Swahili News
3.78K subscribers
108K photos
58.6K videos
28 files
266K links
🐾
Download Telegram
Ni ligi ipi unapenda kuifatilia zaidi? Sasa #mzukacasino imekuletea ligi zaidi ya 50 zinazochezeswa kila baada ya dakika 2, chagua ligi na timu uzipendazo ubet kwa dau dogo tu la sh 100 na ushinde hadi 100,000 papo hapo, kubwa zaidi ushindi wa mamilioni kila Jumapili unatolewa, unasubiri nini? Tembelea tovuti yetu www.mzukacasino.co.tz kisha chagua Virtual ndani kuna ligi zaidi ya 50 za kuchagua ni wewe tu kubet ushinde. Jinsi ya kuweka hela kwenye Mzuka Casino 1) Nenda kwenye menyu yako ya Mpesa au Tigo Pesa 2) Chagua namba Lipia Bili 3) Kisha weka namba ya kampuni 123222 4) Kumbukumbu ni 123 5) kisha weka kiasi unachotaka kuanzia 500 6) Ingiza namba yako ya siri, kisha bonyeza OK kuthibitisha muamala wako 7) Utapokea meseji ya kuthibitisha kupokea muamala wako Cc. @mzukacasinotz #mzukacasino #michezokamayote

@habariTz https://ift.tt/2L14yoN
VIDEO: Mfanyabiashara Hamisi Said (38), anayekabiliwa na kesi ya kumuua Mkewe, Naomi Marijani kisha kumchoma moto, ameieleza Mahakama ya Kisutu kuwa anaomba apatiwe laini zake mbili za simu zenye zaidi ya Tsh.Milioni 5 kwa ajili ya matumizi madogomadogo ya nyumbani kwake pamoja na kumlipia ada Mtoto wake. _ Said ambaye hivi karibuni alitoa vitisho kwa Waandishi wa Habari kwamba atawafanya kitu mbaya, ametoa maombi hayo Mahakamani leo Ila yamepanguliwa na Wakili wa Serikali Wankyo Simon ambaye ameeleza kuwa hawawezi kumpatia laini hizo kwasababu simu ni sehemu ya upelelezi na kama anahitaji fedha zake aandike barua kwenda kwa Mkurugenzi wa Mashitaka. _ Kesi hiyo imeahirishwa hadi September 10, 2019. (📹 via @ayotv_)

@habariTz https://ift.tt/327gpHy
Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kuendelea leo katika dimba la Uhuru. Kocha wa Azam FC, Etienne Ndayiragije leo anaanza Ligi kwa kukutana na timu aliyoifundisha msimu uliopita KMC....katika msimu uliopita KMC na Azam FC walipokutana mechi zote mbili walitoshana nguvu, mechi ya kwanza 2 - 2 na mechi ya pili walitoka 0 - 0, Je leo nani kuanza Ligi kwa ushindi? #SIsiNiSoka #Azamsports2 #AzamTVAppp #KMC #AZAMFC

@MichezoTz https://ift.tt/2zp0vf7
MAGAZETI YA LEO – AZAM TV 27/08/2019 >Lissu ambwaga Job Ndugai, mawakili 15. >Siri ya miaka 37 iliyoiponza ndege ya ATCL Afrika Kusini. >Mambo matano yaliyoiponza Simba kwa UD Songo. >Dakika 180 kuitajirisha Yanga CAF. Kwa dondoo zaidi tembelea chaneli yetu ya Youtube #Azamtvtz

@MichezoTz https://ift.tt/2PhGz8L
SERIKALI YAZINDUA UJENZI WA VIVUKO VIPYA VYA BUGOROLA-UKARA, CHATO-NKOME Serikali imezindua rasmi ujenzi wa vivuko vipya viwili vya kisasa vitakavyotoa huduma ya kusafirisha abiria, mizigo na magari kati ya Bugorola-Ukara Wilaya ya Ukerewe Mkoa wa Mwanza na Chato-Nkome Wilaya ya Chato mkoani Geita. Kivuko cha Bugorola-Ukara kinajengwa na Kampuni ya Songoro Marine Transport Boatyard Ltd kwa gharama ya Tsh bilioni 4.2 na kile cha Chato- Nkome kinagharimu Tsh bilioni 3.1. Vivuko hivi vitajengwa kwa miezi 10. “Vivuko vyote vinagharimu jumla ya Tsh bilioni 7.3 fedha zinazotolewa na Serikali,” - Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA), Mhandisi Japhet Maselle. #AzamTVUpdates #BreakingNews, #AzamTVApp #AzamTV #AzamTWO #AzamTVHabari #Habari #UTV #UFM

@MichezoTz https://ift.tt/2KZKXF6
Matukio ya ajali bado yanaendelea kutokea?Watu 8 wameshikiliwa na polisi mkoani Kagera baada ya kuchota mafuta wakati lori la mafuta lilipoanguka. Swali ni: Je, ajali ya gari la mafuta Morogoro ilioua watu zaidi ya 100 haikuacha fundisho kwa wengine?#kagera#ajali#morogoro 🇹🇿
@HabariTz https://www.instagram.com/p/B1qPaOVAeeC/
Mamlaka nchini Kenya zimepiga marufuku kuchezwa kwa wimbo wa Diamond Platinumz wa Tetema,na wimbo maarufu zaidi nchini Kenya kwa sasa, Wamlambez uliopigwa na kundi la Sailors. Mkurugenzi wa bodi ya kudhibiti filamu nchini Kenya Ezekiel Mutua amesema nyimbo hizo zisipigwe nje ya vilabu vya burudani kwa kuwa na maudhui ya watu wazima. Je alikuwa wapi hadi leo? #wamlambez #tetema #diamondplatnumz #sailors #wamlambezwamnyonyez
@HabariTz https://www.instagram.com/p/B1qYqwmAck0/
Popote ulipo mpenzi wa DW, salamu zetu kutoka Bonn zikufikie. Katika matangazo yetu mchana wa leo: -Iran yasema haitafanya mazungumzo yoyote na Marekani, hadi pale vikwazo ilivyowekewa vitakapondolewa. -Nchini Tanzania, vuguvugu la uchaguzi mkuu ujao lachukua mwelekeo mpya, baada ya Makamu wa Rais Samia Suluhu kusema wazi kuwa hatochukua fomu kuwania urais wa Zanzibar- Kenya nako, Rais Uhuru Kenyatta yakubali shinikizo la makamu wake William Ruto, na kuruhusu chama tawala cha Jubilee kusimamisha mgombea kupambana na chama cha ODM cha Raila Odinga katika uchaguzi mdogo kwenye jimbo la uchaguzi la Kibera. Pichani ni kikosi kizima kitakachokuwa studioni kwa ajili yako leo: Kuanzia kushoto ni Zainab Aziz, Sylvia Mwehozi na Iddi Ssessanga. Usikose kuwa nasi tafadhali.
@HabariTz https://www.instagram.com/p/B1qaDbDASMM/
Waziri Mwinyi aanza ziara Mara Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Dkt Hussein amewasili mkoani Mara kuanza ziara ya kikazi ya siku mbili, ambapo pamoja na mambo mengine atatembelea miradi mbalimbali inayotekelezwa na Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa -SUMA JKT. Akitoa taarifa kwa Waziri Mwinyi, Mkuu wa mkoa wa Mara, -Adam Malima amesema kuwa, uwepo wa JKT mkoani humo, umesaidia kukuza uchumi wa mkoa huo, kwa kuwa Jeshi hilo limekua likitekeleza miradi mbalimbali ambayo ni pamoja na ile ya ufugaji wa samaki na kilimo.

🚭 @HabariTz
https://ift.tt/2NKzQlB