natiririsha kwa jinsi kwamba, kama vile Mtakatifu Yohane Mbatizaji alivyotiririsha maji kichwani pako kwa ajili ya kukubatiza, ndivyo sasa na Wewe uonje kuwa Binti Yako Mdogo kamwe hatakuacha peke yako bali anaambatana nawe kwa njia ya ‘Ninakupenda’ yake. Kwa kutiririsha kauli hiyo katika maji yale anataka akuombe Wewe utoe maji ya ubatizo ya Utashi Wako wa Kimungu kwa ajili ya wanadamu wote, ili huo uwe ndio mwanzo wa Ufalme Wake. Ewe Pendo Langu, katika tendo la kisherehe la Ubatizo wako, napenda nikuombe neema moja ambayo Wewe kwa uhakika hutanikatalia: Ninakuomba kwamba, kwa mikono yako mitakatifu, uibatize hii roho yangu ndogo katika maji yaletayo uzima na ya uumbaji ya Utashi Wako wa Kimungu. Ninaomba hilo ili kusudi roho yangu isionje kamwe, isione, na wala isiujue uhai mwingine isipokuwa uhai wa FIAT Yako. Ah, kweli kabisa, ninakuomba kwamba uwepo wangu usiwe ni kitu kingine, bali uwe ni tendo moja pekee la Utashi Wako.
Ewe Yesu Wangu, Pendo Langu tamu, mimi ninakufuata kwenda jangwani. ‘Ninakupenda’ yangu haitakuacha peke yako katika jangwa hili. Nitabaki kuwa kando yako usiku na mchana. Nitakapokuona, ukiwa na masikitiko sana, ukiwa na mahangaiko, unapokufa kwa pendo, na nitakapokuona ukisali na ukilia kutokana na upweke wa Utashi Wako wa Kimungu baada ya wanadamu kuutoroka, mimi nitabaki kando yako. Wewe unaonja mara moja na hai kabisa maumivu ya Utashi huu wa Kimungu, siyo tu kwa vile hautawali kati ya wanadamu, bali kwa vile Utashi huu umeachwa katika upweke mithili ya jangwani, ni kama umeachwa uhamishoni. Kwa hiyo Ubinadamu Wako Mtakatifu mno unalia na unaomba, kwa niaba ya familia yote ya binadamu, kwamba zile tashi mbili, yaani, ule wa Kimungu na ule wa kibinadamu, budi zikutane na zijipatanishe zenyewe. Utashi wa kibinadamu unauita Utashi wa Mungu, ili kuuruhusu uje utawale, na Utashi wa Mungu unasamehe juu ya kipindi kile kirefu, ambamo wanadamu walikuwa wameushika na kuuzuia uhamishoni. Mimi nayachukua machozi yako na kuyafanya yawe ni ya kwangu, sala zako ziwe ni za kwangu, vionjo vya kifo vya Moyo Wako unaoungua kwa pendo, navyo viwe ni vya kwangu. Naendelea kukifuatilia kila kitu kwa ‘Ninakupenda’ yangu. Natengeneza minyororo mitamu ya pendo, na ninaingiza nafsi Yako yote ya Kimungu ndani yake kwani ninataka nikuvute kwa lazima ukubali kunipa Ufalme wa Utashi Wako wa Kimungu hapa duniani. Ebu sikiliza Ewe, Uhai Wangu, mbona ni yenyewe mapigo ya Moyo Wako, ni matamanio yako Mwenyewe, ni machozi yako, ni maumivu yako, ndiyo hayo yanayotaka na yanayoomba Ufalme wa FIAT Yako. Kwa hiyo basi, endapo hutaki kunisikiliza mimi, basi nakuomba ujisikilize Wewe Mwenyewe, na unipe jibu kusudi tutoke katika jangwa hili huku ukiniambia hivi: “Ah, ndiyo basi! Ufalme wa Utashi Wangu utafika hapa duniani!”

Ewe Yesu Wangu, Moyo wa moyo wangu, ninakuona ukiharakisha mpango wa kutaka kutoka jangwani. Naona unapitia tena kule kwenye mto Yordani ili, kwa upendo, ukamchungulie tena mpenzi wako Yohane. Moyoni mwake unatia mafuriko ya pendo na neema, na halafu kwa haraka haraka unaendelea na safari hadi kuifikia nyumba yako ya Nazareti, ambako pendo la Mama wa Mbinguni linakuita kwa mfululizo. Na tazama, Oh, nini hiki ninachoshuhudia kikinivuta hapa mbele yangu! Mama na mtoto wanarukiana, huyu katika mikono ya mwenzake, na kwa kuyeyushiana, hawa wawili wanatengeneza pendo moja tu. Maadam Malkia wa Mbinguni amekuwa akionja hitaji kali mno la kumwona tena Mtoto wake. Moyo wake wa kimama ulikuwa umeunguzwa moto wakati huu alipokuwa hayupo, wakati yeye Mama alikuwa anatamani kujimwaga ndani ya Mwanae, ili aweze kupokea umande wa Pendo Lake, ili asibaki ameteketezwa na miali ile ya moto, iliyokuwa ikimtafuna. Na Yesu, Mkombozi Wangu wa Mbinguni, kwa upande Wake, alikuwa naye akionja hitaji kali sana ya pendo la Mama. Ni kwa sababu hiyo alirukia mikononi mwa Mama Yake kusudi akatoe pendo na kupokea pendo. Hata mimi, nikiwa nimeshika ule mwali mdogo wa moto wa ‘Ninakupenda’, narukia katika makumbatio yenu hayo yaliyo safi sana, narukia katika makaribiano yenu, narukia katika mioto ya pendo la Mama na Mtoto wake, na kwa wote wawili, Mama na Mtoto, ninawasihi ninyi nyote mnipatie Ufalme wa Utashi Wenu. Ewe Mama Mtakatifu, urudie pamoja nami na usali pamoja nami, kwamba Utashi wa Mungu ujulikane, utawale, hapa duniani kama kule Mbinguni.

Wakati huu ambapo Mama na Mtoto wanajipumzisha kidogo katika pendo lao na wakati wanapochukua uhai, papo hapo wanajiandaa kwa ajili ya kukabili hali ya kuachika ya kipindi kirefu zaidi. Tayari Yesu Wangu, ambaye daima mtu hawezi akamfikia katika kiwango cha Pendo Lake, anachukua njia ile inayoelekea kwenye maisha yake ya hadharani. Anamkumbatia kwa nguvu kabisa Mama Yake, kwenye moyo wake, kwa ajili ya kumtia nguvu huyu Mama, kwa mara nyingine anaaga na anatoka peke yake kabisa, kwa ajili ya kwenda kueneza Neno lake la Kimungu kwa mataifa, kwenda kuunda wafuasi wake, na kwenda kutangaza Injili Takatifu.

Baba yetu...,
Salamu Maria...,
Atukuzwe Baba...
SAA YA KUMI NA SITA

Tumfuate Yesu kwenye Harusi ya Kana na pale tunamwomba augeuze utashi wa kibinadamu na aubadilishe na Utashi wa Mungu. Tuendelee kumfuata katika maisha yake ya hadharani.

Ewe Yesu, Pendo Langu na Uhai Wangu, ninatambua kwamba, kabla ya kuanza maisha yako ya hadharani, Pendo liwakalo la Moyo Wako linakuvuta kwenda kwanza kuhudhuria harusi ya Kana. Mimi, pamoja na Mama Yako, ninafuata hatua zako, nikiwa nimebeba ‘Ninakupenda’ yangu. Ninausikia Moyo Wako ukigonga kwa mapigo ya Pendo na maumivu.

Hapo unakumbuka harusi ile nyingine, iliyohudhuriwa na kubarikiwa Nawe pale katika Bustani ya Edeni. Ni ile ya Adamu na Eva walipokuwa hawana doa la dhambi. Ilikuwa ni ndoa katika nyanja mbili: kwanza ilikuwa ni ndoa kati ya Utashi Wako wa Kimungu na utashi wa kibinadamu, pili ilikuwa ni ndoa kati ya mtu mwanaume na mtu mwanamke. Katika ndoa hii, kama posa, Wewe uliutoa Uumbwa wote na hata Utashi Wako wa Kimungu ulio hai. Wewe uliutia Utashi Wako huo ndani ya moyo wao na ndani ya vitu vyote vilivyoumbwa.

Kwa minajili hiyo, uwepo Wako leo katika harusi hii, kitu kisichokuwa cha kawaida kwako, kunaniambia kwamba Wewe unapenda Utashi Wako wa Kimungu utawale, na unataka upange upya mambo yote ndani ya wanadamu.

Na mimi upande wangu, Ewe Yesu Wangu, nataka nije hapa kando Yako ili, katika mtazamo wako mtamu wa macho, katika sauti yako yenye musiki mtamu, na katika hiyo mitindo yako ya kuringa, niweze kujaza kauli yangu ya ‘Ninakupenda, Ninakuabudu, Ninakuheshimu, na Ninakushukuru’. Kwa nguvu ya Pendo lile lililokusukuma Wewe uyapokee maombi ya Malkia wa juu mwenye mamlaka hata ukatenda muujiza wa kugeuza maji kuwa divai, mimi ninakuomba utende sasa, pia kwa pendo la Mama Yako wa Mbinguni, muujiza mkubwa wa kugeuza utashi wa kibinadamu uwe ni Utashi wa Kimungu, na uufanye huo Utashi wa Mungu utawale hapa duniani sawa kama kule Mbinguni.

Ewe Mama Mtakatifu, wewe uliyekuwa unahangaika sana kwamba Yesu ageuze maji kuwa divai, ili kuwasaidia wale wanaharusi, naomba usimwache Yesu atoke na kwenda kwenye utume wake wa hadharani, bila kwanza kukubali kwamba Utashi Wake ufike na utawale juu ya dunia.

Ewe Chema Changu Kitamu, hii kauli yangu ya ‘Ninakupenda’, pamoja na kale kawimbo bembezi endelevu, kwa ajili ya kukueleza kuwa ninataka Utashi Wako wa Kimungu utawale hapa duniani kama kule Mbinguni, hivyo havitakoma kamwe. Na ili kukulazimisha, nataka nikufuate katika kila kitu kusudi niweze kutia ‘Ninakupenda’ yangu katika matendo yako yote.

Nitaiweka hiyo ikuzunguke, ndani yako na nje yako, kama kikosi cha jeshi kali ili liwe linakupwepea sikioni mwako likisema: Ebu nipatie FIAT Yako hiyo inayogonga Moyoni Mwako, ebu nipe Utashi Wako huo unaozungumza ndani ya neno lako, Utashi huo unaotenda kazi mikononi mwako, huo unaotembea katika hatua zako, na ambao ndani ya nafsi yako nzima unakuambia: Ninataka Utashi Wako unaotawala hapa duniani kama kule Mbinguni. Lo, ebu umsikilize huyo Binti Yako Mdogo, ebu ujisikilize Wewe Mwenyewe, Wewe unayependa kwamba tuishi katika FIAT Yako!.

Baba yetu...,
Salamu Maria...,
Atukuzwe Baba...
SAA YA KUMI NA SABA

Tumfuate Yesu katika maisha yake ya hadharani, katika miujiza yake, na tumwombe atende ule muujiza mkuu wa kuzifufua roho za watu katika Utashi wa Mungu.

Ewe Yesu Wangu, Uhai Wangu Mpenzi, ninakuona unapotoka na kuagana na Mama Yako. Lakini, tashi zenu hazitengani, bali, ni kwa vile tu unapasika kuaga ili ukaanze maisha yako ya hadharani. Miguu yako inaelekea Yerusalemu kwa ajili ya kwenda kufundisha Neno Lako takatifu pale Hekaluni. Na pale utawaambia wazi hadharani kwamba Wewe ndiye Yule aliye Masiha wa kweli wanayemtamani. Lakini, ni maumivu mangapi yanaingia Moyoni Mwako! Ni mateso mangapi! Wanaposikia mahubiri yako, badala ya wao kujitupa miguuni pako na kukupokea kama mwokozi wao wa Mbinguni, wao wanakuangalia kwa macho ya kutisha na ya chuki, wanakusikiliza huku wakinung’unika, kiasi kwamba hakuna hata mtu mmoja kati yao anadiriki kusogea na kukukaribisha akikuambia: “Njoo karibu nyumbani kwangu”. Wewe unaachwa mpweke! Kutokana na utovu wa shukrani kati ya watu wale, unapasika kuombaomba mkate, unapasika kuwa unatoka nje peke yako; tena ni lazima uwe unatoka usiku tu, kwani unalala sakafuni na wala huna cha kujifunika, bali unalala ukitazama nyota za angani wakati wote wa usiku. Nyota zile, kwa memetuko wao mzuri na wa taratibu, zinakusindikiza, na Wewe unapitisha usiku wote katika machozi na katika sala kwa ajili ya hao hao watu ambao hawataki kukujua.

Ewe Yesu Pendo Langu, ebu njoo hapa katika mikono yangu ili uweze kujipumzisha kidogo. Ninataka niwe ninalia na kusali pamoja Nawe, nataka nipange usindikizi wangu wa ‘Ninakupenda, Ninakuabudu, Ninakuheshimu, Ninakushukuru’ katika maumivu unayoyapata, katika machozi yako unayomwaga, katika maneno yako yasiyopokelewa. Nataka niweke ‘Ninakupenda’ yangu mbele ya hatua zako, nyuma na mbele ya hatua zako, ili kusudi miguu yako isiwe inaonja ugumu wa udongo usiokuwa na shukrani, bali badala yake iwe inaonja ulaini wa ‘Ninakupenda’ yangu na ninapenda nikuambie: Ewe Yesu, je waona jinsi unavyoteseka? Basi fanyiza ili Utashi Wako wa Kimungu utawale na ndipo maumivu yako yatakoma.

Yesu Wangu, Uhai wa moyo wangu duni, Pendo lako halisimami. Unaendelea kurejea Hekaluni na unaendelea kuwagawia watu Neno lako takatifu. Ingawa kama watu wakubwa na wasomi hawataki kukutambua na kukuheshimu, kundi kubwa la masikini, la wasiosoma, na wanaoteseka na maradhi mbalimbali, wanakukimbilia na kukusonga, wakiwa wanavutwa na mitindo yako ya upendo na wema, wakivutwa na sauti Yako yenye kuteka, kwani wanapokusikiliza ukizungumza huwa wanaonja kuguswa sana, na kuchomwa moyoni mwao. Ni hawa mafukara ndio wanafungua angalau mshipa wa furaha na raha ndani ya Moyo Wako. Kwa hoja hiyo, unaonja walau kwamba unaweza sasa kuwafariji, kuwafundisha, kuwaponya masikini ambao, wanahesabika kuwa kama takataka za jamii. Wewe unakuwa sasa ni rafiki, mwalimu, na mganga tabibu mwema wa masikini. Kwa hao wote Wewe unayo maneno ya faraja. Na kwa ajili ya kuwaponya, Wewe hunyanyapai kuvigusa viungo vyao vya mwili vilivyo na maradhi mbalimbali.

Unakwenda mji kwa mji, na mimi nataka nifuate hatua zako, ili nikaweke ile alama yangu ya ‘Ninakupenda, Ninakuabudu, Ninakushukuru, ninakuheshimu’ katika njia mbalimbali, na katika miji. Na mara kwa mara nitakuwa nakusogelea na kukubana mkononi nikikupwepea katika sikio Lako: Ebu unipe Ufalme wa Utashi Wako, na ili kukusukuma unipatie hilo ninalokuomba, kwa pendo lile lile la matendo ya kwako.
Lakini, pindi unapozungukia mitaa na miji, panatokea kisa cha kushangaza sana katika makundi yanayokuzunguka Wewe: vipofu, mabubu, viziwi, vilema, waliopooza, wakoma na wenye maradhi na matatizo mbalimbali ya kibinadamu, wanaleta uchungu sana katika Moyo Wako wa Kimungu. Oh, ni jinsi gani unavyotetemeka! Uchungu gani unauelemea Moyo Wako unapoona jinsi hali ilivyogeuka, kuwa matatizo na mahangaiko, na kuwa hali ya kutisha. Ni hali ile ile ya maumbile ya kibinadamu, ambayo hapo awali ilikuwa ni hali nzuri sana, ya kupendeza, na kamilifu wakati ilipotoka katika mikono Yako ya uumbaji. Hayo yote ni matokeo ya utashi wa kibinadamu ulioporomoka na kuharibika. Huo utashi umefurikisha nje yake mambo yake machafu na ukafanya ubinadamu wote upoteze furaha yake.

Lo, Ewe Pendo Langu, ninakuomba kwamba ile FIAT Yako irejee na itawale kati yetu. Kama Wewe ukitaka, unaweza. Na yenyewe FIAT itafukuzia mbali yale matatizo na machungu yote yaliyoletwa na utashi wa kibinadamu. Kwa sababu hiyo mimi ninatiririsha ‘Ninakupenda’ yangu katika tendo lako lile ambapo unafungua macho ya vipofu ili wajipatie tena uwezo wa kuona, ili waweze kuutambua na kuujua Utashi Wako wa Kimungu. Ni vipofu wengi ilioje wa Utashi Wako wa Kimungu! Dunia hii imejaa hawa vipofu duni. Kwa hiyo ninakuomba kwamba wote wapate uwezo wa kuona ili waweze kuutambua na kuutazama Utashi Wako Mtakatifu kabisa.

Lakini natambu, Ewe Pendo Langu, kuwa hatua kwa hatua, unapita kutenda mema mengi kwa watu wale masikini. Anapojitokeza mbele yako yule kiziwi, Wewe, kwa amri ya sauti yako, unamfungulia masikio yake. ‘Ninakupenda’ yangu inatiririkia katika sauti yako inayoamrisha, na pale ninakuomba kwamba ufungue masikio ya wale viziwi wengi wa Utashi Wako wa Kimungu. Katika hatua nyingine, Wewe unafungua ulimi wa yule aliye bubu. Ni bubu wengi wangapi, ambao hawana ulimi tena wa kuweza kuzungumzia ‘FIAT’ Yako ya Kimungu! Na mie hapa, kifudifudi miguuni pako, ninajiegesha penye magoti yako, na ingawa kama ni bado msichana mdogo sana, kamwe sitajitoa hapa mpaka pale utakaponitendea ule muujiza wa kufungua ulimi wa wale bubu wengi, ili hao wote waweze kuzungumzia juu ya Utashi Wako Mwabudiwa. Yesu Wangu, Moyo Wako unaonja dakika za majonzi na maumivu mengi kwa ajili ya mahangaiko ya wanadamu, matatizo yote yakiwa yametokana na utashi wa kibinadamu. Yaelekea sasa unapita kueneza miujiza yako ili kuwakomboa toka matatizo hayo. Tunaomba utujalie neema ya kuuita tena Utashi Wako wa Kimungu ufike kutawala kati ya wanadamu wote. Basi kwa hiyo, uponye na kunyosha viungo vya viwete, uwatakase wakoma, uwaponye waliopooza.

Na mimi, Ewe Mkombozi wa Mbinguni, nitakuwa nikiambatana nawe, nikiwa na hii kauli yangu ya ‘Ninakupenda, Ninakuabudu, Ninakuheshimu na Ninakushukuru’. Na je wajua kwa nini ninakupenda, na kwa nini ninakufuata? Ni kwa vile ninapenda unyoshe miguu ya yule anayechechemea katika Utashi Wako, napenda utakase vizazi vya binadamu kutoka ukoma wa utashi wa kibinadamu, ukoma ulioleta ulemavu wa roho na hata ulemavu wa mwili. Napenda uponye wale wengi waliopooza kutokana na utashi wa kibinadamu.

Ewe Pendo Langu, utashi wa kibinadamu ndio uliopanda mbegu ya maovu yote. Kwa sababu hiyo nakuomba utende ule muujiza wa miujiza: kwamba Utashi Wako utawale, hapa duniani kama vile kule Mbinguni ili kwa njia hiyo maovu yote yapate kukoma.

Baba yetu...,
Salamu Maria...,
Atukuzwe Baba...
SAA YA KUMI NA NANE

Tumfuate Yesu katika matukio mengine ya maisha yake ya hadharani.

Ewe Chema Changu Mpendwa, Wewe unaendelea na maisha yako ya hadharani huku ukiendelea kueneza popote Neno lako la Kimungu, na ukiendelea kuwafariji wale wanaoteseka. Unamsikia mama mmoja anayelia kwa ajili ya mtoto wake aliyefariki, na sasa yupo njiani akienda makaburini kumzika. Mbele ya mama huyo anayelia, Moyo Wako unashindwa kuvumilia kuyaona yale machozi yanayomtoka. Wewe unalijongea jeneza, unayaita yale maiti yaamkie kwenye uzima na unamkabidhi mtoto yule kwa mama yake. Ewe Pendo Langu, ‘Ninakupenda’ yangu haiwezi kukuacha katika tendo lako hili la kutoa uhai kwa mtu aliyekufa. Ninakuomba uziite zile roho nyingi sana, zilizokwisha kufa mbele ya Utashi Wako wa Kimungu, na ufute machozi ya Utashi wako wa Kimungu, ambayo ni machozi yako pia. Utashi Wako, zaidi ya mama yeyote, umekuwa ukilia kwa kipindi cha karne nyingi sana, unapoangalia watoto wake wengi sana wakiwa wamekufa sababu ya kutoishi ndani yake.

Ewe Yesu Wangu, Uhai Wangu Mtamu mno, Pendo Lako linakusukuma uwe unakimbiakimbia huko na kule, kwenda kila mahali. Unapoitwa kumfufua msichana mdogo wewe hukukataa. Kwa mkono wako unamshika mkono wake, na katika tendo la kumwinua juu, unamwita kurejea katika uzima. Unasema: “Msichana huyu hajakufa, bali analala”. Ewe Pendo Langu, ni wengi walioje, ambao wanalala katika usingizi wa utashi wao wa kibinadamu, na mimi ningependa kutiririsha ‘Ninakupenda’ yangu katika tendo lako lile la kunyosha mkono ili kumfufua msichana. Ndipo ninapenda kukuomba, unyoshe mkono wako wa kulia, kuwaita warejee kwenye uhai ndani ya Utashi Wako. Wala hapatakiwi kitu kingine, isipokuwa kuguswa na Mkono Wako wa uumbaji, yaani kuguswa na tendo la Maweza Yako juu ya roho hizo, ambazo zinalala katika usingizi wa utashi wa kibinadamu. Utende hilo sasa kusudi uunde kikosi cha kwanza cha Ufalme wa FIAT Yako ya Kimungu.

Ewe Yesu Wangu Mpole, kuna bado tukio lingine la kushangaza linalokungoja bado: Wanakuja kwako Marta na Magdalena , wakikufuata ili kukutaarifu kuwa kaka yao amekwisha kufariki. Wanalia, na Wewe unashikwa na uchungu hivi, hata unaanza kulia pamoja nao, na unawaomba wakuchukue kwenda kukuonyesha kaburi lake Lazaro. Ulipowasili kaburini, unawaamrisha walifungue kaburi. Ulitazama na kuona kuwa, baada ya siku nne tu mwili wake ulikuwa umeoza, hata hakuweza kutambulikana tena, na wala hakuweza kusogelewa kwani mwili ulikuwa unatoa harufu mbaya. Wewe unatehemu, unatetemeka na kulia machozi, na kwa sauti ya kuamrisha yenye kutetemeka kutokana na uchungu wako mkali, unasema: “Lazaro, amka uje nje!”. Na ndivyo unamfufua.

Ewe Pendo Langu, kwa nini unalia na kwa nini unapata uchungu mkali katika tendo la kumfufua Lazaro? Ndipo Yesu, alinishika na kunibania kwake na mimi nikamshika na kumbana sana ili niweze kusikia mapigo Yake ya Moyo unaoteseka. Mwangwi wa sauti yake ukawa unasikika ndani ya moyo wangu akiniambia: “Binti Yangu Mdogo, huyu Lazaro aliyekufa, kwangu mimi, amekuwa anawakilisha ubinadamu wote uliokuwa umezeekea katika uovu. Kwa utashi wa kibinadamu, ubinadamu umegeuka kuwa ni maiti iliyooza na inayotoa harufu mbaya. Hiyo hali halisi ya maovu yake, imefanya familia nzima ya binadamu iwe inanuka na isiwe inavumilika mbele yangu. Hali hiyo inaniletea machozi, inanifanya nitehemu kwa maumivu. Na wewe tafadhali uwe unalia pamoja nami na uwe unasali”.
Ah, ndiyo, Ewe Uhai wa Moyo Wangu, mimi ninalia pamoja nawe. Maneno yako hayo ya ‘Lazaro, amka uje nje!’, mimi ninataka niyajaze na ‘Ninakupenda’, na ‘Ninakuabudu’, ili kauli hiyo ikushawishi uwe unayarudia rudia juu ya kila moyo. Huku ukiwa unayamwaga machozi yako kama umande uletao baraka, uwe unarudia kusema: “Toka nje ya kaburi hilo la utashi wa kibinadamu, na ebu uingie tena katika uhai wa Utashi wa Mungu”. Kwa minajili hiyo, watakapokuwa wakisikia uamrisho wa sauti Yako, wote waamke na kuuunda Ufalme wa ‘FIAT’ Yako.

Ewe Yesu Wangu Mpendwa, mimi sitakuacha peke yako kamwe. Ingawa kama sijui ni kitu gani cha kukuambia, lakini, angalau ninajua kukuambia ‘Ninakupenda, Ninakupenda’. Ninataka, matendo yako yote, hatua zako, maneno yako, na hata machozi yako yote, niyasuke pamoja na ‘Ninakupenda’ yangu ndogo, na mwishowe nataka nikuombe utupatie FIAT Yako yenye kutawala, na yenye kuamrisha. Kwa sababu hiyo mimi ninakufuata pamoja na wanafunzi wako. Wakati unapolala usingizi pale ndani ya mashuha, ikiwa ni ishara ya pumziko unalotaka kumpatia mtu yule atakayeishi katika Utashi Wako wa Kimungu, dhoruba kali inawatia hofu Mitume, hali inayowafanya wapige kelele wakilia: “Mwalimu, Utuokoe, vinginevyo tutateketea!”. Yesu Wangu, hicho siyo kitu kingine isipokuwa ni dhoruba itokanayo na utashi wa kibinadamu ambao, unapovumisha mawimbi yake ya kutisha na makali katika bahari ya maisha, huwa inatutishia kutuzamisha. Ewe Yesu Wangu Mleta amani, pamoja na Mitume, na kupitia ‘Ninakupenda’ yangu, ninapiga nami kelele kwa nguvu nikisema: “Mwalimu, utuokoe, vinginevyo tutateketea!”. Tafadhali, amrisha hii dhoruba ya utashi wa kibinadamu na uifanye itulie. Kwa nguvu ya amri ile ile uliyoitoa juu ya ile dhoruba iliyowakabili Mitume, sasa upatanishe utashi wa kibinadamu na Utashi wa Kimungu, ili utuwezeshe tupumzike katika mikono ya uhakika ya ‘FIAT’ Yako ya Juu kabisa.

Baba yetu...,
Salamu Maria...,
Atukuzwe Baba...