Utashi wa Mungu na Upendo wa Mungu - Luisa Piccarreta
43 subscribers
298 photos
54 files
630 links
Fahamu kuhusu kutimia kwa Sala ya Baba Yetu kupitia Maandishi ya Mtumishi wa Mungu Luisa Piccarreta, Binti Mdogo wa Utashi wa Mungu - Kuishi Utashi wa Mungu
Download Telegram
Wiito Anaotoa Luisa Binti Mdogo wa Utashi wa Mungu⬇️⬇️⬇️
Mtumishi wa Mungu - Luisa Piccarreta
- Binti Mdogo wa Utashi wa Mungu

‘Ee Yesu, miguuni pako nakuletea uabudu na utiifu wa familia yote ya wanadamu.

Ninaweka ndani ya Moyo Wako ile kauli ya ‘Nakupenda’ kutoka kwa watu wote. Juu ya Midomo Yako nakupigia busu langu ili kukubandikia mhuri wa busu la watu wa vizazi vyote.

Kwa mikono yangu nakukumbatia ili kukubana kwa kumbatio la mikono ya watu wote, kwa ajili ya kukufikishia utukufu wa matendo yote ya viumbe.’

(Kutoka: KITABU CHA MBINGU, Juzuu Na. 12, Tarehe 22 Mei 1919)
Mtumishi wa Mungu Luisa Piccarreta alizaliwa katika Mji mdogo wa Corato, Mkoa wa Bari, Italia tarehe 23 Aprili 1865.

Alibatizwa katika Kanisa la Parokia yake. Ndipo hapo alipopata na Komunyo ya Kwanza na Sakramenti ya Kipaimara (1874).

Katika umri wa miaka 11 alijiunga na Kikundi cha ‘Mabinti wa Maria’ na baadaye akawa Mtersiari wa Wadominikani.

Alipopata umri wa miaka 16, kwa mapenzi yake Yesu, Luisa Piccarreta alianza kuingia hali ya kuwa ‘mhanga’.

Ingawa kama kielimu alikuwa ni Darasa la Kwanza tu la Shule ya Msingi, ilipofika tarehe 28 Februari 1899 , kwa kutii agizo la Padre Mwungamishi wake, yeye alianza kuandika Shajara yake ya Kumbukumbu zake za kimistiki (Shajara ambayo Yesu Mwenyewe baadaye aliipa kichwa cha: KITABU CHA MBINGU - LIBRO DI CIELO): Hiki Kitabu hujumuisha Shajara kubwa kubwa 36 ambazo ndanimo husimulia kumbukumbu za siku kwa siku za jinsi Mwalimu wa Mbinguni alivyokuwa akimfunulia ufahamu juu ya Utashi wa Mungu, na namna ya kuuishi ndani ya huo Utashi wa Mungu.

Akiwa daima katika kutii agizo alilopewa, aliandika ‘SAA 24 Za Mateso Ya Bwana Wetu Yesu Kristo’. Na tarehe 6 Mei 1930 aliandika ‘Bikira Maria Katika Ufalme Wa Utashi Wa Mungu”.

Mwaka 1926, akiagizwa na Mwungamishi wake wa pekee, Padre Annibale Maria di Francia, ambaye pia ndiye amekuwa msimamizi na mkaguzi wa maandiko, Luisa aliandika ‘Kumbukumbu za Utoto” (‘Memorie d’ Infanzia’). Ameacha pia idadi kubwa ya barua zake ambazo zinaweza kuwa hazina ya fikara na maoni juu ya mafundisho ya imani juu ya Utashi wa Mungu.

Luisa, ‘Binti Mdogo wa Utashi wa Mungu’, aliyekuwa amechaguliwa na Mungu kwa ajili ya Utume wa ‘MAPENZI YAKO YATIMIZWE duniani kama Mbinguni’ (“FIAT VOLUNTAS TUA sicut in coelo et in terra), aliaga dunia kwa ajili ya kwenda Mbinguni tarehe 4 Machi 1947.

Yesu alikuwa amemwambia: “Utashi Wangu unayo nguvu ya pekee ya kuzifanya roho ziwe ndogo, naam, kuzifanya ndogo zaidi na zaidi, ili ziweze kuonja hitaji kali kabisa kwa Utashi Wangu kutia uhai ndani yao…… Utashi Wangu wa milele utachukua zama za kale, za leo na zijazo; utazifupisha hadi kuwa nukta tu ambayo itamwagiwa ndani yako...”.

Na Luisa alipofadhaika mbele ya maneno hayo, Yesu alimthibitishia kwa kusema:

“Wewe mwenyewe ilitakiwa uwe umeelewa kwamba ilinipasa kukupatia utume wa pekee wa Utashi Wangu, kutokana na mazungumzo yangu ya daima kwako juu ya Utashi Wangu na pia kutokana na jinsi nilivyokufanya uelewe matokeo Yake ya ajabu…..
Baada ya kukufundisha vema vema, nimekuonyesha utume wako, na pia jinsi ndani yako wewe utatokea mwanzo wa kutimilika kwa neno lile ‘Mapenzi Yako Yatimie’ duniani…..(Fiat Voluntas Tua sicut in coelo….). Wala Usiogope! Utashi Wangu utakuwa ni msaada wako na tegemeo lako
”.

Pro Manuscripto
Prayer Group
‘ Divino Volere e Divino Amore ’
[Divine Will and Divine Love]
EMAIL: albert.norbert@gmail.com
WEBSITE: www.divinewilldivinelove.com
TELEGRAM: t.me/utashiwamungunaupendowamungu
RUMBLE Channel: https://rumble.com/c/c-5818809

Kwa matumizi binafsi tu
“Mimi ndiye Mwalimu Mtukufu,
Mwalimu wa Utashi wa Mungu.
Na watu wale wanaoishi katika Utashi Wangu ndio tabasamu Yangu”

⬇️⬇️⬇️
Yesu Katika Tabasamu Yake
Foto hii ilichukuliwa dakika ile, ambapo Padre alikuwa akiinua Hostia, wakati wa Konsekrasio, katika Misa Takatifu ya kuhitimisha Retriti ya siku tatu juu ya Utashi wa Mungu, katika mji wa Leon, Guanajuato, Mexico, Mei 25, 1998

“Mimi ndiye Mwalimu Mtukufu, Mwalimu wa Utashi wa Mungu. Na watu wale wanaoishi katika Utashi Wangu ndio tabasamu Yangu”

Ukiitazama kwa umakini picha hii, elekeza macho yako kwenye Kifua cha Yesu, hapo penye mwanga mweupe unaoangaza.

Utaweza kugundua umbo la Padre aliyevaa mavazi ya Misa na anaadhimisha Misa Takatifu.

Yupo katika hatua ya kupandisha mikono yake juu akiinua Hostia Takatifu wakati wa Konsekrasio!

Pro Manuscripto
Kwa matumizi binafsi tu

EMAIL: albert.norbert@hotmail.com
WEBSITE: www.divinewilldivinelove.com
TELEGRAM Channel: t.me/utashiwamungunaupendowamungu
RUMBLE Channel: https://rumble.com/c/c-5818809
Luisa Piccarreta - “Binti Mdogo wa Utashi wa Mungu”

Ziara ya Roho katika Utashi wa Mungu

Adveniat Regnum tuum! Ufalme Wako Ufike!

KWA SALA HII YA MFULULIZO, ROHO ANAJIUNGANISHA NA UTASHI WA MUNGU, KATIKA KAZI ZAKE ZOTE, ILI KUUABUDU, KUUHESHIMU, KUUSHUKURU, NA KUUPENDA, NA MUDA HUO ANAOMBA KUWA UFALME WAKE UFIKE
Na sisi, tukifuata mfano wa Luisa Piccarreta, tunajongea magotini mwa Immakulata, Mama wa Neno, Malkia wa Ufalme wa Utashi wa Mungu. Pale tunamtolea Mama utashi wetu wa kibinadamu, na badala yake tunamwomba tuupate Utashi wa Mungu. Katika unyofu wetu, mithili ya watoto wadogo, tunamwomba atutumbukize katika mabahari ya Utashi wa Mungu ambamo sisi tunatarajia kuambatana na kila moja ya Kazi zake kwa lengo la kuutuliza kwa utovu wa shukrani kutoka upande wa binadamu. Tutautuliza kwa wimbo wetu huu: “Ninakupenda Wewe! Ufalme Wako Ufike hima hapa duniani!”

Sala hii, ya Ziara ya kiroho katika Utashi wa Mungu, inayosaliwa moyoni, kwa mfululizo,
inamletea mwanadamu fursa ya juu kabisa ya kujiyeyushia mwenyewe ndani ya kazi ya Utashi wa Mungu

Ili kurahisisha zoezi la kusali sala hii kwa mfululizo, na ili kuwawezesha watu wa aina zote na wa mazingira tofauti tofauti ya shughuli za kila siku, hata kama zinawashika na kuwahangaisha sana, sala imegawanywa katika sehemu 24 kulingana na saa za siku.

Sala kamili inaitwa Saa za siku katika Utashi wa Mungu. Kila mtu anaweza akazisali sala zote kwa mfululizo, au anaweza akazigawa katika vipindi mbalimbali vya kutwa, au anaweza akasali sala moja tu kwa siku, na kama akitaka kumaliza kusali saa zote kila siku, anaweza akashirikiana na watu wengine katika zoezi hilo moja kwa kugawana saa za sala baina yao.
Y.M.Y (Yesu, Maria, Yosefu)

Mtindo ulio rahisi na wa ufanisi wa kutekeleza Ziara katika Utashi Mtukufu wa Mungu, na ili kuomba kuupata Ufalme wa FIAT ya Kimungu hapa duniani.

Mtu ajiinue mwenyewe na kuelekea mikononi mwa Muumba Wake. Anajitosa mwenyewe ndani ya Kifua cha Kimungu ili ajiunganishe Naye katika matendo yote aliyokuwa ameyatenda katika Uumbaji kwa ajili ya kumpenda yeye. Naam, mtu hatakubali kumwacha Muumba peke yake, anataka kumfuata katika kila kitendo. Kishapo, mtu anarejea kwenye dakika ya asili yake ili akashuhudie mianzo yake. Pale anahudhurisha vitu vyote sawa kama katika dakika ile, pale Mungu alipotekeleza kitendo cha kuumba vitu vyote. Anakuwa kama hifadhi anayepokea kila chema toka kwa Mungu. Anapokea Pendo lote la Kimungu litokalo katika Kifua Chake kwa njia ya FIAT yenye Maweza. Na yeye mtu, kwa Pendo lile lile, anamrudishia Mungu utukufu na uabudu.

Basi baada ya hapo, Mungu anamleta mtu ndani ya Eden ili pale akapokee pumzi ya kwanza ambayo Mungu aliingiza ndani ya Adamu. Ndiyo hiyo pumzi yenye kutengeneza uhai, na ambayo huendelea kutengeneza uhai. Halafu mtu anaanza kwenda kutembelea karne zote akipita kukumbatia binadamu wote na kumjazilisha kila mmoja na mema ya Muumba. Kadhalika anapitia kazi zote za Malkia Mama, anazitwaa na kuzifanya za kwake, na hata hizo anazitoa kwa Mungu Wake kana kwamba zingekuwa ni kazi za kwake mwenyewe.

Kishapo, mtu anaanza kufikiria ile kazi ya Neno kutungwa katika mimba, na matendo yote ambayo Neno ameyatekeleza wakati wa maisha yake. Na kwa kila moja ya matendo hayo, yeye anahusianisha na tendo la kwake la upendo hata lingekuwa ni dogo jinsi gani, anahusianisha na tendo lake la shukrani, na tendo lake la kuomba ujio wa Ufalme Wake. Halafu mtu anaendelea kumfuata Neno hatua kwa hatua hadi kifo chake. Aliendelea kutanguzana naye hadi ndani ya Limbo, anamsubiri pale kaburini ili apate kumwomba, kwa mastahili na nguvu ya Ufufuko Wake, anaomba Ushindi wa Ufalme wa Utashi wa Mungu. Mwishowe mtu anatangulizana na Neno katika tendo lake la Kupaa Mbinguni ili akamwombe alete kwa haraka Ufalme wa FIAT ya Kimungu hapa duniani.

FIAT! FIAT! FIAT!
SAA YA KWANZA

Tuufuate Utashi wa Mungu katika Matendo Yake yote, ili tukeshe pamoja nao na ili tuupate Uhai Wake wa Kimungu ndani yetu. Tuufuate katika tendo la kuumba Mbingu na Jua.

Yesu, Uhai Wangu, pigo la moyo wangu duni, pumzi ya roho yangu ndogo, makao ya akili yangu, udogo wangu wote unazamia ndani Yako, unapotelea ndani Yako. Mimi ni mtoto mchanga ambaye hajaweza kutembea bado. Ninakujongea Wewe, najibana kwenye mkono wako, na pamoja nawe nataka niingie katika Mwanga ule usiokoma wa Utashi Wako wa Kimungu.

Haya basi tazama, Baba wa Mbinguni tayari anatamka ile FIAT ya kwanza, na ndipo anafungulia mwanga mkubwa kabisa ambao unaangaza bila kikomo cha mipaka. Ewe Yesu Wangu, lo, unijalie roho yangu ipate nguvu yote, maweza, utakatifu, na mwanga wa FIAT yako abudiwa, ili mimi nisiweze kusikia kitu kingine tena ndani yangu isipokuwa Uhai wake hiyo FIAT! Nitakapokuwa nimetajirishwa tayari na Uhai wa hiyo FIAT, nitaweza kukumbatia na kubeba kila kitu, nitaweza kujaziliza kwenye kila kitu, na hata nitaweza kuiteka na Yenyewe na kuishusha ifike duniani kusudi irejee kwa shangwe kuja kutawala kati ya wanadamu!

Kwa hiyo basi, ewe Pendo Langu, uniache niendelee na hija yangu katika Utashi Wako, ili niendelee kufanya ziara ya kufuatilia Matendo Yake yote. Oh! Ni nzuri na inapendeza ilioje kuutafakari Utukufu Mkuu na wa Juu, ambao kwa kutamka FIAT moja tu unaweza mara kulipanua na kulisambaza hili anga samawati likiwa limejaa miliadi ya nyota zinazometameta kwa mwanga wao! Anapotamka FIAT nyingine anaumba jua; anapotamka nyingine tena anaumba upepo, hewa, bahari, na vitu vyote vilivyomo. Na anaviumba na kuvileta vyote hivyo katika mpangilio na uuwiano unaovutia na kuiteka roho ya yule anayetazama.

Ee Yesu Wangu, Chema Changu! Oh, mimi napenda nilitwae na kulifanya la kwangu, hilo Pendo lililobebwa na FIAT yako ya Kimungu wakati ikiumba anga lenye kufurika na nyota. Nataka niweze pia, kwa upande wangu, kupanua na kueneza anga langu la pendo ndani ya FIAT yako yenye Enzi. Kwa njia hiyo, ninapoijaza anga yote kwa pendo langu, nitapenda nitoe sauti yangu kwa kila nyota inayokuwepo ili nayo irudie pamoja na mimi kusema: “Yesu, Mimi ninakupenda!...... Ebu Ufalme Wako ufike hima hapa duniani!..... Utashi Wako wa Kimungu na upewe Utukufu kwa daima!...... Mimi ninauabudu na ninautukuza udumivu wako wa Kimungu na huo Uwepo Wako usiotetereka. Ndivyo hivyo vinavyoleta udumivu wa wanadamu katika mambo mema, na ndivyo pia vinawaandaa vema wanadamu wawe tayari kuupokea Ufalme wa Utashi Wako”.

Ewe Pendo Langu, naendelea na ziara yangu na ndipo ninafika ndani ya jua: Hapo ninakuwazia Wewe ukiwa katika dakika ile ambapo FIAT yako, toka Kifuani mwa Umungu, ilifungulia nje na kutoa mwanga mkubwa kabisa na kutengeneza tufe la jua, yaani ile sayari ambayo ndiyo ingekumbatia na kuibeba dunia pamoja na vitu vyote vinavyokaa ndani yake. Kwa mwanga huo jua lilitoa, kwa kila kimoja ya viumbe, busu lake la mwanga na la pendo. Na kwa njia ya busu lake hilo, kila kitu kiliweza kurembwa, kurutubishwa, kupewa rangi yake, kutajirishwa na kupambika.

Toka ndani ya Umungu Wako, FIAT yako ililifungulia na kulitolea nje hilo jua, yote kwa ajili ya kuonyesha tu Pendo lako kwangu mimi. Kwa minajili hiyo, mimi nataka, ndani yangu, nipate mwanga wake wote, joto lake lote na matokeo yake yote. Hilo ni kwa lengo kwamba, hata mimi niweze kukutolea Wewe, jua langu la kukuza, la kutukuza, na kwa njia yake niweze pia kubariki na kuusifia huo Mwanga wa Milele, kusifia Pendo Lako lisilozimika, Uzuri Wako pekee, Utamu Wako usiokoma na ladha zako zisizohesabika. Ndiyo kweli, Ee Yesu, mimi ninapenda nikukumbatie kwa nguvu ya huohuo mwanga wa jua, napenda nikupe mabusu yangu motomoto pamoja na ujotojoto wake, na kwa sauti yangu napenda kuimbilia huo mwangaza wake wote na pia kuimbilia matokeo yake yote. Nafanya hivyo kusudi nikuombe Ufalme wa FIAT yako kuanzia kule juu kabisa, kwa sayari ya hilo jua hadi kule chini kabisa, ambako mwonzi wake huwa unafikia.
Ewe Pendo Langu, je Wewe huonji jinsi Utashi Wako unavyopenda kuyapasua hayo mapazia ya mwanga ili uweze kuteremka na kuja kutawala kati ya wanadamu? Na mimi, nikiwa juu ya mabawa ya uangazo wa hilo jua, ninakujia ili kukuomba utupelekee haraka huo Ufalme wa FIAT yako. Kutoka pale katikati ya hilo jua, mimi ninakuomba uteremshe mng’ao wake ndani ya moyo wa binadamu ili kuwaangaza kwa Neema Yako, na ili kuwajalia Pendo Lako lenye kuunguza ndani yao chochote kile kilicho kibovu kisichoendana na Utashi Wako. Oh, ni kweli, endapo Mwanga Wako utateremshwa hadi kuwafikia wanadamu, basi uzuri wa Kimungu utawamulika ndani yao, hasira na uchungu vitakoma, na wote watajipatia utamu wako na hivyo uso wa dunia utafanywa kuwa mpya.

Ni kwa jinsi gani ninavyofurahia, Ewe Uhai Wangu, kuweza halafu kukuambia hivi: “Umenipa jua na mimi ninakupa jua! Mimi ninayo sayari chini ya mamlaka yangu, sayari ambayo inakuomba Wewe ulete Ufalme wa FIAT Yako. Je Wewe unataka kuugomea huo mwanga mkubwa ambao unakuomba? .......” . Kwa hiyo basi, Ee Yesu, fanya haraka hima! Hilo jua ndilo mjumbe wako wa Kimungu. Haya basi, Ewe Pendo Langu, fanyiza kwamba mwangaza wake, utakapowagusa tu wanadamu wote, papo hapo uufunue Ufalme wa FIAT Yako, ufunue utakatifu wake, na ufunue lile tamanio la kuwaona wanadamu wakipenya ndani yake FIAT kwa ajili ya kuwafanya wafurahie na wawe watakatifu.

Baba yetu...,
Salamu Maria...,
Atukuzwe Baba..
SAA YA PILI

Tuufuate Utashi wa Mungu katika tendo la uumbaji wa bahari na wa upepo

Ewe Yesu, Uhai Wangu, FIAT Yako inanisukuma, na kwa hiyo basi ona, mimi nipo hapa tayari kwa ajili ya kufuatilia lile tendo la kuumba bahari. Lakini ni nini hicho ninachosikia? Ninasikia sauti ya mbubujiko wa maji unaoendelea. Ni ishara ya ujimudu Wako wa tangu milele na usiokoma. Mimi naingia ndani ya huo ujimudu wa Kimungu, ujimudu unaoendelea bila kukoma, ujimudu unaoleta uhai kwa watu wote. Ninaufanya huo uwe ni ujimudu wa kwangu ili hatimaye niweze kuugawa wote kwa watu wote kwa ajili ya kukuomba Wewe Ufalme wa Utashi Wako, kwa niaba ya watu wote.

Ebu ona, Ewe Yesu, nikiwa na FIAT Yako ninateremkia kwenda kilindini mwa bahari na popote ninapopita na kuona mtikisiko au ujimudu, ninapoona uhai fulani, ninapoona mbubujiko wowote wa maji, hapo hapo ninatoa mlio wangu usiokoma nikisema: “Ninakupenda Wewe, ninakuabudu, ninaku-shukuru, ninakutukuza, na ninakushangilia!”. Kwa sauti yangu ninapiga kelele kushinda ule mbubujiko wa maji ya bahari, kupita kelele za maji yanayotikiswa na samaki, kupita kelele zozote za mawimbi madogo na makubwa ya maji, na katika kila nafasi ninapaza sauti kuomba Ufalme wa FIAT Yako! Je, Ee Yesu, Wewe husikii jinsi matone yote ya maji, katika mbubujiko wao, sawa na kelele za sauti nyingi sana, nayo yakisema: “FIAT, FIAT, FIAT!”. Na je husikii jinsi mawimbi ya maji na makelele yao makali yanavyopiga na yanavyojaribu kupasua na kufumua tumbo la bahari, na hivyo kutaka kulazimisha Utashi Wako utoke nje, uwameze ndani yake na ukawatawale wanadamu wote, na ili hatimaye wanadamu hao waweze kuruhusu FIAT ya Kimungu itawale ndani yao wenyewe ?

Ndani ya bahari hii, ninapoona na kusikia mbubujiko wa maji yake, mimi nakuja kusifia na kupenda huo ujimudu Wako usiokoma; katika mawimbi yake yanayopanda juu sana, ninapenda kutafakari juu ya Usafi ule usio na doa lolote; katika ukuu na upana wa bahari, ninatafakari Neema Yako na Ukuu Wako unaopita kila kitu, Ukuu unaoficha kila kitu. Nikiwa na hisia hizo zote, ninakuomba Wewe Ee Yesu, umfanye binadamu awe mtu mwadilifu, awe na nguvu, na awe msafi rohoni. Umjalie aweze kuishi amefichama ndani ya Utashi Wako Mtakatifu, lakini papo hapo akiwa anahusiana nao kikamilifu, ili aweze kutembea daima katika ujimudu uleule wa Kwako ambamo alikuwa ametokea!

Ewe Yesu Uhai Wangu, sasa napenda nitafakari juu ya Upepo na ubaridi wake unaoburudisha, juu ya pepo kali na athari zake za kimbunga, na za kisulisuli, juu ya pepo ambazo huwa zinaathiri, zinabomoa, zinazotulia pengine, halafu zinapanda na kuvuma, zinazoa na kuhamisha vitu. Hapo ninawaza juu ya kupenda, juu ya kusifu, juu ya kutukuza, na juu ya kushangilia himaya na mamlaka ambayo Utashi Wako unayo juu ya Upepo. Kuna wakati upepo unalia kimya kimya na kuna wakati upepo unapiga makelele kwa nguvu. Ni Pendo la Utashi Wako wa Kimungu kwa Yule anayelia katika upepo akiwa anatamani ajulikane. Na pale anapoona kuwa hasikilizwi na mtu, huyo anapiga makelele, anazungumza kwa sauti za ajabu ajabu. Ni kwa vile Yeye anataka atawale na kwa vile anadai kuwa na himaya yake mwenyewe kati ya wanadamu. Kwa kutumia mamlaka ya Utashi Wako Mkuu wa Juu, fanyiza kwamba Ufalme Wake FIAT Yako ufike kati ya wanadamu, na ukatawale juu yao wanadamu, kwa namna kwamba pasitokee kamwe mwanadamu anayeweza kuthubutu kuipinga hiyo FIAT. Kwa nguvu ya ubaridi wake mwanana, uwavute na kushawishi hao wanadamu. Tumia nguvu ya mabavu yake na ya mhemuko wake ili kuubomoa utashi wa kibinadamu ndani yao ili kusudi uweze kuwainua na kuwateka waingie katika Utashi Wako. Uwawezeshe hao wanadamu kusikia vilio vyako vyote vinavyoendelea, uwawezeshe pia kuelewa kuwa Wewe unataka kutawala kati yao. Kama utaona kuwa husikilizwi nao, basi piga kelele, zungumza kwa sauti kali ukitumia sauti zako zile za ajabu na za mafumbo, hata masikio yao yapate uziwi kutokana na kelele hizo. Hatimaye fanyiza kwamba kila mtu afikie kutambua na kukiri kwamba huo Utashi Wako Mtakatifu ndio Bwana Mkuu wake.
Kwa hiyo basi, Ewe Pendo Langu, hata mimi sasa napenda kukimbia juu ya mabawa ya huu upepo kusudi, kwa kupitia upepo huo, niweze kukuomba ujio wa Ufalme wa FIAT Yako. Katika kila wimbi la upepo huo napenda nipeleke, busu la FIAT hiyo, kwa kila mwanadamu. Niwapelekee mapapaso yake, na pia makumbatio yake matamu.

Baba yetu...,
Salamu Maria...,
Atukuzwe Baba..
SAA YA TATU

Pindi tunapofuata Utashi wa Mungu , tunaruka juu ya dunia nzima tukipita kugonga mhuri wa kauli yetu ya ‘Nakupenda’ juu ya kila kitu kilichoumbwa
.

Ewe Yesu Wangu, Moyo Wangu, Uhai Wangu. Uumbwa wote umekunywa na kunyonya hadi ukajaa Utashi Wako mwabudiwa. Matendo ya Utashi Wako ni mengi wala hayahesabiki katika vitu vyote vilivyoumbwa. Kwa sababu hiyo mimi, ili niweze kuyafuatilia matendo hayo, naamua kuanza kufanya hija kuzunguka ulimwengu mzima. Nafanya ziara kuzunguka kwenye hewa na pale ndani yake ninagonga mhuri wangu wa ‘Ninakupenda’, ili kukuomba kuwa, wanadamu hawa, wakati wanapopumua, wawe wanavuta hewa ya huo Uhai unaotawala ndani ya Utashi Wako.

Kwa kauli yangu ya ‘Ninakupenda’, ninapenda nibariki, nitukuze, na nipige muhuri juu ya utaratibu na harmonia iliyopo katika Uumbwa wote, ili niwafikishie wanadamu wote ule mpangilio na harmonia ya Ufalme wa Utashi wa Mungu. Nataka niruke juu ya dunia yote na kupita kugonga muhuri wangu wa kauli ya ‘Ninakupenda’, iwe juu ya unyasi mdogo kabisa, juu ya vimimea vyovyote vidogodogo, juu ya maua yote, juu ya miti yote iliyo mirefu kabisa, juu ya vilele vya milima, na hivyo hivyo hadi kule kwenye vilindi vyeusi totoro. Nitapita naruka na kubariki vyote hivyo ili kusudi nikuombe ueneze popote Ufalme wa FIAT Yako. Nitaviimbilia vitu vyote na nitatoa sauti yangu kwa vyote, ili kusudi vitu vyote vifikie kusema hivi: “Utashi Wako ufike kutawala hapa duniani”.

Ebu sikiliza Ee Yesu, mimi nagonga mhuri wa ‘Ninakupenda’ yangu hata ndani ya huyo ndege mdogo anayeimbilia, anayetetemesha, na hata anayekoromesha sauti yake. Pamoja na huyo ndege bado ninakuomba utuletee Ufalme wa FIAT Yako. Naendelea kugonga mhuri wa Ninakupenda yangu hata ndani ya huyo kondoo mdogo anayelia akiita, ndani ya huyo njiwa anayelia kama anasikitika. Hata kwa milio ya hao mimi ninakuomba Wewe utuletee Ufalme wa FIAT Yako. Hamna kitu kingine chochote ambacho hakina hamu ya kuchangia katika kurudia kiitikio hiki: ‘FIAT, FIAT’. Ewe Yesu Wangu, ninataka nipenye hadi ndani na katikati ya dunia, ili nikaweke huu moyo wangu pale ndani. Pigo la moyo wangu, wakati litakapokuwa linagonga, liwe linakupenda kwa niaba ya watu wote, liwe linawapenda watu wote, liwe linawakumbatia wote, na kutoka pale katikati ya dunia, moyo wangu uwe unapiga kelele nakulia: Ufike Ufalme Wako na Utashi Wako utawale!

Baba yetu...,
Salamu Maria...,
Atukuzwe Baba..
SAA YA NNE

Pindi tunapokusanyika sote katika Bustani ya Eden, hapo tunajiunga katika sherehe ya Mungu ya kumwumba Mwanadamu.

Ewe Yesu, Uhai Wangu, ninaonja kuwa Pendo Lako linanisukuma likinilazimisha niendelee kuzunguka, na Utashi Wako unaniita ukinitaka niwe pamoja na matendo Yake yote. Inaelekea kuwa Wewe huridhiki iwapo Binti Yako Mdogo hatakuwa pamoja na matendo ya Utashi Wako. Hata kama hajui bado kitu chochote, hata hivyo kwako Wewe ni raha, ili mradi awepo kama mtazamaji na awe hapo kwa ajili ya kurudia kiitikio cha “Ninakupenda, Ninakuabudu, Ninakuheshimu, Ninakushukuru”.

Ndipo mimi naendeleo na mzunguko wangu hadi ninafikia pale ndani ya Bustani ya Edem. Hapo ninakuona ukiwa katika tendo lile ambapo, Wewe Pendo Langu, pamoja na Utatu Mtakatifu, ulipokuwa ukitengeneza pambo lako penzi, yaani ile sanamu nzuri kabisa ya binadamu. Ni kwa pendo kubwa jinsi gani unavyomtengeneza! Ni uzuri mwingi kiasi gani hujamjazia bado! Ni marembo ya rangi ngapi na mitindo mitindo ya kimungu mingapi ambayo hujamwagia juu yake mpaka kufurika! Na wakati huo unapoendelea kumtengeneza, nakuona ukirudia kumtazama tazama, na unasema: “Ah, ni nzuri ilioje hii sanamu yangu!”. Halafu Pendo Lenu linafurika na kufurika kwa nguvu. Na kwa kukosa kujizuia, Ninyi mnaikumbatia hiyo sanamu nzuri na ya kupendeza, ingawa kama haijapewa roho bado, mnaikumbatia na kuibana kwa nguvu, na kwa nguvu zaidi kifuani penu. Halafu mnailisha kwa kuipatia uhai, na mnaipatia na ufanano wa Kwenu. Kishapo Nyinyi Wenyewe mnaingia ndani yake na kuijaza kabisa, kiasi kwamba hii sanamu, iliyo ni johari lenu, inashindwa kuwabeba ndani yake. Kwa hiyo, na yenyewe inajaa na kufurikia nje yake yenyewe, na inajikuta ikitengeneza bahari zake kwa ajili ya kumpenda Muumba wake. Hilo pendo lililotengenezwa, nalo linavimba sana na kutengeneza mawimbi makubwa makubwa yanayoruka na kuja kujipiga juu ya Pendo umbaji. Yanazuka mashindano ya upendo, ya uabudu, na ya utukufu baina ya Muumba na mwanadamu.

Pendo la kwangu linatetemeka mbele ya hilo tendo la ibada namna ile la kumwumbwa kwa binadamu. Ninasikia sauti yako ya uumbaji isiyokoma kurudia rudia ikisema: “Ni nzuri ilioje hii sanamu iliyotengenezwa na Sisi! Mwangwi wa pendo lake, ni jinsi gani unavyotuvuta na kutushawishi, na kutujeruhi! Ni jinsi gani sauti yake ilivyo tamu, na jinsi gani inavyosikika vizuri! Na ukumbatio wake anaotupatia, ni jinsi gani ulivyo ni laini na papo hapo ni wa nguvu! Ni jinsi gani tupatavyo raha kutambua kwamba tulimpatia uhai! Hii sanamu itaendelea kuwa ni raha yetu, furaha yetu, na itaendelea kuwa ni mchezo wetu wa kutufurahisha.
Yesu Wangu, katika kutetemeka kwangu kutokana na Pendo, ndivyo ninavyoingia kwa kweli ndani ya tendo lile ambamo Utukufu wako Mkuu mno, ukiwa unafurika Pendo, ulianza kuvuta pumzi kwa nguvu, pumzi iliyomvutia binadamu ndani Yenu ili kumjazia pumzi ya uhai. Pamoja na uhai, unampatia ufanano Nanyi, na kama urithi wake, mnampatia FIAT Yako ya Kimungu. Hata mimi napenda nipokee hiyo pumzi Yenu inayohuisha. Ninataka niwapende, na niwaabudu katika ukamilifu na utakatifu ule ule aliotumia yule Baba wa kwanza Adamu. Ninataka nipate yale mabahari Yenu ya Pendo na ya Mwanga. Na ingawa kama mimi ni mdogo bado, hata mimi nataka nitengeneze mawimbi yangu makubwa kabisa ya pendo. Hayo mawimbi yatavimba na kupanda hadi kufikia kifuani penu, yatapiga na kugonga kwenye mawimbi ya Kwenu yasiyokoma wala kukatika. Ndipo nami nitaanza kushindana na Muumba Wangu. Nitakuwa nampa Pendo langu ili niweze kuyapata mabahari mengine zaidi ya upendo. Katika mawimbi hayo, nitakuwa nikikuomba Wewe kwamba Ufalme Wako Ufike na FIAT Yako ijulikane. Ninaingia ndani ya ule umoja wa Utashi Wako, ukiwa ni umoja ule ule uliokuwa ndani ya lile johari lako penzi, naingia hapo ili utashi wangu mimi na Utashi Wako Wewe viwe ni Utashi mmoja, na pendo liwe ni moja. Katika huo umoja unaobeba mambo yote, napenda sauti yangu isikike hadi Mbinguni, na ikawafikie wanadamu wote, ikapenye hadi kwenye giza totoro ya vilindini, na ikapige kelele kwa nguvu ikisema: “Ufike Ufalme wa Utashi wa Mungu! FIAT, FIAT VOLUNTAS TUA, hapa duniani kama kule Mbinguni!”. Na katika umoja huo wa Utashi wa Mungu, nitakuwa ninautwaa utakatifu na kuufanya uwe wa kwangu, na ndivyo nitatwaa na utukufu, uabudu, shukrani za mawazo, za mitazamo, za maneno, za matendo, na za hatua mbalimbali za yule Adamu aliyekuwa bila waa lolote. Kwa namna hiyo nitakuwa nakurudishia Wewe, kwa kurudia rudia, yale matendo yake, ili utakapokuwa unaona ndani yangu huo Utashi Wako wa Kimungu unavyotenda kazi, Wewe utaridhia kuwa Ufalme Wako uweze kufika.

Katika Bustani hii ya Edeni, kulikuwepo daima na sherehe baina ya mwanadamu na Muumba. Binadamu alikuwa ndiye doli la Kimungu, alikuwa furaha Yao, alikuwa ndiye raha iliyomfurahisha zaidi Baba wa Mbinguni. Katika huo umoja wa muungano wa Utashi wa Mungu aliokuwa nao, binadamu alifaidi kuchukua nafasi ya kwanza kati ya Uumbwa wote. Kwa hiyo, mambo yote yalikuwa katika harmonia, na katika mpangilio. Anga, nyota, Jua, na bahari, vyote vilionja kuwa vimepata heshima ya pekee kuweza kumtumikia na kumtii Adamu kila alipokuwa anawaashiria kufanya lolote. Alikuwa yeye ndiyo tabasamu ya vitu vyote, alikuwa ni furaha yao, na mtamaniwa wa kila kitu. Na yeye Adamu alikuwa akipeleka kila kitu kwa Muumba Wake, na Mungu alikuwa akielekeza daima macho Yake juu ya Adamu, ili kuhakikisha kuwa pasikosekane kitu chochote kwa ajili ya kumletea raha zake kikamilifu.

Mungu, akimwangalia na kumwona kuwa yu katika upweke, akapenda kuongeza raha yake Adamu iwe maradufu. Alimtia usingizi wa namna ya ekstasi nzito kabisa, na akamfanya alale mikononi Mwake. Ndipo akamtoa ubavu wake mmoja ambao kwayo alimtengeneza mwanamke aliyekabidhiwa kwake awe mwenzi wa kufanana naye. Kwa tendo hilo alimjalia ujazo wa uwingi wa furaha. Na, lo, huyu Eva, akiwa ndiye mama wa kwanza kabisa, alipoingia na yeye katika muungano wa umoja wa Utashi wa Mungu, naye alijiunga kufanya mashindano na Adamu.

Walikuwa wakishindana kati yao, kuona ni nani kati yao, wakiwa ndani ya mabahari yao ya pendo, angeweza kutengeneza mawimbi mengine makuu zaidi ya pendo, ambayo yangeruka juu zaidi na kwenda kugongana na yale mabahari ya Kimungu katika ukuu wao usio na ukomo. Kwa njia hiyo Adamu na Eva wangefikia kujipatia mabahari mengine ya pendo, na kujipatia neema nyingine za Kimungu. Na mawimbi ya pendo lao yalizidi kupanda na kushuka hata kufanya mabahari yao yazidi kuongezeka, kupanuka na kuenea.
Ewe Yesu Wangu, katika muungano huo wa Utashi moja wa Mungu, ninatumbukiza hata hii roho yangu duni ndani ya hayo hayo mawimbi makuu ambayo kwayo Adamu na Eva, kwa pendo kuu, walikuwa wakiupenda na kuutukuza Utukufu Wako Mkuu Mwabudiwa. Mimi, kamwe sitatoka na kutoroka, toka hapo ndani ya Utashi Wako. Bali nitabaki hapo na kufanya kila kitu kiwe ni cha kwangu: Anga, Jua na dunia. Kwa njia hiyo, hapo chini ya miguu ya kiti chako cha juu, nitakuja kuleta na kuweka pendo lote, sifa zote, utukufu na uabudu ambao, katika Uumbwa wote, ulikuwa ukijitokeza kutoka kwenye Kifua Chenu Kiabudiwa.

Katika mawimbi hayo ya pendo, nitakuwa nikipiga kelele endelevu kusema: “Ufike Ufalme Wako! Utashi Wako ujulikane!”. Ewe Pendo Langu, ni jinsi gani ninavyoonja raha katika hii Bustani ya Edeni! Hapa ninaonja ile nguvu ya muungano wa Utashi Wako mmoja wa Kimungu ndani ya hawa wanadamu wa kwanza. Muungano huu unafanya tendo lao liwe ni tendo moja na lile la Muumba. Umoja huo huleta mema yote na kuyafanya yawe ni mali ya pamoja na ya jumla baina ya Mungu na hawa binadamu wawili.

Furaha Zako na raha Zako, Ewe Yesu Wangu, ni pia furaha na raha za kwao. Na mimi niliye Binti Mdogo wa Utashi Wako, napenda nianze upya maisha yangu, katika muungano huu wa umoja wa Utashi Wako, nikiwa pamoja na wazazi wangu Adamu na Eva. Katika mabahari haya ya pendo ninapenda kutengeneza makao yangu, nataka kutengeneza mawimbi yangu ya furaha na ya raha.

Nitakapoyarusha na kuyagongesha katika mabahari Yako ya milele, nitapenda kukufikishia furaha na raha hata niweze kukuona ukitabasamu daima, na daima ukiwa na raha zako.

Baba yetu...,
Salamu Maria...,
Atukuzwe Baba..
SAA YA TANO

Pindi tunaposhuhudia kosa la Adamu na Eva pale katika Bustani ya Edeni, tushiriki maumivu ya Kimungu na tujitahidi kulipa fidia kwa njia ya kauli yetu ya Nakupenda.

Mimi sitatoka kamwe nje ya muungano huu wa umoja wa FIAT Yako. Ninapenda, hatua kwa hatua, niwe ninawafuatilia wazazi wangu wa kwanza. Nitawafuatilia hata pale ambapo, kwa bahati yao mbaya sana walithubutu kutoka nje ya muungano huo wa umoja wa Utashi Wako, kwa kudiriki kufanya utashi wao. Walianguka kutoka kileleni juu kabisa na kutua chini kilindini kabisa kwenye matatizo yote. Ilikuwa mbaya kiasi kwamba hata Mbingu na dunia zilitikisika kwani zilishuhudia wanadamu wale wazuri wa kupendeza kabisa wakihama toka pale ndani ya Utashi wa Muumba Wao. Wote wakawa wanatetemeka na hata Ninyi Wenyewe, Ewe Utukufu Mkuu Mwabudiwa. Ninyi mlipatwa na uchungu hivi hata mkaamua kujivika koti la Haki dhidi yao pale mliposhuhudia ile sanamu nzuri ya kupendeza ikijing’oa. Na aidha, mlishuhudia kuvurugwa kwa furaha zenu, na kupasuliwa kwa yale madoli, yaliyokuwa yakiwaletea burudani, ambayo lile johari Lenu penzi lilikuwa likiwaletea toka ndani ya Utashi Wenu Wenyewe.

Ndiyo maana, Ewe Yesu Uhai Wangu, mimi sitaki kutoka nje ya huo muungano wa umoja wa Utashi Wako wa Kimungu. Ni kwa vile ninataka nijazilishe na kurudisha kile ambacho wanadamu wa kwanza walikipoteza. Nataka niondoe toka kwao lile kovu kubwa la udhalili lililobandikwa juu ya panda la uso wao kwa vile walitekeleza utashi wao wa kibinadamu. Na ni kwa vile nataka niendelee kushikilia pamoja Nawe zile furaha, zile raha, na hata yale madoli uliyokuwa unayo katika nyakati zile za mwanzoni mwa Uumbwa. Napenda nikupe na busu langu, nikupe na fidia yangu endelevu, kwa ajili ya yale maumivu makali kabisa mliyoyapata hata yalipelekea muamue kuvaa vazi la Haki. Mimi napenda niwavue hilo vazi la Haki na badala yake napenda niwavalishe vazi la amani, vazi la mwanga, la muungano wa umoja wa Utashi Wenu. Na mwishowe nataka niwe na kilio kimoja tu: “Ufike Ufalme wa FIAT Yako, Afadhali zirejee zama zile za mwanzoni mwa Uumbwa; afadhali zikaanza tena zile sherehe, zile furaha, na zile burudani zilizokuwepo baina Yako na wanadamu!”. Mimi sitakuacha, wala sitadiriki kuteremka toka hapa magotini pako, iwapo hutanipatia neno la kunithibitishia kuwa utarejesha tena Ufalme wa Utashi Wako kati ya wanadamu.

Ewe Yesu Wangu, Uhai Wangu, Utatu Mwabudiwa, mimi Binti Yenu Mdogo, sitaweza kuwaacheni peke yenu katika uchungu ndani ya umoja wa Utashi Wenu. Kamwe sitaweza kutoka nje. Ninaahidi na ninaapa kamwe kutotekeleza utashi wa kwangu. Kwa kweli, ili nisiwe ninaufikiria na kuukumbuka, naamua sasa kuufunga kwenye miguu ya Kiti Chako cha kifalme ili uwe unalipa fidia endelevu na rasmi kwa ule utoro na uasi waliokuwa wamefanya Adamu na Eva dhidi ya Utashi Wenu Mwabudiwa. Na Mimi, katika muungano wa umoja wa Utashi Wako, ambao ndio peke yake nataka niwe ninautambua, nikiwa ninajiainisha kuwa kitu kimoja na Wewe uliye Uhai Wangu Mtamu, napenda niyapange mbele yangu, kuanzia wazo lile la kwanza kabisa la Adamu hadi lile wazo la mwisho la wanadamu watakaokuja kuwa hapa duniani, kwa lengo la kuweza kutia mhuri wa ‘Ninakupenda’ yangu juu ya kila wazo, nibandike na fidia yangu, nibandike na utukufu kwako. Na kwa kila wazo la wanadamu, ninataka nikuombe Wewe utujalie Ufalme wa Utashi Wako, utujalie kwamba kila akili iweze kuelewa maana ya ‘Utashi wa Mungu’, na watu wote wawe wanauruhusu Utashi wa Mungu uwe unatawala na unaamrisha.

Katika muungano wa umoja wa Utashi Wako nataka nikajipange ndani ya kila mwono wa jicho la mwanadamu, nataka nikajiweke katika nafsi yangu ndani ya kila neno kusudi nikapige mhuri wa ‘Ninakupenda’ kwa ajili yako na nikapige mhuri wa fidia yangu ili kukuomba Wewe Ufalme Wako. Katika kila kazi, katika kila hatua, na katika kila pigo la moyo napenda kukuambia: “Ninakupenda na Ninakulipa fidia kwa dhambi zote wanazotenda”. Na mwishowe napenda nikuombe utupatie Ufalme wa FIAT ya Kimungu.

Baba yetu...,
Salamu Maria...,
Atukuzwe Baba...
SAA YA SITA

Pindi tunapoendelea kutoa fidia yetu, tutapitia orodha ya watu maarufu waliopo katika Agano la Kale

Katika muungano huu wa umoja wa Utashi Wako wa Kimungu, ninapenda nijazilishe ule utukufu wote na lile pendo lote, ambalo wanadamu walitakiwa wawe wamekutolea, kama wangekuwa wameishi katika muungano na huo Utashi Wako. Nataka nijazilishe kwa ajili ya wanadamu wale wote walioishi tangu mwanzo wa dunia hadi siku ile ya Tufani kuu. Nafanya hivyo kwa ajili ya kukuomba Ufalme Wako kwa niaba ya wanadamu hao wote. Napenda niruke juu nikiwa ndani ya Utashi Wako wa Kimungu ili niweze kufuatilia vitu vyote na wanadamu wote.

Kwa minajili hiyo, nakuja kugonga mhuri wa ‘Ninakupenda’ yangu juu ya sadaka ya Ibrahimu na juu ya utii wa Isaka. Ninalitekeleza hilo, ili kwa ajili ya sadaka hiyo na utii huo, nikuombe Wewe Ufalme wa Utashi Wako wa Kimungu. Kadhalika, ndani ya muungano huo wa umoja wa FIAT Yako ninayaona yale mateso ya Yakobo kama vile pia mateso ya Yosefu pamoja na utukufu wake. Ndipo na mimi, kwa ajili Yako, ninagonga mhuri wa ‘Ninakupenda’ yangu juu ya mateso hayo yote. Wakati huo ninakuwa nikikuomba Ufalme Wako. Bado naendelea kuruka nikifuatilia matendo ya Utashi Wako. Ninagundua Maweza ya miujiza ya Musa, nagundua nguvu za Samsoni, utakatifu wa Daudi, na saburi ya Ayubu. Fadhila hizo zote ni vivuli vilivyoletwa na Utashi Wako hata vikatua juu ya watu hao. Nami, pindi ninapopita kugonga mhuri wa ‘Ninakupenda’ yangu ninakuomba, kwa ajili ya wanadamu wote, kwamba Utashi Wako wa Kimungu utawale.

Hebu angalia, Ewe Pendo Langu, mimi muda wote huu nipo nikifuatilia bado matendo ya Utashi Wako ndani ya wanadamu wote, ili kwa njia ya matendo yao hayo yenyewe, nifikie kukuomba Wewe kwamba, FIAT Yako afadhali ijulikane, ipendwe na itamaniwe na wanadamu wote. Ewe Yesu, Uhai Wangu, ninatambua kuwa Utashi Wako Mpendevu wa Kimungu unazidi kuwakaribia wanadamu. Kwa mwanga wa tochi zake, Utashi Wako tayari unawamulika Manabii, ukiwafunulia hao juu ya ujio Wako hapa duniani. Unawahakikishia juu ya muda halisi, juu ya mahali halisi, na juu ya ishara na mazingira yatakayokuwa yameambatana nao. Na mimi kwa upande wangu, wakati ninapopita nikiruka juu ya kila Nabii na juu ya kila ufunuo unaoutoa, ninapita nikimgonga kila mmoja wao, na kila ufunuo, kwa mhuri wa kauli yangu ya ‘Ninakupenda’, ‘Ninakuheshimu’, na ‘Ninakushukuru’. Na katika kila nafasi ninakuomba Ufalme wa Utashi Wako.

Kila ahadi uliyokuwa ukitoa, kila ufunuo ulioutoa na kuuonyesha mintarafu ujio Wako hapa duniani, vilikuwa ni kauli uliyokuwa ukiwapatia, ya kutuliza na kutumainisha. Ndani ya ahadi na funuo hizo, ulikuwa ukiunganisha daima Ufalme wa Ukombozi Wako na Ufalme wa Utashi Wako. Sasa ni kwa nini, Ewe Pendo Langu, hutaki kuuharikisha huo Ufalme? Mbona Wewe huwezi kutenda kazi Zako kwa nusunusu, na wala Wewe huwa hutoi mema yako kwa nusunusu. Haya basi, fanya hima: Endapo ulikuwa umetupatia nusu ya mema.

Yako, sasa kamilisha kila kitu, kwa kuruhusu Ufalme Wako ufike. Huyu Binti Yako Mdogo wa Utashi Wako, hataweza kukuacha. Ataendelea hadi akuchoshe. Kwa hiyo, nitakuja kusitisha mazungumzo yangu pale tu nitakapouona Utashi Wako ukitawala na ukiamrisha kati ya wanadamu.

Baba yetu...,
Salamu Maria...,
Atukuzwe Baba...
SAA YA SABA

Sasa tunajitumbukiza katika mabahari ya mwanga na ya utakatifu ya Mama wa Mbinguni. Pamoja naye tuwe tunaomba Ufalme wa Utashi wa Mungu ufike duniani.

Ewe Pendo Langu, ninaonja kuwa Pendo Lako limejaa mno na linafurikia ndani yangu. Ninakuona ukivua joho lako la Haki, na Ninyi Nafsi zote Tatu za Mungu mnajipanga na kujiweka tayari kwa ajili ya sherehe mpya; na inaelekea sherehe hii ni kubwa zaidi ya ile iliyokuwa imefanyika katika tendo lile la kumwumba binadamu. Ninyi Wenyewe, mnatoa nje yenu wenyewe, mabahari ya Maweza, ya Hekima, ya Pendo, na ya Uzuri upendezao usioelezeka. Halafu mnayakusanya mabahari hayo mahali pamoja. Kishapo, kutoka kwenye kina cha mabahari hayo, kwa nguvu na uwezo wa neno Lenu la uumbaji, mnamwita Malkia Mdogo ambaye mnamtia na uhai. Mnamtengeza awe safi kabisa, bila doa lolote, na mnamfanya awe amejaliwa na neema za uzuri upendezao. Ni mzuri hivi hata anamteka Yule Mwenyewe aliyemuumba.

Kipindi hicho cha kuibeba mimba ya huyu Malkia Immakulata, panazinduliwa sherehe nyingi baina ya Mbingu na ya dunia. Uumbwa wote unashangilia na unapiga magoti yao. Wote wanampongeza na wanamshangilia kama Malkia wao. Hata mimi ninapiga magoti yangu mbele yake huyu ambaye Mungu Baba, Mwana na Roho Mtakatifu wanamgombania, ili mmoja wao au mwingine anayemtaka ajiburudishe naye zaidi, na kama anamtaka, aweze kumfaidi kwa vikubwa zaidi. Katika hatua hiyo, ninyi Wote, Nafsi Tatu za Mungu, hamtendi kitu chochote tena, isipokuwa kujaa na kufurika Pendo ambalo mnaendelea kummwagia daima huyo Malkia Mzaliwa mpya. Na wala hamuachi kamwe kumwaga viwango vingine zaidi vya neema juu yake ili kukuza mabahari yake yawe makubwa zaidi na mapana bila ukomo wowote. Ndani ya binadamu huyu wa Mbinguni, mnamgundua Yule Mwanamke, ambaye ndiye atapasika kuwapatieni Ninyi kila kitu, atakayepasika kulipa fidia ya mambo yote, na atakayepasika kuwarejeshea ule utukufu wote wa Uumbwa. Kwa minajili hiyo basi, huku mkiendelea kumshikilia, mkimbana penye magoti Yenu ya Kibaba, mnamfunulia kumwonyesha na kumweleza juu ya kisa cha binadamu aliyekuwa ameanguka katika dhambi, mnamweleza juu ya uchungu wenu, na mnamweleza juu ya Utashi Wenu Mwabudiwa, ambao ulikuwa umegomewa na kusukumizwa mbali na binadamu. Mwishowe Ninyi mnayakabidhi mambo yote kwake huyo Malkia.

Katika hatua hii, Ewe Yesu Wangu, mimi ninatehemu, ninaonja uchungu sana sana kushuhudia jinsi Utashi Wako pendevu ukigomewa na kusukumizwa mbali. Papo hapo ninastaajabu ushujaa wa huyu Malkia Mdogo Mzaliwa mpya, ambaye anautoa uhai wake kama zawadi. Anaapa kuwa hapendi kusikia wala kuujua tena, na ndipo anautumbukiza ndani ya FIAT Yako, ambayo sasa ndiyo anayoitwaa iwe ni uhai wake. Anatoa mamlaka kwa FIAT hiyo, na ndani yake anaunda Ufalme wa kwanza wa Utashi Wako ndani ya roho yake. Na kutoka pale ndani ya roho yake ninasikia kiitikio chake hiki endelevu: “Ufike Ufalme wa Ukombozi, afike Neno hapa duniani, ifike na amani kati ya Muumba na mwanadamu! Mimi sitateremka toka hapa penye magoti yenu ya Kibaba, endapo Ninyi hamtanijalia hicho ninachowaombeni”. Na angalia sasa, Malkia Mdogo analia machozi, hata anailowesha mikono Yenu ya Kibaba kwa machozi yake. Mara nyingine anawatazama na kutabasamu na halafu anawaombeni. Kisha, anapojitumbukiza katika yale mabahari mliyompatia, anawaleteeni furaha mbalimbali na raha ya Utashi Wenu, hata anaweza kuwashindeni na kuwalegezeni, ili tu aje ampate Mkombozi ajaye. Oh, ni mbinu ngapi na ujanja gani wa pendo, alizotumia Mama yangu wa Mbinguni juu yenu! Ni jinsi gani alivyokuwa akiwateka kwa mitindo yake ya kupendeza ajabu, kiasi kwamba Wewe, Pendo Langu, mwishowe ukashindwa na kukubalia maombi yake na kilio chake kisichokoma.


Baba yetu...,
Salamu Maria...,
Atukuzwe Baba...